Mjadala mpana: Rais ateue kuzingatia uwezo tu au angalie uwiano wa makundi pia?

Mjadala mpana: Rais ateue kuzingatia uwezo tu au angalie uwiano wa makundi pia?

IslamTZ

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2010
Posts
309
Reaction score
182
Tumesikia malalamiko memgi juu ya baraza jipya la mawaziri la Rais Samia.
  • Kuna malalamiko ya kukosekana usawa wa jinsia, mawazir wanawake ni 36% na manaibu ni 20 tu
  • Kuna malalamiko ya kanda fulani kupendelewa, kama mkoa wa Pwani kuwa na mawaziri (na maanaibu) 5
  • Kuna malalamiko kuwa walioachwa wote ni Wakristo, ingawa kwa upande mwingine hivi sasa mawaziri na manaibu Wakristo ni 32 ukilinganisha na Waislamu 18 tu.
  • Pia yapo malalamiko kuwa watoto wa familia za viongozi wameendelea kuingizwa kwenye baraza, kama yalivyowasilishwa na Malisa GJ na Thabit Jacob aliyewataja kabisa watoto hao kuwa ni Nape Nnauye, Januari Makamba, Pinda, Mavunde, Ndejembi.
Maswali ya msingi:
1. Je Rais na mamlaka nyingine za uteuzi zizingatie uwiano wa makundi au la?
2. Pili, mamlaka zizingatie uwiano wa makundi ya aina gani? Jinsia, rika, dini, kanda, kabila nk?
3. Hali ikoje baraza hili na nini kifanyike?

Nimemsikia Godbless Lema akikosoa mambo ya kuangalia uwiano, amnbapo alitaka weledi tu uzingatiwe? Je iwe hivyo? Wakati tukijadili haya, tukumbuke kuwa wenzetu wa Kenya na baadhi ya nchi nyingine za jirani ni matakwa ya katiba uteuzi uzingatie sura ya kitaifa, ambao ndio huo uwiano? Nasi tufuate msingi huo? Au tupuuzie tu?

Karibuni
 
Hakuna kundi lolote Tz ambalo halina uwezo; azingatie vyote.
 
Katiba mpya ndio muhimu ili mawaziri wawe wanathibitishwa na bunge kwa kura.
 
Lema anachomaanisha ni kwamba waislamu hawana uwezo wa kufanya kazi serikalini na anashangaa kwanini wanateuliwa,, [emoji23][emoji23]
Nabii Lema sio tu ni mdini bali pia hana sense of reality,,,

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Kliuna ubaguzi mwingi katika teuzi zake huku wanawake wakiwa hawaguswi hata wanapoboronga!

Tazama katika list ya mawaziri aliowatema hakuna mwanamke hata mmoja, Je ni kweli mawaziri wa kike wote walikuwa correct 100% kuliko men? Au ni mkakati wa kuelekea 50/50 ?
 
Tazama katika list ya mawaziri aliowatema hakuna mwanamke hata mmoja, Je ni kweli mawaziri wa kike wote walikuwa correct 100% kuliko men? Au ni mkakati wa kuelekea 50/50 ?
Wana-CCM waliokuwa wanamsumbua Mwinyi ni Wanaume... akina Malecela na G55 yao!

Wana-CCM waliokuwa wanamsumbua JK ni wanaume... akina Lowassa na wenzake

Wana-CCM waliomsumbua Magufuli ni wanaume... akina Membe na wenzake!!

Na ukimtoa Bibi Titi, hata wana-CCM/TANU waliokuwa wanamsumbua Mwalimu ni wanaume!!

Kwahiyo kama ataamua kkufyagia anaoona wanamsumbua, hapo tarajia wanaume ndio watakaokuwa wanaendelea kufyekwa!!

Hakuna aliyeondolewa kwa ajili ya utendaji mbovu (ingawaje simaanishi ni watendaji wazuri) bali wote wanaofyatuliwa since Day 1 ni wale anaoamini ama wanamkwamisha au watamkwamisha!
 
Tumesikia malalamiko memgi juu ya baraza jipya la mawaziri la Rais Samia.
  • Kuna malalamiko ya kukosekana usawa wa jinsia, mawazir wanawake ni 36% na manaibu ni 20 tu
  • Kuna malalamiko ya kanda fulani kupendelewa, kama mkoa wa Pwani kuwa na mawaziri (na maanaibu) 5
  • Kuna malalamiko kuwa walioachwa wote ni Wakristo, ingawa kwa upande mwingine hivi sasa mawaziri na manaibu Wakristo ni 32 ukilinganisha na Waislamu 18 tu.
  • Pia yapo malalamiko kuwa watoto wa familia za viongozi wameendelea kuingizwa kwenye baraza, kama yalivyowasilishwa na Malisa GJ na Thabit Jacob aliyewataja kabisa watoto hao kuwa ni Nape Nnauye, Januari Makamba, Pinda, Mavunde, Ndejembi.
Maswali ya msingi:
1. Je Rais na mamlaka nyingine za uteuzi zizingatie uwiano wa makundi au la?
2. Pili, mamlaka zizingatie uwiano wa makundi ya aina gani? Jinsia, rika, dini, kanda, kabila nk?
3. Hali ikoje baraza hili na nini kifanyike?

Nimemsikia Godbless Lema akikosoa mambo ya kuangalia uwiano, amnbapo alitaka weledi tu uzingatiwe? Je iwe hivyo? Wakati tukijadili haya, tukumbuke kuwa wenzetu wa Kenya na baadhi ya nchi nyingine za jirani ni matakwa ya katiba uteuzi uzingatie sura ya kitaifa, ambao ndio huo uwiano? Nasi tufuate msingi huo? Au tupuuzie tu?

Karibuni
Teuzi anazofanya Mhe Rais Samia zina unafuu sana katika uwiano wa kijiografia, kijinsia nk kuliko zile za mtangulizi wake. Wanaozungumza udini ni fanatics tu, uongozi wa Mama umeonyesha religious neutrality kuliko wa mtangulizi wake, na hata approach yake katika mawasiliano ni neutral, kwa mfano ameachana na zile salamu za kidini alizokuwa anazitumia mtangulizi wake, akaja na ya kitaifa ya kusalimia kwa jina la Jamhuri. Hakuna ukanda kwenye uteuzi wake, mawaziri 5 kutoka Pwani wala si kitu, kwani baraza lina mawaziri wangapi? Na ataipendelea Pwani kwa lipi, mwenyewe ni Mzanzibari.
Katika kumbukumbu zangu kuna wakati mkoa wa Kilimanjaro wabunge wake 4 kati ya 6 walikuwa mawaziri, wakati huo Rais akiwa Mzee Ruksa. Mawaziri hao walikuwa Cleopa Msuya (Mwanga) waziri wa fedha, Basil Mramba (Rombo) waziri wa viwanda na biashara, Brig Muhiddin Kimario (Moshi Mjini) waziri wa mambo ya ndani na Charles Kileo (Hai) waziri ofisi ya waziri mkuu. Na wala haikusemwa kuwa ni upendeleo.
Nadhani inafaa Rais akiteua kwa kuzingatia weledi huku akihakikisha kuwa baraza lake lina sura ya kitaifa kwa kujumuisha maeneo tofauti ya nchi na jinsia, lakini sio lazima kila mkoa upate waziri. Suala la dini lina mtego, na ninapenda jinsi Mhe Samia anavyolinyamazia na kuwaacha watu wakaabudu kwa uhuru wao lakini wakiwa kazini wafanye kazi ya nchi, siyo ya dini.
 
Hujasema aangalie uwezo gani
Wakishabalance Hivyo watakuja Kusema Pia Raisi aangalie GPA kuanzia 4.8-5 hapo watakuja tena kusema kwamba wa Second lower nao waangaliwe, Akichukua PHD Holder watasema Wenye Masters na Degree waangaliwe etc; Kimsingi kuja kubalance ni ngumu maana kila mtu anatazama kwa angle yake.
 
Tumesikia malalamiko memgi juu ya baraza jipya la mawaziri la Rais Samia.
  • Kuna malalamiko ya kukosekana usawa wa jinsia, mawazir wanawake ni 36% na manaibu ni 20 tu
  • Kuna malalamiko ya kanda fulani kupendelewa, kama mkoa wa Pwani kuwa na mawaziri (na maanaibu) 5
  • Kuna malalamiko kuwa walioachwa wote ni Wakristo, ingawa kwa upande mwingine hivi sasa mawaziri na manaibu Wakristo ni 32 ukilinganisha na Waislamu 18 tu.
  • Pia yapo malalamiko kuwa watoto wa familia za viongozi wameendelea kuingizwa kwenye baraza, kama yalivyowasilishwa na Malisa GJ na Thabit Jacob aliyewataja kabisa watoto hao kuwa ni Nape Nnauye, Januari Makamba, Pinda, Mavunde, Ndejembi.
Maswali ya msingi:
1. Je Rais na mamlaka nyingine za uteuzi zizingatie uwiano wa makundi au la?
2. Pili, mamlaka zizingatie uwiano wa makundi ya aina gani? Jinsia, rika, dini, kanda, kabila nk?
3. Hali ikoje baraza hili na nini kifanyike?

Nimemsikia Godbless Lema akikosoa mambo ya kuangalia uwiano, amnbapo alitaka weledi tu uzingatiwe? Je iwe hivyo? Wakati tukijadili haya, tukumbuke kuwa wenzetu wa Kenya na baadhi ya nchi nyingine za jirani ni matakwa ya katiba uteuzi uzingatie sura ya kitaifa, ambao ndio huo uwiano? Nasi tufuate msingi huo? Au tupuuzie tu?

Karibuni

Huu ni ujinga kuendesha nchi kwa matabaka badala ya uwezo. Dini na ukabila unasaidia vipi kuendesha wizara kama viongozi wanafuata katiba?
 
mnazungumzia teuzi na wengine tunafikiria nchi kufanyiwa overhaul. Ushauri pekee ambao naweza kuutoa kwa Rais ni kujiuzuru.
 
Back
Top Bottom