Kubishana na huyo kunahitajika moyo wa uvumilivu mkubwa sanaHapo umenidanganya. Kuna sheria ya kulinda taarifa ya mteja. Hii sheria ni ya dunia nzima wala siyo Tanzania tu.
Unafikiri kwanini Max alikataa kutoa taarifa za JF members? Yeye ni nani mpaka alikataa?
Alisimamia sheria ndiyo maana mpaka leo members wa JF wanaenjoy na maisha.
Tupo kwenye ulimwengu wa watu wenye IQ kubwa kwahiyo kabla ya kujibu inabidi utafakari jibu lako.
Umesema kweli. Kinachotofautisha kati ya ushushushu wa Bongo na nchi nyingine ni kuwa, ushushushu wa Bongo wana-deal na pet issues na mbaya zaidi wanataka wawe ndiyo mapolisi na mahakimu pia. Hawahangaiki na maslahi ya Taifa bali ya viongozi wachache. Usalama wa Taifa ulianza kuharibiwa kipindi cha Mkapa, wakati walipokubali kutrumiwa na Lowassa na Kikwete kuingia madarakani.Ni wiki ya Mtandao wa Tigo Tanzania baada ya muajiriwa wake kitengo cha sheria kuwa mmoja wa mashahidi katika kesi ya ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA.
Kampeni zimeanza kushika kasi kila kona kususia huduma za mtandao husika.
Hili lina madhara japo si makubwa. Mwaka jana Vodacom Tanzania ilipitia katika wakati mgumu kuhusiana na kutoa siri za wateja. Wateja wote ni wanasiasa wa upinzani wa chama cha CHADEMA. Kampeni ile ya kususia bidhaa na huduma za Vodacom Tanzania ilikuwa kubwa na mbaya, lakini yalipita japo jina lake lilichafuka kwa kaisi chake, ni zamu ya Tigo sasa.
Hizi kampeni za kususia bidhaa na huduma za mitandao husika haziwezi kufanikiwa kwa asilimia 100 lakini zinapeleka ujumbe kwa sauti ya juu kwa wahusika kwamba haya mambo si sawa na si sahihi hasa linapokuja hili la kulinda siri za wateja
Mimi siilaumu hii mitandao ya simu Tanzania. Ni sahihi kabisa kwa usalama wa nchi kuwa na nyoka na mapandikizi kila mahali.. Na hii sio Tanzania tuu bali ni popote pale ulimwenguni. Usalama wana watu wao kwenye sekta binafsi na za serikali pia. Wana nyoka wao kwenye makampuni makubwa na madogo. Kila mahali wapo na kiusalama sio kosa kabisa
Haya makampuni ya simu na sekta nyingine pia kuna wafanyakazi wanaajiriwa kwa vimemo ama kwa simu moja tuu.. Wengine huajiriwa kwa mlungula kabisa kuficha uhalisia na wengine huajiriwa kwa uwezo wao. Ni kati ya hao kuna nyoka na mapandikizi na kamwe huwezi kuwajua kwakuwa sifa moja ya usalama ni kuwa invisible kama huyu wetu hapa JF[emoji2]
Sasa kosa liko wapi? Kosa hili hapa
Kuna ombwe ama kasoro kubwa kwenye baadhi ya watendaji kwenye mamlaka zetu. Hasa linapokuja swala la kudili na wapinzani kwenye kaliba ya mashtaka na sheria za makosa ya jinai nk
Kama nilivyosema maswala yote ya usalama huwa ni invisible. Kwahiyo hata siku moja huwezi kumkuta mwanausalama wa taifa ngazi ya nyoka au pandikizi akisimama mahakamani na kutoa ushahidi. Kazi ya usalama ni kugundua na kuonesha tatizo lilipo.. Mamalaka za kisheria ndio hutafuta njia sahihi ya kudili nalo.
Kesi ya Mbowe imeonesha madhaifu mengi toka mamlaka zetu namna ya kuwatumia mashahidi vipenyo kama mashahidi visible hii ni hatari sana. Sana, na madhara yake ni mengi kama hilo la kujulikana kuwa kumbe kuna maafisa vipenyo huko na huko na kupelekea kuharibu biashara za wengine
Kitu kingine cha kushangaza ni hili la mashahidi wa ugaidi kuwa wazi na kujulikana na kila mtu. Kwa kanuni za kesi za kigaidi mashahidi hufichwa na ni ngumu mno kujulikana wazi wazi.
Tunapowatia ndimu machoni Tigo tusisayasahau na haya mengine mengi kwakuwa hata tunaokaa nao vijiweni mitaani, vijiweni mitandaoni huku wengine wakiwa ni wasiri wetu kati yao ni nyoka, mapandikizi na maafisa vipenyo
Kuna bid deals hizi wanazifumbia macho..hakuna wezi kama makampuni ya simu, yanaibia wateja yanaibia serikali lakini sijawahi kuona reaction yoyoteUmesema kweli. Kinachotofautisha kati ya ushushushu wa Bongo na nchi nyingine ni kuwa, ushushushu wa Bongo wana-deal na pet issues na mbaya zaidi wanataka wawe ndiyo mapolisi na mahakimu pia. Hawahangaiki na maslahi ya Taifa bali ya viongozi wachache. Usalama wa Taifa ulianza kuharibiwa kipindi cha Mkapa, wakati walipokubali kutrumiwa na Lowassa na Kikwete kuingia madarakani.
Mi nahisi yule ni kipenyo, amewekwa pale kuwaspy Tigo.. sema sasa ni kipenyo CCM. Haiwezekani kesi zote za wapinzani yeye ndo yupo front. His cover have been blown!Pengine kuna nguvu nyuma yake inamlinda
Leak hii sentence umeisoma na kuielewa? .....Tunapowatia ndimu machoni Tigo tusisayasahau na haya mengine mengi.….Nimesoma mjadala nashangaa umeshindwa kabisa kueleza wazi kabisa kuwa sheria ya mawasiliano na posta inatoa mamlaka kwa serikali na taasisi za usalama kupata taarifa za wateja au mteja yeyote kutoka kwa mtoa huduma yeyote yule......
Sheria hiko wazi na inalazimisha wamiliki wa mitandao kutoa taarifa za mteja na kuwa tayari kuwasilisha ushahidi mahakamani inapo hitajika na mamlaka.
Badala ya kuparamia mitandao ya simu na mitandao basi tuparamie sheria inayo lazimisha watoa huduma kutoa taarifa za wateja.... hakuna mtandao ambao unaweza kugomea sheria iliyo ikubali.........
Tujisumbue kujua chanzo na kufatilia tusitoe lawama pasipo stahili.. hata wewe ungekuwa mmiliki wa mtandao wa tigo usingelikwenda kinyume na sheria husika....
Hawa tunawaonea tuu tu deal na sheria...
Mkuu Mshana Jr umeongea ukweli kuntu. Nchi hii imefikia mahali pabaya sana, hasa linapokuja suala la chuki za kiitikadi za kisiasa. Mwendazake na genge lake la Sukuma Gang ndio waliofikisha nchi hii mahali hapa.Ni wiki ya Mtandao wa Tigo Tanzania baada ya muajiriwa wake kitengo cha sheria kuwa mmoja wa mashahidi katika kesi ya ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA.
Kampeni zimeanza kushika kasi kila kona kususia huduma za mtandao husika.
Hili lina madhara japo si makubwa. Mwaka jana Vodacom Tanzania ilipitia katika wakati mgumu kuhusiana na kutoa siri za wateja. Wateja wote ni wanasiasa wa upinzani wa chama cha CHADEMA. Kampeni ile ya kususia bidhaa na huduma za Vodacom Tanzania ilikuwa kubwa na mbaya, lakini yalipita japo jina lake lilichafuka kwa kaisi chake, ni zamu ya Tigo sasa.
Hizi kampeni za kususia bidhaa na huduma za mitandao husika haziwezi kufanikiwa kwa asilimia 100 lakini zinapeleka ujumbe kwa sauti ya juu kwa wahusika kwamba haya mambo si sawa na si sahihi hasa linapokuja hili la kulinda siri za wateja
Mimi siilaumu hii mitandao ya simu Tanzania. Ni sahihi kabisa kwa usalama wa nchi kuwa na nyoka na mapandikizi kila mahali.. Na hii sio Tanzania tuu bali ni popote pale ulimwenguni. Usalama wana watu wao kwenye sekta binafsi na za serikali pia. Wana nyoka wao kwenye makampuni makubwa na madogo. Kila mahali wapo na kiusalama sio kosa kabisa
Haya makampuni ya simu na sekta nyingine pia kuna wafanyakazi wanaajiriwa kwa vimemo ama kwa simu moja tuu.. Wengine huajiriwa kwa mlungula kabisa kuficha uhalisia na wengine huajiriwa kwa uwezo wao. Ni kati ya hao kuna nyoka na mapandikizi na kamwe huwezi kuwajua kwakuwa sifa moja ya usalama ni kuwa invisible kama huyu wetu hapa JF[emoji2]
Sasa kosa liko wapi? Kosa hili hapa
Kuna ombwe ama kasoro kubwa kwenye baadhi ya watendaji kwenye mamlaka zetu. Hasa linapokuja swala la kudili na wapinzani kwenye kaliba ya mashtaka na sheria za makosa ya jinai nk
Kama nilivyosema maswala yote ya usalama huwa ni invisible. Kwahiyo hata siku moja huwezi kumkuta mwanausalama wa taifa ngazi ya nyoka au pandikizi akisimama mahakamani na kutoa ushahidi. Kazi ya usalama ni kugundua na kuonesha tatizo lilipo.. Mamalaka za kisheria ndio hutafuta njia sahihi ya kudili nalo.
Kesi ya Mbowe imeonesha madhaifu mengi toka mamlaka zetu namna ya kuwatumia mashahidi vipenyo kama mashahidi visible hii ni hatari sana. Sana, na madhara yake ni mengi kama hilo la kujulikana kuwa kumbe kuna maafisa vipenyo huko na huko na kupelekea kuharibu biashara za wengine
Kitu kingine cha kushangaza ni hili la mashahidi wa ugaidi kuwa wazi na kujulikana na kila mtu. Kwa kanuni za kesi za kigaidi mashahidi hufichwa na ni ngumu mno kujulikana wazi wazi.
Tunapowatia ndimu machoni Tigo tusisayasahau na haya mengine mengi kwakuwa hata tunaokaa nao vijiweni mitaani, vijiweni mitandaoni huku wengine wakiwa ni wasiri wetu kati yao ni nyoka, mapandikizi na maafisa vipenyo