Mkakati wa Chato kuwa mkoa wapingwa rasmi na RCC ya mkoa wa Kagera

Mkakati wa Chato kuwa mkoa wapingwa rasmi na RCC ya mkoa wa Kagera

Tatizo liko wapi? Tumejua kwamba RCC ya Kagera wamegoma, na kwamba askofu Bagonza ameunga mkono maamuzi ya RCC ila akaenda mbali kutupa faida ya kuwa na Halmashauri nyingi kuliko wilaya au mikoa. Jamani kuna zaidi ya hapo tena?? Mwisho na mimi nawaunga mkono RCC na baba askofu.
Tatizo halipo kwa RCC wala askofu Bangonza; ila tunajaribu ku-mchallenge mwanzisha uzi hakutupa muhitasari wa nini kimeazimiwa na Mkoa wa Kagera, instead kaja na mawazo ya mtu mmoja, jambo ambalo nalo ni sawa.

Henry Ford anasema, kila mmoja yuko sawa maadam anachofikiri ni sawa. Japo kwa mtazamo matokeo baadae huwa yanawatofautisha hao wawili kwa misingi ya fikra zao.
 
Anaandika Askofu Bagoza PhD.

TUNAHITAJI HALMASHAURI NYINGI KULIKO MIKOA NA WILAYA MPYA

Kamati ya Maendeleo ya Mkoa wa Kagera (RCC) imemaliza kujadili mapendekezo ya kuundwa kwa Mkoa mpya wa Chato. Wengi wanakataa mapendekezo hayo. Niliwaunga mkono mapema.

Natamani Taifa lihitimishe uundwaji wa MIKOA na Wilaya mpya. Badala yake, jopo la wataalam wa kada mbalimbali, wajikite katika kupendekeza uundwaji wa HALMASHAURI mpya. Kwa Nini tunahitaji zaidi HALMASHAURI kuliko MIKOA na Wilaya?

1. Masuala karibu yote ya Maendeleo yako TAMISEMI.

2. Halmashauri ni kitovu cha mamlaka ya wananchi kujipanga na kusimamia mambo yao.

3. Tuachane na "developmentalism" (U-maendeleo) na kuingia katika "transformation"(Mabadiliko).

4. Maendeleo endelevu hayahitaji "Uimra" (top to down) bali "uasi Mtakatifu" (bottom up). Ma RC na Ma DC ni alama za unyapara. Wanatupeleka mtoni lakini hawawezi kutulazimisha kunywa maji hata kama tuna kiu.

5. Inawezekana kuwa na Halmashauri hata 5 katika Wilaya moja wakati kwa mtindo wa sasa kuna hatari ya Wilaya 2 kugombania Halmashauri Moja.

6. Jopo la wataalam lizame kutafuta namna nyepesi ya wateule wa Rais kufanya kazi na wateule wa wananchi pasipo mgongano wala kutambiana. Siku hizi wateule wa Rais wanawanyanyasa wateule wa wananchi wakati Rais naye ni Mteule wa wananchi.

Ili haya yafanikiwe, semina elekezi zinatakiwa na zisiendeshwe na Rais. Wateule wengi wamejipa haki ya kumdanganya Rais kwa kusifia, kujipendekeza na kumhakikishia Rais kuwa anajua kila kitu.

Hatukuchagua malaika kuwa RAIS wetu. Na hatukuchagua RAIS ili ageuke malaika. Tunamnyima Rais fursa ya kunyenyekea.

KAZI IENDELEE
Naunga mkono hoja.
Mimi binafsi nilimuona Magufuli kama mtu mkatili na mbinafsi sana ambaye Tanzania hajawahi kutokea.

Akiwa Waziri wa Ujenzi wakati wa B Mkapa alibasidili ramani ya barabara isipite Biharamulo ila ikapita Chato. Alipokuwa Rais ametumia madaraka yake makubwa kupeleka Kijijini kwao Chato miundombinu mikubwa kama Airport, Referral hospital, TRA, CRDB na Mbuga ya Burigi kwa kutumia raslimali za taifa.

Chochote kinachofanyika kuhalalisha UBADHIRIFU wa Magufuli kwa kuifanya Chato kuwa Mkoa nakiita ni UHAYAWANI.

Ile miundombinu inabidi ibakie hivyo hivyo katika ngazi ya wilaya kama ilivyobakia Gbadolite ya Mobutu Seseseko. Tunataka watu wakibisha kuwa tulikuwa na Rais kichaa na mwizi tuwaonyeshe mfano halisi
 
Hoja ya ukabila kuhalalisha mkoa wa CHATO haina mashiko.

Tujiulize faida ya kuanzisha mkoa huo kwa Taifa ni nini?

Tusikurupukeee! Tujenge uchumi kwanza hayo ya mikoa na wilaya yatafuata.

Kuanzisha mkoa ni gharama kubwa sana! Mpaka leo tuna mikoa mipya kadhaa iliyoanzishwa kwa JAZBA za kisiasa haijaweza kusimama kikamilifu kuwa mikoa, mfano mingi bado ofisi za wakuu wa mikoa zimejiegesha kwenye majengo ya watu.

Nyumba za watumishi SHIDA! Huko hatujakamilisha mnataka kuanzisha mikoa mingine! Ni nani aliturogaaaaa?
 
Uwanja wa Chato vijana wa Subaru kutoka kaskazini wauchamgamkie, wautumia kwny 0-60, piga Sana ma-drift etc
 
Hoja ya ukabila kuhalalisha mkoa wa CHATO haina mashiko.
Tujiulize faida ya kuanzisha mkoa huo kwa Taifa ni nini?...
Shida ni justification za wasomi hasa wa kagera..ukisoma hata report ya RCC utachecka,, eti utagawanyisha koo na kabila,, harafu eti watapoteza wilaya zenye ardhi nzuri kwa mifugo na kilimo kama hizo wilaya mbili zitakuwa mkoa tofauti.

Lakini hoja nyingine ikasemwa kwa sbb huko Biharamulo na Ngara kunamadi nayaosaidia kuiedneleza Bukoba na kusema chato kama chato haijaendele kuwa mkoa kwani bado wilaya changa.

Ndo nikajiuliza je serikali ikisema iweke mkoa nyakanazi..Bukoba watashangilia ? wanaposema masuala ya ardhi..je haoa tanzania kunamtua anakatazwa kwenda kuchunga au kulima mkoa mwingine?

Suala la madini...je Geita ilupoundwa na kumegwa kutoka Mwanza..walo mbona walikubali kwanini hawa waone madini kuwa mkoa mwingine mpya ni shida..inamaana basi hata geita ivunjwe ili mkoa mama wa Mwanza ufaidi mapato ya madini kutoka wilayani Geita..Shida ni hoja zinazojengwa zinaonekana hazina mqshiko ..angalu wewe umeleta hoja ya msingi
 
Nyumbs za watumishi mbona huwa zinauzwa,wacha tuwe tunapanga
 
Back
Top Bottom