Mkanganyiko mkubwa bungeni: Wabunge wengine wanasema huu si mkataba, ni makubaliano ya awali tu, wengine wanasema ni msingi wa mikataba itakayofuata

Mkanganyiko mkubwa bungeni: Wabunge wengine wanasema huu si mkataba, ni makubaliano ya awali tu, wengine wanasema ni msingi wa mikataba itakayofuata

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Nafuatilia bunge live saa hii. Ninachokiona ni mkanganyiko mkubwa wa hoja juu ya suala la bandari na "mkataba" na kampuni ya Dubai ya DPW.

Nimegungua kuwa upo mkanganyiko mkubwa kati ya wabunge, huku wengine wakisema haya ni makubaliano ya awali kuhusu mikataba itakayofuata.

Wapo wanaosema kuwa huu sio uwekezaji, wala ubia bali ni makubaliano ya ushirikiano kati ya Tz na Dubai.

Wengine wanasema document hii ni kuhusu mambo makuu matatu; uendeshaji, endelezaji na uboreshaji na sio uwekezaji.

Wengine wanasema huu ni mkataba msingi, juu yake itafuata mikataba katika specific areas. Tusiwe na hofu mikataba itakuja.

Wabunge wengine wanasema "makubaliano" haya yana kikomo cha muda, wengine wanasema hakuna haja ya kuwa na ukomo wa muda kwani mikataba itakayofuata ndio itaonesha ukomo wa mikataba.

Naogopa kuwa wabunge wetu bado hawajui vizuri kinachoendelea kuhusu suala la bandari. Kama "mkataba mama" hautakuwa na misingi mizuri basi tujue kuwa mikataba yote itakayofuata ambayo itajengwa juu wa mkataba msingi wa sasa, haitakuwa na msingi sahihi na kuna uwezekano mkubwa kuwa tukapigwa.

Kwa bahati mbaya leo nimegundua kuwa wabunge wetu walio wengi hawana uelewa mzuri wa mambo na kuna uwezekano mkubwa wa kuisaliti nchi bila hata kujua kutokana na ujinga wa wawakilishi wetu.

TUSISAHAU KUWA IWE NI MKATABA, MAKUBALIANO, MARIDHIANO, ETC, YOTE YANA NGUVU YA KUFUNGA (BINDING FORCE) NA NI HATARI KWETU ENDAPO KUNA VIFUNGU VISIVYOELEWEKA VIZURI.

Wataalamu wetu fafanueni na wekeni wazi mambo haya kwa watanzania.
 
Tuna shida kubwa sana,kama wabunge wetu wapo hivi je umma wa watanzania ukoje?
 
HIVI TANZANIA TUNA WABUMGE KWELI.!!!!!

MBONA NAONA WENGI WAO NI VILAZA.

WAJINGA TUMEWAPA BUNGE VILAZA.
 
hio mikanganyiko ni kwa ajili ya kuchafua maji tu, wazungu wanaita muddying the water, yaani kutia maji matope ili watu wasione ndani kuna nini.
Ilivyo ni hivi huu Khasa ndio mkataba wenyewe, na hii kupelekwa bungeni ni moja ya masharti wadubai wameweka kuwa lazima mkataba huu upitishwe na bunge ili uwe na mizizi ya kimataifa, ili utambulike kimataifa, baada ya kupitishwa na bunge yanayofata yote ni utekelezaji wa mkataba tu hakuna jengine.
Hii njia ya kupitisha mkataba bungeni ni kufuli kubwa sana kisheria za kimataifa, ukikomea kufuli hapo wadubai wanachukua funguo wanaondoka,mnaachwa mpigishane kelele na mpumbazane kisiasa tu watu wanazo funguo
 
Makubaliano yeyote yanayoingiwa kimkataba huambatana na vifungu mbalimbali vyenye masharti yanayokwenda kufungwa kisheria. Makubaliano ya Awali, "Memorandum of Understanding (MoU)" ni hatua ya awali kabla ya kuingia makubaliano rasmi ya kimkataba, hivyo huweka wazi vifungu mbalimbali vitakavyobana kisheria wahusika pindi mkataba husika utakapopitishwa, kuridhiwa, na hatimaye kutiwa saini.

Endapo mkataba ukipita pande zote zinazohusika kwenye mkataba zina haki za dhamana kuendana na masharti ya kisheria yaliyopo ndani yake. Lakini katika hatua ya awali ya MoU wahusika hawafungwi na haki za dhamana. Hivyo basi makubaliano haya ya awali yanawekwa kama dokezo tu la kile ambacho kitakwenda kufungwa kisheria endapo mkataba utapita, kuridhiwa, na hatimaye kusainiwa na pande husika.

Katika hatua hii ya kuridhiwa kwa MoU, bado kuna nafasi ya kurekebisha mapungufu ambayo wananchi wanayalalamikia. Serikali ni lazima ikubali "constructive criticisms" zote zinazotolewa na wananchi, ili iweze kuuboresha mkataba ambao inakwenda kujifunga nao kidhamana. Ni kweli, wabunge wa CCM wamepata fursa ya kujadili na kuridhia kuhusu MoU hii, kwa kuwa wamepata fursa hiyo.

Lakini pia wasijitoe ufahamu kuwa wao pekee ndiyo wenye haki miliki na watu wengine hawana ufahamu wa kina. Wanapaswa kutambua kuna watu wengine wengi ambao ni wakweli, wazalendo, mahiri, wataalamu, na wenye weledi mkubwa kuhusu mikataba ya kimataifa. Ni aibu kwao kutoa lugha za vitisho pale wawapo pekee ndani ya Bunge, na kujibu hoja zilizotolewa nje ya Bunge zenye kupingana na msimamo wao wa kichama.

Wasijifanye kuwa wao pekee ndiyo wenye uelewa, na pia wenye kustahili kuridhia MoU hii kati ya serikali za Dubai na Tanzania kuhusiana na sakata hili la ubinafsishaji wa bandari y(z)etu! Suala kuhusu muda wa mkataba ni vyema lijadiliwe kwa uwazi kabla ya mkataba rasmi kufungwa, ili kuondoa ukakasi na sintofahamu iliyopo hivi sasa.
 
Nafuatilia bunge live saa hii. Ninachokiona ni mkanganyiko mkubwa wa hoja juu ya suala la bandari na "mkataba" na kampuni ya Dubai ya DPW.

Nimegungua kuwa upo mkanganyiko mkubwa kati ya wabunge, huku wengine wakisema haya ni makubaliano ya awali kuhusu mikataba itakayofuata.

Wapo wanaosema kuwa huu sio uwekezaji, wala ubia bali ni makubaliano ya ushirikiano kati ya Tz na Dubai.

Wengine wanasema document hii ni kuhusu mambo makuu matatu; uendeshaji, endelezaji na uboreshaji na sio uwekezaji.

Wengine wanasema huu ni mkataba msingi, juu yake itafuata mikataba katika specific areas. Tusiwe na hofu mikataba itakuja.

Wabunge wengine wanasema "makubaliano" haya yana kikomo cha muda, wengine wanasema hakuna haja ya kuwa na ukomo wa muda kwani mikataba itakayofuata ndio itaonesha ukomo wa mikataba.

Naogopa kuwa wabunge wetu bado hawajui vizuri kinachoendelea kuhusu suala la bandari. Kama "mkataba mama" hautakuwa na misingi mizuri basi tujue kuwa mikataba yote itakayofuata ambayo itajengwa juu wa mkataba msingi wa sasa, haitakuwa na msingi sahihi na kuna uwezekano mkubwa kuwa tukapigwa.

Kwa bahati mbaya leo nimegundua kuwa wabunge wetu walio wengi hawana uelewa mzuri wa mambo na kuna uwezekano mkubwa wa kuisaliti nchi bila hata kujua kutokana na ujinga wa wawakilishi wetu.

TUSISAHAU KUWA IWE NI MKATABA, MAKUBALIANO, MARIDHIANO, ETC, YOTE YANA NGUVU YA KUFUNGA (BINDING FORCE) NA NI HATARI KWETU ENDAPO KUNA VIFUNGU VISIVYOELEWEKA VIZURI.

Wataalamu wetu fafanueni na wekeni wazi mambo haya kwa watanzania.
Hata wao walikuwa wanachingia wasichoelewa na spika hawasahishi lakini kwa mdee akamsahisha
 
Back
Top Bottom