Mkanganyiko wa matamko (Wizara na Polisi) kuhusu kung’olewa viti na fujo za Uwanja wa Mkapa

Mkanganyiko wa matamko (Wizara na Polisi) kuhusu kung’olewa viti na fujo za Uwanja wa Mkapa

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu,

Fujo zilizoibuka katika Uwanja wa Benjamin Mkapa wakati wa mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Simba SC na CS Sfaxien zimeibua mkanganyiko kuhusu uwajibikaji.

Jeshi la Polisi lilibainisha kuwa mashabiki wa CS Sfaxien walihusika moja kwa moja kung’oa viti 256 na kuanzisha vurugu baada ya kutoridhishwa na maamuzi ya mwamuzi wa kuongeza dakika saba za nyongeza, zilizoiwezesha Simba SC kupata goli la ushindi.
IMG_1667.jpeg

Hata hivyo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Waziri Prof. Palamagamba Kabudi imeelekeza Simba SC na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kubeba gharama za uharibifu huo.
IMG_1666.jpeg

Hatua hii imeibua maswali kwani haijaeleza wazi uhusiano wa Simba SC na vitendo vya uharibifu vilivyofanywa na mashabiki wa timu pinzani na iweje matamko yapishane?

Pia, Soma:

Simba yatakiwa kulipa gharama viti kung'olewa kwa Mkapa

Jeshi la Polisi latoa tamko baada ya mashabiki wa Simba kuvunja viti Uwanja wa Taifa
 
Hata hivyo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Waziri Prof. Palamagamba Kabudi imeelekeza Simba SC na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kubeba gharama za uharibifu huo
Ni sahihi Simba walipe gharama zote na wasiruhusiwe tena kuchezea uwanja huo maana hii ni mara ya pili wanafanya hivyo
 
Jeshi la polisi inamaana sisi hatuna macho au? Mnafikiri tulikua hatuoni kwenye TV?
 
Mkuu wizara wako sahihi kuwadai tff na Simba hata kama hawajafanya uharibifu wao coz wanawadai walio wakabidhi kiwanja sasa Simba na tff watajua wanalipa vipi au watatafuta namna ya kuwapata waliofanya uharibifu



Usitegemee umwazime mtu kitu halafu kiibiwe halafu mwenye Mali akamdai mwizi aliyeiba mwenye Mali anakujua wewe alokuazima mengine utajua wewe unatatua vp hyo changamoto
 
Mkuu wizara wako sahihi kuwadai tff na Simba hata kama hawajafanya uharibifu wao coz wanawadai walio wakabidhi kiwanja sasa Simba na tff watajua wanalipa vipi au watatafuta namna ya kuwapata waliofanya uharibifu



Usitegemee umwazime mtu kitu halafu kiibiwe halafu mwenye Mali akamdai mwizi aliyeiba mwenye Mali anakujua wewe alokuazima mengine utajua wewe unatatua vp hyo changamoto
Walipe kila gharama tena ikiwezekana walipishwe mara 2 ili next time iume zaidi
 
Wakuu,

Fujo zilizoibuka katika Uwanja wa Benjamin Mkapa wakati wa mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Simba SC na CS Sfaxien zimeibua mkanganyiko kuhusu uwajibikaji.

Jeshi la Polisi lilibainisha kuwa mashabiki wa CS Sfaxien walihusika moja kwa moja kung’oa viti 256 na kuanzisha vurugu baada ya kutoridhishwa na maamuzi ya mwamuzi wa kuongeza dakika saba za nyongeza, zilizoiwezesha Simba SC kupata goli la ushindi.
View attachment 3177861
Hata hivyo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Waziri Prof. Palamagamba Kabudi imeelekeza Simba SC na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kubeba gharama za uharibifu huo.
View attachment 3177862
Hatua hii imeibua maswali kwani haijaeleza wazi uhusiano wa Simba SC na vitendo vya uharibifu vilivyofanywa na mashabiki wa timu pinzani na iweje matamko yapishane?
1: polisi
Hutafuta vyanzo vya tulio kujua vinasaba mpk tukio kutokea hivyo wao wameona kua bila mpinzani wa simba kutoanzisha fuji wa simba wasingefanya hivyo.
2: Wizara
Mwenyeji wa mchezo jana alikua simba na ndio anamiliki or ndio mwenye dhamana ya kulinda uwanja mpk mpira uishe hio ndio haki nawapo sahihi.
NB:
Kuna kosa hua linafanywa siku zote na vyombo vya ulinzi pale taifa,wanakuwepo lkn wanachukulia mambo Poa sana,Kwa game za kimataifa kuzunguka eneo waliokaa wapinzani polisi walitakiwa kulizunguka eneo lile kwakua always waarabu ni maji ya moto muda wwt wanakiwasha so ilitakiwa kuwe na ulinzi madhubuti eneo lile,mpk wanakuja kutuliza ghasia uharibifu ulikua umefanyika muda mrefu sana
 
Huu uwanja si uko ktk matengenezo na ulitengewa 31 billion katika bajeti iliyopita,na mpk sasa imekarabatiwa sehemu ya pitch na kukimbilia,jukwaani pamoja na viti vyake bado hakujaguswa....sasa hizo hela zikilipwa zitaenda kununua vipi tena?
 
Ni sahihi Simba walipe gharama zote na wasiruhusiwe tena kuchezea uwanja huo maana hii ni mara ya pili wanafanya hivyo
Kulipa si tatizo, kipi ni chanzo cha hizo vurugu mkuu. Mashabiki sio vichaa waanze kung’oa viti tu. Hakuna fujo bila sababu
 
Wakuu,

Fujo zilizoibuka katika Uwanja wa Benjamin Mkapa wakati wa mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Simba SC na CS Sfaxien zimeibua mkanganyiko kuhusu uwajibikaji.

Jeshi la Polisi lilibainisha kuwa mashabiki wa CS Sfaxien walihusika moja kwa moja kung’oa viti 256 na kuanzisha vurugu baada ya kutoridhishwa na maamuzi ya mwamuzi wa kuongeza dakika saba za nyongeza, zilizoiwezesha Simba SC kupata goli la ushindi.
View attachment 3177861
Hata hivyo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Waziri Prof. Palamagamba Kabudi imeelekeza Simba SC na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kubeba gharama za uharibifu huo.
View attachment 3177862
Hatua hii imeibua maswali kwani haijaeleza wazi uhusiano wa Simba SC na vitendo vya uharibifu vilivyofanywa na mashabiki wa timu pinzani na iweje matamko yapishane?

Pia, Soma:

Simba yatakiwa kulipa gharama viti kung'olewa kwa Mkapa

Jeshi la Polisi latoa tamko baada ya mashabiki wa Simba kuvunja viti Uwanja wa Taifa
Hakuna mkanganyiko hapo ni swala la mtizamo tu.uwanja una CCTV camera hivyo msipaniki mbivu na mbichi zitajulikana tu
 
Huu uwanja si uko ktk matengenezo na ulitengewa 31 billion katika bajeti iliyopita,na mpk sasa imekarabatiwa sehemu ya pitch na kukimbilia,jukwaani pamoja na viti vyake bado hakujaguswa....sasa hizo hela zikilipwa zitaenda kununua vipi tena?
😂😂 unataka kusemaje mkuu? Kwamba wamewasaidia kuviondoa?
 
Back
Top Bottom