Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha ‘Sitasahau’ cha Radio Free Africa
Sehemu ya 15
Mimi nikawa nimepata mwanzo mpya wa maisha,kitendo ambacho kimetokea siku yajana,juzi,siku za nyuma,ikazaa tabia mpya katika maisha yangu kwani mimi nilikuwa ni kijana wa kitaa,nilipata pesa kwa ghafla lakini nilistuka nilipoziona pesa na najua hizi ni za kwangu lakini ndani yangu niliamini katika kujisimamia kwamba mimi hii pesa kwa sababu ni ya kwangu haitanibadilisha kwa chochote,mimi nitabaki vile vile kama nilivyo,wav wanasema watu wanabadilishwa na pesa nami nikasema pesa haitanibadilisha lakini nguvu sasa imenishinda,pesa imenishinda nguvu na tabia zangu zikaanza kubadilika kwani kwa masuala ya wanawake ikawa kama nimefungua mlango na hata kama leo utaniuliza mlango wa kuhusudu wanawake,kupenda wanawake kiwango kisicho kawaida ilianza lini? Ni usiku ule mtoto wetu kupata graduation na mimi baada ya kuambatana na huyu msichana baada ya kutumia kilevi na kupata matamanio kwani tangu hapo ni kama ukurasa mpya ulifunguliwa maishani mwangu.
Hatia ya kujisikia vibaya kwa kutembea na yule msichana ilidumu kwa muda mfupi sana na hata kaka yangu aliniuliza "hivi Rojas wewe unaweza ukaona maisha ya furaha ni yapi,maisha ya furaha kwa mwanaume ni yapi,ni kuwa na vitu anavyovitaka, sasa hivi unaweza kuwa na mwanamke yoyote unayemtaka,kuna furaha gani zaidi ya hiyo? Huyu ni kaka yangu alinambia maneno hayo,sitaki kumuhukumu kusema maneno yake pia yalichangia mimi kuwa hivi,siwezi kusema hivyo lakini mimi nilibadilishwa kwani Rojas mimi niliyekuwa sipendi wanawake nikaanza kupenda wanawake na hasa nnapotumia kilevi,nnapotumia kilevi matamanio kwangu yanakuwa makubwa kuliko kawaida,nikaanza kuishi maisha ambayo mwanzo sikuwa nayo,pesa ikaanza kunipeleka puta na hata nikawa muhudhuriaji mzuri kwenye hizi bendi za muziki na nikifika pale lazima niwe na kampani kubwa na hizo kampani hata ukiniuliza zimetokea wapi nakuwa sina jibu,mimi na kampani yangu nikawa ni mtu wakubadili viwanja mara tupo hapa,mara hapa panaboa twende huku mara kule, katika gari yangu nyuma ya gari nakuwa na briefcase yenye hela yaani hizi ni kwa matumizi yangu ya kuwel heshima bar!
Mwenendo wangu ulibadirika na nikisema niseme jinsi ulivyobadilika yaani ni kwa kiwango kikubwa sana tena kwa muda mfupi sana,mabadiliko yangu yalifikia kiwango cha hadi kuwa natmwanamke mmoja haitoshi kwani si pesa ndio inayoongea na wanawake wanataka nini,wanawake wanataka pesa na pesa ipo kiasi nikawa hata kulala na wanawake wawili kwa pamoja kwangu haikuwa ishu,yaani pesa ilinibadilisha kwa kiwango kikubwa sana,nakumbuka hatua za mwanzo nikiwa na ujasiri wakujiambia kuwa pesa haitanipeleka,pesa haitaniharibu na nitabbki **** Rojas yuleyule na nitaendelea kufanya majukumu yangu kama kawaida lakini pesa inayo nguvu kuliko vile watu tunawaza,pesa ina macho,pesa ina mdomo,pesa ina masikio,pesa ina miguu yaani kuliko vile tunawaza,niliwaza hivyo lakini kumbe pesa inaenda kunifanyia vitu vipya kwenye maisha yangu.
Nakumbuka siku moja hapo nikiwa nimeishi katika mifumo hiyo hata mwaka ulipita,mwaka ulipita mimi nikiwa ni mtu wa starehe tu ingawa napata muda natizama maendeleo ya biashara lakini nilikuwa nimetawaliwa na starehe kwa kiwango kikubwa ikawa hata nikitumia kilevi nakuwa sitoshelezeki nacho nakuwa nasaka kilevi kipya almradi kujaribu kila aina ya ulevi nikapelekea hadi katika uvutaji wa sigara huku shauku ya kufanya tena na tena ikinijia,kuna mshkaji wangu miongoni mwa vijana ambao nimewakabidhi taxi ninazozimiliki aliniomba kuzungumza nami,ni mmoja kati ya watu waaminifu na uko nyuma yeye alikuwa akinipa mimi deiwaka katika gari lake nami ndio nilipopata pesa na kununua zangu sasa nimekuwa bosi wake,alinambia maneno haya "yaani Rojas kila siku ninapokuona naona sio Rojas ninayekufahamu" nikamwambia "kwanini unasema hivyo" akasema "wewe ni mdogo wangu,wewe ni mshkaji nimesena nikutafute siku ambayo naamini utakuwa hauna hang over,naamini huu muda uko fresh kabisa,Rojas kuna kitu kwako hakiko sawa" nikamwambia "kwanini,kwanini unasema hivyo" akasema "hapana,mshkaji unakunywa sana ,unakunywa sana Rojas alafu wanawake,sikwambii kwa ubaya wewe ni kama mdogo wangu alafu tena mshkaji alafu tena ni bosi wangu nakwambia tu katika roho nzuri kaka yako anakuharibu,kaka yako haiwezekani akawa anakutafutia wanawake akutegee wakati huo huo anakusifia na wakati huo huo anataka akuchume wewe pesa,mimi sizungumzi kwa ubaya yule ni kaka yako lakini Rojas kuna kitu kwako hakiko sawa"
nikamwambia "wewe unanionaje yaani kitu gani kwangu kimebadilika " akanambia "Rojas pesa zisije zikawa zinakutumikisha katika mambo ya uovu,yaani mimi nakujua Rojas ingekuwa mtu mwingine tu baki mimi hata nisingezungumza hivyo,mimi nazungumza hivyo kwa sababu nakujua" nikamwambia "kwahiyo unataka nifanyaje sasa" akanambia "unajua Rojas unatakiwa upate muda wewe mwenyewe ujitathmini na kujiuliza wewe ndio Rojas au kuna mtu mwingine amezaliwa ndani yako" mtu huyu alizungumza na mimi,ni mshkaji ni mkubwa kwangu pia,alizungumza na mimi maneno ambayo pengine ni nadra kukutana na mtu kwani hata kaka yangu mimi haniambii hata washkaji ambao tunakutana nao kula bata,tunatega mingo tumpate msichana gani mfano kuna msichana huyo ndio mwenyewe mwenyewe yaani mtaa flani ndio funga kazi lakini mgumu kweli kweli nasema "nileteeni huyo,nileteeni huyo mimi huyo nampata" wapo washkaji ambao tunajadiliana hayo na jana ilikuwaje? Demu wa jana ilikuwa moja,mbili,tatu,nilikuwa na watu wengi wakujadiliana nayo hayo na nilikuwa nasikia raha kunapokuwa na stori za muundo huo,nasikia furaha,kwahiyo mtu anaponiambia mambo haya kwa kukuface na kukwambia ukweli kwamba bwana umebadilika,nikamind kiukweli maana niliona kama anataka kuniambia jambo la maana alafu kumbe jambo lenyewe la kipuuzi,akanambia "hapana Rojas sio jambo la kipuuzi,mimi ingawa ni mkubwa lakini naweza kuwa sina chochote ambacho naweza nikakwambia lakini naweza nikakushauri,wewe ni mdogo wangu alafu sipendi kukuona unaharibikiwa,Rojas hauwezi kumaliza wanawake wa dunia nzima,hauwezi,yaani wanazaliwa kila siku na wana urembo wa kila aina lazima urudi ujijue ujirudishe wewe kama Rojas,wewe Rojas uliyekuwa na displine yako wewe mwenyewe binafsi" mazungumzo ya deep sana alinambia,deep sana na sikuwa nimelewa kabisa nilikuwa niko fresh kabisa.
Nakumbuka katika mengi tulizungumza kwakuwa ni mtu ninayemheshimu sana nikamwambia sentensi moja nikamwambia "sijui,sijui hata nimepatwa na nini kwani muda wote najisikia kufanya starehe,nasikia kusukumwa kufanya starehe yaani" akanambia Rojas hauko sawa,kuna kitu kwako hakiko sawa Rojas,unajua pesa na hasa kwa sisi ambao tumezaliwa katika familia maskini tukipata pesa lazima pesa zinaweza zikatupeleka kama tutakosa ushauri mzuri tukakosa watu sahihi ambao watatuambia ukweli na kuturudisha kwenye mstari pale tunapokuwa tunakosea tofauti na yule aliyezaliwa katika mazingira ya umiliki wa pesa,kwao wana pesa,hizo pesa zipo,wanapata mahitaji yote kwahiyo eneo la mwanamke anaweza kumpata mwanamke yoyote kwa sababu pesa ipo yaani hashoboki na vitu lakini sisi ambao tumezaliwa katika familia maskini tunapopata nafasi kama hivi unaweza kuta ile hali ya uhalisia wako sasa inaanza kutumikishwa kwa sababu kuna hali inazaliwa ndani yako ya kujiamini,ya kumiliki kila kitu,ya kujitukuza unajikuta unafanya vitu ambavyo awali haukuwa unavifanya lakini Rojas haimaanishi kila mtu anayepata pesa anatakiwa abadilishwe na pesa,pesa inatakiwa wewe ndio uicontrow na sio yenyewe pesa ikucontrow wewe,Rojas sasa hivi pesa inakucontrow wewe,unaweza kuwa katika mambo yako muhimu lakini washkaji zako ambao wamezaliwa baada ya wewe kupata pesa hata wakikwambia njoo unaenda,wakikwambia tunakuja wanakubeba,unaharibu mipango yako,ratiba zako,unaharibu vitu vyako kwa sababu tu umeshaingia katika utumwa" alinambia maneno mengi mengi sana mpaka nikawa nasikia kuchanganyikiwa kuendelea kuyasikia,nikamwambia "naomba uniache,naomba uniache" akanambia "Rojas naomba yafikirie haya pia nafikiri unahitaji msaada Rojas angalau wa kuongea na watu wanaokupenda pia,mimi nasikitika (akawa ananitajia msichana mmoja ambaye mimi nimetoka nae )wewe Rojas wakutoka na msichana kama yule kweli? Wasichana ambao wana sifa mbaya kwelikweli unafanya kwa mashindano ili uonekane nawe umepita pale,wewe sio Rojas bwana,wewe sio Rojas ninayemjua mimi ambaye anajipenda,anayejiamini"
Yote haya alinambia kwa uchungu na kaka yangu hajawahi kuniusia kuhusu haya mambo ya wanawake yaani yeye ananambia sifa ya mwanaume na hasa mwanaume aliyebarikiwa uchumi miliki mwanamke ambaye moyo wako unasikia una washawasha,unasikia furaha nae,kwahiyo leo nikisikia furaha na huyu niwe nae,kesho nikisikia furaha na yule kwahiyo kwa mapana kabisa pesa ikanibadilisha nikawa mtu mbaya,mtu ambaye sikujali tena hisia za mwanamke yoyote,mimi nikipita napita na za kwangu yeye kama ataona mimi nadumu hapo kumbe mimi ni msafiri tu bado nasafari sijafika hata yule mwanamke wa mshkaji ambaye nasema mwanzo ilikuwa bahati mbaya nilimjeruhi kwa sababu nilimwambia "hapana,hapana usinicontrow hapana ilitokea bahati mbaya lakini inaonekana ni mtu aliyeniamini kwa sentensi zangu za mwanzo katika ulevi lakini kote uko mimi niliendelea kupita,naendelea kupita,nikaja kugundua kitu pesa kinabadilisha watu wengi sana,watu wengi walio katika hali ya umaskini walipopata pesa nyingi asilimia kubwa wanabadilika,uhalisia ule wandani ambao uwa hauonekani majira akiwa hana pesa ndio unaonekana sasa,kitu ambacho sikuweza kusahau katika starehe zangu zote ni kwenda kuwatizama wale watoto wa mshkaji kwa sababu yule mama alipambana (yule mama niliyempa mtaji wa biashara ya vinywaji)huyu mama kweli alikuwa mpambanaji kama kweli alivyosema kwamba mimi sitahangaika tena na wanaume,sitahangaika tena mbdam nimepata kitu changu cha kuniingizia shilingi mbili tatu nitasimama nacho hiki,kwahiyo mara nyingi akawa ananipigia simu "watoto wanakusalimia" kwahiyo yeye hata katika mabadiliko yangu,hata katika hali ya ulevi niwe naenda pia kuwatizama wale watoto na kuwapa mahitaji mbalimbali kwa hao watu sikusahau lakini kwa yule nilikuwa ni mtu wa kukata kamba labda anikumbuke yeye tu na kama akinikumbuka akinifosi hivyo yaani sina ile mambo yakusema nikae nitulie,nikaanza mambo ya kuhangaika kuhangaika ndio kama nilivyoelezea kwa mapana katika eneo hilo.
Kuna biashara mwanzo ambayo nilitamani sana kuifanya,nilitamani kufanya na nilipata watu ambao niliamini nimepata watu sahihi kwenye eneo la madini,kuna eneo mwanzo nilifanya niliona kama kuna matunda mazuri,eneo hili kunahitaji umakini na kunahitaji watu sahihi kwa sababu kuna nyakati nilipigwa yaani niliingia mkenge watu waliamua kunitengeneza na kunipiga masuala mazima ya utapeli kwahiyo ikanijeruhi sana hiyo kwa sababu ni harakati ambazo naendelea kupamcna nazo lakini sikurudi tena kule gerezani nyakati hizo zote sikuwahi kurudi gerezani,mimi ulipita mwaka mmoja mzima sikukanyaga gerezani,ukafika mwaka mmoja na nusu sikufika gerezani mpaka ikafika miaka miwili sikurudi gerezani,maisha yananipeleka resi sana lakini uzuri pia zile biashara ambazo nilizidi kuwekeza ziliendelea kuzalisha.
Kuna mambo uwa hatupendi kuyasikia kwa sababu yanakera sana kwa sababu mimi huyu aliyekuwa dereva wangu hakuacha kuniusia,hakuacha kuniusia kutokana na tabia yangu,nakumbuka siku hiyo alinambia "vipi bosi leo nina shida nawe nataka tuonane,natamani hata twende nyumbani kwangu tuandae chakula,tupate chakula pamoja" nikamwambia "kuna nini" kumbuka huyu mtu tuna mahusiano mazuri toka siku za nyuma,akanambia "kuna vitu tu vya msingi sana natamani tuongee" nikamwambia "yaani wewe hubadilishagi mada zako kila siku ni hizo hizo" akanambia "Rojas ni kitu muhimu sana nataka tuongee,hatuwezi kungea kwenye gari,hatuwezi kuongea kwenye mahoteli yako uko unakokuwa na wanawake zako mimi nataka tuongee hili jambo nyumbani kwangu" nikamwambia "poa basi tutacheki muda siku nikiwa free" akanisumbua akanambia "iwe leo leo bwana,iwe leo leo" nikamwambia "nina ratiba nyingine" lakini akanisihi sana,nikamwambia "nitakuja mida ya usiku" akanambia "mida ya usiku siwezi kukupata Rojas washkaji zako watakuwa wameshakudaka Rojas" nikamwambia "hamna nitakuja,nitakuja alafu ndio nitaendelea na mambo mengine" kwa sababu alinisumbua sana na mpaka akanifata mahali nilipo na mahali nilipo nilishaanza kunywa pombe.alinichukua na nikamwambia "si tuongee hapa hapa" akasema "hapana mimi twende tu nyumbani kwanza mimi nasimamisha kila kitu kwa sababu mke wangu kaandaa chakula" kweli tukaenda hadi kwake na nikamwambia "yaani hata sijui unachoniitia mimi muhimu hivyo mi najua utanikwaza tu pale ntakapojua ni habari zako zisizobadilika"
Nilifika na kumkuta mke wake na alifurahi sana kuniona na kwa sababu ananifahamu kwa sababu anajua mimi nilikuwa kijiweni tu sema nimepata pesa nimetoboa kwahiyo kimaisha hatufanani lakini ni mwanamke anayenifahamu basi nami nilitamani kujua nini hasa hadi wameniita mpaka huku na huyu mama aliandaa chakula lakini mimi niliwaambia nimeshiba lakini yule mama akasema "hiki ni chakula maalum kwa ajili yako maana nimemwambia mume wangu natamani kumuona Rojas angalau tule nae chakula akanambia ratiba zako zimekuwa ngumu ,ninamshukuru Mungu sana angalau leo umekuja asante sana shemeji yangu yaani nimefurahi sana" nikasema "asante"
Tukala pale na kiukweli chakula kilikuwa kitamu sana,huyu shemeji yangu alikuwa mahiri katika mapishi,baada ya kula na kupumzika kidogo kupisha chakula kishuke tumboni yule shemeji yangu alinambia "Rojas nimekwita,naomba unisamehe mimi ndiye nilikwita baada ya kuzungumza na mume wangu nikaona nimshirikishe kiundani ili akuambie tuonane lakini mimi ningesema nije pengine usingeweza kunielewa lakini kwa sababu najua unamheshimu ndugu yako huyu nikasema ngoja nimtumie huyu huyu angalau tuzungumze,nikawa najiuliza sasa huyu mama anataka kuniambia nini? Akaniambia "Rojas wewe ni ndugu yetu kabisa,sisi tunakuhesabu ni ndugu yetu lakini pia wewe ni bosi wetu,utanisamehe kwa maneno ambayo nitazungumza lakini nayazungumza haya yanatoka ndani ya moyo wangu,moyo wangu unaugua sana juu ya maisha yako,moyo wangu unajeruhika kuhusu maisha yako,najua sitakiwi kuzungumza chochote kwa habari ya maisha yako lakini mara zote nimekuwa nikimwambia mume wangu Rojas kila ninapomtizama usoni nikipata nafasi simuoni Rojas katika macho yake,simuoni Rojas hata nikimtazama naona mtu mwingine na sio Rojas" mimi nikacheka na nikamwambia "kwanini unasema hivyo shemeji yangu,kwanini useme hivyo? Akasema "ni kweli,samahani kwa kukwambia haya pengine nakosea lakini Rojas umebadilika sana na mabadiliko yako sio mazuri sana" wakati ananielezea haya maneno hasira zikawa zinajijenga kichwani mwangu na kujiuliza huyu ananifatilia maisha yangu kama nani.
Unajua ukiwa na pesa kuna watu wakiongea unakuwa unawaona kama sijui wanaongea nini au waongee haraka haraka amalize na unaona kama anakupotezea muda ndio mimi kwa huyu mama nilikuwa nataka kusikia haraka haraka kwa sababu mume wake kanitoa sehemu napata moja mbili nimfanya heshima nimekuja huku alafu huyu mtu anakuja kama kunisema,kama maonyo flani alafu yeye kama nani kwangu yaani ila nikajitahidi kujicontrow hasira zangu,akanambia "nimemwambia mume wangu na mimi nakuambia wewe unahitaji msaada na msaada unaohitaji wewe ni msaada wa kumruhusu Mungu aingilie kati kwenye pesa zako,pesa zako zinamhitaji Mungu Rojas,pasipo Mungu utajiri wote si kitu maana utajiri huo utakupeleka kaburini mapema kabla ya wakati,Mungu anataka wewe uishi miaka mingi na mpaka amekupa hizo pesa ina maana ana mpango mzuri sana wakuwasaidia watu ambao ni wahitaji,kuwatia moyo wengine pia na kufanya vitu vikubwa ambapo utaajiri watu zaidi ya mume wangu ambaye umempa ajira kwahiyo Mungu anategemea wewe utafungua miradi mikubwa na hiyo miradi utaajiri watu lakini shetani amedaka pesa zako,amedaka umiliki wa pesa zako,sasa hivi shetani ndio anatumia pesa zako kwa sababu wewe haujamruhusu Mungu yeye ndio atawale hizo pesa zako" maneno haya nayakumbuka mpaka kesho katika safari ya maisha yangu,mpaka kesho na nafikiri ntaendelea kuyakumbuka,nilimuangalia huyu mama na kumwambia "kwanini unaniambia hivyo? Akanambia "kwa sababu nakujua Rojas,nakujua Rojas,najua harakati zako,najua mapambano yako,najua hata changamoto ulipitia kipindi kile ambapo tulilia na kukuombea sana ili usiendelee kubaki kwenye matatizo lakini Mungu leo amekupa pesa na mimi naaminini ni Mungu ndio kakupa pesa lakini pesa leo zimegeuka zimekufanya wewe umekuwa mtumwa,Rojas umekuwa mtumwa,wewe sio Rojas mwenye sifa mbaya,sio Rojas wakuumiza mioyo ya wanawake,wewe ni Rojas mtu mwenye busara tena ni mtu mwenye upendo sana,ni mtu ambaye unajituma sana,ni mtu ambaye ni mfano wa kuigwa,mimi nimekuita kwa sababu nataka tuombe pamoja tumruhusu huyu Mungu atawale pesa zako,unatakiwa uwe unamtolea Mungu,ukimtolea Mungu,Mungu atalinda pesa zako,sasa hii ni elimu pana sana kwa sababu utajiri unalindwa wenzako unaowaona wanamiliki utajiri na utajiri unadumu wana njia zao ambazo wanalinda pesa zao,wengine pesa zao si pesa za kawaida ni pesa za sadaka,wanatolea sadaka pesa zao,utajiri wao sasa wewe umezipata pesa je uko upande gani? Uko upande wa shetani? Mi naamini Rojas hauko upande wa shetani kwa sababu nakujua wewe,nakujua wewe kuwa moyo wako hauko uko kwenye kutumika na mashetani kwa ajili ya kupata pesa,pesa hizi umezipata kwa njia halali Mungu amekupa wewe ndio unajua lakini basi mpendeze Mungu kwa pesa hizi alizokupa,zilinde hizi pesa ili ziendelee kudumu na wewe,unajua kwanini watu uwa wanatajirika alafu wanakuja kufirisika kabisa? Pengine wamesahau sijui wewe katika utajiri wako kwa nafasi ya utandawazi sasa hivi pengine unaweza kupata hiyo nafasi" lakini mimi watu wengi wanajipendekeza kwangu,watu wengi wananiambia mazuri ninayopenda kuyasikia mabaya hawanambii kwa sababu ukinikorofisha wanahisi pengine sitakupa nafasi,ukiniomba kitu labda nitakunyima lakini huyu mama alinieleza haya mambo ambayo sijawahi kuelezwa na mtu.
Tuliongea kwa kirefu pale na yule rafiki pamoja na shemeji yangu na akajaribu kunipa njia tofauti tofauti ya namna gani naweza kutoa sadaka ya shukrani na ya kuweza kupata ulinzi wa Mungu kwa pesa zangu na katika mapendekezo aliyonipa kulikuwa na pendekezo la kuhudumia kituo cha watoto yatima nami bila kusita nikakubaliana na kuamua kubeba jukumu la kukihudumia kituo flani na kwa kuanza siku iliyofuata tukaelekea pale kituoni kuona mazingira yake,mahitaji yake na mengineyo,kiukweli niliumia na hali niliyoikuta pale kituoni na nikaamua mara moja kufanya ukarabati wa miundombinu na pia kuongeza fungu la chakula na mahitaji mengine ya lazima,niliwaunganisha wahusika wa kituo na mhasibu wangu endapo kama kutakuwa na changamoto yoyote basi wanaweza kumtafuta huyo kwa haraka kuweza kukamilisha kwa wakati na tukajumuika na watoto wale mimi,shemeji yangu pamoja na watu kadhaa waliofika na tukapata chakula cha pamoja na watoto walishukuru sana wao na walezi wao kwa ujumla,baada ya zoezi na wenzangu tuliaga na kuahidi muda si mrefu nitafika tena kuja kuwatembelea hawa vijana.
ITAENDELEA!