BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Watoto wawili wamefariki dunia na mmoja kunusurika kifo, baada ya mama yao mzazi kuwapa sumu ambayo ni dawa aina ya Tiktik ya kuoshea mifugo, kisha na yeye kunywa.
Akizungumza leo Jumanne, Novemba 22,2022, Kamada wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Filemon Makungu amesema tukio hilo limetokea Novemba 20, 2022 saa tatu usiku, mtaa wa Shede, Manispaa ya Kigoma Ujiji.
Kamanda Makungu amesema mwanamke huyo Christina Akoonay (36), alikutwa amejifungia ndani ya nyumba anayoishi akiwa na watoto wake watatu hajitambui huku mtoto mmoja Daniel Deogratius (5),akiwa tayari amefariki dunia.
Kamanda Makungu amesema mwanamke huyo pamoja na watoto wake walikimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa Kigoma Maweni, kwaajili ya kupatiwa matibabu na wakati wakiendelea na matibabu mtoto mwingine David Deogratias (1), alifariki dunia.
Kamanda Makungu amesema mtoto aliyebakia ni Davina Deogratias ((7) na mama yake ambao wanaendelea na matibabu hospitalini hapo na kwamba jeshi hilo linamshikilia mwanamke huyo kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani.
Mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa Maweni, Dk Stanley Binagi amethibitisha kuwepo kwa vifo hivyo akisema familia hiyo ilikunywa sumu ambayo ni dawa ya kuua wadudu kwenye mifugona mimea inayoitwa Tiktik.
Binagi amesema mwanamke huyo amekunywa sumu hiyo akiwa ni mjamzito na kwamba sumu hiyo haijaweza kumuathiri mtoto aliyeko tumboni na hali yake imeanza kuwa nzuri baada ya kuzimia kwa muda mrefu akiwa hospitalini hapo.
MWANANCHI
Akizungumza leo Jumanne, Novemba 22,2022, Kamada wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Filemon Makungu amesema tukio hilo limetokea Novemba 20, 2022 saa tatu usiku, mtaa wa Shede, Manispaa ya Kigoma Ujiji.
Kamanda Makungu amesema mwanamke huyo Christina Akoonay (36), alikutwa amejifungia ndani ya nyumba anayoishi akiwa na watoto wake watatu hajitambui huku mtoto mmoja Daniel Deogratius (5),akiwa tayari amefariki dunia.
Kamanda Makungu amesema mwanamke huyo pamoja na watoto wake walikimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa Kigoma Maweni, kwaajili ya kupatiwa matibabu na wakati wakiendelea na matibabu mtoto mwingine David Deogratias (1), alifariki dunia.
Kamanda Makungu amesema mtoto aliyebakia ni Davina Deogratias ((7) na mama yake ambao wanaendelea na matibabu hospitalini hapo na kwamba jeshi hilo linamshikilia mwanamke huyo kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani.
Mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa Maweni, Dk Stanley Binagi amethibitisha kuwepo kwa vifo hivyo akisema familia hiyo ilikunywa sumu ambayo ni dawa ya kuua wadudu kwenye mifugona mimea inayoitwa Tiktik.
Binagi amesema mwanamke huyo amekunywa sumu hiyo akiwa ni mjamzito na kwamba sumu hiyo haijaweza kumuathiri mtoto aliyeko tumboni na hali yake imeanza kuwa nzuri baada ya kuzimia kwa muda mrefu akiwa hospitalini hapo.
MWANANCHI