Miungu yetu ilishindwa, Mizimu yetu ikapigwa, Sasa tumekuwa Jamii iliyoanguka na hatuna Tumaini la kusimama

Shetani hawezi mshinda Mungu,
Kabla ya ujio wa dini waafrika waliabudu wasichokijua thus waliokufa kabla ya dini watahukumiwa Kwa Sheria ya maadili yaani do and don't do, au sheria za asili Sheria ya mema na mabaya.
 
Iko hivi;
Kuna uhalisia, kuna zana na kuna maana walizonazo watu kuhusu uhalisia na zana.

Uhalisia ni jumla ya mambo yote yaliyo nje ya utawala wa mtu.

Zana ni jumla ya vifaa anavyotengeneza mtu ili kumsaidia kuenenda katika mazingira na kukabiliana na changamoto na vikwazo vya kimazingira.

Maana ni ule ukweli au upotofu alionao mtu kuhusu uhalisia au zana.

Sasa katika hayo matatu, mazingira ndio kigezo msingi. Kulingana na mazingira tofauti kati ya wazungu na waafrika, kimsingi tulikuwa na uhalisia tofauti, zana tofauti na maana tofauti. Wazungu walikuwa katika mazingira magumu ambayo yaliwafanya wawe na zana tofauti na zenye nguvu sana katika mazingira ya kivita na pia walikuwa na mtazamo(maana) uliotegemea sana zana dhidi ya uhalisia.

Kwa mantiki hiyo, unaweza kutabiri kitakachotokea pale wazungu na waafrika watakapokutana. Mzungu atakuwa na silaha na atazitegemea sana dhidi ya mwafrika.

Makundi haya mawili pia hayakuwa na maana sawa kuhusu vita, kuhusu ukarimu kwa wageni, kuhusu heshima na UTU. Hivyo mzungu aliweza kumwin mwafrika kwa sababu mzungu alikuwa amejengeka kwa Hila na uovu dhidi ya kundi lisilo lake. Alikuwa amejengeka katika vita vya kikatili na wizi na uuaji.

Sasa mazingira ya mwafrika ni tofauti na kwa hakika mwafrika anatakiwa kuwaza kwa namna tofauti ili aweze kujinasua dhidi ya ukoloni na uonevu wa mzungu. Kwasasa kundi kubwa bado limelala lakini kadiri mzungu anavyoendelea kutunyoosha Nina imani akili zitaamka na tutaacha mazoea ya kizamani.

Siku waafrika wakitambua kusudi na hatma yao katika dunia hii na wakamtambua mzungu kama adui ndipo safari sahihi na ya uhakika ya ukombozi wa mwafrika na amani na usawa kwa viumbe wote itaanza.
 
Shukran sana mkuu kwa maelezo mazuri.

Swali linakuja, je MUUMBA Hawezi kuimba miungu ya kufanya kazi fulani fulani?
Kwa sababu Muumba sio Mhitaji lakini Mungu ukifuatilia anasifa ya uhitaji kama vile miungu mingi.
Ndio maana nikasema Kuna utata katika kiuelewa haya mambo. Uelewa kuhusu Mungu una utata mwingi maana Kila kundi linafafanua Mungu kwa uelewa wao. Binafsi sipendi kulejelea uumbaji kwa kutumia Mungu.

MUUMBA aliweka taratibu au Sheria zitakazosimamia Uumbaji na viumbe wote bila ubaguzi au upendeleo. Ni jitihada za viumbe kujua Sheria hizo na kujiweka katika misingi ya kuzishika ili waweze kuwa na maisha mazuri huku wakitimiza kusudi na hatima yao katika uwepo.
 
Kama miungu yeti ilipigwa ko,basi kazi ipo
 
Mizimu ilishindwa kutulinda dhidi ya wakoloni na pia dhidi ya biashara ya watumwa.
Hata sisi tulishindwa kuilinda mizimu maana swala la ulinzi ni la pande zote.

Unavyoona waislam wanafanya jihad na wanasambaza dini kwa njia zote wanazoweza, wanalinda jina la Allah na nguvu zake. The same kwa Wakristo.

Unatakiwa kuwalinda mizimu yako na kuorithisha kwa kizazi kijacho ili iweze kuendelea kuwepo na nguvu zao zidhihirike katika uwepo.

Badala yake tumegeukia kwenye mizimu ya kigeni na tunailinda kwa jasho na damu. Sasahivi wale wanalinda mizimu ya kiafrika tunawaona kama washamba na wajonga lakini tunawaogopa maana ni dhahiri kwamba wananguvu kubwa wakiamua.
 

JE huyo muumbaji anahitaji kuabudiwa?
 

Umeeleza kwa ufasaha zaidi.
So ishu hapa ni kuwa hakuna cha Allah wala Yehova. Isipokuwa jamii husika ndio waliunda na kubuni miungu yao ambayo kimsingi haipo.

Ila Muumbaji wa yote yupo
 
Huwezi linda kitu dhaifu,wao ndio wanakazi ya kutulinda na sio sisi
 
JE huyo muumbaji anahitaji kuabudiwa?
Hapana, Ibada ni kwa Mizimu au Wahenga au Mababu.

Hierakia iko hivi;
MUUMBA ambaye kihalisia ni Giza la Kimiminika (Fluid Darkness)

Sheria za MUUMBA (Divine Laws)

Viumbe katika familia zote. Hapa ndipo wanakaa na Wahenga.

Maat au Sheria za watu kuhusu mazingira. Hapa ndipo mahusiano ma mazingira yanakiwepo.

Ubuntu au UTU ambazo ni Sheria za watu kuhusu mahusiano baina yao.


Tunaabudu mizimu au Mababu kwa kusudi la kuomba msaada wao katika kuishi vema katika uhalisia huu maana wao wamewahi kuishi hapa na ndio wanajua vema ramani ya kuishi kwetu tangu kale. Tunaomba ili kwa msaada wao tusipotee njia. Kimsingi Ibada ni tafakari kwa lengo la kurejesha kumbukumbu.

Yote tunayohitaji kujua kama watu walipewa watu wa kwanza kuumbwa na ndio. Hivi ndivyo ilivyo kuwa pia kwa viumbe wengine wote.
 
Kwa Kipimo kingine, mizimu ndiyo miungu pia. Kuna jamii ambazo ziliamua kuabudu wale watu ambao walionesha uwezo mkubwa sana na hivyo hata wale watu walipokufa sifa zao ziliendelea kutangazwa kwa utukufu mkubwa.

Yesu ni mfano wa watu waliotukuzwa na kuitwa Mungu.
Krishina na wengine wengi katika historia.

MUUMBA ni kesi tofauti maana ndio mwanzo wa yote lakini Mungu ni zao la jamii. I'm
 
Hili nalo neno.
 
Yaan ni kuwa siyo Africa tu unawajuwa wahindi wekundu walichofanywa yaani ni kuteketeza kabisa,latin america yote ikachukuliwa, kuna nchi currently zinajikuta haziingiliki lakin utaona ,na kama utakumbuka wakati wa kombe la dunia pale brazil walifanya ibada za kishetan pale lakin kilichowapata ilikuwa ni kuonyesha yakuwa their are gods are so weak
 
Huyo mnaesema Mungu wa Israel mbona aliwaachaga watu wake miaka mingi utumwani misri na huko babylon na baadae wakaibuka tena,,,,hio pia ni kwa Afrika,,,,hawajashindwa ni muda tu
Mungu huyo wa Israel ni mdhaifu sana.

Alishindwa kuwaokoa waisraeli kwenye concentration camps za Adolph Hitler wakauwawa maelfu kwa maelfu.

Halafu kuna waafrika wajinga kazi kukesha makanisani wakipayuka kama mbayuwayu kumuomba huyo Mungu wa Israel..
 
We mwenye akili umevumbua nini mpaka sahivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…