Mkanganyiko wa umri wa Mtoto na umri wa kuolewa Kisheria

Mkanganyiko wa umri wa Mtoto na umri wa kuolewa Kisheria

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
1611048263164.png

Kwa mujibu wa kifungu namba 4 (1) ya Sheria ya Mtoto inaeleza Mtoto ni mtu yeyote aliye chini ya miaka kumi na nane (18)

Lakini Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 katika kifungu cha 13 kinaruhusu Mtoto wa kike kuozwa akiwa na umri wa miaka 14.

Hivyo Sheria hizi mbili zinakinzana na kusababisha harakati za kulinda ustawi wa Mtoto wa Kike kuzorota

Wataalamu wa Afya wanaeleza kuwa Msichana akiwa na umri wa chini ya miaka 18 anakuwa hajapevuka kiakili au kukomaa sawa sawa via vyake vya uzazi.
 
Upvote 0
Unaruhusiwa kumuoa akiwa na miaka 14 ila haurusiwi kufanya naye tendo la ndoa mpaka afikishe miaka 18, kabla ya umri huo ukifanya naye sex utafunguliwa kesi ya ubakaji japo ni mke wako halali wa ndoa
 
Unaruhusiwa kumuoa akiwa na miaka 14 ila haurusiwi kufanya naye tendo la ndoa mpaka afikishe miaka 18, kabla ya umri huo ukifanya naye sex utafunguliwa kesi ya ubakaji japo ni mke wako halali wa ndoa
Sasa hao wanaozaa kabla ya kufika miaka 18 hua hawafanyi tendo la ndoa?
Ni wangapi wapo jela kwa hilo?
Sheria hii ni tata
Mbona haisemi kuhusu wavulana
 

Kwa mujibu wa kifungu namba 4 (1) ya Sheria ya Mtoto inaeleza Mtoto ni mtu yeyote aliye chini ya miaka kumi na nane (18)

Lakini Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 katika kifungu cha 13 kinaruhusu Mtoto wa kike kuozwa akiwa na umri wa miaka 14.

Hivyo Sheria hizi mbili zinakinzana na kusababisha harakati za kulinda ustawi wa Mtoto wa Kike kuzorota

Wataalamu wa Afya wanaeleza kuwa Msichana akiwa na umri wa chini ya miaka 18 anakuwa hajapevuka kiakili au kukomaa sawa sawa via vyake vya uzazi.
Hiyo sheria ya mtoto ni ya mwaka gani? Ukinzani huo lazima utakuwa unatokana na kukosa umakini kwa waandaa miswada na wapitisha sheria. Pia kutokushirikisha wanachi walio wengi kwenye utungaji wa sera na sheria.
 
Sasa hao wanaozaa kabla ya kufika miaka 18 hua hawafanyi tendo la ndoa?
Ni wangapi wapo jela kwa hilo?
Sheria hii ni tata
Mbona haisemi kuhusu wavulana
Hapa suala nafikiri ni ubebaji mimba na kujifungua, na sio tendo la ndoa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom