Mjadala kipi kifanyike cha kudumu ili kukomesha mambo ya mizengwe yanayochangia kughairisha mechi?

Mjadala kipi kifanyike cha kudumu ili kukomesha mambo ya mizengwe yanayochangia kughairisha mechi?

Wanyama na ndege wa kufugwa hawaruhusiwi eneo la mchezo timu itakayobainika kuleta viumbe hao itapewa adhabu kali
Bila kusahau kupiga marufuku vizee vyenye mavazi ya asili kama vibwaya na kaniki vikiwa vimebeba tunguri na ambao sio sehemu yeyote ya benchi la ufundi la timu siku ya mazoezi ya mwisho ya timu kabla ya mechi.
 
Bila kusahau kupiga marufuku vizee vyenye mavazi ya asili kama vibwaya na kaniki vikiwa vimebeba tunguri na ambao sio sehemu yeyote ya benchi la ufundi la timu siku ya mazoezi ya mwisho ya timu kabla ya mechi.
Hahah
 
Hapa tunajadili solution ya wakati huu, siyo mambo ya miaka 50 ijayo.
Hiyo mechi iliisha ahirishwa, hakuna anayeweza kurudisha muda nyuma.

Tunajadili ya mbele. Simba wmalize uwanja wao Bunju wafanye mazoezi hata usiku kucha, na Yanga wamalize uwanja wao Jangwani au Kigamboni, na wao wakeshe huko sawa tu, lakini viwanja vya ligi visiwe viwanja vya mazoezi, isipokuwa kwa timu za mikoani au zitokazo nje ya nchi.

Vilabu vinapesa, mnawaacha watu wapuuzi wana filisi halafu mnataka mfanye mazoezi viwanja vya ligi.
 
Lawama hazijawahi kuondoa tatizo,
Kila jambo lina faida na hasara!
Moja ya faida ya mizengwe iliyotokea katika mpira wetu ituamshe ili tuboreshe kanuni na sheria ili kulinda hadhi ya ligi!

Pasipo kunyoosheana vidole kipi kitakuwa suruhisho la kudumu ili haya mambo ya mizengwe yasiendelee kiasi cha kuumiza wapenzi na washabiki wa mpira?

Kwa maoni yangu! Tuboreshe kanuni isomeke hivi.

1. Timu ngeni itahitaji kuutumia uwanja siku moja kabla ya mechi pasipo kuomba ridhaa ya timu mwenyeji, Timu wenyeji wakibainika wameihujumu timu ngeni kwa namna isiyofaa ili kukwamisha zoezi watapokonywa point 6
2. Timu hairuhusiwi kugomea mechi kabla ya malalamiko ya shauri lao kutolewa maamuzi na bodi ya ligi, kutangaza kutoshiriki kabla ya maamuzi ya bodi itatafsiliwa kuwa ni kuizarau mamlaka ya ligi
3. Timu yoyote itayothibitika kuzarau mamlaka ya ligi itashushwa daraja
4. Mechi iliyo ahirishwa kwa sabababu za kinanuni haitakuwa na kiingilio kwa mashabiki endapo timu zote mbili zitakapokutana awamu inayofuata.
5. Bodi ya ligi itatoa ufafanuzi wa malalamiko masaa 6 kabla ya mechi kuchezwa, Bodi ya ligi haitakuwa na mamlaka ya kuahirisha mechi kwa makosa ya kikanuni ndani ya masaa 12 kabla ya mechi
6. Uongozi unaosimamia uwanja utalazimika kuwepo eneo la uwanja masaa 60, kutokuwepo eneo la uwanja kutatafsiliwa kuahilishwa kwa mechi na bodi ya ligi itatangaza hilo.
7. Waamuzi wa mchezo wanaweza kubadilishwa kuamua mechi endapo kuna malalamiko yatayowasilishwa kwa nakala kabla ya saa 6 za mchezo kuchezwa

HAYA NI MAONI YANGU; WEWE UNA Maoni gani ili kuwepo kanuni za kudumu kukomesha mizengwe karibu katika mjadala!
Hebu tuongee ukweli, simba ni mgeni na uwanja wa mkapa? Game ya azam si alichezea pale?

Suluhisho la kudumu ni kuondoa usimba na uyanga kwenye ligi yetu. Hii inaathiri mpaka ustawi wa timu nyingine.

TFF na bodi ya ligi hawana meno kwasababu ya huu usimba na uyanga. Kanuni zimekaa vizuri ila msimamiaji hayupo
 
1. Polisi walinde Uwanja kama inahitajika kulinda Uwanja. Badala ya kutumia watu wasiotambulika kisheria.
2. Watu maalumu wabainishwe ktk timu inaporuhusiwa kuingia kufanya mazoezi kabla ya mechi wanapoambatana na timu.
3. Wamiliki wa Uwanja waanishe muda maalumu wa timu kufanya mazoezi, e.g masaa
4. Kanuni zifuatwe na zitafsiriwe endapo zitavunjwa
 
1. Polisi walinde Uwanja kama inahitajika kulinda Uwanja. Badala ya kutumia watu wasiotambulika kisheria.
2. Watu maalumu wabainishwe ktk timu inaporuhusiwa kuingia kufanya mazoezi kabla ya mechi wanapoambatana na timu.
3. Wamiliki wa Uwanja waanishe muda maalumu wa timu kufanya mazoezi, e.g masaa
4. Kanuni zifuatwe na zitafsiriwe endapo zitavunjwa
Hoja nzuri sana
 
Hiyo mechi iliisha ahirishwa, hakuna anayeweza kurudisha muda nyuma.

Tunajadili ya mbele. Simba wmalize uwanja wao Bunju wafanye mazoezi hata usiku kucha, na Yanga wamalize uwanja wao Jangwani au Kigamboni, na wao wakeshe huko sawa tu, lakini viwanja vya ligi visiwe viwanja vya mazoezi, isipokuwa kwa timu za mikoani au zitokazo nje ya nchi.

Vilabu vinapesa, mnawaacha watu wapuuzi wana filisi halafu mnataka mfanye mazoezi viwanja vya ligi.
Hahah
 
Back
Top Bottom