chambi1509
Member
- Mar 29, 2018
- 95
- 42
Tatizo ni namna gani unavyolima una lima kwa moyo au unalima kwa kuambiwa tu utapata gunia flani , ekari moja gunia 18 mpaka 20 ukilima kawaida ila ukilima kisasa na ukawekeza hela yako vizuri na eneo likawa lina mbolea vizuri basi utafikisha gunia 25 kwa ekariHabari wadau, natarajia kulima mpunga msimu wa masika, lakini kabla hujaingia LAZIMA ufanye udadis ili kujiridhisha!
Ukiwauliza wakulima wenyewe wanakuambia heka moja inatoa magunia 20-30
Wengine magunia 15-20
Sasa UPI ukweli?
Naomba mwenye maelezo ya kina, kama inawezekana anieleze ni aina gani ya mbegu ya mpunga inayovumilia hali ya hewa na yenye mavuno mengi /mazuri!
Naomba kuwasilisha wakuu!
Karibuni nyote!
Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba tuwasiliane mkuu 0652603278 tuyajenge vizuriMimi nililima msimu wa 2017/18 na msimu huu 2018/19 nitalima tena.
Msimu uliopita, nililima ekari sita (06). Kati ya hizo, ekari tatu (03) nilipanda mbegu iitwayo super mkombozi ambayo hutumia siku 90 shambani tangu kupanda hadi kuvuna..na ekari tatu (03) nyingine, nilipanda mbegu aina ya Sarro ambayo hutumia siku 120.
Matokeo:-
Kwa ekari nilizopanda super mkombozi, nilivuna wastani wa magunia 17 Kwa kila ekari. Na Kwa zile ekari nilizopanda sarro, nilivuna wastani wa magunia 25 Kwa kila ekari. SIKUTUMIA MBOLEA HATA ROBO KILO
Changamoto:-
Kutegemea mvua ni changamoto kubwa. Mavuno yaliathiriwa na ukame wa takribani siku 24.
Changamoto nyingine, ni umbali. Mimi nipo mjini na pia ni mwajiriwa. Kutegemea mtu mwingine akukodie shamba, akulimie na kazi zote za shamba akufanyie yeye..LABDA AWE MALAIKA. ILA MSIMU HUU NALIMA TENA
Nashykuru sana kwa maelezo mazuri!Kabla ya kulima wewe unataka mpunga wa nini?, kufanyia biashara (kuuza) , au kula mwenyewe na familia yako tu. Kama nusu biashara nusu matumizi ya nyumbani, cha kufanya ni lazima ujue katika eneo lako aina gani ya mpunga unaopendwa na walaji.
Aina za mpunga zipo nyingi ila kuna mbegu ndefu na mbegu fupi
Mbegu ndefu
- super Shinyanga, super mbeya, super Kilombero (super india) hizi hotofautiana majina kutokana na mikoa ila wengi huzitambua kwa sifa zake
- mbawa mbili, pamba ( huwa nyeupe kabisa) kitumbo, n. k
Mbegu fupi
- sallo S5 ( hufanana kidogo na super), salo chekechea, sali 360 n. k zipo nyingi sana
MAANDALIZI
Inategemea na ukanda wenu lkn kwa Morogoro huandaa shamba baada ya kuchoma majani na kuja kulima kuanzia mwezi wa 11 mwishoni hadi wa 12. Majani yanapoanza kuota yakiwa mateke piga dawa aina ya Round up ( hufanya kazi kwa siku 21) au dudusate ( hufanya kazi kuanzia siku 15) au dynasate au kiua magugu kizuri. Kama mfuko wako unakidhi unaweza ukalima tena ili kupunguza ng'olezi ila kama hautoshelezi inatosha kwa hapo
KUPANDA
Mbegu za mpunga mrefu humwagwa kwa kutawanywa na trekta hufukia. Mbegu ya salo unaweza ukamwaga na kufukia kwa trekta au kuotesha kitaru kisha kupandikuza japo ya kitaru inagharama kubwa ila mavuno mengi pia.
PALIZI
Hapa wakati mpunga umeanza kutoka una kama mwezi unakuwa umeshika udongo vizuri unaweza ukapiga dawa aina ya 2 4D ukichanganya na Rice paddy au kuna dawa inaitwa white gold nadhani jina limenitoka huuzwa bei ghali kidogo kama 50,000 hivi hii. Kisha unakuja kuokoteza baadhi ya majani machache tu shambani.
Baada ya hapo kwa mikoa mingine huamia ndege ila kwa mikoa mingine baadhi ya pande za Ifakara huwa hawana usumbufu wa ndege
KUVUNA
Mpunga mzuri huvunwa ukiwa nyama nono yaani kabla ya kukauka sana na gharama za uvunaji hutegemeana na eneo / mkoa husika
. Mpunga mrefu kuna uwezekano wa heka moja kama umehudumia vizuri ikatoa gunia 9 hadi 12 ya debe saba na gunia 7 hadi 10 za debe 10 kwa heka
Mpunga mfupi wa salo unaweza ukatoa gunia 20 hadi 30 kwa heka kwa gunia la debe saba
MAUZO
inategemea soko lako ulilolenga kama mwezi wa 12 gunia huuzwa kwa bei ya Tsh 100,000 /=, lakini unaweza ukakoboa gunia la debe saba na kutoa kilo 60 hadi 67 na kuuza mchele kwenye mashine kwa bei za jumla ambapo mwezi wa 12 kilo huwa Tsh 1600, 1800 hadi 2000
CHANGAMOTO
Kuna magonjwa ambayo husababishwa na ufinyu wa mvua kama serenge, ugonjwa wa mabaka baka, kama unalima kilimo shadidi kupambana na panya, na mpunga kukosa madini ya nitrojeni kwa wengine huweka mbolea au kupiga booster ya maji pale wanapoona mpunga umeanza kudumaa.
Binafsi nataka kulima maeneo ya Bahi, wanapendelea kulima mbegu ya mpunga aina ya nganyaro, mbawa mbili Na super mkombozi!Kabla ya kulima wewe unataka mpunga wa nini?, kufanyia biashara (kuuza) , au kula mwenyewe na familia yako tu. Kama nusu biashara nusu matumizi ya nyumbani, cha kufanya ni lazima ujue katika eneo lako aina gani ya mpunga unaopendwa na walaji.
Aina za mpunga zipo nyingi ila kuna mbegu ndefu na mbegu fupi
Mbegu ndefu
- super Shinyanga, super mbeya, super Kilombero (super india) hizi hotofautiana majina kutokana na mikoa ila wengi huzitambua kwa sifa zake
- mbawa mbili, pamba ( huwa nyeupe kabisa) kitumbo, n. k
Mbegu fupi
- sallo S5 ( hufanana kidogo na super), salo chekechea, sali 360 n. k zipo nyingi sana
MAANDALIZI
Inategemea na ukanda wenu lkn kwa Morogoro huandaa shamba baada ya kuchoma majani na kuja kulima kuanzia mwezi wa 11 mwishoni hadi wa 12. Majani yanapoanza kuota yakiwa mateke piga dawa aina ya Round up ( hufanya kazi kwa siku 21) au dudusate ( hufanya kazi kuanzia siku 15) au dynasate au kiua magugu kizuri. Kama mfuko wako unakidhi unaweza ukalima tena ili kupunguza ng'olezi ila kama hautoshelezi inatosha kwa hapo
KUPANDA
Mbegu za mpunga mrefu humwagwa kwa kutawanywa na trekta hufukia. Mbegu ya salo unaweza ukamwaga na kufukia kwa trekta au kuotesha kitaru kisha kupandikuza japo ya kitaru inagharama kubwa ila mavuno mengi pia.
PALIZI
Hapa wakati mpunga umeanza kutoka una kama mwezi unakuwa umeshika udongo vizuri unaweza ukapiga dawa aina ya 2 4D ukichanganya na Rice paddy au kuna dawa inaitwa white gold nadhani jina limenitoka huuzwa bei ghali kidogo kama 50,000 hivi hii. Kisha unakuja kuokoteza baadhi ya majani machache tu shambani.
Baada ya hapo kwa mikoa mingine huamia ndege ila kwa mikoa mingine baadhi ya pande za Ifakara huwa hawana usumbufu wa ndege
KUVUNA
Mpunga mzuri huvunwa ukiwa nyama nono yaani kabla ya kukauka sana na gharama za uvunaji hutegemeana na eneo / mkoa husika
. Mpunga mrefu kuna uwezekano wa heka moja kama umehudumia vizuri ikatoa gunia 9 hadi 12 ya debe saba na gunia 7 hadi 10 za debe 10 kwa heka
Mpunga mfupi wa salo unaweza ukatoa gunia 20 hadi 30 kwa heka kwa gunia la debe saba
MAUZO
inategemea soko lako ulilolenga kama mwezi wa 12 gunia huuzwa kwa bei ya Tsh 100,000 /=, lakini unaweza ukakoboa gunia la debe saba na kutoa kilo 60 hadi 67 na kuuza mchele kwenye mashine kwa bei za jumla ambapo mwezi wa 12 kilo huwa Tsh 1600, 1800 hadi 2000
CHANGAMOTO
Kuna magonjwa ambayo husababishwa na ufinyu wa mvua kama serenge, ugonjwa wa mabaka baka, kama unalima kilimo shadidi kupambana na panya, na mpunga kukosa madini ya nitrojeni kwa wengine huweka mbolea au kupiga booster ya maji pale wanapoona mpunga umeanza kudumaa.
Mmmh hongera kwa mavuno makubwa hivyo ila naomba nikuulize we ulilima mkoa gani kwa mazao hayo bila mboreaMimi nililima msimu wa 2017/18 na msimu huu 2018/19 nitalima tena.
Msimu uliopita, nililima ekari sita (06). Kati ya hizo, ekari tatu (03) nilipanda mbegu iitwayo super mkombozi ambayo hutumia siku 90 shambani tangu kupanda hadi kuvuna..na ekari tatu (03) nyingine, nilipanda mbegu aina ya Sarro ambayo hutumia siku 120.
Matokeo:-
Kwa ekari nilizopanda super mkombozi, nilivuna wastani wa magunia 17 Kwa kila ekari. Na Kwa zile ekari nilizopanda sarro, nilivuna wastani wa magunia 25 Kwa kila ekari. SIKUTUMIA MBOLEA HATA ROBO KILO
Changamoto:-
Kutegemea mvua ni changamoto kubwa. Mavuno yaliathiriwa na ukame wa takribani siku 24.
Changamoto nyingine, ni umbali. Mimi nipo mjini na pia ni mwajiriwa. Kutegemea mtu mwingine akukodie shamba, akulimie na kazi zote za shamba akufanyie yeye..LABDA AWE MALAIKA. ILA MSIMU HUU NALIMA TENA
Ujue bro maeneo mengi watu wanalima bila hata mbolea!Mmmh hongera kwa mavuno makubwa hivyo ila naomba nikuulize we ulilima mkoa gani kwa mazao hayo bila mborea
nice explanation,why mbegu ndefu inatoa gunia chache compare to mbegu fupi?na ipi inapendwa sokoni kati ya mbegu ndefu na mbegu fupi?Kabla ya kulima wewe unataka mpunga wa nini?, kufanyia biashara (kuuza) , au kula mwenyewe na familia yako tu. Kama nusu biashara nusu matumizi ya nyumbani, cha kufanya ni lazima ujue katika eneo lako aina gani ya mpunga unaopendwa na walaji.
Aina za mpunga zipo nyingi ila kuna mbegu ndefu na mbegu fupi
Mbegu ndefu
- super Shinyanga, super mbeya, super Kilombero (super india) hizi hotofautiana majina kutokana na mikoa ila wengi huzitambua kwa sifa zake
- mbawa mbili, pamba ( huwa nyeupe kabisa) kitumbo, n. k
Mbegu fupi
- sallo S5 ( hufanana kidogo na super), salo chekechea, sali 360 n. k zipo nyingi sana
MAANDALIZI
Inategemea na ukanda wenu lkn kwa Morogoro huandaa shamba baada ya kuchoma majani na kuja kulima kuanzia mwezi wa 11 mwishoni hadi wa 12. Majani yanapoanza kuota yakiwa mateke piga dawa aina ya Round up ( hufanya kazi kwa siku 21) au dudusate ( hufanya kazi kuanzia siku 15) au dynasate au kiua magugu kizuri. Kama mfuko wako unakidhi unaweza ukalima tena ili kupunguza ng'olezi ila kama hautoshelezi inatosha kwa hapo
KUPANDA
Mbegu za mpunga mrefu humwagwa kwa kutawanywa na trekta hufukia. Mbegu ya salo unaweza ukamwaga na kufukia kwa trekta au kuotesha kitaru kisha kupandikuza japo ya kitaru inagharama kubwa ila mavuno mengi pia.
PALIZI
Hapa wakati mpunga umeanza kutoka una kama mwezi unakuwa umeshika udongo vizuri unaweza ukapiga dawa aina ya 2 4D ukichanganya na Rice paddy au kuna dawa inaitwa white gold nadhani jina limenitoka huuzwa bei ghali kidogo kama 50,000 hivi hii. Kisha unakuja kuokoteza baadhi ya majani machache tu shambani.
Baada ya hapo kwa mikoa mingine huamia ndege ila kwa mikoa mingine baadhi ya pande za Ifakara huwa hawana usumbufu wa ndege
KUVUNA
Mpunga mzuri huvunwa ukiwa nyama nono yaani kabla ya kukauka sana na gharama za uvunaji hutegemeana na eneo / mkoa husika
. Mpunga mrefu kuna uwezekano wa heka moja kama umehudumia vizuri ikatoa gunia 9 hadi 12 ya debe saba na gunia 7 hadi 10 za debe 10 kwa heka
Mpunga mfupi wa salo unaweza ukatoa gunia 20 hadi 30 kwa heka kwa gunia la debe saba
MAUZO
inategemea soko lako ulilolenga kama mwezi wa 12 gunia huuzwa kwa bei ya Tsh 100,000 /=, lakini unaweza ukakoboa gunia la debe saba na kutoa kilo 60 hadi 67 na kuuza mchele kwenye mashine kwa bei za jumla ambapo mwezi wa 12 kilo huwa Tsh 1600, 1800 hadi 2000
CHANGAMOTO
Kuna magonjwa ambayo husababishwa na ufinyu wa mvua kama serenge, ugonjwa wa mabaka baka, kama unalima kilimo shadidi kupambana na panya, na mpunga kukosa madini ya nitrojeni kwa wengine huweka mbolea au kupiga booster ya maji pale wanapoona mpunga umeanza kudumaa.
Na Mimi nasubiria majibu yatayotolewanice explanation,why mbegu ndefu inatoa gunia chache compare to mbegu fupi?na ipi inapendwa sokoni kati ya mbegu ndefu na mbegu fupi?
Hapa utoaji wa magunia mengi na machache umetofautiana katika lugha ya wakulima tunaita inapacha, mbegu ndefu haipachi sana (kupacha ni ile hali ya mche wa mpunga kutoa masuke mengi zaid).nice explanation,why mbegu ndefu inatoa gunia chache compare to mbegu fupi?na ipi inapendwa sokoni kati ya mbegu ndefu na mbegu fupi?
Ok ni vizuri na kama umefanya randomly research ukajua ukanda huo tabia ya hali ya hewa, majira ya mvua na aina ya udongo, na katika mbegu hizo tatu zipi zinavumilia jua, magonjwa n. k, na je udongo wenyewe umejitosheleza hauhitaji mbolea au kuna ulazima wa kuweka mbolea kutokana na mimea kukosa aina fulani ya madini. Utapoendelea kulima na kushare na watu wengi zaidi kuhusu kilimo ndivyo utavyokuwa na upana zaid na ubunifu ktk kilimoBinafsi nataka kulima maeneo ya Bahi, wanapendelea kulima mbegu ya mpunga aina ya nganyaro, mbawa mbili Na super mkombozi!
Ushauri wako tafadhali!
Nakufata WhatsApp mkuuOk ni vizuri na kama umefanya randomly research ukajua ukanda huo tabia ya hali ya hewa, majira ya mvua na aina ya udongo, na katika mbegu hizo tatu zipi zinavumilia jua, magonjwa n. k, na je udongo wenyewe umejitosheleza hauhitaji mbolea au kuna ulazima wa kuweka mbolea kutokana na mimea kukosa aina fulani ya madini. Utapoendelea kulima na kushare na watu wengi zaidi kuhusu kilimo ndivyo utavyokuwa na upana zaid na ubunifu ktk kilimo
Kiongozi naomba unitumie namba yako inbox pia nami nahtaji kulima pia.Hivi mbegu hutofatiana eneo hadi eneo jingine? Maana wakulima utawasikia wakisema huu mchele wa kahama, wengine mchele wa Mbeya,
Na hapa Bahi wanalima mbegu wanaiita mbawa mbili, nganyaro (sina hakika haya majina kama ni ya kitaalamu au wameamua kuya rename tu)
Sent using Jamii Forums mobile app
0652603278Kiongozi naomba unitumie namba yako inbox pia nami nahtaji kulima pia.