sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,407
- 19,264
Kwa kipindi kama cha miaka mitatu amekuwa akiwa na msimamo wa kutaka kufanyiwa mazshi kwa kuchomwa mauti yakimkuta
Sababu zake mpaka sasa hazijaniingia akilini, yeye hataki mwili wake uoze taratibu, sijui mambo ya mwili kutumika msukule, kuhofia kwamba ataamka akizikwa 😂 😂 n.k.
Familia yake ilikataa kwa hio kaja kwangu, kaniomba nimsaidie hio ishu na pia niende kupeperusha majivu yake kijijini sehemu aliyokuwa akiipenda utotoni.
Huduma hii ya mazishi natambua kwamba ipo hata hapa nchini, inaitwa cremation, lakini imezoeleka kwa kiasi kikubwa kutumika na wahindi wanaofata mila na tamaduni zao.
Kwa tamaduni zetu hizi za hapa kwetu na hata kwa dini, huu utaratibu haujazoeleka kiukweli, kwa hiyo hata mimi siwezi kumtekelezea anachotaka, pia hata familia yake nayo imekataa, sipendi kuanzisha taharuki.
Huwa nampaga tu sapoti ya kinafki 😁 maana ni mjomba tuliezoeana sana.
Je nimwambie ukweli kwamba sitaweza kutekeleza anachotaka au nimdanganye tu ili kumfurahisha ila kama kawaida maafa yakimkuta atazikwa tu kwa utaratibu wa kawaida.