Ninakumbuka Marehemu Mwalimu J.K. Nyerere ndiye alileta msamiati wa neno "hodhi" (monopoly), "kuhodhi" (monopolization). Lakini pia baadhi ya maneno aliyatoa kwenye kizanaki kwa mfani neno Mkurugenzi (Director).
sio kizanaki tu, yapo maneno kayatoa hata katika lugha zingine Mfano BUNGE amelitoa toka kibarbaig BUNG'EED/BUNG'EDA likimaanisha mkutano wa viongozi wa kijamii wakiwakilisha watu wao.
Historia yake
Ilianzishwa mnamo mwaka 1930 kama Inter-territorial Language (Swahili) committee ya Nchi za Afrika ya Mashariki, baadaye ikaitwa Kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki. Mnamo mwaka 1964 kamati ilifanywa kuwa Sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaamu. Baadaye ikaitwa Chuo cha Uchunguzi wa Lugha ya Kiswahili. Tangu 1970 kimepewa jina la Taasisi ya Uchunguzi wa Lugha ya Kiswahili.