Mizaha tunayofanya kwenye mambo ya maana inaonesha jinsi watanzania tusivyojiheshimu!!

Mizaha tunayofanya kwenye mambo ya maana inaonesha jinsi watanzania tusivyojiheshimu!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Wakati mwingine mtu unatamani kusema sisi watanzania ni majuha lakini unaheshimu uumbaji wa Mungu wetu.

Jinsi mambo ya hovyo yanayofanywa na baadhi ya watu tuliowapa madaraka yanavyotia kinyaa, mtu unatamani kusonya lakini ukweli ulio mbele yetu unakutia aibu.

Wakati mwingine unaposikia mtu anasema "Kuna watu ni mazuzu" unaanza kudhani anatusema sisi, hasira zinakupanda lakini unatulia unapokumbuka uhovyo hovyo tulio nao.

Ni lini watanzania tutajua kwamba Hawa wanaofuja, kutapanya na kuiba mali za Umma/serikali huwa wanatuibia sisi!??

Kifanyike nini kwetu hadi tuone kwamba tunatakiwa kuasi dhidi ya mafisadi na wezi wanaotuibia kupitia nafasi za kimadaraka walizo nazo!?

Ni lini tutajitofautisha kiakili na utashi kati ya sisi tulioumbwa binadamu na Ng'ombe!?

Kuvumilia kwetu mambo ya hovyo hakuoneshi kuwa sisi hatukustahili kujitawala!!??
 
Watu wako Serious kwenye Simba na Yanga mpaka wengine wanajiua.
 
Ni lini watanzania tutajua kwamba Hawa wanaofuja, kutapanya na kuiba mali ya Umma/serikali huwa wanatuibia sisi!??
Haitatokea hiyo siku ifike, kwasabb wajinga ni wengi na ndiyo tumewapa mpk madaraka.

1. Fikiria tunampa urais form 4 failure urais. Hana vision wala mission, anachowaza ni kukopa na kuuza rasilimali za nchi tu.

2. Tunamchagua jambazi mwenye fedha kuwa mbunge aliyeishia darasa la 2 au la 7, na akiwa bungeni anatukana wasomi na kudharau elimu.

3. Fikiria maiti inateuliwa.

Labda Mungu alete gharikaaue hiki kizazi cha watanzania mazuzu, halafu kije kizazi kipya.
 
Shida iko kwa baadhi ya watu, fikiria ufisadi mkubwa unafanyika. Watu wanajaribu kupaza sauti. Linatokea jitu huko, sijui anafaidika na nini anashusha magazeti kusifia.

Hawa ndiyo wanaoturudisha nyuma, uchawa sijui kunguni. Hata South Africa wameanza kuamka. Wamechoshwa na ufisadi. Hii ni last warning, njoo Tz sasa kuna watu kichwani wanafuga nywele tu.
 
Shida iko kwa baadhi ya watu, fikiria ufisadi mkubwa unafanyika. Watu wanajaribu kupaza sauti. Linatokea jitu huko, sijui anafaidika na nini anashusha magazeti kusifia.

Hawa ndiyo wanaoturudisha nyuma, uchawa sijui kunguni. Hata South Africa wameanza kuamka. Wamechoshwa na ufisadi. Hii ni last warning, njoo Tz sasa kuna watu kichwani wanafuga nywele tu.
Tena wanafuga nywele juu ya mabox waliyobeba kichwani na wale sii kwenye mafuvu ya vichwa vyao☺️
 
Mimi nafikiri kuna mambo ya kishirikina yamefanywa kuwafanya Watanzania wote kuwa mazuzu vizazi na vizazi kwa sababu haiwezekani kwa akili ya kawaida hawa watawala wanatufanyia kila aina ya ujinga na kutuonesha jinsi wanavyotudharau lakini sisi wenyewe tumetulia tu kama mapimbi fulani!
 
Wakati mwingine mtu unatamani kusema sisi watanzania ni majuha lakini unaheshimu uumbaji wa Mungu wetu.

Jinsi mambo ya hovyo yanayofanywa na baadhi ya watu tuliowapa madaraka yanavyotia kinyaa, mtu unatamani kusonya lakini ukweli ulio mbele yetu unakutia aibu.

Wakati mwingine unaposikia mtu anasema "Kuna watu ni mazuzu" unaanza kudhani anatusema sisi, hasira zinakupanda lakini unatulia unapokumbuka uhovyo hovyo tulio nao.

Ni lini watanzania tutajua kwamba Hawa wanaofuja, kutapanya na kuiba mali za Umma/serikali huwa wanatuibia sisi!??

Kifanyike nini kwetu hadi tuone kwamba tunatakiwa kuasi dhidi ya mafisadi na wezi wanaotuibia kupitia nafasi za kimadaraka walizo nazo!?

Ni lini tutajitofautisha kiakili na utashi kati ya sisi tulioumbwa binadamu na Ng'ombe!?

Kuvumilia kwetu mambo ya hovyo hakuoneshi kuwa sisi hatukustahili kujitawala!!??
Hiyo unayoiona ni mizaha inafanywa na watu basi ndio sifa kuu ya Mtanzania.

Kelele zote Huwa ni fitina za kukosa
 
Mambo 2 mwendazake aliletwa na Supreme Power ayafanye ili nchi izaliwe upya..moja kuhamisha makao makuu kutoka Dar kwenda Dodoma..kwa nini, makao makuu ya nchi ni mlango, mlango ukitumika kupitisha mambo mabaya, wizi, ushirikina, ubinafsi, ufujaji, utoaji kafara..nk mambo mazuri..upendo, uaminifu, kujali wengine, ibada/dua nk hayana nafasi, pili aliletwa afute mbio za mwenge, sababu ni tambiko la giza kupumbaza watu..! alifanikiwa kutekeleza la kwanza, wakati anajiandaa lile la pili hakufanikiwa sababu alitamka kuonyesha anataka kuufuta mwenge..hapo ndipo alikosea, alipaswa kutamka moja kwa moja kama alivyosema makao makuu sasa ni dodoma bila kushirikisha mtu yeyote...kwamba mwenge mwisho mwaka huu! Mission uncomplished..hizo nguvu zinazotambikiwa mwenge zikammaliza kabla hajatekeleza alichosema! Ndio hali hii tuko nayo! Nchi ina umri zaidi ya miaka 60 lakin raia wake hawaelewi walikotoka, walipo na wanakotaka kwenda!
 
Kuna mada mtu kaleta analalamika kama rais anaweza mteua mfu na wakatangaza kabisa je huko kwenye kusaini Mikataba ya kimataifa watu wapo makini kweli? Haina hata wachangiaji


Ila kuna zuzu kaleta mada ya kuvaa Pedi matakoni iliyolowekwa na konyaji Uzi unakimbia balaa


Ndo maisha tuliyochagua hayo
 
Wakati mwingine mtu unatamani kusema sisi watanzania ni majuha lakini unaheshimu uumbaji wa Mungu wetu.

Jinsi mambo ya hovyo yanayofanywa na baadhi ya watu tuliowapa madaraka yanavyotia kinyaa, mtu unatamani kusonya lakini ukweli ulio mbele yetu unakutia aibu.

Wakati mwingine unaposikia mtu anasema "Kuna watu ni mazuzu" unaanza kudhani anatusema sisi, hasira zinakupanda lakini unatulia unapokumbuka uhovyo hovyo tulio nao.

Ni lini watanzania tutajua kwamba Hawa wanaofuja, kutapanya na kuiba mali za Umma/serikali huwa wanatuibia sisi!??

Kifanyike nini kwetu hadi tuone kwamba tunatakiwa kuasi dhidi ya mafisadi na wezi wanaotuibia kupitia nafasi za kimadaraka walizo nazo!?

Ni lini tutajitofautisha kiakili na utashi kati ya sisi tulioumbwa binadamu na Ng'ombe!?

Kuvumilia kwetu mambo ya hovyo hakuoneshi kuwa sisi hatukustahili kujitawala!!??
Shida inaanzia kwenye miungu tunayoiabudu kwenye taifa. Kinachoitwa mwenge wa uhuru ni kifungo kibaya sana kwenye ulimwengu wa kiroho kwa taifa. Na shida kubwa inapoanzia. Tunaabudu moto badala ya kumuabudu Mungu wa mbinguni muumbaji wa vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Tuuteketeze huo mwenge na tuombe oba kwa Mungu atafungua nuru kwa taifa letu.
 
Shida iko kwa baadhi ya watu, fikiria ufisadi mkubwa unafanyika. Watu wanajaribu kupaza sauti. Linatokea jitu huko, sijui anafaidika na nini anashusha magazeti kusifia.

Hawa ndiyo wanaoturudisha nyuma, uchawa sijui kunguni. Hata South Africa wameanza kuamka. Wamechoshwa na ufisadi. Hii ni last warning, njoo Tz sasa kuna watu kichwani wanafuga nywele tu.
Watanzania ni kama Nyumbu, kila mmoja anaangalia maslahi yake. Ukijifanya mwanaharakati unageuzwa target na watawala na watakudhuru huku Watanzania wenzio wakikaa pembeni na kukuzodoa. Ile Element ya Solidarity ilikufa na Nyerere mwenyewe.
 
Back
Top Bottom