MJADALA: Je, ni sahihi waimbaji wa nyimbo za dini kushiriki matamasha ya kidunia?

Waimbaji wa gospel (hujiita pia wasanii wa nyimbo za injili) wa kizazi hiki hawaendi katika misingi ya neno la Mungu. Wao pia wamegeuka watumishi wa shetani na ndio maana wamefuata mfumo wa mziki wa dunia. Tofauti tu ni maneno wanayotia kwenye tungo zao, lakini mfumo mzima ni ule ule, hivyo kushiriki fiesta kwao ni sawa tu kwani wanamtumikia aliye baba yao.
 
mngekuwa Kenya msingeuliza maswali hayo ya kipuuzi, Huwa mnaangalia channel za Kenya mkaona hiyo miziki Yao ya Gospel? sasa hao wasanii Wana perform hadi club
Kwa hiyo kama wakenya wanafanya basi ni sahihi
 
Nyimbo zake hazina Theology kwahiyo hatuwezi kumweka kwenye maimbaji wa injili,labda tumweke kwenye inspirational singers😂.
 
Nyimbo zake hazina Theology kwahiyo hatuwezi kumweka kwenye maimbaji wa injili,labda tumweke kwenye inspirational singers[emoji23].
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] umemtafutia jina zuri sana
 
Nyimbo zake hazina Theology kwahiyo hatuwezi kumweka kwenye maimbaji wa injili,labda tumweke kwenye inspirational singers[emoji23].
Natamani kusikia Roho Mtakatifu alishuka mahali hapo
 
Neno la uzimq. Unaweza kuniambia ni watu wangapi walimwamini Yesu Kristu baada ya matumbuizo yaliyojaa mauno hatari aliyotoa?
Hayo ni matokeo tu boss na mimi siwezi kujua maana sikuwepo
 
Sema neno madame
Daah haya mambo ya imani siku hizi hata sitakagi kuhukumu sana, maana tunaweza tukawa tunahukumu hapa kumbe hatujui labda mwenzetu alivyotoka pale alitambua kosa lake akaenda kumlilia Mungu wake amsamehe ila sisi tumekaa huku tunamjadili vibaya.

Tukumbuke kwamba kuwa mtumishi wa Mungu hakukufanyi uwe malaika kwamba hautatenda dhambi hilo hata Mungu analijua, hata kina Solomon na David na unabii wao walitenda dhambi (walizini waliua) lakini walikuwa na imani kali na mwisho wa siku walimlilia Mungu awasamehe na bila shaka aliwasamehe.

One thing I believe for sure hawa watumishi wa Mungu (wengi wao) wanajua sana kuishi na Mungu, tunaweza tukaona huku wanatenda dhambi tunasikia oohh sijui mchungaji amezini sijui padre ameua tunawahukumu na kuwatolea kashfa za kila aina kana kwamba sisi ni watakatifu sana.

Lakini hatujui wakiwa peke yao majumbani mwao wanaongea nini na Mungu hatujui wanamlilia Mungu kiasi gani awasamehe, na tukumbuke kuwa hakuna dhambi chini ya jua isiyosameheka isipokuwa dhambi moja tu ya kumkufuru Mungu basi and to God there is always a second chance for as long as we are still alive.
 
Kwa hiyo ni kwamba alikosea si ndio
 
Daah nikisema alikosea nitakuwa nimehukumu, which brings me back to my point up there.
Usiogope kumwambia mtu umekosea, ni kwa sababu sisi sio wakamilifu ndio maana tunatakiwa kuambiana pale tunapoenda tofauti tusijifiche kwenye kichaka cha kuhukumu ili tusiambiwe pale tunapoenda tofauti. Hata biblia inatuagiza kuonyana na kurejezana kwenye mstari sisi kwa sisi ila kwa upole
 
Gospel ni injili maana yake kutangaza habari za kristo. Sasa kwa formula ya paulo jichanganye usitende dhambi. Kama alienda kubiashara kosa! Lakini kama nia yake ni kumtangaza yesu sawa kabisa. Je dhamiri yake ilikuwa wapi? Piano hutumika makanisani lakini hutumika katika macasino. Je utahukumu matumizi ya piano? Tuangalie message aliyoitoa labda kuna mtu mmoja alipata ujumbe na akaokolewa
 
Ile ni sehemu ya burudani, watu walienda kuburudika pale sio kuhubiriwa... kwa lugha rahisi yenye alienda kuburudisha waliofika pale ndio maana alitumbuiza mpaka na viuno alikata ili watu wafurahi.

Kwani ni dhambi kumuimbia Mungu kwa furaha? Wewe umekremisha kuwa ukimwimbia Mungu ni umekaa umetulia na kisura cha huzuni
 
Yeah uko sahihi, na ninajua kwamba tunatakiwa kuonyana kwa sababu ukimuona mwenzio anatenda dhambi hautakiwi kumuangalia tu maana siku ya hukumu utaulizwa fulani alifanya dhambi hii na hii na ulikuwa unamuona je ulimuonya ikiwa ni ndiyo au hapana tutajua huko huko kwenye hukumu.

Lakini kwenye huu uzi kuanzia mtoa mada hadi baadhi ya watoa comments sijaona walichofanya zaidi ya kumhukumu GG, hivyo na mimi ningechangia huu uzi kwa kumsapoti mtoa mada ningekuwa mmoja wa wanaohukumu kwa sababu biblia hiyo hiyo imemuita mnafiki mtu anayetoa boriti kutoka kwenye jicho la mwingine kabla hajatoa kibanzi kilichopo kwenye jicho lake mwenyewe.
 
Hakuna mahali amehukumiwa, wengi wanaonesha ni kwa nini hayuko sahihi kwenda kwenye tamasha lile anyways nimekuelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…