Mitsubishi Outlander ni gari bora na ngumu sana ila hazina wapiga kelele kuzifanya zishike chati midomoni mwa Watanzania

Tatizo letu Watanzania tunajifanya tunajua kila kitu, hakuna gari iko comfortable kama hiyo! Achana na toyota zinazovibrate dashboard! Unaweza kuta mtu hapa anachangia kwamba sio gari nzuri wakati hakuwahi kumiliki hata boxer pikipiki!!
Nikazie hapo kwenye kuvibrate dashboard, kuna siku nilichukua cariana Ti ya jamaa aisee ile kuwasha vibration niliyokutana nayo ni kubwa nikawa najiuliza mbona Mitsubishi Outlander haivaibrate?

Ni kweli watu wamekariri na hawana ufahamu zaidi
 
Hata mimi nishaagiza mara mbili moja kwa moja. Document ndo walituma kwenye office za Dar. Na walinipa discount kutoka kwenye bei ile unayoona mtandaoni
Sure thing unapata discount nzuri tu, na ni kweli docs wanazituma Mighty Investment Company dar na agent wako anazichukulia hapo kuprocess gari bandarini. Isitoshe jamaa wana customer care ya kuridhisha tangu mwanzo hadi unachukua gari yako
 
So kwa matumizi ya rough road mara kwa mara inahimiri kumbe?

Hii SUV inavutia sana kimuonekano, ipo kibabe sana!

-Kaveli-
Ground clearance yake ni kubwa isitoshe hata kwenye rough road unatembea vizuri tu, kwenye mafuta ukitaka uifaidi vizuri na isikupasue wallet yako sana pendelea kujaza full tank naweza sema ulaji wake mafuta utaupenda zaidi kwenye high way.

Mimi ninayo na naitumia kwenye harakati zangu iwe ni kwenye rough road au town, mwisho kabisa mnyama anajitahidi kufunguka sio poa.
 
Mkuu kuna hii Outlander PHEV, vipi hii tofauti yake na Common Outlander?? Details please.
Je ninnzuri kibongobongo??

Nimelitamani dude hilo, Mungu akijalia kabla mwaka haujaisha nichukue.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Price yake hii imekaa ya 2020 na 2022 0km
Kama wabongo tungekuwa tunatoa taarifa sahihi ingekuwa jambo zuri sana.
Mtu unakuta anaongea kaneno kamoja tu mara janja janja,,, tujitahidi vijana tubadili mitazamo yetu. Tuwe kama vijana wa nnchi zilizo endelea.

Mind set ya kulalamika na kuleta mizaha, kuongea kitu usichokua na uhakika ili kukatisha watu tamaa zinaboa na kurudisha maendeleo sana.


Katika uzi huu niliouleta nashukuru wengi wameongea mengi mazuri, ila watu wawili au watatu, ndio wamekuja kuleta.na vijicomment vya maneno matatu ya kukatisha tamaa. Inasikitasha sana. Kama unaishu unayoijua juu ya uzi hii kiwa gari hizo sio basi tunaomba uelezee kwa kina, naamini vijana mkiwa hivi mtabadili sana mambo mengi ndani ya nnchi yetu na kuaminika.



Kuhusu PHEV Mistubish Outlander

Hii ni gari ya siku zijazo, hasa kwa technolojia inayokuja, hivyo ni gari zuri sana. Dunia inaelekea kwenye nishati mbadala. Hivyo ukiweza kuchukua hiyo ni njema mno.
 
Sijajua umenielewa au umelielewa vipi swali langu, ila nilitaka nijue bei ya hizo hybrid zake, tofauti na be forward ambako sina uzoefu uo wa kuchagua magari, moja ya 2020 na nyingine ya 2022 ambayo ni 0Km.
 
Sijajua umenielewa au umelielewa vipi swali langu, ila nilitaka nijue bei ya hizo hybrid zake, tofauti na be forward ambako sina uzoefu uo wa kuchagua magari, moja ya 2020 na nyingine ya 2022 ambayo ni 0Km.
Nimekuelewa mkuu sema nilikuwa ninajibu mtu mwingine juu kumbe nime quote kwenye comment yako. Pole sana. Kwa sasa sijafutilia bei ya Okm hiyo ya 2020 au 2022.nitaifutilia kwenye soko lake. Nakukujuza tena
 
Nimekuelewa mkuu sema nilikuwa ninajibu mtu mwingine juu kumbe nime quote kwenye comment yako. Pole sana. Kwa sasa sijafutilia bei ya Okm hiyo ya 2020 au 2022.nitaifutilia kwenye soko lake. Nakukujuza tena
Fresh
 
Kapicha mkuu....
 
Mkuu kuna hii Outlander PHEV, vipi hii tofauti yake na Common Outlander?? Details please.
Je ninnzuri kibongobongo??

Nimelitamani dude hilo, Mungu akijalia kabla mwaka haujaisha nichukue.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Mkuu nilichelewa kuona notification, kimsingi tofauti kuu nayoiona ni muonekano wa body na show ya mbele engine ni ile ile. Lakini pia PHEV kwa ndani iko tofauti na Outlander ya kawaida, kwa maoni yangu PHEV imekaa kibabe zaidi.

Jichange uvute mzigo na ukitaka kuagiza cheki na jamaa wa Autocom Japan hawa jamaa wako njema sana in terms of price, yangu niliagiza kupitia wao. Kila la kheri mkuu
 
We jamaa acha uchawi.
Mimi nina Mitsubish na gereji hawanijui.
Zaidi ni service za kumwaga oil na service za tairi.
Ni gari ngumu mno.
Na Mimi ndio namshangaa , mitsubish pajero ni gari ambayo nimekuwa nayo Kwa miaka 10+ sasa na sijawahi kupata matatizo makubwa ya kwenda gereji tofauti na services za kawaida ambazo kila Aina ya gari inapata
 
Walekalili Toyota , Tanzania kuna " Toyota syndrome " na kufanya vitu Kwa kuigana , wakati Hiyo Outlander bonge la gari utakuta jitu mpaka litembee na kibaby walker linaridhika ,akili za kikapuku
Hahaaaaaa.
Unajuwa jana nimeona jamaa mmoja anatangaza kwa mbwembwe kweli juu ya kifaa cha kubadili umeme wa gari kwenda ac yaani inverter.
Wakati kwenye outlander hii ni kitu ipo tena og kutoka Japan.

Sijui Changamoto kwetu iko wapi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…