SongambeleEN
Member
- Mar 23, 2013
- 25
- 12
Wanabodi,
Kwa kuwa wengi wetu tulidhubutu/tumedhubutu kuitathmini dhana hii ya ujasiriamali sambamba na kujitathmini binafsi juu ya njia sahihi zaidi za kufikia mafanikio ya kweli maishani. Tathmini ambayo ilitupelekea/imetupelekea, kudhubutu kufanya maamuzi sahihi ya kujiajiri wenyewe iwe ni katika mfumo ulio rasmi na ule usio rasmi.
Na kwa kuwa mikiki mikiki ya shughuli hizi za kujiajiri wenyewe zinategemea sana afya bora, nguvu, akili na ustahimilivu wa hali ya juu, sifa ambazo mwanadamu anaweza kupungukiwa kwa kadri siku zinavyokwenda mbele, au kadri anavyozeeka. Sasa basi kwa kuzingatia kuwa wajasiriamali wengi waliojiajiri wenyewe hawajajiunga katika mifuko ya hifadhi ya jamii, njia ambayo ingewawezesha kupata mafao pindi wanapozeeka au kupoteza uwezo wa kuzalisha.
Na kwa kuzingatia kuwa suala la uzee au kupoteza uwezo wa kufanya shughuli za uzalishaji ni mojawapo ya vitu ambavyo sisi kama wajasiriamali hatuna mamlaka navyo, (yaan kuamua visitokee au vinginevyo) isipokuwa tunaweza kuchagua mbinu za kukabiliana navyo. Na ni katika kuzitafuta mbinu za kukabiliana na hali hizo ndio tunajikuta na maswali kama haya;
Je wewe kama mjasiriamali una security katika shughuli zako?
Je security yako ni ya namna gani? Na inakidhi matakwa ya Dunia ya sasa?
Je kitatokea nini katika maisha yako pale utakapopoteza uwezo wa kuzalisha mali, iwe ni kwa kutokana na uzee au ajali?
Ikumbukwe kuwa, moja ya sababu kuu inayomfungamanisha mfanyakazi na ajira yake ni security ya ajira hiyo. Ni security hiyo ambayo inamuhakikishia mfanyakazi uhakika wa maisha yake, kitu ambacho kinaweza hata kumkosesha ujasiri wa wakuiacha ajira hiyo na kujiajiri mwenyewe. Sasa Je, mjasiriamali naye anaweza kuwa na security ya namna hiyo katika shughuli zake?
Kwa kuwa wengi wetu tulidhubutu/tumedhubutu kuitathmini dhana hii ya ujasiriamali sambamba na kujitathmini binafsi juu ya njia sahihi zaidi za kufikia mafanikio ya kweli maishani. Tathmini ambayo ilitupelekea/imetupelekea, kudhubutu kufanya maamuzi sahihi ya kujiajiri wenyewe iwe ni katika mfumo ulio rasmi na ule usio rasmi.
Na kwa kuwa mikiki mikiki ya shughuli hizi za kujiajiri wenyewe zinategemea sana afya bora, nguvu, akili na ustahimilivu wa hali ya juu, sifa ambazo mwanadamu anaweza kupungukiwa kwa kadri siku zinavyokwenda mbele, au kadri anavyozeeka. Sasa basi kwa kuzingatia kuwa wajasiriamali wengi waliojiajiri wenyewe hawajajiunga katika mifuko ya hifadhi ya jamii, njia ambayo ingewawezesha kupata mafao pindi wanapozeeka au kupoteza uwezo wa kuzalisha.
Na kwa kuzingatia kuwa suala la uzee au kupoteza uwezo wa kufanya shughuli za uzalishaji ni mojawapo ya vitu ambavyo sisi kama wajasiriamali hatuna mamlaka navyo, (yaan kuamua visitokee au vinginevyo) isipokuwa tunaweza kuchagua mbinu za kukabiliana navyo. Na ni katika kuzitafuta mbinu za kukabiliana na hali hizo ndio tunajikuta na maswali kama haya;
Je wewe kama mjasiriamali una security katika shughuli zako?
Je security yako ni ya namna gani? Na inakidhi matakwa ya Dunia ya sasa?
Je kitatokea nini katika maisha yako pale utakapopoteza uwezo wa kuzalisha mali, iwe ni kwa kutokana na uzee au ajali?
Ikumbukwe kuwa, moja ya sababu kuu inayomfungamanisha mfanyakazi na ajira yake ni security ya ajira hiyo. Ni security hiyo ambayo inamuhakikishia mfanyakazi uhakika wa maisha yake, kitu ambacho kinaweza hata kumkosesha ujasiri wa wakuiacha ajira hiyo na kujiajiri mwenyewe. Sasa Je, mjasiriamali naye anaweza kuwa na security ya namna hiyo katika shughuli zake?