Wiston Mogha
Senior Member
- Feb 13, 2014
- 168
- 141
Karibu sana kigoma. Fursa za kuwekeza na biashara mbalimbali na nchi jirani kama congo na burundi zinabadilisha kabisa kipato cha watu kwasasa. Karibuni kigomaKigoma mko vizuri, naona mipango kazi yenu itaifanya Kigoma kuwa kama Dubai huko mbeleni.
Jukumu letu ni kuwaunga mkono kwenye mchakato huu wa maendeleoThread za maendeleo hazichangamkiwi kama zile za matukio hasa matukio hasi....Binafsi nimesoma kuanzia mwanzo na nimefurahi sana. Msichoke kutupa mrejesho wa yaendeleyayo. Zitto akiwekaga siasa cheap pembeni, yuko njema sana. Wananchi nawashauri kupokra haya positively na wajitoe zaidi maana Kigoma itajengwa na wakazi wake. Asante
Kesho baraza la ardhi la Manispaa linazinduliwaKigoma inapaswa kuwa jiji kuu ukanda wa magharibi ya Tanzania:
1.Nchi za DRC,Burundi na Rwanda wanaweza kuwa wanakuja na kupitia Kigoma kabla ya kwenda miji mingine ya Tanzania.
2.Nchi nilizozitaja hapo juu zinaweza kuwa wateja wa bidhaa za kilimo na viwanda,endapo Kigoma itatenga maeneo ya viwanda.
3.Kigoma inastahili kupewa uwanja wa ndege za kimataifa ili kuhudumia nchi jirani.
Tatizo la Kigoma,kila mwananchi ni mjuaji na ubishi,hali inayochangia migogoro ya ardhi isoyoisha.
Utatuzi wa ardhi:
Mji wote wa Kigoma na maeneo ya nje ya mji yapimwe kwa sattelite