Mjadala kuhusu Babu wa Loliondo na dawa yake.

Mjadala kuhusu Babu wa Loliondo na dawa yake.

Rostam anachanganya mambo hapa.hao ndugu zake hawajapona kutokana na dhambi zake alizotufanyia watanzania.na si ajabu hta lowasa nae akaponza ndugu zake wasipone.
laana yao haiondoki wala hawasameheki kama wamemtukana Roho Mtakatifu.
maskini mjomba Hassan kaponzwa na rostam
 
Lakini sio kwa sababu Rostam basi kila kitu apingwe.
Yeye amesema ndugu zake watano walipewa hiyo tiba ya babu na hawajapona so ana haki ya kutoiamini hiyo tiba lakini ndugu zake hao wangepona na angesema kuwa haiamini hapo ndipo tungemshangaa.
 
unajua dawa zoote zilizopo hazitibi watu wote kwa 100% lazima utasikia mwingine anakuambia akiwa na malaria akinywa mseto haponi mwingine fansida haponi hata ARV kuna wengine haziwakubali, kikubwa dawa ya babu ni ya kiimani km imani yako ni ndogo na matendo ysko machafu km ya huyu rostam na ukoo wake kamwe haiwezi kukuponya. so kashfa ni mfa maji haishi kutapatapa!! shuhuda zipo kibaaaaao watu wamepona.
 
Rostam anachanganya mambo hapa.hao ndugu zake hawajapona kutokana na dhambi zake alizotufanyia watanzania.na si ajabu hta lowasa nae akaponza ndugu zake wasipone.
laana yao haiondoki wala hawasameheki kama wamemtukana Roho Mtakatifu.
maskini mjomba Hassan kaponzwa na rostam
Uncle wake Dowans hajapona kwa babu?? whaaaaaaayyyyyyyyyy,,,,,, this is so sad Dowans, enewei sio shida cheki ya $96 million ipo atakuwa well taken care of,,,:wof: :rolleyez:
 
Ila bwana ulimwengu una kingeledha kigumu! mbona hata wadhungu wenye lugha yao wakiandika makala hawaweki mavocabulari kama yako? Lengo ni watu wote hata wenye kujua cha kuibia kama sisi tuelewe au ni nini? Anywei nimedonoa kama kuku......
 
Uncle wake Dowans hajapona kwa babu?? whaaaaaaayyyyyyyyyy,,,,,, this is so sad Dowans, enewei sio shida cheki ya $96 million ipo atakuwa well taken care of,,,:wof: :rolleyez:
maskini mjomba hassan hata akipewa cheki ya bilioni 10,bado kivuli Rostam kitasababisha asipone
 
Yani ameona ya BABU ndiyo anaweza kuzungumza, mambo tunayotaka ayazungumzie hatumsikii. Aache kupotezea......
 
Wana Jf tuwaombe wale wasemao tiba kwa babu haifai, watupe njia mbadala mf;
Wajenge hospitali na huduma/tiba zenye viwango ambapo kila m/nchi atamudu.
Waone kama watu watahangaika na usumbufu wa foleni kwa babu ili atibiwe malaria sugu!
 
Itafaa nini mwanadamu kupata uzima wa muda na vyote viijazavyo dunia na kuipoteza roho yake ambayo itaishi milele? Naomba kuwaeleza kuwa my father was in a critical condition at Nairobi hospital and was discharged kwa kuwa hakuna msaada zaidi ya kusubiri siku zake of which cancer was aproaching his spinal cord. At that particular state was sent back home where I had to travel to see him for I was outside the country. Nilifanya jitihada kutafuta wachungaji niende nao kumwombea. Kila niliemweleza alikuwa na tight time table. I had to go as everybody was not knowing what to do; huku madaktari ndani ya familia yetu wakishauri akapigwe mionzi. Lakini the same bother 9ambaye leo amempeleka Loliondo) akakataa kwani yy ndo alikuwa nae Nairobi na aliambiwa katika state ile na umri wake mionzi lazima imchukue. So my brother alikuwa na tumaini moja tu kwamba mimi nikamwombee for he once got saved from my prayers. Kwangu it was a challenge for my faith was not there labda kwakuwa ni baba na hofu ilikuwa imenijaa. I had to...Guess what after two months of pain and no normal feeding...maumivu yakaondoka and he ate his food kwa mara ya kwanza. Hali ikaenda inaimarika mpaka akaweza kutembea na hakuwa na maumivu.

Sasa hapo ni kipi kinampeleka Loliondo? A person who was bed ridden leo ameweza kutembea no pain anasahau hiyo neema na kwenda Loliondo to make sure eti anapona kabisa hiyo kabisa ni ipi? Doent this show short of faith? Well am not blaming him lakini I can see how its easy for christians to be swayed by miracles na kusahu the basics za christianity ambayo ni kumjua Mungu na nguvu zake. Kama leo unashindwa kujua kuwa ni Mungu amekuponya na huhitaji mzizi ku complement nguvu za Mungu basi kesho likija lingine utakimbilia huko. Ni kama mwanamke anayeshindwa kumstahi mumewe akipata shida na hivyo kwenda kwa mwingine asiyemjua ili apate vilivyopelea kwa muda huo huku akimwacha mumewe kwa kisingizo cha matatizo. Nobody can complement your husband kama huwezi kumpa heshima yake kwa kuvumilia basi ujue hata yeye kesho atashindwa kusimama mbele ya wenzake na kudai kuwa yeye ni mwanaume kwakuwa mkewe amemvua nguo hadharani.

Vile vile na Mungu hawezi kujivunia na mtu ambaye anampenda kwa kutaka ishara tu bila kupenda kujua chanzo cha hizo ishara. Kumbuka neno la Mungu lina sema, God was known by Musa in his ways but to the children of Israel by miracles. Alfu kwenye new tastament anasema in 1cor 1:22-23 For Jews require a sign and Greeks seek after wisdom: But we preach christ crusfied, unto Jews a stumbling block and unto the greeks foolishness. Going through JF utaona Jews: wapenda ishara ambao wanajaustify watu waende kwani Mungu ndo ameleta msaada na Greeks: wanaojidai science ndo ithibitishe kama kweli hiyo ni dawa au la!

Please christians let us be rooted in the word of God. Let us know our God's Love in length, breadth and depth which is His fullness. Refuse to be carried away by winds and unknown teachings.

Nimefurahishwa sana na maelezo yako. Mungu akubariki sana kwa kusema ukweli huu. Wakristo tafadhali tuwe macho, tusibali kuchuliwa na kila upepo wa elimu unaotokea
 
Rostam aponda tiba ya Mchungaji Loliondo Send to a friend Tuesday, 15 March 2011 21:22 0diggsdigg

Shija Felician, Igunga
WAKATI Watanzania wengi wakimiminika kwenda wilayani Loliondo, mkoani Arusha kupata dawa inayodaiwa kutibu magonjwa sugu, Mbunge wa Igunga (CCM), Rostam Aziz ameibuka na kusema tiba hiyo haina lolote akidai kwamba ndugu zake watano wameitumia lakini hawajapona.

Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru wapigakura uliofanyika kwenye Viwanja vya CCM wilayani Igunga, Tabora mbunge huyo alisema haiamini dawa hiyo kwa kuwa ana ushahidi kwa ndugu zake hao ambao anadai kwamba wanaendelea kuugua kisukari licha ya kutumia dawa hiyo siku saba zilizopita.

Aliwataka wale watakaokwenda Loliondo ambao wanatumia dawa za hospitalini kuendelea kuzitumia badala ya kuzipuuza na kuzitupa... “Ndugu zangu wananchi wa Igunga, mimi mjomba wangu Hassan mnamfahamu karibu wote hapa mjini ni mgonjwa wa siku nyingi wa kisukari. Ameshakunywa dawa hiyo lakini mpaka sasa ni mgonjwa kama mnavyomuona sasa hiyo dawa inaponyesha nani?”

Hata hivyo, aliwataka wananchi wote wenye imani juu ya dawa hiyo waende huku akiwasisitizia kutopuuza ushauri wa madaktari kwani.

Wakati Rostam akipinga dawa hiyo, wilayani Kahama, mamia ya wafanyabiashara wamefunga shughuli zao na kukimbilia Loliondo kwa Mchungaji Mwasapile kunywa dawa hiyo huku baadhi ya waliorejea baada ya kuinywa wakidai kuwa hali zao sasa ni nzuri.

Wafanyabiashara hao wengi wao wanaondoka kwa siri wakidai wanakwenda Dar es Salaam katika shughuli zao, lakini siri imefichuka baada ya baadhi yao kuoneka katika runinga wakiwa katika foleni wakisubiri kupatiwa huduma hiyo.

Mbali ya kuzungumzia suala hilo la tiba ambalo limegusa hisia za wananchi wengi wa Afrika Mashariki, mbunge huyo aliwapa pole wananchi wa Igunga ambao nyumba zao zimeezuliwa na upepo uliosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha wiki iliyopita ambazo ziliathiri kaya 19. Aitoa msaada wa Sh500,000 kwa kila kaya iliyokumbwa na maafa hayo.



Dhu inaelekea naye alishaenda huko kupata kikombe chake!!!
 
Ila bwana ulimwengu una kingeledha kigumu! mbona hata wadhungu wenye lugha yao wakiandika makala hawaweki mavocabulari kama yako? Lengo ni watu wote hata wenye kujua cha kuibia kama sisi tuelewe au ni nini? Anywei nimedonoa kama kuku......

Anajifanya tu; Kiingereza kigumu kiko England na wala hawaandiki hivyo kama yeye wanapotaka kuwasiliana na Umma.
 
Kwani Rostam hana mawasiliano best wake Jakaya Mrisho Kikwete akampa ushuhuda wa tiba ya babu?
 
Low thinkers utawafahau tu. Chuki zao zipo kila mahali, Hayo ni mawazo yake Rostam, si kila kitu mnakipeleka katika siasa. Mnona tunaambiwa Lowassa nae kapata kikombe na ametoa magari na nauli za kuwapeleka wapiga kura wake kwa babu?

Zaidi ya yote, mbona Kadinari PENGO wa RC, MWINGIRA wa EPHATA, KAKOBE wa FGBF, Askofu MUSHI wa KANISA HALISI LA AFRIKA na Gazeti la ANNUR wote wamemponda Babu? Kakobeamemuita Babu kuwa ni wakala wa Shetani na Mwingira amemlaani Babu!

Si kila kitu ni siasa. Kama hamuwezi kufikiri deeply, hameni JF

Na Bwana Mungu akamwambia Abram, hutaitwa tena Abram ila tangu sasa utaitwa Ibrahim. Atakayekulaani wewe atalaaniwa, naye atakayekubariki atabarikiwa. Tumsifu Yesu Kristu.
 
Hawo ndugu zako wapeleke ulaya wakatibiwe kwani zimeisha? Sisi tutaendelea tibiwa na babu tu hatuelewi kitu.Ww mwenye nazo na nduguzo huwezi pona kwa sababu huna huruma na watanzania.Kama ungekuwa na huruma ungewekeza kwy matibabu.Acha kuponda tiba za sie wanyonge wapeleke jamaa zako Iran na canada wakatibiwe
 
unajua dawa zoote zilizopo hazitibi watu wote kwa 100% lazima utasikia mwingine anakuambia akiwa na malaria akinywa mseto haponi mwingine fansida haponi hata ARV kuna wengine haziwakubali, kikubwa dawa ya babu ni ya kiimani km imani yako ni ndogo na matendo ysko machafu km ya huyu rostam na ukoo wake kamwe haiwezi kukuponya. so kashfa ni mfa maji haishi kutapatapa!! shuhuda zipo kibaaaaao watu wamepona.

Asante ndugu kwa ufafanuzi.
 
Kwa nini Mungu asiamuru kirusi cha Ukimwi kife duniani kote katika jina la Yesu?

Kwa nini Mungu anapenda kubembelezwa, na hela za dawa na sadaka analipwa?

Halafu Mr. Mungu ameshatawala miaka mingi mpaka anamkaribia Gaddafi, na matatizo ya health care system yake hayaishi, tumuondoe madarakani.


Nilikuwa nisichangieee hii..mada lakini kwa upupu wako huu..naona nikujuze nafikiri umechoka kuishi wewe kwa maaana haya unayoandika hapa ni laana tuupu...
 
Hawa wachungaji wengine kama Kakobe, Mwingira na wengineo wanaona kuwa sababu kubwa ya kupata idadi kubwa ya waumini walionao ni kutokana na hao waumini kutafuta tiba mbadala (neno la Mungu) kuwaponya maradhi yao; hivyo kutokana na babu kutibu maradhi kwa njia ambayo ni rahisi bila kumlazimisha mtu kuokoka na dawa kufanya kazi kwa muda mfupi na kutolewa ushuhuda wa kweli ambao ni tofauti na wa kwao wa kupanga, wanaona inakula kwao.

Makelele yote wanayotoa ni katika kuhakikisha kuwa wanaendelea kuhodhi hisa ya soko lao (Market Share) katika suala zima la makanisa ya Kipentekoste. Kuna madhara makubwa wameyaona kibiashara zaidi. Kwani kama jamaa zao wakienda kupata tiba halafu wakapona kutakuwa hamna haja ya kuendelea kwenda kwenye makanisa yao. Kwani hata babu anawaambia kama umepona katoe sadaka kwenye nyumba yako ya ibada. Hii ni dalili kuwa wale waumini watarudi kwenye imani zao za awali kabla ya kwenda kwenye hayo makanisa ya Manabii.

Waumini watakuwa wanawashitukia hawa manabii, kwani kwa kipindi choote walichokuwa wakihudhuria ibada kwenye hayo makanisa ya Manabii kwa matumaini ya kupona lakini lah na kwa kikombe cha uzima wamepona... Wengi watawakimbia na hivyo wao (Manabii) kukosa "market share".

Kwa upande mwingine babu ameongeza changamoto kwenye nyanja ya tiba. Hata wale waliokuwa wakifanyia utafiti baadhi ya magonjwa wanapigwa na butwaa ni vipi hiki kikombe kinatibu. Lakini wanasahau kuwa kila jambo wanalofikiri kuwa ni njia muafaka ya kupambana na magonjwa kuwa ni kutokana na elimu waliyoipata kwa mapokeo. Ila babu amekuja na njia ambayo ni mapinduzi kwenye nyanja ya Tiba.

Mtu unapotoa maoni na kusema kuwa kikombe cha uzima kithibitishwe kwa njia za kisayansi naomba nitoe angalizo. Hizo njia za kisayansi ni zipi? Maabara ? Kwani hizo njia zilitokea wapi? Hayo yalikuwa ni mawazo ya watu katika kipindi chao ambapo nao walionekana kama wanafanya miujiza. Hivyo kwa hili la babu, mimi nina imani kabisa kuwa tunaishi katika historia. Baada ya kipindi, muda, wakati fulani tutapata jibu ni kitu gani kilikuwa kikiendelea. Wahenga walisema "Muda utasema".

Tumwache babu aendelee kutoa tiba. Tujaribu kufanya tafiti tuweze kujua ni nini hasa kinachojiri. Tusiongee tu kwa kuketi kwenye computer zetu na kutoa maoni bila kufanya tafiti na kupata takwimu sahihi.

Nawasilisha.

Good explanation and I hope watu kama Miss Judy wataelewa sasa
 
BlueBalaa (sijui ina maana Chelsea?) Naungana nawe kuwe kuwa hao wote ni wafa maji wameona kwao kumedoda sasa wanatafuta namna ya kumkandia Babu. Washindwe na walegee hakuna sababu ya kudharau jitihada au maono aliopewa Babu. Mpeni muda na tafuteni mengine ya kwenu sio kujihangaisha na ya Loliondo. Mmekwama kiaina.

Thanks ndugu, mi watu nashangaa wewe kama huamini si ukae kimya.
 
ndugu, labda utusaidie ni nini maana ya uhuru wa kutoa maoni? kwani huyo babu ni nani hadi watu wasimtolee maoni?

mitume na manabii walitolwa maoni, sembuse yeye?

acha kila mtu awe huru kutoa anaochoona ni sawa, ili mradi hawamkashifu wala kumkufuru Mungu

Glory to God

Kwahiyo wewe unaona aliyosema Rostam, Mwingira na Kakobe ni MAONI SIYO. Wao walikandia na siyo maoni. Naomba usiniharibie siku dada yangu
 
Back
Top Bottom