Natamani babu aongezewe maono haya kwenye tiba yake kama masharti ya kupona!
1. Mafisadi wote wanaokunywa warudishe kwanza na wasirudie tena maana wakirudia itakuwa mara kumi.
2. Maofisa wa mapolisi, wawe wastaafu au kazini waliosababisha watu wabambikiwe kesi na kufungwa kwa hila, wafanye hivyo hivyo warudi uraiani.
3. Wanasiasa waongo, walioukwaa ubunge kwa hila na kupoka haki ya watu warudishe mara moja kwa wahusika maana dawa itawaondoa mara moja duniani.
4. Wale wanaotegemea utabiri na ulinzi wa giza wasiende kabisa kutest kule maana kama wakitest tu, wataharisha mpaka mfumo wa maisha, vinginevyo hakuna kifo, ni kuhara tuu.
hiyo haiwezekani, we hujui kuwa Mungu huwanyeshea mvua walio wema na wabaya?
Nimepata taarifa kwamba waliokunywa dawa ya abu wa liliondo sasa wanaanza kuumwa na matumbo. waanza kuvimba. TAYARI Jjamaa, ndugu na marafiki wa karibu wanafanya harakati za kumkimbiza muhimbi ili aangalie nini kimezidi. lkn anavyosmea yeye mwenyewe kwamba maumivu hayo yamekuja baaa ya kunywa dawa hiyo.haya nimeyapata kutoka kwa mmoja wa mtumiaji AMBAE AKIIMWA NA UKIMWI.
nimepata taarifa kwamba waliokunywa dawa ya abu wa liliondo sasa wanaanza kuumwa na matumbo. Waanza kuvimba. Tayari jjamaa, ndugu na marafiki wa karibu wanafanya harakati za kumkimbiza muhimbi ili aangalie nini kimezidi. Lkn anavyosmea yeye mwenyewe kwamba maumivu hayo yamekuja baaa ya kunywa dawa hiyo.haya nimeyapata kutoka kwa mmoja wa mtumiaji ambae akiimwa na ukimwi.
Wakati watanzania wakimiminika kwenda wilayani Loliondo,kwa Babu kupata dawa inayodaiwa kutibu magonjwa sugu, Mbunge wa Igunga (CCM), Rostam Aziz ameibuka na kusema tiba hiyo haina lolote akidai kwamba ndugu zake watano wameitumia lakini hajapona hata mmoja.
... Ndugu zangu wananchi wa Igunga, mimi mjomba wangu Hassan mnamfahamu karibu wote hapa mjini ni mgonjwa wa siku nyingi wa kisukari. Ameshakunywa dawa hiyo lakini mpaka sasa ni mgonjwa kama mnavyomuona sasa hiyo dawa inaponyesha nani?
na mimi nilifikiria hivyo..lolLabda ana mimba lol
Low thinkers utawafahau tu. Chuki zao zipo kila mahali, Hayo ni mawazo yake Rostam, si kila kitu mnakipeleka katika siasa. Mnona tunaambiwa Lowassa nae kapata kikombe na ametoa magari na nauli za kuwapeleka wapiga kura wake kwa babu?
Zaidi ya yote, mbona Kadinari PENGO wa RC, MWINGIRA wa EPHATA, KAKOBE wa FGBF, Askofu MUSHI wa KANISA HALISI LA AFRIKA na Gazeti la ANNUR wote wamemponda Babu? Kakobeamemuita Babu kuwa ni wakala wa Shetani na Mwingira amemlaani Babu!
Si kila kitu ni siasa. Kama hamuwezi kufikiri deeply, hameni JF
Kwa maana hiyo hakuna hatammoja atakae pona, maana watu wote pamoja na Babu wamejaa zambi
Inawezekana ni kweli au ni uongo......Huyu Babu inahitaji kuwa na nguvu ya kimungu ili kugundua kuwa ni kweli au la....................
Namuunga mkono jenerali pia wa2 hawakatai babu kutibu bt masharti anayotoa babu ni ya kitapeli na cyaki mungu ki ufupi BABU + 500 = DECI MPYA