Mizigo na SGR: Muda umefika kuondoa malori barabarani

Mizigo na SGR: Muda umefika kuondoa malori barabarani

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
images-2.jpeg

Mafanikio ya treni ya abiria kwa sasa kufika Dodoma yanatia moyo.

Hata hivyo ufanisi wa reli kiuchumi ni usafirishaji wa mizigo.

Muda umefika sasa kwa wizara ya uchukuzi kuanza kuratibu namna ya kuyaondoa malori barabarani.

Juhudi za kufufua Central Railway ziendane sambamba na kufufua reli ya TAZARA.

Hongera SGR kwa mwanzo mzuri.
 
Tumbili na Bundi wameigomea hii reli ..wameapa kitukwamisha na wameshaanza tayari.

Je, inawezekana wenye mabasi wanasaidiana na hawa wadudu kupitia nguvu ya giza kuihujumu reli yetu?
 
View attachment 3059159

Mafanikio ya treni ya abiria kwa sasa kufika Dodoma yanatia moyo.

Hata hivyo ufanisi wa reli kiuchumi ni usafirishaji wa mizigo.

Muda umefika sasa kwa wizara ya uchukuzi kuanza kuratibu namna ya kuyaondoa malori barabarani.

Juhudi za kufufua Central Railway ziendane sambamba na kufufua reli ya TAZARA.

Hongera SGR kwa mwanzo mzuri.
Sisi wenye Maroli mtoa mada tutakuroga
 
Uwepo wa Treni yenye Standard ya Kimataifa ni afya kwa taifa letu. Pongezi kwa serikali kuendeleza maono ya JPM. Ni kwa bahati mbaya sana maadui wa mradi huu ni wengi na ni kwa sababu ya ufinyu wa uelewa. Wanahofia kwamba mabasi na malori ya usafirishaji yatatoweka.

Ukweli ni kwamba, katika uwanja wa biashara vyote vitafanya kazi pamoja na vizuri tu. Tanzania ni kubwa na abiria ni wengi. Tunashuhudia hata nchi za wenzetu ambazo zina treni kwa wingi hususani zilizopo Ulaya zikifanikisha hili. Treni zipo, malori yapo, sambamba na mabasi.
 
Swala hapa sio kuzuia malori bali ni kutengeneza Bandari kavu , mfano dodoma na sehem zingine za kimkakati ambapo malori yatakua yanachukulia mizigo ,ili kupungu msongamano wa malori barabarani, lakini pia wafanyabiasha wa malori waweze fanya kazi kwa unafuu zaidi,
 

Mafanikio ya treni ya abiria kwa sasa kufika Dodoma yanatia moyo.

Hata hivyo ufanisi wa reli kiuchumi ni usafirishaji wa mizigo.

Muda umefika sasa kwa wizara ya uchukuzi kuanza kuratibu namna ya kuyaondoa malori barabarani.

Juhudi za kufufua Central Railway ziendane sambamba na kufufua reli ya TAZARA.

Hongera SGR kwa mwanzo mzuri.
Kwani malori yanaondolewa Kwa amri au ushindani wa kibiashara?
 

Mafanikio ya treni ya abiria kwa sasa kufika Dodoma yanatia moyo.

Hata hivyo ufanisi wa reli kiuchumi ni usafirishaji wa mizigo.

Muda umefika sasa kwa wizara ya uchukuzi kuanza kuratibu namna ya kuyaondoa malori barabarani.

Juhudi za kufufua Central Railway ziendane sambamba na kufufua reli ya TAZARA.

Hongera SGR kwa mwanzo mzuri.
Yanasumbua sana njiani hayo
 
Uwepo wa Treni yenye Standard ya Kimataifa ni afya kwa taifa letu. Pongezi kwa serikali kuendeleza maono ya JPM. Ni kwa bahati mbaya sana maadui wa mradi huu ni wengi na ni kwa sababu ya ufinyu wa uelewa. Wanahofia kwamba mabasi na malori ya usafirishaji yatatoweka.

Ukweli ni kwamba, katika uwanja wa biashara vyote vitafanya kazi pamoja na vizuri tu. Tanzania ni kubwa na abiria ni wengi. Tunashuhudia hata nchi za wenzetu ambazo zina treni kwa wingi hususani zilizopo Ulaya zikifanikisha hili. Treni zipo, malori yapo, sambamba na mabasi.
Treni ya abiria haiwezi kulipa uwekezaji wa SGR.
 

Mafanikio ya treni ya abiria kwa sasa kufika Dodoma yanatia moyo.

Hata hivyo ufanisi wa reli kiuchumi ni usafirishaji wa mizigo.

Muda umefika sasa kwa wizara ya uchukuzi kuanza kuratibu namna ya kuyaondoa malori barabarani.

Juhudi za kufufua Central Railway ziendane sambamba na kufufua reli ya TAZARA.

Hongera SGR kwa mwanzo mzuri.
Mimi kama mdau wa sekta ya usafirishaji kwa kutumia malori bado siioni SGR kuyatoa molori barabarani na itachukua muda sana kwa namna miundo mbinu ilivyo

Mfano Leo hii mfanya biashara amenunia ngano kwa bakhresa 30t anataka apeleke Arusha kwa Morombo


Akisema asafirishe kwa njia ya relief itamgarimu muda wake na garama kubwa sana

Atapaswa akodishe gari Toka kiwandan Hadi stesheni aipelekee treni mzigo wake alafu ikifika Arusha akodishe gari nyingine aupeleke dukani kwake

Sambamba na hilo treni haiwez kuonza safari kwa mzigo wa tan 30 analazimika kuungana na wenzake Hadi wajaze behewa nyingi Ili TRC waweze kupata faida

Tukumbuke mfanyabiadhara ni mtu wa kwenda na muda sana hapa atakua amekwama atalazimika kutafuta usafiri ambao ni WA haraka na usiokua na mambo mengine

Ukipakia mzigo dsm mchana Lori likaondoka kesho yake mchana tiyari litakua Arusha kwa mfanyabiadhara

Kwa iyo bado watu wa malori na sisi kampuni za usafirishaji tunayo nafas ya kuendelea kuwepo na kuchangia uchumi wa nchi na hata kulete ushindani mkubwa kwa SGR


NB: SADIRISHA mizigo Yako na FSF COMPANY LTD ndani na nje ya nchi

FSF NLni wamiliki wa malori na wasafirishaji wa mizigo kama vile mazao,mbolea,kontena, vyakula vya mifugo, n.k

Tunapatikana Arusha na Dar wa salaam

Wasiliana nasi 0714797079
Vitalis Ndossi - Logistics and transport manager
 

Mafanikio ya treni ya abiria kwa sasa kufika Dodoma yanatia moyo.

Hata hivyo ufanisi wa reli kiuchumi ni usafirishaji wa mizigo.

Muda umefika sasa kwa wizara ya uchukuzi kuanza kuratibu namna ya kuyaondoa malori barabarani.

Juhudi za kufufua Central Railway ziendane sambamba na kufufua reli ya TAZARA.

Hongera SGR kwa mwanzo mzuri.
Tumefurahia SGR lakini hawahawa vigogo kwenye siasa wanaojikomba kutafuta sifa kuwezesha mradi ndio wataikwamisha SGR. Biashara yao ya usafiri wa malori bila wananchi kua wakali hawataacha ife hivyo kuruhusu sera na sheria zitakazowapendelea wenye malori. Badala ya mizigo kuhamia kwenye reli kutokana na bei nafuu ya usafiri na usafirishaji na ubora wa huduma utashangaa kuona gharama kubwa na usumbufu wa kutengenezwa na wanasiasa kwa niaba yao na matajiri wa malori. Lazima ziwepo sheria na taratibu kuhakikisha mizigo kwa wingi inahamia kwenye reli na kupungua malori barabarani. Hivi sas ajali nyingi pia zinasababishwa na uwepo wa malori heavy duty yanayoenda masafa marefu.
 
Huu mradi utakuwa umehujumiwa sana huko mwanzo ila tulipofikia ni ngumu maana viongozi wengi wana mabasi na malori, hawautaki kabisa ila Bimkubwa kashika sterling, siku zote mvunja nchi ni mwananchi
Mmesahau na wauza MAFUTA
Petrol station zinaendakuathirika!!!
 
Back
Top Bottom