Ukiingalia katiba ya Tanzania, ni kama vile ilifikiriwa kuwa wakati wote Rais atakuwa Mtanganyika.
Tanganyika iliungana na Zanzibar kwenye mambo machache, nadhani wakati ule yalikuwa 17 tu.
Hayo mambo 17 pekee ndiyo yalikuwa chini ya Serikali ya JMT. Mambo hayo yalikuwa ni pamoja na Ulinzi, Mambo ya ndani, Uhusiano wa Kimataifa, Sarafu, Elimu ya juu, n.k.
Mambo yaliyobakia kama vile Afya, Elimu, Utamaduni, Kilimo, Biashara, yalibakia kuwa chini serikali za maeneo (Tanganyika na Zanzibar). Mambo haya kwa upande wa Zanzibar yangesimamiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya Rais wa Zanzibar. Na kwa upande wa Tanganyika, yangesimamiwa na Serikali ya JMT chini ya Rais wa JMT. Kwa mantiki hiyo, ni kwamba kuna wakati Rais wa JMT anakuwa Rais wa nchi ya Tanzania (anaposimamia utekelezaji wa yale mambo ya Muungano), na kuna wakati anakuwa Rais wa Tanganyika (anapotekeleza mambo yale ya Tanganyika yasiyo chini ya Muungano).
Mambo ya Kufikirisha:
1) Kila raia wa Zanzibar ni raia wa Tanzania
2) Siyo kila raia wa Tanzania ni raia wa Zanzibar.
3) Kila raia wa Zanzibar na Tanganyika ana haki ya kushika uongozi au kuwa mtumishi kwenye taasisi zinazosimamia mambo yale ya Muungano.
?? Jana nimesikia kuwa eti Rais wa JMT ameagiza serikali ya JMT inunue CT scan machines kwaajili ya hospitali zote za mikoa ya bara na visiwani. Ina maana suala la Afya, nalo limeingizwa kwenye mambo ya muungano? Au mkanganyiko wa katiba unamfanya Rais akose kutambua mipaka ya mamlaka ya Rais wa JMT kwenye mambo yasiyo ya muungano?
JUMUISHO
Kuna wakati Rais wa JMT anafanya kazi kama Mkuu wa nchi ya JMT (wakati huo anasimamia yale mambo ya Muungano tu) na kuna wakati anafanya kazi kama Rais wa Tanganyika (anasimamia mambo yale yasiyo ya Muungano).
SWALI
Raia wa Zanzibar, ambaye siyo raia wa Tanganyika, anakuwa na uhalali gani kuwa Rais wa Tanganyika (ili kusimamia mambo yale yasiyo ya muungano)? Au Mwalimu Nyerere alidhani wakati wote, Rais wa JMT atatoka bara tu?
Waliosema katiba ina mkanganyiko, naona wapo sahihi sana. Na aliyesema Tanganyika imejivika koti la muungano, naye yupo sahihi.
KATIBA MPYA YENYE UFAFANUZI SAHIHI NA WENYE MANTIKI HAIIEPUKIKI.
Tanganyika iliungana na Zanzibar kwenye mambo machache, nadhani wakati ule yalikuwa 17 tu.
Hayo mambo 17 pekee ndiyo yalikuwa chini ya Serikali ya JMT. Mambo hayo yalikuwa ni pamoja na Ulinzi, Mambo ya ndani, Uhusiano wa Kimataifa, Sarafu, Elimu ya juu, n.k.
Mambo yaliyobakia kama vile Afya, Elimu, Utamaduni, Kilimo, Biashara, yalibakia kuwa chini serikali za maeneo (Tanganyika na Zanzibar). Mambo haya kwa upande wa Zanzibar yangesimamiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya Rais wa Zanzibar. Na kwa upande wa Tanganyika, yangesimamiwa na Serikali ya JMT chini ya Rais wa JMT. Kwa mantiki hiyo, ni kwamba kuna wakati Rais wa JMT anakuwa Rais wa nchi ya Tanzania (anaposimamia utekelezaji wa yale mambo ya Muungano), na kuna wakati anakuwa Rais wa Tanganyika (anapotekeleza mambo yale ya Tanganyika yasiyo chini ya Muungano).
Mambo ya Kufikirisha:
1) Kila raia wa Zanzibar ni raia wa Tanzania
2) Siyo kila raia wa Tanzania ni raia wa Zanzibar.
3) Kila raia wa Zanzibar na Tanganyika ana haki ya kushika uongozi au kuwa mtumishi kwenye taasisi zinazosimamia mambo yale ya Muungano.
?? Jana nimesikia kuwa eti Rais wa JMT ameagiza serikali ya JMT inunue CT scan machines kwaajili ya hospitali zote za mikoa ya bara na visiwani. Ina maana suala la Afya, nalo limeingizwa kwenye mambo ya muungano? Au mkanganyiko wa katiba unamfanya Rais akose kutambua mipaka ya mamlaka ya Rais wa JMT kwenye mambo yasiyo ya muungano?
JUMUISHO
Kuna wakati Rais wa JMT anafanya kazi kama Mkuu wa nchi ya JMT (wakati huo anasimamia yale mambo ya Muungano tu) na kuna wakati anafanya kazi kama Rais wa Tanganyika (anasimamia mambo yale yasiyo ya Muungano).
SWALI
Raia wa Zanzibar, ambaye siyo raia wa Tanganyika, anakuwa na uhalali gani kuwa Rais wa Tanganyika (ili kusimamia mambo yale yasiyo ya muungano)? Au Mwalimu Nyerere alidhani wakati wote, Rais wa JMT atatoka bara tu?
Waliosema katiba ina mkanganyiko, naona wapo sahihi sana. Na aliyesema Tanganyika imejivika koti la muungano, naye yupo sahihi.
KATIBA MPYA YENYE UFAFANUZI SAHIHI NA WENYE MANTIKI HAIIEPUKIKI.