raphael andrew
JF-Expert Member
- Aug 27, 2017
- 817
- 938
Story imekua boring hivi [emoji52]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Japo sifahamu hii Stori ,Ila naona huyu Rojas ataharibu tuRojas amejaliwa roho nzuri ila akili kichwani hakujaliwa.
Endelea kuifatilia kuna mafundisho makubwa.Japo sifahamu hii Stori ,Ila naona huyu Rojas ataharibu tu
Asante sana nishafika! Huyu Rojaz huyu Rojaz [emoji16],Ulweso ukuje,
Najaribu tuOyaa, hongera Sana mkuu, we ni hatari kwenye maandishi
Kitu kipya hewani nduguShukrani kwa utu na utulivu,nitag ukileta vitu mkuu plz
SaluteEndelea kuifatilia kuna mafundisho makubwa.
Usijali na pale patakapokuwa na story yoyote yenye kuvutia kweli ndugu yenu sitakuwa mchoyo tutashea ktk jukwaa hili,kikubwa uzima na nguvu na muda tu,mbarikiwe wasomaji wangu wote!Mkuu shukrani sana kwa kutuletea hii story hakika inasisimua , sikubahatika kuisikiliza. Hii ndio first time kwangu na nimeielewa
Ndugu yangu Fei 😂😂😂 pole sana najua kiu imekuwa kubwa ila nakuahidi utakapofumbua jicho asubuhi ya kesho kitu kitakuwa mtamboni
Halali mtu Niko machoNdugu yangu Fei [emoji23][emoji23][emoji23] pole sana najua kiu imekuwa kubwa ila nakuahidi utakapofumbua jicho asubuhi ya kesho kitu kitakuwa mtamboni
Kweli pata pesa tukujue tabia zako.Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha sitasahau cha radio free africa
Sehemu ya 8
Ahadi ambayo nilimuahidi huyu kaka ambaye nilikutana nae gerezani nakunifanyia yote haya sijaitimiza bado yaani kama kungekuwa na mtu angekuwa anaijua hii stori angeniuliza kwanini hadi muda huu sijaenda gerezani kwa mtu aliyenipa mwongozo kuhusu hizi pesa,yaani kwanini naanza kufanya kinyume na makubaliano tuliyoyafanya,kiukweli nilikuwa sina jibu,mipango ikaanza kuwa mingi sana yaani kila ninachofikiria kufanya naona sahihi,kila nikiwaza naona hiki ni bora zaidi ya kile kwa sababu sijawahi kuwaza katika maisha yangu kama naweza kukutana na pesa nyingi kiasi hiki,pengine ningewahi kuwaza ningelishakuwa na mipango thabiti lakini kwa sababu nilikuwa na fight for food yaani maisha ya kupambana kwa ajili ya tumbo tu yaani siku nenda siku rudi na sasa nimepata pesa,nikajiwazia hivi kula ni nini yaani kwa pesa niliyokuwa nazo hizi ni za kwenda kufanya vitu vikubwa sana na wala si za kuwaza tena kuhusu kula,nikajikuta nawauliza watu "hivi kwa mfano ukipata pesa nyingi unaweza kufanya kitu gani?" Kila mmoja ana mawazo yake wengine wanasema "nitajenga nyumba nyingi sana na nitapangisha huku mwenyewe nikiwa nimekaa tu nakula kodi" yaani mawazo ni mengi nawezaje kufanya kiukweli akili ilikuwa inawaka moto.
Katika harakati hizi nakumbuka sana siku moja,naikumbuka sana hiyo siku,nakumbuka ilikuwa ni majira ya saa nne usiku nilikuwa nimechoka sana nikasema ngoja nijiegeshe nipumzike tu,sikuwa nimejipumzisha kitandani bali ilikuwa kwenye kochi,wakati nimejipumzisha nikaota ndoto na uwaga sinaga kumbukumbu mimi ya mambo ya ndoto kwani kile ntakachokiota kinapotelea juu kwa juu lakini ndoto hii kwanini naizungumza pengine naiona kwangu haikuwa ya kawaida kwani nimeota ndoto niko kwenye kijiji kile nilichokuwa nimeenda kwenda kuchukua hizi pesa na nimejiona nipo ndani ya kile kijumba ambacho mshkaji amenielekeza na taratibu zote mpaka kufanikiwa kupata hizi pesa,nikiwa katika hiki kijumba nikawa najiona nimelala katika kile kitanda cha kamba,kitanda ambacho ndicho nilielekezwa kufata zile pesa,yaani nimelala hapo alafu nikawa najiuliza kwanini nimelala hapa ilihali mimi ni mtu mwenye pesa nyingi na nikiwa katika hiki chumba hakikuwa na mwangaza wakutosha yaani kama mshumaa umewashwa yaani mwangaza wake ni hafifu,nilisikia sauti ya mwanamke akinambia maneno haya "geuka huku unione" nami katika ndoto nikageuka,yaani sasa huu mwangaza ambao niliuelezea kuwa ni hafifu na sikujua unatokana na nini na fikara zangu zikawa zinahisi labda ni mshumaa kwa sababu ilikuwa ni ngumu kitu kukiona vyema na nilimuona mwanamke mmoja mnene sana,mnene mno katika kona ya hiki chumba,sauti ya huyo mwanamke naikumbuka siku zote katika maisha yangu kwa sababu alinambia "maisha yako wewe ni ya hapa,hizo pesa unazoziwaza uko nazo ziko wapi? Hizo pesa si za kwako,unajua yeye kazitoa wapi? Kwanini unaingiwa tamaa? Mbona ni mapema sana unaingiwa tamaa? Ni rahisi sana mtu kupata pesa? Mbona wewe katika maisha yako haujawahi kupata pesa kama ni rahisi,unajua huyu alifanya nini mpaka kupata hizi pesa?" Kiukweli katika ile ndoto huyu mwanamke mnene alinifokea sana na alinambia "usile jasho la mtu bila ya ruksa yake,rudisha jasho la mwenzako maana haujui vyanzo vya pesa hizi,fanya haraka rudisha pesa za mwenzako" nimekuja kustuka kwende ndoto niko kawaida nimelala pale kwenye kikochi kiukweli niliogopa sana yaani huyu mwanamke mnene ambaye sura yake sikuiona vyema ambaye kiumbile ni mwanamke sikuwahi kumuona wala kumsikia kabla,yaani ni vitu vipya kabisa kwangu,nikawa najiuliza "ndoto gani hizi au kwa sababu nawaza sana kuhusu pesa?" Yaani kama alarm ikalia kwenye kichwa changu,nikawaza lakini ni kweli mtu azifukie pesa kule mashambani na bila kumpa mtu yoyote ambaye ni ndugu yake,watoto wake wanateseka kule,amesema ana mwanamke wa maisha wake je ameshindwa kumueleza hata huyo mwanamke anayempenda sana pengine hasiteseke kwa maisha anayoishi uko uraiani aje anipe mimi? Au ni pesa za mambo ya nguvu za giza? Hofu iliingia ndani yangu,nilipatawa na hofu sana kwa sababu ni kweli kupata pesa si kitu rahisi mbona mie napambana sana,mbona mie napambana katika kazi nyingi ninazofanya na sijawahi kupata za kusema angalau nipate pesa nijenge,ninunue gari na nipate hivyo vitu angalau moyo wangu unatamani,mbona sijawahi kupata? Yeye hizi pesa alipata wapi? Kiukweli mpaka kumepambazuka sikupata usingizi kabisa yaani nikajiwa na hofu sana kwa sababu kama nilitishwa katika hii ndoto sikujua imekuja katika mazingira ya wema,sijui kwanini ndoto inijie lakini imekuja kunipa hofu.
Nilikaa kama siku mbili nikaamua kwenda kule gerezani,mimi mwenyewe nikaenda kule gerezani na nilipofika nikapata nafasi ya kuzungumza na yule mshkaji wangu na kiukweli aliponiona alifurahi sana,alifurahi sana akanambia "nilijua tu Rojas utakuja lakini mbona umekuja kwa kuchelewa?" Nikamwambia "unaona nimechelewa? Mbona sijachelewa" akasema "hapana nilitegemea ungekuja mapema zaidi kuliko leo ambavyo umekuja" nikatabasamu nikamwambia "nimekuja huu ni wakati sahihi" akanambia "mbona nakuona huna furaha,kwanini hauna furaha kwani haujafanikiwa katika jambo letu? Nikamwambia "nimefanikiwa" akanambia "najua una shauku ya kutaka kujua nini kipo ndani ya ile mizigo,unadhani ulitegemea kukuta dhahabu kama dhahabu zikiwa wazi lakini umekuta vitu vimefungwa na kufuli" nikamwambia "kwani nilitakiwa nisijue kilichomo ndani mpaka ntakapokuja na mzigo mpaka huku? Akanambia "ndio" nikamwambia "ningewezaje kutembea na kitu ambacho sijui kuna nini ndani?" Akanambia "Rojas lakini nilikwambia utakapokuja na huo mzigo utakuja kwangu na mimi ndio ntakupa maelekezo" nikamwambia "ni kitu ambacho hakiwezekani wewe unajua,tazama mambo yalivyo barabarani kukaguliwa na isitoshe mimi nimeenda kule nikiwa siko vizuri kiuchumi kwahiyo sikuweza kuhatarisha maisha yangu ilibidi nijue nini nabeba isije nikabebeshwa maiti za watu au nikabebeshwa viungo vya watu bila kujua nikajikuta nimeingia tena katika matatizo pasipo kujua na si nitaonekana mimi ni kijana mpumbavu" akanambia "mbona Rojas unaongea maneno hayo" nikamwambia " hapana nimekuja,nimekuja kukusikiliza" akasema "sawa,nashukuru sana,nashukuru sana umekuja nilikuwa nasikia sauti ndani yangu ikinambia hautakuja Rojas,hautakuja,ulivyoziona pesa ulijisikiaje? Haukujisikia kuchanganyikiwa?" Nikacheka,.nikamwambia "kwanini" akanambia "ndivyo inavyokuwa kama haujawahi kama mtu haujawahi kukutana na pesa labda katika maisha yako umeshawahi kuona shilingi ngapi,umeshashika shilingi ngapi? Labda milioni tano,milioni kumi,milioni ishirini au thelasini au hata milioni hamsini,sabini au mia lakini pindi unapokutana na pesa nyingi sana unaweza jikuta unachanganyikiwa,haujawahi kuchanganyikiwa?" Nikamwambia "kwanini unambie hivyo,pesa ambazo sijazitafuta nawezaje kuchanganyikiwa nazo zaidi tu yakupewa mwongozo" akasena "vizuri,Rojas umefanya vizuri sana kuja,si nilikuambia? Umeniamini katika kila nililolisema? Basi na wewe timiza ahadi uliyonipa" nikamwambia "kwani nilikosea kufungua yale matranka na kuzitoa zile pesa na kuzihifadhi katika mazingira mazuri?" Akasema "nilitamani uyabebe matranka yote lakini nimekuelewa mambo yamebadilika na ningekuwa mimi ningefanikiwa kuyabeba matranka lakini mambo uko uraiani sijui yakoje wewe ndio unajua siwezi kukupinga unachosema,kuna kiasi cha pesa chochote ulichotumia?
Nikamwambia "ndio,si nilikwambia nimeenda katika mazingira gani nikawa nahitaji pesa kwa ajili ya kuhonga ili nipite,nilitoa zile pesa na kuweka katika visalfeti" akasema "pesa zote zile? Ulizipangaje? Nikamwambia "nilitumia akili ya ziada kama ulivyonielekeza" akanambia "jicho langu lilipokuona mara ya kwanza lilikuwa na imani na wewe,nashukuru sana" nikamuuliza "hizi pesa umezipata wapi,pesa nyingi kiasi hiki na kwanini pesa hizi haukuzihifadhi benki sehemu ambako ni salama,kwanini umezihifadhi pesa kwenye kijumba tena cha zamani" akanambia "nilijenga kile kijumba kwa kusudi sana,kwani ni mimi peke yangu ndio nimefanya hivyo? Ngoja nikusimulie jambo moja,hizi fedha ni fedha halali kabisa,hizi fedha wala si fedha bandia,hizi ni fedha ambazo nimezipata mimi kwa jasho langu,kwa nguvu zangu,kwa kutumia akili zangu na uwezo wangu wote,niliona sehemu sahihi yakuzihifadhi ni pale" nikamwambia "bado haujanipa majibu lakini kwakile nataka kujua,mbona benki zipo ambapo watu wanahifadhi pesa nyingi sana" akasema "unajua mimi nilikuwa nafanya kazi gani? Nikamwambia "sijui" akasema "mimi nilikuwa ni raia tu nilikuwa nafanya shughuli zangu mbalimbali japo nilikuwa na kipaji cha tofauti kidogo ambacho nilikuwa naweza kuwasaidia watu wengine ambao hawana kipaji nilichokuwa nacho mimi" nikamwambia "kipaji gani hicho" akajibu "ni kipaji ambacho naweza kuzungumza hata na watu wenye elimu kubwa sana,watu wenye uwezo mkubwa wanaweza wakanifata na hata wakazungumza na mimi na wakaniuliza nina shauri kipi katika haya,ndipo nilipo pata pesa hizi kwa jasho langu na kwa nguvu zangu,nikazihifadhi pale na wala usiniulize maswali mengi kwa sababu pesa umeshazipata na ni muda wa kutumia pesa,Rojas kuanzia sasa maisha yako yanaenda kubadilika" nikamwambia "naomba niambie chanzo cha wewe kupata pesa ili niwe na amani na hizi pesa" akanambia "pesa hizi zina amani tu kama utafata na kusikiliza yale nitakayosema lakini kama utaenda kinyume na yale unayoyazungumza hizi pesa haziwezi kuwa pesa nzuri sana kwako" nikamwambia "mbona unanitishia? Mbona sentensi hiyo haukuniambia toka mwanzo" akanijibu "nilikwambia,nilikwambia na ndio maana nikakwambia uape au nani aliapa? Wewe si ndio uliyeapa Rojas? Mbona naona sasa hivi sentensi zako na sauti yako vimekuwa kama vimebadilika,kwani Rojas pesa zimekuchanganya? Mbona mimi nakuona una utulivu sana na katika watu niliowaamini ni wewe,kuna kitu kimebadilika kwako? Kuna vitu ambavyo tulizungumza mwanzo unaona hauwezi kuendelea kuvishikilia? Rojas hizi pesa ni zetu sote na mimi nilizitafuta lakini siwezi kuzitumia kwa sababu niko gerezani lakini wewe waweza kuzitumia hizi pesa lakini kwa makubaliano ambayo tumekubaliana" nikamwambia "sawa,nimekuwa na hofu sana kuhusu hizi pesa" akanambia "kwanini" nikamwambia "sijawa na amani nazo" akaniuliza "kwanini hauna amani nazo? Kwanini ukose amani nazo au uliziwazia mabaya? Kama uliziwazia mabaya lakini kama uliziwazia mema hakuna jambo lolote baya Rojas" kiukweli sentensi zake zikaanza kama kunipa ukakasi hivi kwa sababu ni kweli nilianza kuwaza mabaya na mimi nimekuja huku kwa sababu ya ile ndoto tu niliyoota ndio kimenisukuma ndio nimekuja hapa,kwanini aniambie sentensi hizi niliziwazia mabaya na nini hivyo yaani,nikamwambia "nilishafanya ulichonielekeza sasa nipe maelekezo mengine kwa sababu hizi ni pesa nyingi ni hatari zaidi kukaa nazo pengine nitastahili kuzipeleka benki au unanielekeza vipi" akanambia "hata senti moja haitakiwi kwenda benki" nikamwambia "kwanini,kwanini zisiende benki na nawezaje kukaa na pesa nyingi ndani kiasi hicho,vipi kuhusiana na usalama wangu? Nawezaje kukaa na hizo pesa zote? Kama pesa ni halali hakuna shida yoyote kwanini tusipeleke benki? Akanambia "Rojas kumbe hujui? Si utaulizwa maswali mengi ukizingatia wewe ni dereva taxi tena ambaye hata usafiri hauna ni deiwaka unapata wapi pesa kama hizo,unaweza kuthibitisha kuwa pesa umepata wapi? Kama una mahali unaweza kuorodhesha maelekezo yakujitosheleza kuhusiana na hizo pesa basi unaweza ukazipeleka kwa sababu watu wanaweka pesa benki sama sawa na kile wanachokipata kwenye movement za maisha yao ya kila siku,ebu niambie mzunguko wa pesa yako,pesa nyingi kama zile umezipaja wapi,utasema umezipata mashambani,kwenye shamba la nani? Utasema ulioteshwa,ulioteshwa vipi? Unataka pesa zote nilizozipambania kwa maisha yangu yote zishikiliwe kwa ajili ya uchunguzi?"
Nayakumbuka haya maneno aliyonambia huyu kaka,tunazungumzia pesa nyingi ambazo mpaka sasa hivi nimezikusanya idadi yake ya pesa nimezihesabu mpaka nachanganyikiwa,nikatulia na kusubiria maelekezo yaidi kujua nini sasa nafanya na hizi pesa,akanambia "nini unawaza kichwani mwako,kuna kitu ambacho umekuwa ukitamani kufanya pale utakapopata pesa nyingi?" Nikamwambia "hapana,sikuwahi kuwaza hata siku moja kama ntakuja kupata pesa kiwango kama hiki" akanambia "pale ulipofanikiwa kuzileta hizi pesa na kuwa nazo ndani nini ulifikiria kichwani kwako,nini,kufanya kitu gani?" Nikamwambia "vitu vingi sana nimefikiria ila kwa sababu pesa sio yangu nikarudi kwa mwenye pesa anipe maelekezo kwa sababu najua ulihifadhi hizi pesa kwa siku zote ina maana ulikusudia kufanya kitu labda nisikie ulikusudia kufanya kitu gani" akanambia "nyakati hizo wakati nimepata hizi pesa sikuwa na uwezo wakuzitumia kwa nyakati hizo japo kuna vitu niliviwaza ingawa najua kwa sasa hivi mambo uko nje yatakuwa yamebadilika,wewe unaendesha taxi vipi? Unauonaje ulimwengu wa taxi kwa ujumla je niku chenye faida? Unajua kwa pesa zile tunaweza kununua taxi ngapi? Nikamwambia "na ndio maana nikazungumzia habari yakupeleka pesa benki kwa sababu mojawapo ni tujue zile pesa ni shilingi ngapi" akasema "hauwezi kujua idadi ya zile pesa,wewe ni kuzitumia tu" nikamwambia "kwanini unasema hivyo,mbona unanipa wakati mgumu sana na ni pesa gani ambazo hazihesabiki wakati watu wanahesabu hadi mabilioni na mabilioni na mabilioni lakini inajulikana ni kiasi gani cha pesa kwanini zile ziwe shida kuzihesabu?" Nilimuuliza hivyo na mengineyo kadhaa ila kwa sababu muda ni mdogo haujitoshelezi kuzungumza hayo yote na alinambia "muda ni mdogo lakini nikupe muda ukajifikirie,rudi baada ya muda mfupi usikawie sana,utakachokiwaza njoo unishirikishe nakutegemea sana kwa sababu wewe ndio unajua hali ya uko nje,angalia ulimwengu wa udereva wa taxi kwa ujumla uone unaweza kuagiza magari mangapi" nikamwambia "siwezi kuagiza magari ngapi wakati sijui idadi ya kiwango cha pesa,ni dhambi kujua kiasi cha pesa nilichokuwa nacho mule ndani? Akasema "Rojas hauwezi kujua kiasi cha pesa kilichomo mule ni nyingi sana" nikamwambia "naomba hata nipambane nitafute hata mashine nihesabu zile pesa" akasema "uliahidi kunisikiliza kwa kila ntakachokisema mbona tena kama unataka kuzungumza vya kwako wakati pesa ni ya kwangu? Nikamwambia "pesa ni ya kwako lakini usinitumikishe" akanambia "kwanini unanambia hivyo" nikamjibu "hapana kwa sababu unavyozungumza vitu mimi sivielewi" akanambia "nenda nyumbani kidogo pumzika,tafuta nyumba nzuri Rojas,tafuta nyumba nzuri ya wewe kuishi,tafuta kitu uanze kukifanya mapema ili watu watakapoanza kuona macdiliko yako wasihisi vitu vibaya" nikamwambia "una maana gani? Akanijibu "tafuta hata biashara ndogo" nikamuuliza " kwa mfano kama nini" akanambia "fungua duka la nafaka" nikamwambia "sina hobie na hivyo vitu" akanisisitiza "fungua duka la nafaka muweke hata ndugu yako hapo na naamini mtaji unaweza kufika milioni ishirini,mtaji wa milioni ishirini kwenye nafaka unaweza kuuza nafaka za jumla,wewe unauza vitu vya jumla" nikamwambia "kumbe una mawazo" akanambia "nina mawazo,milioni ishirini inaweza kukuwezesha kwanza,tafuta nyumba nzuri,usijenge panga nyumba nzuri haraka sana,usipange kwenye nyumba ndogo kwani zile pesa zinahitajiwa kuchimbiwa chini unakuwa unaweka mazingira mazuri kabisa kwani wewe ndio utakuwa unaenda kuzichukua,ndio usalama na ni lazima uzihifadhi katika matranka"
Baada ya maagizo haya ya mwisho nikayabeba na kuondoka zangu kurejea nyumbani ingawa mara baada ya kutoka katika mazungumzo na huyu mtu hofu ikawa juu zaidi kutokana na majibu aliyokuwa akinipa,hofu ikanijia katika hali ya kibinadamu kwani kweli pesa anazo lakini kwanini hazihesabiki na wakati idadi ya pesa zinaweza kuhesabika yalinipa hofu!
Yajayo yanafurahisha!
ITAENDELEA
Rojaz naye badala afanye matumizi, habari ya kujua kiasi za nini wakati hukuzitafuta !Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha sitasahau cha radio free africa
Sehemu ya 9
Siku mpya ikafika na mawazo yakiendelea kunitawala kichwani mwangu kwani mzigo wa pesa ulikuwa mkubwa sana pamoja na mawazo aliyonipa ndugu yangu kule jela yakufungua duka la nafaka lakini bado mawazo hayakuondoka kwani nikifikiria wingi wa pesa zile,maneno yale aliyonambia kule kiukweli mtanziko ulikuwa mkubwa tena sikuwa nimesema mwanzoni katika zile pesa kulikuwamo na pesa za kigeni aina ya dola,kiukweli mawazo juu ya chanzo cha pesa hizi hayakwisha kichwani,kiukweli napenda pesa ila nilitaka kujua kama kumefanyika dili hadi kupatikana kwake je ni dili la kiwango gani? Na mtu wa kunambia chanzo chake ni huyu ndugu naye kashanambia nisiulize chanzo nijue tu ni pesa halali,nikaanza kufanyia kazi yale mawazo yakufungua duka la nafaka kwani nikakubali kuwa sitaweza kujua ni kiasi gani cha pesa nilicho nacho na nikaachana na mawazo hayo na nikachukua milioni ishirini zakufanyia zoezi kama tulivyopanga na liwe duka la nafaka la jumla,nilitafuta nyumba nzuri ya kupanga, watu wanajua maisha yetu unajua na hata familia yangu wanajua mwenendo wangu,wanajua wapi napata pesa na kaka alipojua nimekwenda kupanga nyumba ya thamani kama ile aliniuliza "mdogo wangu unawezaje kuishi kwenye nyumba kama ile,naona sasa hivi unatukwepakwepa mishe zako sizielewi,unaweza kunishirikisha lolote?"
Nampenda sana kaka yangu tena ni kaka mwema kabisa hilo ndilo ninalolijua ni kaka mzuri sana lakini nawezaje kumshirikisha hili jambo japo kiukweli ndani yangu natamani kushea na mtu kuhusiana na hili jambo uenda akanishauri kitu kikanifaa kwa leo au kwa siku za baadae maana sasa hivi mawazo yote najiuliza mwenyewe na kujijibu mwenyewe lililo sahihi na lisilo sahihi yote nayawaza mimi mwenyewe kwani zaidi ya yule mtu hakuna mwingine anayeijua hii siri wakusema naweza nikashea nae na amenambia hata siku moja nisitoe siri hii kwa mtu yoyote,nilimwambia kaka "ni mtu tu ndio amepanga sio mimi ila amenambia mimi naweza nikakaa lakini yeye atakuja kukaa siku sio nyingi" akanambia "ni mfanyabiashara gani huyo,yuko hapa hapa nchini? Nikamwambia "ana mishe mishe zake tu anafanya" zaidi kaka alinisisitiza kuwa mwangalifu sana "kuwa makini sana na watu" nikamwambia "ni kweli kaka ila ni mtu mwema" akasema "kuwa mwangalifu unajua kwa shughuli unayofanya unakutana na watu wengi wengine sio wazuri si unaona kwa mfano ishu iliyokukuta kipindi kile ikatuletea taharuki kubwa,usije kuingia kwenye matatizo napenda kushirikisha ndugu katika mambo ambayo unakutana nayo hata katika watu ambao unakutana nao" lakini sikuweza kumwambia chochote kaka zaidi ya haya niliyomwambia.
Kwa wingi wa pesa nilionao yaani nikisema nianze kufanya matanuzi lazima nitaleta taharuki hasa kwa familia yangu na hata jamii inayonizunguka zaidi zaidi nikajikuta ni mtu wa kujiongelesha,nakumbuka niliwaambia familia yangu nina mpango wa kukopa,kuna mtu amenipa connection ya kukopa,wakanambia "unakopa kwa kipi ambacho utakirejesha yaani kwa hazina ipi itatumika kama dhamana ya mkopo maana unapoenda kukopa kuna taratibu zao kwamba una nini" nikasema "kuna mtu uko yupo anafanya kazi anasema kuna namna" "kuna namna ipi?p" ndugu wanahoji kwakuwa wote wanajua kama mimi nafanya deiwaka tu kwahiyo nakosa vitu vya kutetea hoja yangu lakini sikuacha kujisemesha nikaendelea kujisemesha ili mambo yatakapoanza kutokea yasije kuwashangaza wakumbuke matetezi yangu ambayo niliyasema awali kwamba kuna mtu yuko benki anataka kunikopesha,anataka kunifanyia mpango na vitu kama hivyo.
Katika ile nyumba niliyopanga nilifanya mchakato kama nilivyoelekezwa,katika chumba ambacho mimi ndio ninalala nilitindua mwenyewe kwa sababu ilikuwa hauwezi kusema niite mtu aje afanye hilo zoezi lazima atagundua kwamba kwanini huyu anachimba hapa chini anataka kuhifadhi nini na watu ni wepesi katika kushea vitu na watu kwahiyo ataenda kusema mbona yule alichimba hivi kwahiyo wakataka kujua kuna nini,hili zoezi nililifanya mwenyewe na halikuwa gumu kivile na ukizingatia makuzi yangu mimi ni kijana mpambanaji toka kitaa chochote ukinipa nafanya,niite kwenye ujenzi mi naendaa,niite kwenye jambo loloje mimi nafanya kwahiyo nilichimba kwa kadri nilivyoweza mwenyewe inatosha nikaweka sawa mazingira vizuri ili fedha zikikaa zikae vizuri na nikafanikiwa kufunika kwa namna sahihi kabisa ambayo mimi nikitaka naweza kwenda kuzichota sehemu salama na kuwa ngumu mtu kugundua kama mimi nina pesa ndani kwa nilivyohifadhi.
Nikaanza kufatilia mchakato wa suala zima la nafaka kwani nilimpata mtu akanipa mwongozo na nilimwambia mimi nina mtaji wa milioni ishirini na akanambia kwa mwanzo kwa biashara ya nafaka milioni ishirini ni mtaji mzuri kabisa,akasema "pesa hiyo hata ukitaka kuwekeza katika biashara nyingine inaweza kukupush ila wewe umesema nafaka yafaa sana,tutafungua duka na kuuza nafaka za jumla" nikamwambia "basi naomba mwongozo wako,naomba nisaidie katika hili kwa sababu nimekuwa nikitamani sana" ndipo alipofatilia na kupata eneo na kulipa eneo,yaani kulipia flemu na michakato mingine ikaendelea ili kuweza kuanza biashara na mimi ni mtanzania wa asili ya kutoka hapahapa Tanzania na nikalipa jina fremu yangu kwa jina la asili ya kutoka nyumbani kwetu,nilianza kuwa bize sana na kuna muda nilipata wakati nikaenda kuwatizama watoto wa mshkaji na safari hii sikuenda kinyonge kama nilivyokuwa naenda safari za nyuma,nilikwenda na vitu vingi sana kwa sababu nilienda kufanya shopping ya vyakula vya kutosha kabisa na hata yule mama yao alishangazwa sana na kitendo changu chaa mimi kupeleka vyakula vingi kama vile yaani karibu vyote vilivyokuwa vikihitajika nyumbani nilipeleka na akasema "eeh vyote unatuletea sisi? Nikasema "ndio" akasema "kwanini,kwanini? Kwani wewe hauna ndugu?" Na yeye ananiuliza nami nikacheka na kumwambia "hata nyinyi ni sehemu ya ndugu zangu kwa sababu nimeshakuwa marafiki na nyinyi" nikamwambia naomba nitoke na watoto,nikatoka na watoto na kuwapeleka shopping katika maduka na sikuwapeleka maduka madogo madogo ni maduka ya ukweli na kuwapa uhuru wachague wanachotamani kuvaa,yaani watoto walifurahi wakachagua viatu,majinzi,fulana,mashati nami nikalipa kwa ukweli watoto walifurahi sana,walifurahi mno na kikubwa mimi niliwaambia "baba yenu anawapenda sana" na kwakuwa baba yao yupo gerezani na watoto hawa wamekuwa hawapati nafasi kwa baba yao kwahiyo wanapokea tu sio ile usiliasi sana katika mapokeo ya kuhusu baba yao lakini mimi nikawa nimefanya kwa nafasi na niliyakamilisha hayo na nikarudi tena kule gerezani.
Nilipofika gerezani nikampa salamu zake kutoka kwa watoto na nikamuelezea kuwa nimewafanyia shopping na ni kwa kiasi gani watoto wamefurahia naye akafurahi sana kwa maelezo yangu na kusema "nakushukuru sana Rojas,nakushukuru na sina neno jingine zuri lakusema,nakushukuru sana lakini mbona wewe haujavaa mavazi yale ninayotamani kukuona nayo umevaa?" Nikamwambia "unatamani kunionaje?" "Nenda kanunue nguo nzuri sasa maisha yako Rojas yameshabadilika haiwezekani una pesa ndani uwe unavaa hivyo bwana" nikacheka nikamwambia "nimekuelewa" akasema "zile pesa ni za kwako Rojas,nikisema zile pesa ni za kwangu na zangu ujue ni za kwako kwakuwa wewe ndio upo uraiani hata ukisema uniletee haya mimi nafanya matumizi gani hapa? Sina matumizi ya kufanyia hapa ila wewe unayo,furahia maisha Rojas tena uwe na amani kabisa kwani mimi nafurahi unaponiletea habari za watoto wangu mimi moyo wangu unajawa na furaha,sina furaha nyingine zaidi ya watoto wangu mimi,nataka nione wanasoma vizuri sijui una mpango gani sasa?" Nikamwambia nimefanya moja,mbili,tatu nikamueleza mengi ambayo nimefanya akafurahi sana na nikamueleza kuwa kuna haja ya watoto sasa kuwapa elimu iliyo bora na akasema iliyobora sioni kama nimechelewa? Nikasema "kwa mfano huyo mdogo wala usiwaze nitatafuta shule nzuri kwa namna yoyote ile waingie uko" akaniuliza "unawaza nini kingine" nikamjibu "mengi nayawaza kuhusu watoto wake ikiwapo kuwapa elimu bora na maisha mazuri,nataka niwahamishe pale wanapokaa" basi ninapozungumza hivi anafurahi sana,anafurahi kweli kweli,alifurahi sana na katika mazungumzo akanigusia swala ambalo tulilizungumza mwanzoni "Rojas wewe ni bosi sasa,wewe ni tajiri mtoto" nikacheka na akanambia "biashara ya taxi kwakuwa unaifahamu na una uzoefu nayo kwanini usinunue taxi nyingi" nikamuuliza "nyingi ngapi bwana?" Akanijibu " kwa pesa ulizonazo unaweza unaweza kununua ngapi? Nunua gari tano,nunua gari tano alafu zitupe sokoni naamini hautajuta" nikamuuliza "kweli?" Unajua mimi nimekulia kitaa nimekuwa sina connection zozote sifahamu naanzia wapi?" Akanambia "najua,najua na sasa mimi nipo gerezani je nikusaidie kukukutanisha na mtu?"
Nikamwambia "mtu? Kuna mtu uko uraiani unafahamiane nae kwa ukaribu hivyo anaweza kunisaidia?" Akasema "yupo kuna mshkaji mmoja alikuwa anadili na mambo ya magari sasa umekuwa muda umeshaenda sana sijajua kama bado anaendelea kufanya hivyo " nikamwambia "wala usiwaze kwa sababu niko uraiani hakuna sab kitakachoshindikana nitatafuta namna yoyote kujua wapi naweza nikapata na sio mambo ya kutapeliwa" akasema "hilo la msingi sana,sawa,lini tena utaenda kuwaangalia watoto" nikamwambia "naangalia,naangalia namna bora lakini mimi nimewaza jambo moja zuri sana" akasema "jambo gani?" Nikamjibu "ikiwezekana,ikiwezekana kama yule mama atakataa habari ya kuwapeleka watoto boarding ikiwezekana niwachukue nikae nao" akasema "hatakubali yule mwanamke,hatakubali kabisa,hawezi kukuamini hivyo kukupa wale watoto hata kama umekuwa unaenda,hawezi kuruhusu kitu kama hicho,wala usiwaze kuhusu hilo pengine litakuja kufanyika baadae akishajenga imani na wewe na mimi nataka wale wakaa na mama yao pia wala sitaki kumnyang'anya yule mwanamke watoto maana yake na yeye ni faraja yake pia ila waweza watengenezea mazingira mazuri,wakaishi pazuri wakapata mahitaji yote,hilo ndio naona bora zaidi" nikamwambia "sawa,nimetamani kukuletea vitu vingi sana huku gerezani ila vichache hivyo nimeleta" akasema "si unajua hivyo vingi ntaviweka wapi tena lakini nashukuru sana,asante sana" alishukuru saana yaani kiwango cha kushukuru kilikuwa cha juu mno,ile hofu aliyonipa mwanzoni hakunipa safari hii,niliondoka nikiwa na furaha nasikia moyo wangu umeanza kuwa na amani kwa mazungumzo tuliyoyafanya.
Biashara iliposimama sasa na kaka alipojua kuhusiana na hili kiundani kwamba ni mimi ndio nimefungua hili duka alinambia "mdogo wangu njoo tuzungumze,njoo tuzungumze hauwezi kuendelea kunikwepa njoo tuongee" nikapata muda nikakaa na kaka,kaka alinambia "mimi ni nani kwako?" Nikamjibu "wewe ni kaka yangu" akaendelea "unaweza kunificha jambo lolete mimi na ukafanya mambo kwa siri? Pesa ya kufungua duka la nafaka umezipata wapi? Sisi tunajua maisha ya familia yetu,umekuwa unatoa pesa hata mimi nikasema labda ni huyo mfadhili lakini na hili duka ni nani tena? Ni yule mtu aliyekwambia upange ile nyumba kule? Nikamwambia "kaka kwani shida ni nini,inamaana kila kitu katika maisha yangu natakiwa kukiongea kwako? Nilipomwambia kaka alishangaa akanambia "Rojas unanijibu mimi hivyo?" Kwa sababu naweza kumueleza nini kaka kuhusiana na hizi pesa zaidi zaidi nitamdanganya nami sitaki kumdanganya na ndio maana sitaki kuzungumza habari kuhusiana na hizi pesa.
Nampenda sana kaka yangu lakini siwezi kumueleza huu ukweli lakini aliniambia sentensi moja "waweza kuona umewin kwa kutokusema au kunidanganya lakini Rojas wewe ni mdogo wangu na ninakupenda sana na sisi kama familia tunakupenda,hatutaki kukupoteza wala upatwe na matatizo yoyote,usiwaze kunishirikisha mimi naweza kukuharibia dili lako zaidi zaidi ntakushauri yaliyo mema,sijajua unafanya dili gani,sijajua la halali au sio la halali lakini mimi nipo kwa ajili ya kukushauri yaliyo mazuri,mimi ni kaka yako" hatukuelewana na kaka nikaondoka zangu niliendelea na mishe zangu kama kawaida.
Nilipata muda na nikamtafuta yule mwanamke ambaye yule mshkaji wangu wa jela alikuwa anampenda sana (yule mchumba wake),iwapo yule kaka angekuwa uraiani huyu ndio angekuwa mke wake wa ndoa kabisa,anasema "mwanamke wa ndoto yangu,mwanamke ambaye nilimpenda sana" nilipoenda kumtembelea nilimpelekea pia vitu mbalimbali hasa vyakula vya nyumbani,hii ni mara ya pili namtembelea huyu mwanamke na kikubwa nilienda kumwambia "nina salamu zako kutoka kwa mwanaume ambaye anakupenda sana" alicheka na akafurahi nilipompatia zile zawadi na akanambia "kwanini unaniletea hizi zawadi mimi,mimi nilishbmua kuanza maisha yangu mapya,hajakwambia chochote kwani? Nikamwambia pengine anajua umeshaamua kuanza maisha mapya lakini upendo alionao kwako ni mkubwa sana na kwa sababu anaishi anasema upendo wake kwako hauwezi kupotea na amenitumia kuja kukwambia nami ni mjumbe mwema,rafiki mwema nimekuja,nimekuja kukujulia hali,kukupa salamu na kukuletea hivi vitu,akasema "usijisumbue kuingia gharama na kuniletea mimi hivi vitu" nikamwambia "usijali nimekuja kukusalimia kwa upendo" akapokea na nikampatia kiasi cha pesa,nilimuachi laki nne akashangaa na kunambia "kwanini unanipa pesa? Yaani Kwanini?" Angejua kama hizi pesa zinatoka kwa mwanaume ambaye yuko gerezani ila ndio hivyo hauwezi kusema na kwakuwa mimi ni mjumbe tu nimekuwa nikiwatendea wema watu hawa ambao huyu mtu alitamani kama angekuwa uraiani wafurahie maisha,sikuishia hapo kwani nilirudi tena kwa yule mama na kuketi na kuzungumza nae anataka kufanya nini,alicheka sana siku niliyomuuliza hilo swali,alisema "eeh unataka kujua mimi nataka kufanya nini ili wewe ufanye nini?"
Nikamwambia naweza kukushauri kitu au kama unahitaji mtaji au kukukopea mtaji mahali ukafanya biashara" akasema "nina mawazo mengi ila sina tu msingi maisha yangu yamevurugwa,si unaona yule mwanaume yuko kule gerezani anafanya cha maana nini,maisha yake yameishia uko,ndugu zake hawajali lolote kuhusu mimi na siwataki hata kuwaona,watoto hawa naangaika nao mimi ndio kila kitu" nakumbuka nikamwambia "basi angalia biashara gani unaweza ukafanya alafu nishirikishe,kitu kingine pia naona hapa unapoishi naona mazingira sio mazuri kwa watoto,nina jambo nilifikiria na jambo nililofikiria kwanini nisitafute nyumba ambayo itakufaa zaidi wewe pamoja na watoto" akanambia "unitafutie nyumba mimi? Unitafutie nyumba kwa sababu gani? Nikamuuliza "kwanini umestuka nami nimeshakuwa sehemt ya familia" akaniuliza "unamaanisha nini,unataka nini kwangu? Nakumbuka huyu mama aliniuliza hili swali,unajua mimi ni kijana mdogo na huyu kwangu age ilikuwa imeenda kidogo,sio age zangu kidogo sio age zangu lakini kwa jinsi nilivyomwambia akaona labda ni wale vijana wahuni nini (wapenda majimama[emoji23])au kijana anakuja kuja amenitamani nini? Yaani akili kama hizo na nikajua ndio mawazo anayoyawazia hayo,nikamwambia "mimi ninawapenda sana hawa watoto kwa sababu ya rafiki yangu na kama mimi Mungu amenibariki napata chochote kwanini nishindwe kufanya vitu vilivyo bora kwa watoto ambao ni wa rafiki yangu,fikiria kuhusu hilo alafu ntakapokuja utaniambia" huyu mama mara zote nyuma nilizokuwa nakuja uwaga ananikaziaga macho,tukiwa tunazungumza uwaga na maneno flani mfano ni nini? Umekuja kufanya nini na maneno kadha wa kadha ya shombo lakini leo huyu mama hata angalia yake ilikuwa ya uoga na nidhamu,unajua mtu anakuangalia anaona haya flani kwa matendo yake ya nyuma kwako,akanambia "kwahiyo utakuja lini?" [emoji23]
Nikawa naulizwa mimi tena hapo wakati uwaga hana hata swaga hizo wakati ukija atakupa maneno ya shombo kama yote lakini leo nikaliona tabasamu lake,akaniuliza "utakuja lini?" Nami nikamjibu "nitakuja,kwani wewe ulitaka nije lini?" Akanijibu "wakati wowote hata kesho jioni ntakuwa nshapata majibu" nikawa najisemea moyoni mwangu "pesa,pesa ni kitu kingine kabisa katika maisha ya mwanadamu hapa duniani,pesa ina nguvu,pesa inasema,pesa inaongea,pesa ina siri nzito sana mimi katika maisha niliyopitia nikagundua siri ya nguvu ya pesa ni ya ajabu sana" nikaondoka kwa huyu mama nikiwa natabasamu lakini kaka yangu alizidi kunisumbua sana akitaka kujua vyanzo vyangu vya mapato vinatoka wapi,akiwauliza washkaji zangu,watu zangu wa karibu lakini hakuna hata mtu mmoja anayejua chochote kwa sababu sijawahi na mtu yoyote yule,wakati huo nikiendelea na michakato ya kujikita kwenye biashara ya taxi yaani naagiza magari mazuri na natafuta vijana na kwa sababu mimi nina uzoefu si haba hii inaweza kuwa mwanzo wa biashara hii kuweza kufanikiwa.
Itaendelea!
ITAENDELEA!
Ndio ninavyotaka watu kama popo!
Kimuhemuhe kinamuwasha[emoji23][emoji23][emoji23]Rojaz naye badala afanye matumizi, habari ya kujua kiasi za nini wakati hukuzitafuta !
Sent using Jamii Forums mobile app
Bado nitaanza
Kweli kinamuasha anaweza hata kushindwa kufanya la maana [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kimuhemuhe kinamuwasha[emoji23][emoji23][emoji23]