Miungu yetu ilishindwa, Mizimu yetu ikapigwa, Sasa tumekuwa Jamii iliyoanguka na hatuna Tumaini la kusimama

Miungu yetu ilishindwa, Mizimu yetu ikapigwa, Sasa tumekuwa Jamii iliyoanguka na hatuna Tumaini la kusimama

Shetani hawezi mshinda Mungu,
Kabla ya ujio wa dini waafrika waliabudu wasichokijua thus waliokufa kabla ya dini watahukumiwa Kwa Sheria ya maadili yaani do and don't do, au sheria za asili Sheria ya mema na mabaya.
 
Nimependa huu uzi, lakini nina mtazamo na Imani tofauti nawewe

Ulipaswa kusema Imani katika miungu yetu ikishindwa, kwasababu hakuna miungu yeyote ya Kizungu wala kiafrika iliyowahi kuwepo kiuhalisia wala kufanya kazi...isipokuwa tu watu ndio walikuwa na Imani hizo ambazo hazipo

Waafrika tulizidiwa Kiakili, Kimbinu na Kiteknolojia

Kama kungekuwa na miungu ifanyayo kazi japo kidogo tu basi isingewezekana Mwafrika kuteswa kwa ku overwork, kutobolewa miguu na kuvalishwa minyororo, Kunyongwa na kuhasiwa

Aidha, isingewezekana Wanaume shababy wa kiafrika wanne au sita kumbeba mkoloni mmoja kutoka Arusha au Mzizima mpaka Tanga na Same kwenye mashamba ya mikonge kisa ana gobole moja tu kibindoni

MASWALI TAFAKURI:

- Kwanini Waafrika hatukujitahidi kwa kutumia akili na maarifa kugundua silaha kama gobole au risasi kuuwa wakoloni watesao ilihali tulikuwa na wafua chuma wengi wa kutosha huko Ugweno, Engaruka, Meroe, Axum na kwingineko? Jibu ni kuwa tulikuwa Wajinga

- Kwanini hatukuwa na UMOJA ilihali ndio Nguvu? Wao walikuwa wachache sana kuliko sisi tena walituma tu wawakilishi wao wakiwa Ulaya, kwanini walitushinda? Jibu ni kuwa tulikuwa wajinga

Huwa nasema kuwa Watu weusi ni jamii Dhaifu kiakili na kimaarifa kuliko jamii zozote katika dunia hii

So, napinga kuwa tulizidiwa kiimani ya kimiungu, Ukweli ni kuwa tulizidiwa kimbinu, kimaarifa na kiteknolojia kama ilivyo hata leo hii.
Iko hivi;
Kuna uhalisia, kuna zana na kuna maana walizonazo watu kuhusu uhalisia na zana.

Uhalisia ni jumla ya mambo yote yaliyo nje ya utawala wa mtu.

Zana ni jumla ya vifaa anavyotengeneza mtu ili kumsaidia kuenenda katika mazingira na kukabiliana na changamoto na vikwazo vya kimazingira.

Maana ni ule ukweli au upotofu alionao mtu kuhusu uhalisia au zana.

Sasa katika hayo matatu, mazingira ndio kigezo msingi. Kulingana na mazingira tofauti kati ya wazungu na waafrika, kimsingi tulikuwa na uhalisia tofauti, zana tofauti na maana tofauti. Wazungu walikuwa katika mazingira magumu ambayo yaliwafanya wawe na zana tofauti na zenye nguvu sana katika mazingira ya kivita na pia walikuwa na mtazamo(maana) uliotegemea sana zana dhidi ya uhalisia.

Kwa mantiki hiyo, unaweza kutabiri kitakachotokea pale wazungu na waafrika watakapokutana. Mzungu atakuwa na silaha na atazitegemea sana dhidi ya mwafrika.

Makundi haya mawili pia hayakuwa na maana sawa kuhusu vita, kuhusu ukarimu kwa wageni, kuhusu heshima na UTU. Hivyo mzungu aliweza kumwin mwafrika kwa sababu mzungu alikuwa amejengeka kwa Hila na uovu dhidi ya kundi lisilo lake. Alikuwa amejengeka katika vita vya kikatili na wizi na uuaji.

Sasa mazingira ya mwafrika ni tofauti na kwa hakika mwafrika anatakiwa kuwaza kwa namna tofauti ili aweze kujinasua dhidi ya ukoloni na uonevu wa mzungu. Kwasasa kundi kubwa bado limelala lakini kadiri mzungu anavyoendelea kutunyoosha Nina imani akili zitaamka na tutaacha mazoea ya kizamani.

Siku waafrika wakitambua kusudi na hatma yao katika dunia hii na wakamtambua mzungu kama adui ndipo safari sahihi na ya uhakika ya ukombozi wa mwafrika na amani na usawa kwa viumbe wote itaanza.
 
Shukran sana mkuu kwa maelezo mazuri.

Swali linakuja, je MUUMBA Hawezi kuimba miungu ya kufanya kazi fulani fulani?
Kwa sababu Muumba sio Mhitaji lakini Mungu ukifuatilia anasifa ya uhitaji kama vile miungu mingi.
Ndio maana nikasema Kuna utata katika kiuelewa haya mambo. Uelewa kuhusu Mungu una utata mwingi maana Kila kundi linafafanua Mungu kwa uelewa wao. Binafsi sipendi kulejelea uumbaji kwa kutumia Mungu.

MUUMBA aliweka taratibu au Sheria zitakazosimamia Uumbaji na viumbe wote bila ubaguzi au upendeleo. Ni jitihada za viumbe kujua Sheria hizo na kujiweka katika misingi ya kuzishika ili waweze kuwa na maisha mazuri huku wakitimiza kusudi na hatima yao katika uwepo.
 
Asili ya Akili au wazo ni utata mkubwa.
Huwezi kuwa na akili bila nguvu isiyoonekana (miungu) mawazo huwezi kuyadhibiti au kuyazalisha.
Ni kama chembe ya uhai.

Miungu au Mungu ndio hukupa wazo(akili) na kuiweka katika ubongo wako. Kinachobaki ni juu yako.

Miungu na Mungu ndio hutoa mambo yasiyo onekana katika mwili. Kama uhai na Akili.
Kama miungu yeti ilipigwa ko,basi kazi ipo
 
Mizimu ilishindwa kutulinda dhidi ya wakoloni na pia dhidi ya biashara ya watumwa.
Hata sisi tulishindwa kuilinda mizimu maana swala la ulinzi ni la pande zote.

Unavyoona waislam wanafanya jihad na wanasambaza dini kwa njia zote wanazoweza, wanalinda jina la Allah na nguvu zake. The same kwa Wakristo.

Unatakiwa kuwalinda mizimu yako na kuorithisha kwa kizazi kijacho ili iweze kuendelea kuwepo na nguvu zao zidhihirike katika uwepo.

Badala yake tumegeukia kwenye mizimu ya kigeni na tunailinda kwa jasho na damu. Sasahivi wale wanalinda mizimu ya kiafrika tunawaona kama washamba na wajonga lakini tunawaogopa maana ni dhahiri kwamba wananguvu kubwa wakiamua.
 
Ndio maana nikasema Kuna utata katika kiuelewa haya mambo. Uelewa kuhusu Mungu una utata mwingi maana Kila kundi linafafanua Mungu kwa uelewa wao. Binafsi sipendi kulejelea uumbaji kwa kutumia Mungu.

MUUMBA aliweka taratibu au Sheria zitakazosimamia Uumbaji na viumbe wote bila ubaguzi au upendeleo. Ni jitihada za viumbe kujua Sheria hizo na kujiweka katika misingi ya kuzishika ili waweze kuwa na maisha mazuri huku wakitimiza kusudi na hatima yao katika uwepo.

JE huyo muumbaji anahitaji kuabudiwa?
 
Nimependa huu uzi, lakini nina mtazamo na Imani tofauti nawewe

Ulipaswa kusema Imani katika miungu yetu ikishindwa, kwasababu hakuna miungu yeyote ya Kizungu wala kiafrika iliyowahi kuwepo kiuhalisia wala kufanya kazi...isipokuwa tu watu ndio walikuwa na Imani hizo ambazo hazipo

Waafrika tulizidiwa Kiakili, Kimbinu na Kiteknolojia

Kama kungekuwa na miungu ifanyayo kazi japo kidogo tu basi isingewezekana Mwafrika kuteswa kwa ku overwork, kutobolewa miguu na kuvalishwa minyororo, Kunyongwa na kuhasiwa

Aidha, isingewezekana Wanaume shababy wa kiafrika wanne au sita kumbeba mkoloni mmoja kutoka Arusha au Mzizima mpaka Tanga na Same kwenye mashamba ya mikonge kisa ana gobole moja tu kibindoni

MASWALI TAFAKURI:

- Kwanini Waafrika hatukujitahidi kwa kutumia akili na maarifa kugundua silaha kama gobole au risasi kuuwa wakoloni watesao ilihali tulikuwa na wafua chuma wengi wa kutosha huko Ugweno, Engaruka, Meroe, Axum na kwingineko? Jibu ni kuwa tulikuwa Wajinga

- Kwanini hatukuwa na UMOJA ilihali ndio Nguvu? Wao walikuwa wachache sana kuliko sisi tena walituma tu wawakilishi wao wakiwa Ulaya, kwanini walitushinda? Jibu ni kuwa tulikuwa wajinga

Huwa nasema kuwa Watu weusi ni jamii Dhaifu kiakili na kimaarifa kuliko jamii zozote katika dunia hii

So, napinga kuwa tulizidiwa kiimani ya kimiungu, Ukweli ni kuwa tulizidiwa kimbinu, kimaarifa na kiteknolojia kama ilivyo hata leo hii.

Umeeleza kwa ufasaha zaidi.
So ishu hapa ni kuwa hakuna cha Allah wala Yehova. Isipokuwa jamii husika ndio waliunda na kubuni miungu yao ambayo kimsingi haipo.

Ila Muumbaji wa yote yupo
 
Hata sisi tulishindwa kuilinda mizimu maana swala la ulinzi ni la pande zote.

Unavyoona waislam wanafanya jihad na wanasambaza dini kwa njia zote wanazoweza, wanalinda jina la Allah na nguvu zake. The same kwa Wakristo.

Unatakiwa kuwalinda mizimu yako na kuorithisha kwa kizazi kijacho ili iweze kuendelea kuwepo na nguvu zao zidhihirike katika uwepo.

Badala yake tumegeukia kwenye mizimu ya kigeni na tunailinda kwa jasho na damu. Sasahivi wale wanalinda mizimu ya kiafrika tunawaona kama washamba na wajonga lakini tunawaogopa maana ni dhahiri kwamba wananguvu kubwa wakiamua.
Huwezi linda kitu dhaifu,wao ndio wanakazi ya kutulinda na sio sisi
 
JE huyo muumbaji anahitaji kuabudiwa?
Hapana, Ibada ni kwa Mizimu au Wahenga au Mababu.

Hierakia iko hivi;
MUUMBA ambaye kihalisia ni Giza la Kimiminika (Fluid Darkness)

Sheria za MUUMBA (Divine Laws)

Viumbe katika familia zote. Hapa ndipo wanakaa na Wahenga.

Maat au Sheria za watu kuhusu mazingira. Hapa ndipo mahusiano ma mazingira yanakiwepo.

Ubuntu au UTU ambazo ni Sheria za watu kuhusu mahusiano baina yao.


Tunaabudu mizimu au Mababu kwa kusudi la kuomba msaada wao katika kuishi vema katika uhalisia huu maana wao wamewahi kuishi hapa na ndio wanajua vema ramani ya kuishi kwetu tangu kale. Tunaomba ili kwa msaada wao tusipotee njia. Kimsingi Ibada ni tafakari kwa lengo la kurejesha kumbukumbu.

Yote tunayohitaji kujua kama watu walipewa watu wa kwanza kuumbwa na ndio. Hivi ndivyo ilivyo kuwa pia kwa viumbe wengine wote.
 
Kwa Kipimo kingine, mizimu ndiyo miungu pia. Kuna jamii ambazo ziliamua kuabudu wale watu ambao walionesha uwezo mkubwa sana na hivyo hata wale watu walipokufa sifa zao ziliendelea kutangazwa kwa utukufu mkubwa.

Yesu ni mfano wa watu waliotukuzwa na kuitwa Mungu.
Krishina na wengine wengi katika historia.

MUUMBA ni kesi tofauti maana ndio mwanzo wa yote lakini Mungu ni zao la jamii. I'm
 
Hata sisi tulishindwa kuilinda mizimu maana swala la ulinzi ni la pande zote.

Unavyoona waislam wanafanya jihad na wanasambaza dini kwa njia zote wanazoweza, wanalinda jina la Allah na nguvu zake. The same kwa Wakristo.

Unatakiwa kuwalinda mizimu yako na kuorithisha kwa kizazi kijacho ili iweze kuendelea kuwepo na nguvu zao zidhihirike katika uwepo.

Badala yake tumegeukia kwenye mizimu ya kigeni na tunailinda kwa jasho na damu. Sasahivi wale wanalinda mizimu ya kiafrika tunawaona kama washamba na wajonga lakini tunawaogopa maana ni dhahiri kwamba wananguvu kubwa wakiamua.
Hili nalo neno.
 
MIUNGU YETU ILISHINDWA, MIZIMU YETU IKAPIGWA, SASA TUMEKUWA JAMII ILIYOANGUKA NA HATUNA TUMAINI TENA LA KUSIMAMA.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Mila zetu, Desturi zetu, tamaduni zetu, utambulisho wetu na kila kilichokuwa chetu kiliitwa Potofu baada ya kushindwa.
Upotofu upo kwa walioshindwa. Kama tungeshinda katika vita Ile wala istilahi "POTOFU” Isingesikika.
Ni potofu kwa sababu tulishindwa.

Miungu ya Mababu zetu ilishindwa vibaya katika vita ya miungu "god's War" sijajua nini kilipelekea kushindwa kwao. Bado najiuliza.
Je Haikuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na Miungu ya kigeni?
Je Haikuwa na akili na mbinu kabambe za kuwashinda maadui?
Nini kilitokea mpaka Anguko kuu la kutisha lilipotokea ambalo limedumu mpaka leo na hatujui litaendelea mpaka Lini.

Miungu ikishapigwa waumini hawana ujanja tena.
Wakati Ukristo na uislamu unaingia Afrika Wazee na Babu zetu walipambana vilivyo kuukataa kwa nguvu zote lakini ninawasiwasi Miungu yao haikuwapa sapoti ya kutosha kukabiliana na ugeni Ule mbaya.
Au miungu ile ilitoa sapoti lakini haikuwa na nguvu kushinda Maadui waliokuja.

Hatuwezi kusema Waafrika walisaliti miungu yao. Ila ninachokiona ni kuwa miungu ya kiafrika ilizidiwa na haikuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na miungu ya kigeni.

Nakumbuka mpaka nazaliwa zilikuwepo jitihada mbalimbali za wazee wetu wakijitahidi kufurukuta kujaribu kupambana na ujio wa wageni na miungu yao lakini walikuwa wanapambana wakiwa wameshashindwa kwani miungu yao ilikuwa aidha imekimbia au imetekwa au pengine hata kuuawa na miungu ya kigeni.

Miungu ndio imebeba mila, desturi, tamaduni na utambulisho wa jamii husika. Sasa kitendo cha miungu hiyo kupigwa Katiak vita na kufukuzwa au kuangamizwa kabisa kunaiathiri na kuua kabisa desturi , mila na tamaduni ya jamii zao.

Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo haina nguvu na haina vigezo na uhalali wa kuitwa miungu.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa kutetea Watu wake.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa kulinda rasilimali za himaya zao mpaka zinaibiwa na wageni.

Ni mila potofu kwa sababu, miungu hiyo imeshindwa kuwapa Watu wake Akili na kutatua kero na changamoto za jamii yao ikiwemo Umaskini na ujinga.

Miungu na mizimu yako inaposhindwa hauna chochote utakachofanya zaidi ya kujisalimisha kwa miungu ya kigeni.
Ni pigo takatifu ambalo kunyanyuka haiwezekaniki.

Vita ya Miungu, waafrika walipoteza na hatujui miungu yetu ilikimbia, au ipo mateka au iliuawa.
Nyota ya matumaini ya Ukombozi haipo kwa sababu huwezi kukomboa jamii au taifa pasipo Miungu ya kwenu.

Acha Nipumzike sasa.
Nawatakia maandalizi mema ya Sabato.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Yaan ni kuwa siyo Africa tu unawajuwa wahindi wekundu walichofanywa yaani ni kuteketeza kabisa,latin america yote ikachukuliwa, kuna nchi currently zinajikuta haziingiliki lakin utaona ,na kama utakumbuka wakati wa kombe la dunia pale brazil walifanya ibada za kishetan pale lakin kilichowapata ilikuwa ni kuonyesha yakuwa their are gods are so weak
 
Huyo mnaesema Mungu wa Israel mbona aliwaachaga watu wake miaka mingi utumwani misri na huko babylon na baadae wakaibuka tena,,,,hio pia ni kwa Afrika,,,,hawajashindwa ni muda tu
Mungu huyo wa Israel ni mdhaifu sana.

Alishindwa kuwaokoa waisraeli kwenye concentration camps za Adolph Hitler wakauwawa maelfu kwa maelfu.

Halafu kuna waafrika wajinga kazi kukesha makanisani wakipayuka kama mbayuwayu kumuomba huyo Mungu wa Israel..
 
Mungu huyo wa Israel ni mdhaifu sana.

Alishindwa kuwaokoa waisraeli kwenye concentration camps za Adolph Hitler wakauwawa maelfu kwa maelfu.

Halafu kuna waafrika wajinga kazi kukesha makanisani wakipayuka kama mbayuwayu kumuomba huyo Mungu wa Israel..
We mwenye akili umevumbua nini mpaka sahivi
 
Back
Top Bottom