Mjeshi aliyemchapa Trafiki,aenda nyea debe!

Mjeshi aliyemchapa Trafiki,aenda nyea debe!

Mpandafarasi

Member
Joined
Dec 7, 2008
Posts
57
Reaction score
11
Mjeshi aliyemchapa Trafiki,anyea debe!

Jeshi letu la Wannanchi (JWTZ), limenasa na kumtupa lupango Koplo Steven Sagana, kwa kuhusika na kosa la kuongoza kichapo kwa askari wa Usalama Barabarani, Sajini Thomas, juzi Dsm.

Koplo Sagana na wenzake walitenda shambulio hilo la kikatili kwenye mataa ya Ubungo...ambapo ni makutano ya barabara za Morogoro, Mandela....kwa madai ya kucheleweshwa na Trafiki huyo aliyekuwa akiongoza magari katika eneo.

Taarifa ilidodonshwa kwa vyombo vya mijinews na Kurugenzi ya Habari ya jesho hilo,ilisema kuwa jeshi hilo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi nchini limeunda timu ya pamoja kuchunguza na kubaini undani wa mazingira ya tukio hilo ili hatua stahiki zichukuliwe kwa wote waliohusika.

“Hatua za awali za kinidhamu zilizochukuliwa na JWTZ kufuatia tukio hilo baya ni pamoja na kumkamata na kumburuza ndani Koplo Steven Sagana wakati wakibainishwa wenzake waliohusika na tukio hilo,” ilisema taarifa ya JWTZ ambayo ilieleza kusikitishwa na kitendo hicho cha utovu wa nidhamu kilichofanywa na askari wake.

“Tunapenda kuwahakikishia wananchi kuwa JWTZ itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kudhibiti nidhamu ya wanajeshi wote, kuimarisha ushirikiano na vyombo vyote pamoja na wananchi kwa ujumla sambamba na kuwa tayari wakati wote kutekeleza jukumu la ulinzi wa taifa letu pamoja na majukumu mengine mbalimbali,” iliongeza taarifa ya Jeshi hilo.

Source: Darhotwire.com
 
Mjeshi aliyemchapa Trafiki,anyea debe!

Jeshi letu la Wannanchi (JWTZ), limenasa na kumtupa lupango Koplo Steven Sagana, kwa kuhusika na kosa la kuongoza kichapo kwa askari wa Usalama Barabarani, Sajini Thomas, juzi Dsm.

Koplo Sagana na wenzake walitenda shambulio hilo la kikatili kwenye mataa ya Ubungo...ambapo ni makutano ya barabara za Morogoro, Mandela....kwa madai ya kucheleweshwa na Trafiki huyo aliyekuwa akiongoza magari katika eneo.

Taarifa ilidodonshwa kwa vyombo vya mijinews na Kurugenzi ya Habari ya jesho hilo,ilisema kuwa jeshi hilo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi nchini limeunda timu ya pamoja kuchunguza na kubaini undani wa mazingira ya tukio hilo ili hatua stahiki zichukuliwe kwa wote waliohusika.

“Hatua za awali za kinidhamu zilizochukuliwa na JWTZ kufuatia tukio hilo baya ni pamoja na kumkamata na kumburuza ndani Koplo Steven Sagana wakati wakibainishwa wenzake waliohusika na tukio hilo,” ilisema taarifa ya JWTZ ambayo ilieleza kusikitishwa na kitendo hicho cha utovu wa nidhamu kilichofanywa na askari wake.

“Tunapenda kuwahakikishia wananchi kuwa JWTZ itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kudhibiti nidhamu ya wanajeshi wote, kuimarisha ushirikiano na vyombo vyote pamoja na wananchi kwa ujumla sambamba na kuwa tayari wakati wote kutekeleza jukumu la ulinzi wa taifa letu pamoja na majukumu mengine mbalimbali,” iliongeza taarifa ya Jeshi hilo.

Source: Darhotwire.com

Kutupwa lupango kwa Koplo Steven Sagana kumeonyesha wazi kuwa yeye ni kondoo wa muhanga kwani katika kulipuka kwa mabobu Mbagla mmoja wa mkubwa wa jeshi alisikika akisema kuwa wanajeshi wetu wana nidhamu panapokuwa na mkubwa wake basi huwa mdogo anasikiliza amri, na kwa kuthibitisha hayo hata katika ushahidi wa kesi ya mauwaji inayomkabili zombe na wenziwe. sasa kama palikuwa na mkubwa wao mwenye cheo cha Luteni Canal na akaweza kuwaondoa hao wanajeshi basi wazi wazi inaonekana kuwa walikuwa wakitekeleza amri ya mkubwa wao ambaye ni LUTENI CANAL. Sasa yeye ndiye anapaswa kuwekwa lupango kwanza kabla ya hata huyo Kondoo!!
 
For a foolish person like him, thats the best place he

deserves...!

Hiyo mambo ya kuwa MBUZI WA SADAKA yatafuatia

baadaye kama thread ingine.

But at least by now any dog has been locked up! Kudos!
 
Hii inavunja sheria ya natural justice na habeas corpus. Huwezi kumtupa mtu ndani kabla ya ku-prove mashtaka yake!! mnakuwa kama Guantanamo Bay bwana!
 
Sasa ku-prove mashtaka yake yapi tena? Si amempiga Traffic Officer watu wakiwa wanamuona???
 
For a foolish person like him, thats the best place he

deserves...!

Hiyo mambo ya kuwa MBUZI WA SADAKA yatafuatia

baadaye kama thread ingine.

But at least by now any dog has been locked up! Kudos!

..,..
He is not a fool but fooled by his superior!
According to military personnel,there is what they call SUPPORT your superior even though you disagree.These means you have to act immediately to the boss' order or even on his mood.
That Lt col must get his due share of what his subordinate did
 
Kinachofanyika ni usanii tu wa danganya toto, huyo Luteni Kanali ndiye alikuwa mkuu wa msafara, na alipaswa kukamatwa pamoja na wengine wengi. Walioshuhudia waliona wanajeshi wengi wakimchangia huyo Polisi, sasa kwanini akamatwe huyo Koplo mmoja tu?

Wakamatwe wote na washtakiwe Mahakama ya kiraia kwani walifanya kosa nje ya eneo la Jeshi.

Huyo Koplo anatolewa kama kafara tu. Hakuna lolote la maana lililofanyika so far.
 
Wakuu mie sina comments nyingi sana lakini siku hiyo mimi pia nilikuwa ubungo nikitokea mwenge kwenda kimara jioni. Sina hakika wajeshi wetu walikuwa wanatoka wapi kwenda wapi lakini honestly traffic aliyekuwepo alituboa maana alikuwa anaruhusu magari upande mmoja tu wa morogoro kwenda city centre na mjini kwenda morogoro. Wengine tulibaki zaidi ya nusu saa bila kuruhusiwa. Pia traffic huyo alionekana kutumia simu ya mkononi kusoma messages mbele ya watu waliokata tamaa ya kusimama na kusubiri. Mimi simhukumu yeyote lakini naomba haki itendeke kwa kuangalia pia mazingira, yawezekana maafande walichukua hatua kuingilia kati uzembe kama huu.
 
Si yule traffic mwembamba mrefu eti, yule anayependelea foreni ya kutoka kimara na kituo cha daladala ubungo au sio yeye.Kama ni yeye basi walimpiga kidogo wangetoa meno maana jamaa uwa anapendelea magari yanayotoka kimara/morogoro zaidi ya njia zote.Lakini nasikia madreva wa daladala huwa wanampatia kidogo halafu anaachia njia.Mtoeni meno wakati mwingine
 
Wakuu mie sina comments nyingi sana lakini siku hiyo mimi pia nilikuwa ubungo nikitokea mwenge kwenda kimara jioni. Sina hakika wajeshi wetu walikuwa wanatoka wapi kwenda wapi lakini honestly traffic aliyekuwepo alituboa maana alikuwa anaruhusu magari upande mmoja tu wa morogoro kwenda city centre na mjini kwenda morogoro. Wengine tulibaki zaidi ya nusu saa bila kuruhusiwa. Pia traffic huyo alionekana kutumia simu ya mkononi kusoma messages mbele ya watu waliokata tamaa ya kusimama na kusubiri. Mimi simhukumu yeyote lakini naomba haki itendeke kwa kuangalia pia mazingira, yawezekana maafande walichukua hatua kuingilia kati uzembe kama huu.

Huenda traffic alikuwa na shida lakini hekima na busara si kumshambulia kwa mateke na magumi hadharani! Zipo taratibu za kulalamikia swala kama hilo si ubabe walio utumia. Let them face it, kwanza wamezidi ubabe wao hata hupiga raia wasio na hatia mitaani!
 
Sasa ku-prove mashtaka yake yapi tena? Si amempiga Traffic Officer watu wakiwa wanamuona???

Sidhani kama unaelewa kitu kinaitwa natural justice mzee. Huruhusiwe kuweka mtu ndani bila kumsomea mashtaka. Sema bongo kwa sababu ya kuburuzwa ndo maana hamuwezi kuona hichi kitu. Mshatikiwa yeyeto (the accused) lazima apelekwe mahakamani kabla ya kuwekwa ndani. Polisi wanaruhusa ya kumshika kwa masaa tu. Kama hawatafungua mashtaka, basi ni sharti wamuachie huru!
 
Sidhani kama unaelewa kitu kinaitwa natural justice mzee. Huruhusiwe kuweka mtu ndani bila kumsomea mashtaka. Sema bongo kwa sababu ya kuburuzwa ndo maana hamuwezi kuona hichi kitu. Mshatikiwa yeyeto (the accused) lazima apelekwe mahakamani kabla ya kuwekwa ndani. Polisi wanaruhusa ya kumshika kwa masaa tu. Kama hawatafungua mashtaka, basi ni sharti wamuachie huru!


Mtu ameonwa kabisa anamchapa askari alafu wamwachie aende zake! Du! We kweli Mtoto.
 
Wabongo kwa kuunda kamati ndio wenyewe ndugu zangu. Ameshakamatwa na mashtaka yake yanafahamika kwanini tena tume au ndio kujitafunia tu
 
Mtu ameonwa kabisa anamchapa askari alafu wamwachie aende zake! Du! We kweli Mtoto.

We nawe ni nanga? Wewe umeshasikia kitu kinaitwa imprisonment without trial? hichi ndo chenyewe, ndo maana nikasema ni sawa na guantanomo bay. Hata kama watu millioni moja walimwona akitenda kosa, ni lazima mtu asomewe mashtaka kabla ya kutupwa jela! UNAELEWA HILO? Ndo maana kuna writ inaitwa habeas corpus. Katafute jinsi inavyotumika ndo utaelewa nina maana gani!
 
Back
Top Bottom