Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #121
CUF & MAALIM WABEBA ZIGO
JECHA AJA NA MAPYA
Mazungumzo ya mufaka yamevunjika. Hakuna taarifa isipokuwa huyu anasema yule kasema
Kwa muda tulieleza jinsi mazungumzo yalivyolenga kuvuta muda, kupoza joto na kisha kushtukiza
Kama tulivyosema ndivyo ilivyojiri na tulisema, mwisho wa siku mzigo utakuwa mabegani mwa CUF
Leo Maalim ana vibarua viwili .
Kwanza, kuwaeleza wafuasiéwananchi nini kilitafutwa, kimekwama wapi na kwanini.
Pili, Jinsi gani ya kuondoka katika mkwamo unaolenga uhalali kwa CCM kufuatia uchaguzi marudio
Jecha ametangaza March 20 siku ya marudio.
Kama wakati anatangaza kufuta hili nalo limetokea katika njia ile ile.,bila kuambatana na wajumbe
Jecha anasema hakutakuwa na kampeni, na majina yaliyokuwepo ni yale yale.
Hapa kuna nadharia mbili au tatu
1. Kukataza kampeni ni kunaweza leta hisia kuzuia mikutano kwa njia ya kificho ili yaliyotokea yasijulikane zaidi.Kinachotakiwa ni watu kupiga kura si kupata habari nyingine
2. Majina ni yale yale imelenga mambo mawili kwa mtazamo na maoni yetu wengine
a) Kubakiza majina ili ikitokea watu wamesusa,uwepo wa majina utajenga uhalali wa uchaguzi.
Kwamba, kulikuwa na wagombea na X kashinda.
Hili pia linaungana na lile la kupiga marufuku kampeni.
Maana yake,watu wasijeuliza mbona jina lipo mgombea hakupiga kampeni au alitangaza kutoshiriki
b) Majina kubali yale yale kumelenga kuhakikisha hata kama chama au baadhi ya vyama havitashiriki, vile ``vinavyotaka`` ambavyo vingine vinaweza kuwa na ``ushirika`` vinaendelea na uchaguzi
Ikitokea mshiriki anafukuzwa katika Chama chake, bado jina lake litakuwepo.
Lengo ni kukabiliana na vyama vitakavyofukuza wanachama wao wanaotaka ``kushiriki`
Unaweza kuona hesabu zinavyopangwa kIufundi kuujengea uchaguzi sura na uhalali unaotakiwa.
CHANGAMOTO ANAZOKUMBANA NAZO JECHA
Kwanza, kuonyesha bila shaka kuwa maamuzi ni ya tume nzima na si kama alivyofuta peke yake
Hakuna kumbu kumbu zozote za kikao kilichofuta uchaguzi licha ya kutokuwa na mamlaka, je, kuna kikao au kumbu kumbu zozote za tume kutangaza tena siku ya uchaguzi!!
Wajumbe wa tume wakajitokeza na kutoa kauli tofauti a, tume itabaki Jecha
Ile akidi inayokamilisha tume au ule mchanganyiko utazua maswali mengine magumu sana kwa jecha
Pili, kwa wanachama wanaogombea wengine wamefukuzwa na vyama vyao.
Hivi karibuni habari za mgombea wa ADC kufukuzwa uanachama zimeandikwa kwa kirefu.
Maana yake, kiongozi huyo hata kama anataka kushiriki uchaguzi wa marduio kisheria hataweza.
Kisheria usajili wa vyama ni suala la muungano.
Msajili wa vyama anapelekewa taarifa za kufukuzwa wanachama .
Mwanachama akifukuzwa tayari anapoteza masilahi (privilege)ikiwemo kugombea uongozi
Katika mazingira hayo Jecha hatakuwa na la kufanya
Ili afaninikiwe anahitaji kufanya kazi na msajili kutengua kitendawili hicho
Vingievyo itabidi ajitokeze ku-clarify hali hiyo, na katika mazingira yaliyopo atavuruga Zaidi
Tusemezane
JECHA AJA NA MAPYA
Mazungumzo ya mufaka yamevunjika. Hakuna taarifa isipokuwa huyu anasema yule kasema
Kwa muda tulieleza jinsi mazungumzo yalivyolenga kuvuta muda, kupoza joto na kisha kushtukiza
Kama tulivyosema ndivyo ilivyojiri na tulisema, mwisho wa siku mzigo utakuwa mabegani mwa CUF
Leo Maalim ana vibarua viwili .
Kwanza, kuwaeleza wafuasiéwananchi nini kilitafutwa, kimekwama wapi na kwanini.
Pili, Jinsi gani ya kuondoka katika mkwamo unaolenga uhalali kwa CCM kufuatia uchaguzi marudio
Jecha ametangaza March 20 siku ya marudio.
Kama wakati anatangaza kufuta hili nalo limetokea katika njia ile ile.,bila kuambatana na wajumbe
Jecha anasema hakutakuwa na kampeni, na majina yaliyokuwepo ni yale yale.
Hapa kuna nadharia mbili au tatu
1. Kukataza kampeni ni kunaweza leta hisia kuzuia mikutano kwa njia ya kificho ili yaliyotokea yasijulikane zaidi.Kinachotakiwa ni watu kupiga kura si kupata habari nyingine
2. Majina ni yale yale imelenga mambo mawili kwa mtazamo na maoni yetu wengine
a) Kubakiza majina ili ikitokea watu wamesusa,uwepo wa majina utajenga uhalali wa uchaguzi.
Kwamba, kulikuwa na wagombea na X kashinda.
Hili pia linaungana na lile la kupiga marufuku kampeni.
Maana yake,watu wasijeuliza mbona jina lipo mgombea hakupiga kampeni au alitangaza kutoshiriki
b) Majina kubali yale yale kumelenga kuhakikisha hata kama chama au baadhi ya vyama havitashiriki, vile ``vinavyotaka`` ambavyo vingine vinaweza kuwa na ``ushirika`` vinaendelea na uchaguzi
Ikitokea mshiriki anafukuzwa katika Chama chake, bado jina lake litakuwepo.
Lengo ni kukabiliana na vyama vitakavyofukuza wanachama wao wanaotaka ``kushiriki`
Unaweza kuona hesabu zinavyopangwa kIufundi kuujengea uchaguzi sura na uhalali unaotakiwa.
CHANGAMOTO ANAZOKUMBANA NAZO JECHA
Kwanza, kuonyesha bila shaka kuwa maamuzi ni ya tume nzima na si kama alivyofuta peke yake
Hakuna kumbu kumbu zozote za kikao kilichofuta uchaguzi licha ya kutokuwa na mamlaka, je, kuna kikao au kumbu kumbu zozote za tume kutangaza tena siku ya uchaguzi!!
Wajumbe wa tume wakajitokeza na kutoa kauli tofauti a, tume itabaki Jecha
Ile akidi inayokamilisha tume au ule mchanganyiko utazua maswali mengine magumu sana kwa jecha
Pili, kwa wanachama wanaogombea wengine wamefukuzwa na vyama vyao.
Hivi karibuni habari za mgombea wa ADC kufukuzwa uanachama zimeandikwa kwa kirefu.
Maana yake, kiongozi huyo hata kama anataka kushiriki uchaguzi wa marduio kisheria hataweza.
Kisheria usajili wa vyama ni suala la muungano.
Msajili wa vyama anapelekewa taarifa za kufukuzwa wanachama .
Mwanachama akifukuzwa tayari anapoteza masilahi (privilege)ikiwemo kugombea uongozi
Katika mazingira hayo Jecha hatakuwa na la kufanya
Ili afaninikiwe anahitaji kufanya kazi na msajili kutengua kitendawili hicho
Vingievyo itabidi ajitokeze ku-clarify hali hiyo, na katika mazingira yaliyopo atavuruga Zaidi
Tusemezane