Mitihani kidato cha sita 2013: Vurugu vurugu, wanafunzi waanza kelele.

Bado inatuchanganya kwa kweli sisi ambao tupo form six mwaka huu kwa sababu hata wakuu wetu wa shule wapo pia kwenye sintofahamu kama inaanza na sisi au hawa walio nyuma yetu.
HAKUNA UTATA!. Mtihani ni mwezi wa tano. Mtihani utafanyika mwezi wa pili pale tu wadau wakishinikiza na kuwa na sababu nzito kama:1. Elimu ya form 5 na 6 ni miaka miwili, je hii miezi mi3 ya nini?2. Nani atalipia miezi hii mi3 wanafunzi kukaa shule? Serikali?, Wazazi? Wamiliki wa shule?3. Shule nyiingi makini, silabus inakaribia kwisha, MIEZI 3-5 wanafunzi watafundishwa nini?4. Kwa nini Maamuzi haya yamefanyika ghafla namna hii? BARAZA la mitihani tayari limetoa ratiba. Je, taasisi za serikali hazina mawasiliano?
 

utata bado upo wanafunzi wameshalipia pesa kwa akili ya mitihani mwezi wa pili na si mwezi may. Na huo mwongozo unatakiwa uwaguse form five watakaoanza mwakani na si hawa waliopo shuleni kama kweli tunaamua kufuata utawala wa sheria na si kulazimisha mambo.
 
Waraka huu, unaanza kutumika tarehe 01 Januari, 2013 na kufuta Waraka wa
Elimu Na. 5 wa Mwaka 2004.


Waraka unaanza kutumika tarehe 1/1/2013, form six waliopo sasa hawahusiki, (lakini ni kama tu bado tuna watu ndani ya wizara na taasisi zake walio makini)
 
Kweli wizara ya elimu itoe taarifa rasmi kwa suala la mitihani ya kidato cha sita.Inamaana wazazi watatakiwa kulipia muhula mwingine na tayari walimu wengi wa shule zenye A level wamesha maliza sylabuss sasa wanafunzi wakae shuleni wafanye nini?Wananchi na serikali yao isiingie kwenye mgogoro usio wa lazima.Ushauri wangu kwa Form six wa sasa wafanye mtihani February wan wanaofuata wafanye Mwezi may.
 
Mabadiliko lazima yagharamiwe, kwa kuwa Walimu wanahitaji muda mwingi wa kusahihisha na kutoa matokeo kwa usahihi, kuweni tayari kugharamia. Wakuu wa Shule walikuwa wakiumiza vichwa pindi waalimu wanapokwenda kusahihisha.
Tatizo ni kwamba Watanzania wengi tunataka vya dezo. Wizara ipo sahihi kabisa! Kuna wakati 'udikteta' unahitajika ili kuleta mabadiliko.
 
kwaio muda wa kujiunga chuo nao utasogezwa ama? maana purukushani za bodi ya mikopo zile duuh..vitu vingine vinawezekanaga tanzania tu..atakuja waziri mwingine anaweza sema mtihani ni desemba..tanzania bana
 
Mitihani ikifanyika mwezi wa tano, usahihishaji mwezi wa sita, matokeo mwezi wa saba, application mwezi wa nane, na kujiunga vyuo vikuu itakuwa septemba mwishoni na oktoba mwanzoni.
sasa hapo basi vyeti vya form 6 vitauzwa sana maana mpaka waje kustukia mtu kesha dahiliwa chuoni
 
sasa vurugu za nn,mbona sisi ndo tulikuwa tunafanyaga mei,tena washukuru wamepewa muda mzuri zaidi wa kukomaa na kufukia mashimo,waache vxuzes wakamue huwezi jua may b baraza la mitihani wana logic ya kufanya hvyo,wausome vzuri waraka na c kukurupuka tu
 
Mtiani unaanza tare 12 mwez wa 2! Sasa awa wengne wanataka ku2changanya... Am 4m6,, ujinga uu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…