Nimependa huu uzi, lakini nina mtazamo na Imani tofauti nawewe
Ulipaswa kusema Imani katika miungu yetu ikishindwa, kwasababu hakuna miungu yeyote ya Kizungu wala kiafrika iliyowahi kuwepo kiuhalisia wala kufanya kazi...isipokuwa tu watu ndio walikuwa na Imani hizo ambazo hazipo
Waafrika tulizidiwa Kiakili, Kimbinu na Kiteknolojia
Kama kungekuwa na miungu ifanyayo kazi japo kidogo tu basi isingewezekana Mwafrika kuteswa kwa ku overwork, kutobolewa miguu na kuvalishwa minyororo, Kunyongwa na kuhasiwa
Aidha, isingewezekana Wanaume shababy wa kiafrika wanne au sita kumbeba mkoloni mmoja kutoka Arusha au Mzizima mpaka Tanga na Same kwenye mashamba ya mikonge kisa ana gobole moja tu kibindoni
MASWALI TAFAKURI:
- Kwanini Waafrika hatukujitahidi kwa kutumia akili na maarifa kugundua silaha kama gobole au risasi kuuwa wakoloni watesao ilihali tulikuwa na wafua chuma wengi wa kutosha huko Ugweno, Engaruka, Meroe, Axum na kwingineko? Jibu ni kuwa tulikuwa Wajinga
- Kwanini hatukuwa na UMOJA ilihali ndio Nguvu? Wao walikuwa wachache sana kuliko sisi tena walituma tu wawakilishi wao wakiwa Ulaya, kwanini walitushinda? Jibu ni kuwa tulikuwa wajinga
Huwa nasema kuwa Watu weusi ni jamii Dhaifu kiakili na kimaarifa kuliko jamii zozote katika dunia hii
So, napinga kuwa tulizidiwa kiimani ya kimiungu, Ukweli ni kuwa tulizidiwa kimbinu, kimaarifa na kiteknolojia kama ilivyo hata leo hii.