TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Kigoma Mjini

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Kigoma Mjini

Hongereni sana ndugu wiston Mogha..
Kwa mipango mikakati imara na yenye kutoa taswira njema zaidi juu ya kesho kwa wakazi wa kigoma kupitia good implementation mechanism..
 
UTEKELEZAJI AHADI NAMBA 2
Kuboresha mazingira ya Biashara, kuondoa kero ya ushuru Kwa wafanyabiashara wadogo Kwa mujibu wa Sheria ndogo za Manispaa na kujenga Bandari(Jetty) mpya eneo la Forodha ya Ujiji ili kurudisha hadhi ya mji wa Ujiji, na Bandari ya Kibirizi."

[emoji115]Leo nimetembelea Kibirizi na nimekuta pamevunjwa tayari Kwa mradi wa jetty...
1477947227225.jpg
1477947236251.jpg
1477947247764.jpg
 
UTEKELEZAJI WA AHADI NAMBA 2
Ujenzi wa ukuta na maduka katika Kituo cha mabasi Masanga kuzunguka maeneo yote ya Kituo cha mabasi yaendayo mikoani na nje ya wilaya za kigoma. Hii itasaidia kurahisisha huduma za masoko na bidhaa kwa wasafiri na wakazi wa kata ya Gungu,katubuka,businde,kibirizi na mwanga kaskazini.
1477947510384.jpg
1477947520989.jpg
1477947530474.jpg
 
UTEKELEZAJI WA AHADI NAMBA 3.
Kuhamasisha na kusaidia urasimishaji wa vikundi. Diwani wa kata ya Rusimbi Ndugu Hamis Butije ameendesha semina ya mradi wa WEKEZA ambapo amekuwa akitoa elimu ya uwekezaji katika miradi ya kiuchumi ili jamii iweze kujikwamua kwenye lindi la umaskini. Katika picha ni Afisa Uvuvi wa manispaa ya kigoma ujiji Bw. Aziz Daudi akifundisha ufugaji bora wa samaki
1478153867708.jpg
1478153878094.jpg
1478153887124.jpg
1478153897062.jpg
1478153909882.jpg
1478153917466.jpg
. Pia diwani huyo leo ameendelea na mafunzo ya ujasiriamali kwa kikundi cha TUJIKOMBOE kilichopo mtaa wa Vamia. Mafunzo hayo yalihusu kilimo bora cha zao la muhogo na ufugaji bora wa kuku za asili.
1478154048201.jpg
1478154078457.jpg
1478154091812.jpg
1478154096894.jpg
 
UTEKELEZAJI WA AHADI NAMBA MOJA "kusafisha mji" na UTEKELEZAJI WA AHADI NAMBA 2 "Kuboresha mazingira ya biashara" Mwenyekiti wa mipango miji Ndg Butije akiwa pamoja na diwani wa mwanga kaskazini BABALEVO na maafisa wa afya wa manispaa ya kigoma ujiji wakishughulikia tatizo la kuzagaa kwa uchafu soko la Nazareth. Pamoja na kutoa semina elekezi kwa wananchi na wafanya biashara kuweka taka kwenye makontena husika. Watu wamekuwa wakiweka taka nje ya kontena au pembezoni mwa makontena husika. Babalevo Alisema;-Ndugu wananchi naomba niwakumbushe kuwa makontena hayo ni maalum kwa kuweka taka kisha magari yanakuja kuzibeba na kuzipeleka mahali palipotengwa kwa ajili ya kuzihifadhi au kuziteketeza. Napenda kuwaomba wananchi tuhifadhi taka katika makontena hayo ili kuleta tija kwa uwepo wa mradi huo
1478156531951.jpg
1478156598045.jpg
1478156647639.jpg
1478156674356.jpg
1478156687390.jpg
1478156708695.jpg
1478156716277.jpg
1478156749984.jpg
1478156766176.jpg
1478156775088.jpg
1478156780738.jpg
1478156813926.jpg
1478156823922.jpg
 
MWENDELEZO WA UTEKELEZAJI WA AHADI NAMBA 4. Kama tulivyoona awali mradi wa maji kigoma ujiji ulikuwa umesimama toka mwezi machi mwaka 2015 ambapo ndio ulipaswa kumalizika. Lakini kwa jitahada za mbunge tukaona mradi huo umeanza kutekelezwa. Mradi huu ulikuwa katika ahadi za mbunge na sasa umefikia hatua za mwisho na tulitegemea ungemalizika mwezi Disemba 2016 lakini mradi huo umeanza tena kusuasua.
BUNGENI LEO KAMA SWALI NAMBA.(46) Mheshimiwa Zitto Ruyagwa Kabwe ameuliza;-
Mradi wamaji wa manispaa ya kigoma unaogharimu zaidi shillingi billion 32 ambao unafadhiliwa na shirika la KFW la ujerumani na jumuiya ya ulaya ulipangwa kukamilika mwezi Machi 2015:
(a)Je, kwanini mradi huu umechelewa kukamilika kwa mujibu wa mkataba;
(b)Je, Serikali inachukua hatua gani dhidi ya mkandarasi kwa kuchelewa kukamilisha mradi huo.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Akajibu
Mheshimiwa Spika,naomba kujibu swali la mheshimiwa zitto Ruyagwa kabwe lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
MHESHIMIWA SPIKA, Mradi wa maji wa manispaa ya kigoma unagharimiwa na serikali kwa kushirikiana na umoja wa ulaya na serikali ya ujerumani kupitia benki ya maendeleo ya KFW kwa gharama ya Euro million 16.32 sawa na shillingi billion 39.13
MHESHIMIWA SPIKA, Ujenzi wa mradi huu unaotekelezwa na mkandarasi SPENCON SERVICES LTD ulianza mwezi machi 2013 na ulitarajiwa kukamilika mwezi machi 2015. Hata hivyo baada tu ya kuanza kwa ujenzi , mkandarasi alichelewa kupewa eneo la ujenzi kutokana na matatizo ya fidia. Hali hii ilisababisha mkandarasi kupewa nyongeza ya muda wa kazi hadi kufikia nwezi December,2015. Pia kubadilika kwa menejiment ya SPENCON SERVICES LTD na mtaji mdogo kifedha kumechangia kuchelewa kwa ukamilishaji wa mradi wa maji ambapo hadi kufikia mwezi Oktoba 2016 utekelezaji wa mradi ulikuwa umefikia wastani wa asilimia kubwa.
MHESHIMIWA SPIKA, Kwa kuzingatia masharti ya mkataba, Serikali imechukua hatua dhidi ya mkandarasi ikiwa ni pamoja na kumkata fidia (liquidated damages) ya Euro 1,632,315.27 sawa na billion 3.9 ambayo ni asilimia 10 ya mkataba kuanzia mwezi januari 2016. Vilevile mkandarasi ameagizwa kuongeza nguvu kazi, vifaa na pia kufanya kazi muda wa ziada zikiwemo siku za mapumziko pia mkandarasi ameandikiwa barua ya kumfahamisha kuwa Wizara imemuweka katika kundi la Non Performing Contractors na mamlaka zinazohusika za PPRA na CRB zimejulishwa.
MHESHIMIWA SPIKA, Kwa kuwa miundombinu ya msingi kama manteki amekwisha jenga,pampu zote ameleta, wananchi wa kigoma mjini wataanza kupata maji kuanzia mwezi April,2017.
KATIKA SWALI KA NYONGEZA
Zitto Kabwe ameuliza kuhusu kuweka solar pumps za kusukuma maji ili kupunguza gharama za uendeshaji na pia ameomba kuunganisha mji mdogo wa Mwandiga katika mradi huu wa maji wa manispaa ya kigoma ujiji. Tunashukuru kuutarifu Umma kuwa serikali imekubali kuwa itachukua ushauri wa mbunge wa kutumia umeme wa jua katika kusukuma maji ili kupunguza gharama na pia serikali imekubali kuunganisha mji wa Mwandiga kwenye mradi huu wa maji wa manispaa ya kigoma ujiji

1478253581096.jpg
 
UTEKELEZAJI WA AHADI NAMBA 4
Kuanzisha High School 2 na kuboresha shule za msingi.
Wanafunzi waliohitimu kidato cha nne 2015 katika shule zilizopo ndani ya manispaa ya kigoma ujiji na wamechaguliwa kujiunga kidato cha tano 2016. Walifika ofisi ya mkurugenzi kuchukua barua zao ambazo watazipeleka kwa wakuu wa shule walizochaguliwa ili waweze kuanza masomo yao ya kidato cha tano. Kwa mujibu wa barua iliyotolewa na manispaa kwenda kwa wakuu wa shule za sekondari ambapo nimefanikiwa kuona nakala yake inasema kuwa hatua hiyo imefuatia maamuzi ya halmashauri ya manispaa hiyo ya kuwalipia wanafunzi wake waliochaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano kwa mwaka 2016/2017. Barua inasema mwanafunzi atalipiwa 112,000 ikiwa ni ada ya mwaka,tahadhari,kitambulisho,taaluma,ulinzi,nembo na matibabu. Pia atalipiwa gharama ya vitabu kiasi cha 200,000 na kufanya jumla kuwa 32,000 kwa mwanafunzi mmoja kwa mwaka.
Pia kupitia usimamizi wa halmashuri ya manispaa ya kigoma ujiji kumekuwa na mafanikio ya kuanzisha shule mpya ya elimu ya juu ya sekondari kwa kuanzisha shule ya "BURONGE HIGH SCHOOL" iliopo kata ya Kibirizi iliopo chini ya Diwani Ruhomvya Yunus.

Chini ni picha zinazoonyesha majengo ya shule ya Buronge High School.
1478448070199.jpg
1478448092373.jpg
1478448100936.jpg
1478448116731.jpg
1478448140705.jpg
1478448208691.jpg
1478448210256.jpg
1478448219483.jpg
 

Attachments

  • 1478448147619.jpg
    1478448147619.jpg
    77.1 KB · Views: 82
Uzinduzi wa Bodi mpya ya Maji Manispaa ya Kigoma Ujiji umefanyika leo 14/11/2016 wajumbe wa bodi ya zamani, Mpya na Viongozi wa MANISPAA, Wilaya na MKOA walianza kwa kukagua mradi mpya wa MAJI unaoendelea matarijio ni kukamilika mwezi wa March 2017, Mradi huu ni mkombozi kwa wakazi wa MANISPAA ya kigoma UJIJI na wilaya za JIRANI unaotarajia kuzalisha Lita 42 mln kwa siku huku mahita ya MJI ni Lita 21mln kwa siku na kuwa na ziada ya Lita 21mln ambayo itatumiwa na wilaya zingine. Kwa sasa KUWASA huzalisha 12mln za maji na kuwa na upungufu wa Lita 9mln ambayo imekuwa nimatezo kwa wakazi wa KIGOMA waliojaaliwa na mwenyezimungu kuwa na Mito mingi na ziwa la pili lenye kina kirefu DUNIANI.
Pamoja na mradi huu wa MAJI SAFI pia unatekelezwa mradi wa MAJI TAKA eneo la kagera, Kupitia mradi huu upatikanaji wa Mbolea kwa wakulima itapatikana ambayo imekuwa ikitumiwa na mikoa mingine kama IRINGA hatahivyo bado miundombinu ya barabara kufika eneo hilo ni mibovu kupitia mradi huu maombi maalum ya Tsh 800 mln imeombwa kurekebisha urefu wa Km 3.

Hussein Ruhava
Mayor Kigoma Ujiji.
a8486e795430878ac935a6d731b5836a.jpg
1479194013847.jpg
1479194023534.jpg
1479194033763.jpg
 
UTEKELEZAJI WA AHADI NAMBA 1
Kata ya Mwanga Kusini chini ya diwani wa chama cha Mapinduzi Ndg Mussa Maulid akishirikiana na Mbunge Zitto Kabwe kwa ushirikiano wamefanikisha mradi wa barabara kwenye kata hio inayounganisha toka barabara kuu ya kigoma ujiji tokea mtaa wa maweni mpaka kilimahewa eneo la Awimo Bar nakuendelea moja kwa moja mpaka burega nakuunganisha katika barabara ya buzebazeba mpaka Bangwe. Barabara hio toka maweni ina madaraja madogo matano ambayo ni kwaajili ya wanaovuka kwa miguu na magari.
1479921650512.jpg
1479921660550.jpg
1479921679589.jpg
1479921690730.jpg
1479921702631.jpg
1479921715924.jpg
1479921723034.jpg
1479921736616.jpg
1479921745959.jpg
 
Wananchi WA Kigoma ujiji tunafurahia sana kazi zinazofanywa Na Halmashauri yetu Na Mbunge wetu.
Barabara hii itamaliza changamoto iliyokuwa inawapata wakazi WA mwanga
 
Nimelishuhudia kwa macho yangu kiukweli inatia faraja sana na Kigoma mpya tunaiona
 
UTEKELEZAJI WA AHADI NAMBA 1
Kata ya Mwanga Kusini chini ya diwani wa chama cha Mapinduzi Ndg Mussa Maulid akishirikiana na Mbunge Zitto Kabwe kwa ushirikiano wamefanikisha mradi wa barabara kwenye kata hio inayounganisha toka barabara kuu ya kigoma ujiji tokea mtaa wa maweni mpaka kilimahewa eneo la Awimo Bar nakuendelea moja kwa moja mpaka burega nakuunganisha katika barabara ya buzebazeba mpaka Bangwe. Barabara hio toka maweni ina madaraja madogo matano ambayo ni kwaajili ya wanaovuka kwa miguu na magari.View attachment 438572View attachment 438574View attachment 438575View attachment 438576View attachment 438578View attachment 438579View attachment 438581View attachment 438583View attachment 438584
Hizi barabara zitatusaidia sana sisi wa kilimahewa na kigoma kwa ujumla sio lazima tupite barabara kubwa
 
LEO KULIKUWA NA MASWALI KWA MHESHIMIWA MBUNGE NDUGU ZITTO KABWE NA KILA SWALI LIMEJIBIWA KWA MAHOJIANO YA VIDEO KAMA TUNAVYOONA HAPO CHINI ;-
 
2.Unazungumzia vipi mradi wa sanamu ya mgebuka kwa maana ya changamoto,mafanikio na matarajio.

 
3.Unazungumziaje utekekezaji wa elimu bure kwa kidato cha tano na sita katika manispaa ya kigoma ujiji
 
Back
Top Bottom