Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha ‘Sitasahau’ cha Radio Free Africa​



Sehemu ya 17



Nilipata muda kweli kwa sababu moyo wangu ulijaa vitu na mtu ambaye labda naweza nikazungumza nae kwa uhuru pengine nikazungumza zaidi ni yule kaka wa kule gerezani kwani ndio anayejua mambo yanayoendelea kwenye maisha yangu lakini nimekuwa nikitunza siri nyingine kwa kuwa kaka nilishawahi kumshirikisha japo sikumshirikisha kaka wapi pesa zangu natunza,mifumo yangu ya pesa iko vipi ingawa kaka alijitahidi kwa hali zote lakini kwa hilo hakufanikiwa pengine amefanikiwa yale aliyoyaamini ni ya maana sana kwa sababu kaka yangu amefanikiwa mpaka kujenga,kiukweli nimegeuka kuwa baraka kwa familia yangu sio kama najisifia kiukweli sikula pekeyangu kwani hata sasa hivi nakosa amani mimi ila kuna watu wanafurahia pesa ambazo nimezipata,nakumbuka maneno ambayo nilimwambia Mungu. Unaambiwa Mungu ni wa sisi sote,Mungu ni wa wote wenye mwili haijalishi,ni maneno ambayo niliambiwa na yule mama na ni kweli mimi najua hivyo lakini kuyaishi katika hilo ndio shughuli,nalijua hilo na navyoambiwa tena na tena nakuwa napata msisitizo na ninakumbushwa kile ambacho najua.

Nilizungumza maneno haya "Mungu mimi ni mkosaji sana mbele zako na pia nimemkosea rafiki yangu ambaye nilishawahi kuapa mbele zako kwamba nitafata yale aliyoniambia lakini nimeenda kinyume na vile niliwahi kuahidi,nasikia huzuni ndani yangu,nasikia kukosa raha ndani yangu,naomba Mungu wangu unisaidie,naomba kwanza unisamehe lakini pia unisaidie,hali ya huzuni ninayoisikia,kukosa raha ninakokusikia kusiendelee kudumu katika maisha yangu" sikuwa na mengi yakusema kwa sababu na mengi yakusema na Mungu yapi? Yaani sina kwa sababu pia mimi sikuwa muombaji kwamba najua kuomba na nini kwahiyo nilizungumza hayo kwakuwa ndio yalikuwa yanajaza moyo wangu.nilichokuwa nataka ni amani ya moyo,hicho tu ndio nahitaji,ushawahi kukosa amani? Pengine katika maisha ushawahi pitia situation kama hiyo yaani unakosa amani kabisa,unakosa raha kabisa,yaani hiyo hali ndio mimi naipitia kwa sasa hivi.

Nakumbuka baada ya kuzungumza maneno hayo nikalala na kukapambazuka na yule shemeji yangu alinipigia akanambia "vipi Rojas unajisikiaje? Nikamwambia "najisikia vizuri" akanambia "muda wowote,wakati wowote ukitaka kwenda pale kituoni waweza kwenda pale ukakaa na watoto kwani ni faraja tosha sana "nikamwambia "sawa nikijisikia ntafanya hivyo"

Wakati hizi harakati zote kuanzia yule mshkaji wangu dereva taxi kunialika kwake,mke wake kuniambia juu ya kujiepusha na shetani na kumrejea Mungu hadi harakati za kwenda kule katika kituo cha watoto yatima na kufanya haya maombi kwa Mungu mtaani nilikuwa na mwanamke ambaye ndio alikuwa amenishika hatamu,huyu mwanamke kiukweli amekuwa kwenye maisha yangu kwani nimekutana na wanawake wengi lakini huyu alifanikiwa kuninasa kwa sehemu kubwa sana vitu vingi sana nimeshamfanyia kwani nimewekeza,nimewekeza na nimewekeza tena yaani nimekutana na mwanamke ambaye anajua kuchuna,kweli nimetumika na nikakubali kutumika kwa sababu nilimpenda mwanamke huyu,kwahiyo hata yeye ananiuliza "beby vipi mbona sikuelewi? kwa sababu anaona si kawaida yangu "au umesharudi kwenye mambo yako? Yaani nimesharudi kujichanganya tena na wanawake wengine kwa sababu yeye ndio mwanamke aliyefanikiwa sana kunikamata yaani kwa sababu anajua mimi nina kona kona kwahiyo muda mwingi akawa ananishika na mimi kwa sababu nampenda nikajikuta kuna muda hata naona ngoja nikae na huyu,ngoja nikae na huyu kwahiyo hata idadi ikapungua na hata kuna wanawake walizidi kunisumbua kwa sababu mimi ni mtu wakutoa sana pesa na sio hivyo tu kuna wanawake nilikuwa nimewapangia,kuna wanawake walikuwa wanaendelea kusoma vyuo uko mimi ndio nalipa ada kwahiyo sasa wanakucheki tena ili uweze kuwawezesha sasa huyu mwanamke akawa ananibana kwelikweli kwani hata simu akawa anapokea yeye "wewe ni nani nakuuliza wewe ni nani?" kwa sababu mimi nilikwama hapa sikuona shida hata nikiwapoteza hao,yaani sio muhimu kwangu,kwahiyo alipoona hali kama hiyo kwangu alinambia "ni nini ambacho unapitia? Nikamwambia "nina hali naipitia sio ya kawaida,sina amani,moyo wangu hauna amani" "kwanini sasa? Nikamwambia "hata sielewi" akanishawishi kuhusu pombe na nini lakini kuna hali flani unafikia ya kukosa amani hata pombe ukinywa haisikii,yaani mi nasikia roho inaangaika tu inaangaika kweli kweli na hata akanambia "au wenzako wanaanza kukuchezea? michezo ya kuchezeana hivi labda kulogwa,nikasema "hata sijui" "eeh kwa sababu gani usikie hivyo,kwanini usikie hivyo wakati una vitu vyako unavipenda ukivifanya uwa unaskia raha? Mengi ambayo aliniambia hata washkaji waliniambia kwa mfano niliwaeleza nilishaanza kutumia vilevi mbalimbali mpaka madawa ya kulevya nikawa nimeshaingia umo lakini sikusikia relief,sikusikia nafuu yoyote.

Baadae nakumbuka nilipokaa nikiendelea kupitia katika hali kama hii niliamua kutoka tena na kwenda tena kumuona mshkaji kule gerezani,nimefika hapo nikaambiwa hali yake ilikuwa sio nzuri yupo anapata matibabu nikafosi sana mimi nipate nafasi ya kumuona tuzungumze nae,nikapewa tarehe niweze kuja ili naweza nikamuona,mambo yakawa ni mengi,utaratibu ukawa umenivuruga kwelikweli lakini nikawa siko sawa lakini nilipigania hilo,nilipigania kumuona hadi nikapata nafasi ya kumuona rafiki yangu ambaye nilimuhesabu kama kaka yangu,mengi tulipanga pamoja nyakati ambazo nilikwenda gerezani lakini baadae nikabadilika,nikambadilikia nikaishi katika njia yangu na nikaiacha njia yake ambayo yeye aliitamani aiishi akiwa uraiani,nilipata nafasi ya kumuona kiukweli alikuwa mgonjwa sana,nasikia hatia ndani ya moyo wangu,mshkaji ana hali mbaya,ana hali mbaya sana na mimi ni kama ndio ndugu niliyebaki,yaani kuna watu wamefungwa gerezani,yaani watu wanasahaulika,unasahaulika na vizazi vyako wote wanakusahau wewe,hakuna watu wanakuja kukutembelea,hakuwa watu wanakuja kukuona yaani wewe uko uko pambana na mazingira yako ndio hali ya mshkaji na mshkaji aliniamini sana mimi na akiamini sitamuacha kama ambavyo nilivyomuacha kwahiyo sasa hivi mimi kinachonipitisha katika wakati mgumu ni kusikia hatia ndani ya moyo wangu lakini Mungu ni mwema.
Mungu alimsaidia akarecovery akarejea katika maisha yake ya kawaida hicho ndicho kitu nimemshukuru sana Mungu,nikamwambia "natamani niwe sehemu ya mtu ambaye tutaipigania afya yako iweze kuamka tena,uweze kupata matibabu ya uhakika na mimi kwa sababu niko hapa sitakuacha uondoke kwa huo ugonjwa,tutapigana kadri tunavyowezakwa sababu madaktari wanasema kuna njia tu nzuri ya kupata matibabu" nakumbuka aliniambia "kama itakupendeza hivyo basi nitashukuru" alikuwa amepunguwa sana mtu huyu,nikamwambia "basi sawa" akaniuliza hali za watoto nikawaambia wanaendelea vizuri na akanambia "Rojas waweza leo kugeuza kichwa chako na kunigeuzia kisogo chako na kuanza safari kwenda kwenye majukumu yako lakini kuna siku Rojas utakuja na hautanikuta na pengine utaambiwa tayari nimeshazikwa" nikamwambia "hapana kwanini unasema hivyo,usiseme maneno kama hayo" akanambia "Rojas mimi nimeshakusamehe na hata kama utakuja hapa na ukanikosa mimi nimeshakusamehe Rojas.

Nimekusamehe wewe na kizazi chako wote nimewasamehe,nilifanya kwa mapenzi yangu lakini nimeona vile moyo wako umerudi,umenipigania sana kwa mazingira magumu ambayo si rahisi lakini umepenya,umehakikisha napata matibabu,umenipigania na hata watu wanauliza ni nani huyu anayempigania mtu huyu amesahaulika humu gerezani na hata watu wanataka kujua ni nani huyu anayempigania lakini kumbe umerudi katika ule urafiki wetu wa mwanzo,umerudi kwenye undugu ule ambao tuliuanzisha mwanzoni na mimi hata leo Mungu ananichukua napumzika nitakuwa na amani kwa sababu najua kama umerudisha mapenzi kwangu ndivyo utakavyoendelea kuwakumbatia watoto wangu ,ndivyo utakavyowashika mpaka wakuwe wakubwa na naamini wewe utashiriki katika baraka na mafanikio yao,hautawaacha,utawafanya sehemu ya familia yako" maneno yaliniumiza sana na kunifanya kujisikia kuumia sana,mtu huyu anawapenda watoto wake sana lakini maisha yanavyokwenda tofauti na jinsi ambavyo mtu unaweza ukawaza,mtu ambaye amesahaulika gerezani na anaonekana atadumu maisha yote uko matumaini kwenye mioyo ya watu haipo na huyu mama ni kitu ambacho alikataa yaani mama wa watoto ambao alipaja na huyu baba alisema "

Hata siku moja usije ukawatonesha watoto wangu vidonda ukaenda kuwaonesha baba yao ambaye alifanya uovu na yuko gerezani na atafia uko uko gerezani,sitaki watoto wangu wawe na kumbukumbu za kuwaumiza mimi mama yao nipo na nitapambana,ndugu zake akina nani wote walishamtelekeza" kwahiyo nilisikia pain sikutakiwa kumtenda haya mtu huyu pengine mimi naye tungeshikamana kwa mazingira yoyote labda apate haki,apate uhuru kwa sababu kwa maelezo huyu mtu alifungwa kwa kile ambacho anastahiki,nilimwambia "rafiki yangu,ndugu yangu najua ninaondoka nitarudi nitakukuta na tutazungumza pamoja na naondoka mimi nikiwa na mawazo ya kwamba matibabu sahihi yanahitajika,kukupigania nilikokukupigania sasa hivh naenda hatua ya mbele zaidi kwa pesa hizi ambazo zipo nataka kupenya mahali ambapo sio rahisi kupenya ili wewe upate matibabu sahihi iwe kwa kuhonga,iwe kwa kufanyaje mimi ntafanya kwa ajili yako" aliniambia "sawa basi utaenda kuwasalimia pia nyumbani,Rojas pata mke sahihi,oa,oa mke sahihi mwenye upendo wa kweli jenga nae maisha upate nae watoto.watoto ni baraka usiendelee tu kuwa na wanawake wa kila namna,wakati ufike uoe na ujenge maisha yako yenye furaha" yaani nikawa nakinzana na maneno anayoyazungumza kwa sababu naona kwanini aniambie hivi na wakati mimi ntarudi na harakati za matibabu zitaendelea.

Niliondoka japo sikutaka kuondoka,nilikaa hapa toka nimekuja kujua mgonjwa kwa awamu hii sikutulia ina maana niliendelea kuhakikisha mtu huyu anapata matibabu,nikakaa wiki mbili nikiwa mbali kabisa na mazingira yangu,nimerudi mtu ukiwa na pesa na una kundi kubwa sana la watu unapokuwa hupatikani huonekani kuna watu wanateseka ,kuna watu wanataabika kweli kweli wote wanataabika uko wapi wakati umeshawajuza kuwa niko mbali kidogo nina majukumu yangu binafsi,watu ambao wamezoea kufanya starehe na wewe wanapata shida kweli kweli.
Kwahiyo niliporudi kampani yangu inataka tujoin tena inataka kula raha na maisha mengine yaendelee,nakumbuka nilikataa,nilikataa nikasema "siko sawa leo,nahitaji muda wa kupumzika lakini nitalipa bili,chochote mtakatumia ntaniambia mtaclea bili ntalipa" walistahajabu yaani mimi Rojas nina nguvu hizo za kutoa wapi kwa sababu chakula changu ni pombe na ni sehemu ya starehe na mimi mara zote uwa nasema hakuna starehe nyingine zaidi ya pombe,pombe ndio starehe,mwanaume unatakiwa unywe pombe,mwanaume unatakiwa uwe na watoto wazuri yaani wanawake warembo ndio furaha ya mwanaume,nini unaweza kufurahia mwanaume unafanya kazi kwa bidii pata muda uenjoy katika hivyo vitu,kwahiyo mimi ndio nimekuwa naviona vilevi na wanawake ndio starehe yangu lakini sasa najiona nimekata mood kabisa,siko sawa,mimi ni mlevi sana lakini ukiniuliza nasemaje sina mood nikashindwa kunywa pombe kwa wale watumiaji wa vilevi wanaelewa yaani ukiwa na msongo wa mawazo ukataka kushushia kidogo angalau uwe sawa lakini mimi siko sawa nasema sijisikii kunywa ,hayo ni mabadiliko mapya ndani yangu kwa sababu hata washkaji waliniambia hauko sawa,kwa tunaokujua wewe hauko sawa,wako marafiki wao furaha yao wewe ulewe,wewe uchangamke kwa sababu kuchangamka kwako kunakufanya wewe ufanye ya zaidi ambavyo ungekuwa kawaida usingevifanya sasa kwa mfano kama mshkaji amekwambia "mshkaji hapa ana shida ya hela" "shilingi ngapi? "Milioni" ukiwa na akili timamu utasema "ah mshkaji wewe si nilikupa siku flani tena" lakini ukishalewa mtu akikupa sifa "aah Rojas wewe ndio mwenyewe bwana,wewe ndio baba lao,hakuna mtu kama wewe Rojas" unaona pombe pamoja na sifa zinaenda kwelikweli unajikuta unasema "kitu gani,baadae njoo uchukue ile hela" hata kama mwanzo ulikuwa haujaplan lakini kwa sababu ya sifa unajikuta unafanya,kwahiyo wale washkaji wanasikitika nini nimepatwa na nini lakini ni mabadiliko automatically nilianza kuyaona kwangu lakini ni nyakati ambazo niliendelea kushikilia msimamo wangu mpya.

Nilipata wasaa wa kwenda kuwasabahi watoto na katika wale watoto kuna mmoja kati ya hawa watoto anafanana sana na yule mshkaji kule gerezani,anafanana nae sana basi stori mbili tatu nikafurahi kupiga nao stori nikamkumbuka sana na nikasema "nikipata muda ntapigana sana ili niweze kwenda" kwahiyo katika ratiba ya jumapili ile baada ya kuachana na wale watoto nikasema "jumanne sasa yaani uko naweza nikatumia muda mrefu zaidi kwa ajili ya kukamilisha hilo zoezi.

Nakumbuka jumanne niliyotaka kusafiri mambo yangu yalikuwa hayakukaa vizuri,sijasettle mambo kwahiyo nikapanga siku za mbeleni ikishindikana basi ijumaa niondoke au jumamosi niondoke niende kule,nakumbuka nilipigiwa simu,mimi kutokana na hali ya mshkaji nilihakikisha napata taarifa vile anavyoendelea na ukiniuliza ni kwa namna gani yaani ni kwa namna yoyote inayowezekanaga taarifa ya kile kinachoendelea,siku za mwanzo sikufanya hivyo na ndio maana hata taarifa za mtu huyu kuhamishwa kwenda gereza jingine mimi taarifa sikuwanazo lakini mimi safari hii niliona anastahili mtu wa kumuangalia,kwahiyo nilipokea simu na nilipopokea akanambia "bwana Rojas unaendeleaje? Nikamwambia "naendelea vizuri,simu yako ina jambo jema? Akanambia "sina jambo jema,wewe ni mwanaume siwezi kusema nitapoteza muda maana sina habari nzuri,nina habari mbaya sana" nikastuka sana na nikamuuliza "ni nini kinaendelea" akasema "ulisema utakuja lakini ndugu yako hali yake imebadilika sana,amefunga kauli,amefunga kauli tunajitahidi kama utaweza kumuwahi pengine unaweza hata ukawahi kumuona maana hawezi kuongea chochote,unaweza kumuwahi hata dakika za mwisho hata ukamuaga bwana"

Kiukweli nilistuka sana,kwa wema alionitendea na pesa aliyoielekeza kwangu na kufikia leo mimi kuwa nilivyo je ana ndugu wangapi lakini ameniamini mimi tena kwa kauli yake kuwa "sina ndugu aliye karibu na mimi wote wamenitelekeza gerezani basi nitampa mtu ambaye moyo wangu utanisukuma kumpa" na akaniona mimi kijana deiwaka wa mtaa tu ambaye nimebambikiwa kesi nikaenda gerezani akanitunuku hizo pesa "nenda bwana katika harakati zangu mimi kuna pesa nilishawahi kuzipata,nenda utaziona na ukizipata njoo bwana tuzungumze" lakini mimi ndani yangu mambo ya uovu yakapata nafasi,nilijisikia shauku na hata sikuweza kulala siku hiyo,nikawasha gari na moja kwa moja kuanza safari,nilianza safari ili nifike niweze kukutana na mtu huyu angalau niweze kumuona,naambiwa amefunga kinywa sijui Mungu anaweza kufanya muujiza wake wowote jambo likatokea lolote hata akazungumza na mimi kwa machache.
Nilipata nafasi ya kufika mahali hapa lakini moyo wangu ulikuwa unaugua sana katika maisha yangu ninapoyazungumza haya,nimefika shauku niliyonayo nimkute mtu huyu lakini nikawa nimechelewa,nimemkuta mtu huyu amepoteza maisha ,kwenye maisha yangu nimekutana na misiba mingi mpaka nimefika hapa,naweza nikalia waweza kuniona mnafikikwa sababu kama nilikuwa rafiki mwema mtu ambaye aliyenibadilishia maisha je nilistahili kumtelekeza nilivyomtelekeza?

Mbona sikwenda kumpelekea hata mahitaji? Tena ndugu zetu waliopo gerezani wanahitaji sana faraja wakati natumia mali ambazo amekuwa sababu ni yeye,nakula vyakula vizuri vyakunona sikuwa namuwazia yeye kumpelekea hata kipande cha sabuni? Sikuweza kumuwazia chochote mbona nilimtelekeza,unaweza kuniona mnafiki,moyo wangu uliugua na kujisikia vibaya sana,nikasema mimi naweza kuwa katika kundi la wanadamu wanaowavunja moyo watu wema kuwatendea binadamu wengine wema kwa sababu mimi nilitendewa wema lakini mimi sikutenda wema kwa mtu huyu,kwanza nimekuwa na mahusiano na mwanamke ambaye alinizuia nisiwe na mahusiano nae,mengi ambayo tumepanga pamoja mengi nimeenda kinyume nae lakini leo hayupo tena akiniambia "Rojas mimi nimekusamehe wewe na kizazi chako,niliyafanya kwa mapenzi mema kabisa"

Hakuna kuugua moyo kukubwa na kuzito kama unajiona ndani yako una usaliti,nilijisikia kusaliti pakubwa sana,nililia sana,nakumbuka niliomba "naombeni nipate nafasi mtu huyu nikampumzishe katika nyumba yake ya milele,mtu huyu nimjengee jeneza kubwa la thamani nikampumzishe mtu huyu,mtu huyu ambaye amepoteza ndugu zake wote baada ya yeye kupatwa na kesi gerezani,amesahaulika hana hata ndugu aliyekuwa anakuja kumuangalia,angalau basi nimpe heshima ya mwisho,angalau nimfanyie katika hili na kaburi lake nilijenge katika ustadi mkubwa" lakini haya yote nikiyazungumza utaniona mnafiki kwa sababu nilikuwa wapi angalau kwenda kumtembelea mtu huyu angalau hata kujua maendeleo ya kiafya angalau kuweza kupata matibabu mapema labda kutokana na pesa ambazo yeye mwenyewe alizitafuta na akanipa mimi,wema mtu huyu alionitendea umekuwa ni bure,mimi ni mmoja kati ya watu ambao nimetendewa wema na nimesikia hatia,najihukumu kwa kuchelewa kwangu kuja kumtembelea mtu huyu gerezani,nalia kama mtoto kwa sababu niliamini katika awamu hii ntakaporudi nitapenya zaidi kwa sababu utaratibu nilishaanza kuufanya ili mtu huyu apate matibabu anayostahili ili arudi arejee katika hali ya kawaida lakini mara zote amekuwa akiniambia "Rojas mimi maisha yangu pengine yanaweza yakaishia huku huku" ni mtu ambaye hakuwa na stress zozote za kutaka kurudi uraiani kwa sababu nilikuwa namsisitiza akawa ananambia "wewe nenda kayafanye hayo kwanza" lakini mimi ndio nilikuwa wakwanza kutokomea na kutaka uhuru wa pesa ambazo aliyezitafuta ni mtu mwingine.




ITAENDELEA!
 
story nzuri sana
lakini mbona maneno yanarudiwarudiwa sana?
Ndugu hoja yako ina tija ila changamoto ninayoipata kwanza ninakubali urudiaji wa maneno unapunguza ladha,pili mimi ni mpya katika fani ya uandishi naomba kuvumiliwa ktk hilo na naamini kupitia ukosoaji chanya nami ntakuwa bora siku moja,tatu kama nilivyosema awali masimulizi yako katika mfumo wa sauti nami nayaleta ktk maandishi na msimuliaji anaswaga hizo nami najikuta ktk uandishi wangu naingia ktk mtego wa kurudiarudia maneno,nne kutokana na wingi wa maneno na kubanwa na harakati nyingine nakuwa nakosa muda wa kuweza kuhariri ingawa hata hayo unayoyasoma nimejitahidi sana kupunguza urejeaji wa matamshi,tano natumai nitakapoleta kisa kingine nitajitahidi kuzingatia hilo na mengine kadri nitakavyojaaliwa kwani hata ukitazama paragraph unajua tu huyu mwandishi bado Lena katika fani.
NB: Mfano sehemu ya 12 wakati nataka kuipost saa 12 jioni episode siioni ikanilazimu kuanza kuiandika upya na muda wa saa 4 hv usiku ndio nikaihitimisha na kuweza kuipost,sasa hapo hata kama kumekosewa neno inakuwa ngumu kurekebisha,tuvumiliane ndugu zangu natumai siku moja tutapata hadithi nzuri yenye mpangilio mzuri kuanzia uandishi hadi mvuto wa maneno kwani nakuwa nasikiliza na kuandika kwa kutumia simu,mbarikiwe wasomaji!
 
Ndugu hoja yako ina tija ila changamoto ninayoipata kwanza ninakubali urudiaji wa maneno unapunguza ladha,pili mimi ni mpya katika fani ya uandishi naomba kuvumiliwa ktk hilo na naamini kupitia ukosoaji chanya nami ntakuwa bora siku moja,tatu kama nilivyosema awali masimulizi yako katika mfumo wa sauti nami nayaleta ktk maandishi na msimuliaji anaswaga hizo nami najikuta ktk uandishi wangu naingia ktk mtego wa kurudiarudia maneno,nne kutokana na wingi wa maneno na kubanwa na harakati nyingine nakuwa nakosa muda wa kuweza kuhariri ingawa hata hayo unayoyasoma nimejitahidi sana kupunguza urejeaji wa matamshi,tano natumai nitakapoleta kisa kingine nitajitahidi kuzingatia hilo na mengine kadri nitakavyojaaliwa kwani hata ukitazama paragraph unajua tu huyu mwandishi bado Lena katika fani.
NB: Mfano sehemu ya 12 wakati nataka kuipost saa 12 jioni episode siioni ikanilazimu kuanza kuiandika upya na muda wa saa 4 hv usiku ndio nikaihitimisha na kuweza kuipost,sasa hapo hata kama kumekosewa neno inakuwa ngumu kurekebisha,tuvumiliane ndugu zangu natumai siku moja tutapata hadithi nzuri yenye mpangilio mzuri kuanzia uandishi hadi mvuto wa maneno kwani nakuwa nasikiliza na kuandika kwa kutumia simu,mbarikiwe wasomaji!
Very humble
 

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha ‘Sitasahau’ cha Radio Free Africa​



Sehemu ya 17



Nilipata muda kweli kwa sababu moyo wangu ulijaa vitu na mtu ambaye labda naweza nikazungumza nae kwa uhuru pengine nikazungumza zaidi ni yule kaka wa kule gerezani kwani ndio anayejua mambo yanayoendelea kwenye maisha yangu lakini nimekuwa nikitunza siri nyingine kwa kuwa kaka nilishawahi kumshirikisha japo sikumshirikisha kaka wapi pesa zangu natunza,mifumo yangu ya pesa iko vipi ingawa kaka alijitahidi kwa hali zote lakini kwa hilo hakufanikiwa pengine amefanikiwa yale aliyoyaamini ni ya maana sana kwa sababu kaka yangu amefanikiwa mpaka kujenga,kiukweli nimegeuka kuwa baraka kwa familia yangu sio kama najisifia kiukweli sikula pekeyangu kwani hata sasa hivi nakosa amani mimi ila kuna watu wanafurahia pesa ambazo nimezipata,nakumbuka maneno ambayo nilimwambia Mungu. Unaambiwa Mungu ni wa sisi sote,Mungu ni wa wote wenye mwili haijalishi,ni maneno ambayo niliambiwa na yule mama na ni kweli mimi najua hivyo lakini kuyaishi katika hilo ndio shughuli,nalijua hilo na navyoambiwa tena na tena nakuwa napata msisitizo na ninakumbushwa kile ambacho najua.

Nilizungumza maneno haya "Mungu mimi ni mkosaji sana mbele zako na pia nimemkosea rafiki yangu ambaye nilishawahi kuapa mbele zako kwamba nitafata yale aliyoniambia lakini nimeenda kinyume na vile niliwahi kuahidi,nasikia huzuni ndani yangu,nasikia kukosa raha ndani yangu,naomba Mungu wangu unisaidie,naomba kwanza unisamehe lakini pia unisaidie,hali ya huzuni ninayoisikia,kukosa raha ninakokusikia kusiendelee kudumu katika maisha yangu" sikuwa na mengi yakusema kwa sababu na mengi yakusema na Mungu yapi? Yaani sina kwa sababu pia mimi sikuwa muombaji kwamba najua kuomba na nini kwahiyo nilizungumza hayo kwakuwa ndio yalikuwa yanajaza moyo wangu.nilichokuwa nataka ni amani ya moyo,hicho tu ndio nahitaji,ushawahi kukosa amani? Pengine katika maisha ushawahi pitia situation kama hiyo yaani unakosa amani kabisa,unakosa raha kabisa,yaani hiyo hali ndio mimi naipitia kwa sasa hivi.

Nakumbuka baada ya kuzungumza maneno hayo nikalala na kukapambazuka na yule shemeji yangu alinipigia akanambia "vipi Rojas unajisikiaje? Nikamwambia "najisikia vizuri" akanambia "muda wowote,wakati wowote ukitaka kwenda pale kituoni waweza kwenda pale ukakaa na watoto kwani ni faraja tosha sana "nikamwambia "sawa nikijisikia ntafanya hivyo"

Wakati hizi harakati zote kuanzia yule mshkaji wangu dereva taxi kunialika kwake,mke wake kuniambia juu ya kujiepusha na shetani na kumrejea Mungu hadi harakati za kwenda kule katika kituo cha watoto yatima na kufanya haya maombi kwa Mungu mtaani nilikuwa na mwanamke ambaye ndio alikuwa amenishika hatamu,huyu mwanamke kiukweli amekuwa kwenye maisha yangu kwani nimekutana na wanawake wengi lakini huyu alifanikiwa kuninasa kwa sehemu kubwa sana vitu vingi sana nimeshamfanyia kwani nimewekeza,nimewekeza na nimewekeza tena yaani nimekutana na mwanamke ambaye anajua kuchuna,kweli nimetumika na nikakubali kutumika kwa sababu nilimpenda mwanamke huyu,kwahiyo hata yeye ananiuliza "beby vipi mbona sikuelewi? kwa sababu anaona si kawaida yangu "au umesharudi kwenye mambo yako? Yaani nimesharudi kujichanganya tena na wanawake wengine kwa sababu yeye ndio mwanamke aliyefanikiwa sana kunikamata yaani kwa sababu anajua mimi nina kona kona kwahiyo muda mwingi akawa ananishika na mimi kwa sababu nampenda nikajikuta kuna muda hata naona ngoja nikae na huyu,ngoja nikae na huyu kwahiyo hata idadi ikapungua na hata kuna wanawake walizidi kunisumbua kwa sababu mimi ni mtu wakutoa sana pesa na sio hivyo tu kuna wanawake nilikuwa nimewapangia,kuna wanawake walikuwa wanaendelea kusoma vyuo uko mimi ndio nalipa ada kwahiyo sasa wanakucheki tena ili uweze kuwawezesha sasa huyu mwanamke akawa ananibana kwelikweli kwani hata simu akawa anapokea yeye "wewe ni nani nakuuliza wewe ni nani?" kwa sababu mimi nilikwama hapa sikuona shida hata nikiwapoteza hao,yaani sio muhimu kwangu,kwahiyo alipoona hali kama hiyo kwangu alinambia "ni nini ambacho unapitia? Nikamwambia "nina hali naipitia sio ya kawaida,sina amani,moyo wangu hauna amani" "kwanini sasa? Nikamwambia "hata sielewi" akanishawishi kuhusu pombe na nini lakini kuna hali flani unafikia ya kukosa amani hata pombe ukinywa haisikii,yaani mi nasikia roho inaangaika tu inaangaika kweli kweli na hata akanambia "au wenzako wanaanza kukuchezea? michezo ya kuchezeana hivi labda kulogwa,nikasema "hata sijui" "eeh kwa sababu gani usikie hivyo,kwanini usikie hivyo wakati una vitu vyako unavipenda ukivifanya uwa unaskia raha? Mengi ambayo aliniambia hata washkaji waliniambia kwa mfano niliwaeleza nilishaanza kutumia vilevi mbalimbali mpaka madawa ya kulevya nikawa nimeshaingia umo lakini sikusikia relief,sikusikia nafuu yoyote.

Baadae nakumbuka nilipokaa nikiendelea kupitia katika hali kama hii niliamua kutoka tena na kwenda tena kumuona mshkaji kule gerezani,nimefika hapo nikaambiwa hali yake ilikuwa sio nzuri yupo anapata matibabu nikafosi sana mimi nipate nafasi ya kumuona tuzungumze nae,nikapewa tarehe niweze kuja ili naweza nikamuona,mambo yakawa ni mengi,utaratibu ukawa umenivuruga kwelikweli lakini nikawa siko sawa lakini nilipigania hilo,nilipigania kumuona hadi nikapata nafasi ya kumuona rafiki yangu ambaye nilimuhesabu kama kaka yangu,mengi tulipanga pamoja nyakati ambazo nilikwenda gerezani lakini baadae nikabadilika,nikambadilikia nikaishi katika njia yangu na nikaiacha njia yake ambayo yeye aliitamani aiishi akiwa uraiani,nilipata nafasi ya kumuona kiukweli alikuwa mgonjwa sana,nasikia hatia ndani ya moyo wangu,mshkaji ana hali mbaya,ana hali mbaya sana na mimi ni kama ndio ndugu niliyebaki,yaani kuna watu wamefungwa gerezani,yaani watu wanasahaulika,unasahaulika na vizazi vyako wote wanakusahau wewe,hakuna watu wanakuja kukutembelea,hakuwa watu wanakuja kukuona yaani wewe uko uko pambana na mazingira yako ndio hali ya mshkaji na mshkaji aliniamini sana mimi na akiamini sitamuacha kama ambavyo nilivyomuacha kwahiyo sasa hivi mimi kinachonipitisha katika wakati mgumu ni kusikia hatia ndani ya moyo wangu lakini Mungu ni mwema.
Mungu alimsaidia akarecovery akarejea katika maisha yake ya kawaida hicho ndicho kitu nimemshukuru sana Mungu,nikamwambia "natamani niwe sehemu ya mtu ambaye tutaipigania afya yako iweze kuamka tena,uweze kupata matibabu ya uhakika na mimi kwa sababu niko hapa sitakuacha uondoke kwa huo ugonjwa,tutapigana kadri tunavyowezakwa sababu madaktari wanasema kuna njia tu nzuri ya kupata matibabu" nakumbuka aliniambia "kama itakupendeza hivyo basi nitashukuru" alikuwa amepunguwa sana mtu huyu,nikamwambia "basi sawa" akaniuliza hali za watoto nikawaambia wanaendelea vizuri na akanambia "Rojas waweza leo kugeuza kichwa chako na kunigeuzia kisogo chako na kuanza safari kwenda kwenye majukumu yako lakini kuna siku Rojas utakuja na hautanikuta na pengine utaambiwa tayari nimeshazikwa" nikamwambia "hapana kwanini unasema hivyo,usiseme maneno kama hayo" akanambia "Rojas mimi nimeshakusamehe na hata kama utakuja hapa na ukanikosa mimi nimeshakusamehe Rojas.

Nimekusamehe wewe na kizazi chako wote nimewasamehe,nilifanya kwa mapenzi yangu lakini nimeona vile moyo wako umerudi,umenipigania sana kwa mazingira magumu ambayo si rahisi lakini umepenya,umehakikisha napata matibabu,umenipigania na hata watu wanauliza ni nani huyu anayempigania mtu huyu amesahaulika humu gerezani na hata watu wanataka kujua ni nani huyu anayempigania lakini kumbe umerudi katika ule urafiki wetu wa mwanzo,umerudi kwenye undugu ule ambao tuliuanzisha mwanzoni na mimi hata leo Mungu ananichukua napumzika nitakuwa na amani kwa sababu najua kama umerudisha mapenzi kwangu ndivyo utakavyoendelea kuwakumbatia watoto wangu ,ndivyo utakavyowashika mpaka wakuwe wakubwa na naamini wewe utashiriki katika baraka na mafanikio yao,hautawaacha,utawafanya sehemu ya familia yako" maneno yaliniumiza sana na kunifanya kujisikia kuumia sana,mtu huyu anawapenda watoto wake sana lakini maisha yanavyokwenda tofauti na jinsi ambavyo mtu unaweza ukawaza,mtu ambaye amesahaulika gerezani na anaonekana atadumu maisha yote uko matumaini kwenye mioyo ya watu haipo na huyu mama ni kitu ambacho alikataa yaani mama wa watoto ambao alipaja na huyu baba alisema "

Hata siku moja usije ukawatonesha watoto wangu vidonda ukaenda kuwaonesha baba yao ambaye alifanya uovu na yuko gerezani na atafia uko uko gerezani,sitaki watoto wangu wawe na kumbukumbu za kuwaumiza mimi mama yao nipo na nitapambana,ndugu zake akina nani wote walishamtelekeza" kwahiyo nilisikia pain sikutakiwa kumtenda haya mtu huyu pengine mimi naye tungeshikamana kwa mazingira yoyote labda apate haki,apate uhuru kwa sababu kwa maelezo huyu mtu alifungwa kwa kile ambacho anastahiki,nilimwambia "rafiki yangu,ndugu yangu najua ninaondoka nitarudi nitakukuta na tutazungumza pamoja na naondoka mimi nikiwa na mawazo ya kwamba matibabu sahihi yanahitajika,kukupigania nilikokukupigania sasa hivh naenda hatua ya mbele zaidi kwa pesa hizi ambazo zipo nataka kupenya mahali ambapo sio rahisi kupenya ili wewe upate matibabu sahihi iwe kwa kuhonga,iwe kwa kufanyaje mimi ntafanya kwa ajili yako" aliniambia "sawa basi utaenda kuwasalimia pia nyumbani,Rojas pata mke sahihi,oa,oa mke sahihi mwenye upendo wa kweli jenga nae maisha upate nae watoto.watoto ni baraka usiendelee tu kuwa na wanawake wa kila namna,wakati ufike uoe na ujenge maisha yako yenye furaha" yaani nikawa nakinzana na maneno anayoyazungumza kwa sababu naona kwanini aniambie hivi na wakati mimi ntarudi na harakati za matibabu zitaendelea.

Niliondoka japo sikutaka kuondoka,nilikaa hapa toka nimekuja kujua mgonjwa kwa awamu hii sikutulia ina maana niliendelea kuhakikisha mtu huyu anapata matibabu,nikakaa wiki mbili nikiwa mbali kabisa na mazingira yangu,nimerudi mtu ukiwa na pesa na una kundi kubwa sana la watu unapokuwa hupatikani huonekani kuna watu wanateseka ,kuna watu wanataabika kweli kweli wote wanataabika uko wapi wakati umeshawajuza kuwa niko mbali kidogo nina majukumu yangu binafsi,watu ambao wamezoea kufanya starehe na wewe wanapata shida kweli kweli.
Kwahiyo niliporudi kampani yangu inataka tujoin tena inataka kula raha na maisha mengine yaendelee,nakumbuka nilikataa,nilikataa nikasema "siko sawa leo,nahitaji muda wa kupumzika lakini nitalipa bili,chochote mtakatumia ntaniambia mtaclea bili ntalipa" walistahajabu yaani mimi Rojas nina nguvu hizo za kutoa wapi kwa sababu chakula changu ni pombe na ni sehemu ya starehe na mimi mara zote uwa nasema hakuna starehe nyingine zaidi ya pombe,pombe ndio starehe,mwanaume unatakiwa unywe pombe,mwanaume unatakiwa uwe na watoto wazuri yaani wanawake warembo ndio furaha ya mwanaume,nini unaweza kufurahia mwanaume unafanya kazi kwa bidii pata muda uenjoy katika hivyo vitu,kwahiyo mimi ndio nimekuwa naviona vilevi na wanawake ndio starehe yangu lakini sasa najiona nimekata mood kabisa,siko sawa,mimi ni mlevi sana lakini ukiniuliza nasemaje sina mood nikashindwa kunywa pombe kwa wale watumiaji wa vilevi wanaelewa yaani ukiwa na msongo wa mawazo ukataka kushushia kidogo angalau uwe sawa lakini mimi siko sawa nasema sijisikii kunywa ,hayo ni mabadiliko mapya ndani yangu kwa sababu hata washkaji waliniambia hauko sawa,kwa tunaokujua wewe hauko sawa,wako marafiki wao furaha yao wewe ulewe,wewe uchangamke kwa sababu kuchangamka kwako kunakufanya wewe ufanye ya zaidi ambavyo ungekuwa kawaida usingevifanya sasa kwa mfano kama mshkaji amekwambia "mshkaji hapa ana shida ya hela" "shilingi ngapi? "Milioni" ukiwa na akili timamu utasema "ah mshkaji wewe si nilikupa siku flani tena" lakini ukishalewa mtu akikupa sifa "aah Rojas wewe ndio mwenyewe bwana,wewe ndio baba lao,hakuna mtu kama wewe Rojas" unaona pombe pamoja na sifa zinaenda kwelikweli unajikuta unasema "kitu gani,baadae njoo uchukue ile hela" hata kama mwanzo ulikuwa haujaplan lakini kwa sababu ya sifa unajikuta unafanya,kwahiyo wale washkaji wanasikitika nini nimepatwa na nini lakini ni mabadiliko automatically nilianza kuyaona kwangu lakini ni nyakati ambazo niliendelea kushikilia msimamo wangu mpya.

Nilipata wasaa wa kwenda kuwasabahi watoto na katika wale watoto kuna mmoja kati ya hawa watoto anafanana sana na yule mshkaji kule gerezani,anafanana nae sana basi stori mbili tatu nikafurahi kupiga nao stori nikamkumbuka sana na nikasema "nikipata muda ntapigana sana ili niweze kwenda" kwahiyo katika ratiba ya jumapili ile baada ya kuachana na wale watoto nikasema "jumanne sasa yaani uko naweza nikatumia muda mrefu zaidi kwa ajili ya kukamilisha hilo zoezi.

Nakumbuka jumanne niliyotaka kusafiri mambo yangu yalikuwa hayakukaa vizuri,sijasettle mambo kwahiyo nikapanga siku za mbeleni ikishindikana basi ijumaa niondoke au jumamosi niondoke niende kule,nakumbuka nilipigiwa simu,mimi kutokana na hali ya mshkaji nilihakikisha napata taarifa vile anavyoendelea na ukiniuliza ni kwa namna gani yaani ni kwa namna yoyote inayowezekanaga taarifa ya kile kinachoendelea,siku za mwanzo sikufanya hivyo na ndio maana hata taarifa za mtu huyu kuhamishwa kwenda gereza jingine mimi taarifa sikuwanazo lakini mimi safari hii niliona anastahili mtu wa kumuangalia,kwahiyo nilipokea simu na nilipopokea akanambia "bwana Rojas unaendeleaje? Nikamwambia "naendelea vizuri,simu yako ina jambo jema? Akanambia "sina jambo jema,wewe ni mwanaume siwezi kusema nitapoteza muda maana sina habari nzuri,nina habari mbaya sana" nikastuka sana na nikamuuliza "ni nini kinaendelea" akasema "ulisema utakuja lakini ndugu yako hali yake imebadilika sana,amefunga kauli,amefunga kauli tunajitahidi kama utaweza kumuwahi pengine unaweza hata ukawahi kumuona maana hawezi kuongea chochote,unaweza kumuwahi hata dakika za mwisho hata ukamuaga bwana"

Kiukweli nilistuka sana,kwa wema alionitendea na pesa aliyoielekeza kwangu na kufikia leo mimi kuwa nilivyo je ana ndugu wangapi lakini ameniamini mimi tena kwa kauli yake kuwa "sina ndugu aliye karibu na mimi wote wamenitelekeza gerezani basi nitampa mtu ambaye moyo wangu utanisukuma kumpa" na akaniona mimi kijana deiwaka wa mtaa tu ambaye nimebambikiwa kesi nikaenda gerezani akanitunuku hizo pesa "nenda bwana katika harakati zangu mimi kuna pesa nilishawahi kuzipata,nenda utaziona na ukizipata njoo bwana tuzungumze" lakini mimi ndani yangu mambo ya uovu yakapata nafasi,nilijisikia shauku na hata sikuweza kulala siku hiyo,nikawasha gari na moja kwa moja kuanza safari,nilianza safari ili nifike niweze kukutana na mtu huyu angalau niweze kumuona,naambiwa amefunga kinywa sijui Mungu anaweza kufanya muujiza wake wowote jambo likatokea lolote hata akazungumza na mimi kwa machache.
Nilipata nafasi ya kufika mahali hapa lakini moyo wangu ulikuwa unaugua sana katika maisha yangu ninapoyazungumza haya,nimefika shauku niliyonayo nimkute mtu huyu lakini nikawa nimechelewa,nimemkuta mtu huyu amepoteza maisha ,kwenye maisha yangu nimekutana na misiba mingi mpaka nimefika hapa,naweza nikalia waweza kuniona mnafikikwa sababu kama nilikuwa rafiki mwema mtu ambaye aliyenibadilishia maisha je nilistahili kumtelekeza nilivyomtelekeza?

Mbona sikwenda kumpelekea hata mahitaji? Tena ndugu zetu waliopo gerezani wanahitaji sana faraja wakati natumia mali ambazo amekuwa sababu ni yeye,nakula vyakula vizuri vyakunona sikuwa namuwazia yeye kumpelekea hata kipande cha sabuni? Sikuweza kumuwazia chochote mbona nilimtelekeza,unaweza kuniona mnafiki,moyo wangu uliugua na kujisikia vibaya sana,nikasema mimi naweza kuwa katika kundi la wanadamu wanaowavunja moyo watu wema kuwatendea binadamu wengine wema kwa sababu mimi nilitendewa wema lakini mimi sikutenda wema kwa mtu huyu,kwanza nimekuwa na mahusiano na mwanamke ambaye alinizuia nisiwe na mahusiano nae,mengi ambayo tumepanga pamoja mengi nimeenda kinyume nae lakini leo hayupo tena akiniambia "Rojas mimi nimekusamehe wewe na kizazi chako,niliyafanya kwa mapenzi mema kabisa"

Hakuna kuugua moyo kukubwa na kuzito kama unajiona ndani yako una usaliti,nilijisikia kusaliti pakubwa sana,nililia sana,nakumbuka niliomba "naombeni nipate nafasi mtu huyu nikampumzishe katika nyumba yake ya milele,mtu huyu nimjengee jeneza kubwa la thamani nikampumzishe mtu huyu,mtu huyu ambaye amepoteza ndugu zake wote baada ya yeye kupatwa na kesi gerezani,amesahaulika hana hata ndugu aliyekuwa anakuja kumuangalia,angalau basi nimpe heshima ya mwisho,angalau nimfanyie katika hili na kaburi lake nilijenge katika ustadi mkubwa" lakini haya yote nikiyazungumza utaniona mnafiki kwa sababu nilikuwa wapi angalau kwenda kumtembelea mtu huyu angalau hata kujua maendeleo ya kiafya angalau kuweza kupata matibabu mapema labda kutokana na pesa ambazo yeye mwenyewe alizitafuta na akanipa mimi,wema mtu huyu alionitendea umekuwa ni bure,mimi ni mmoja kati ya watu ambao nimetendewa wema na nimesikia hatia,najihukumu kwa kuchelewa kwangu kuja kumtembelea mtu huyu gerezani,nalia kama mtoto kwa sababu niliamini katika awamu hii ntakaporudi nitapenya zaidi kwa sababu utaratibu nilishaanza kuufanya ili mtu huyu apate matibabu anayostahili ili arudi arejee katika hali ya kawaida lakini mara zote amekuwa akiniambia "Rojas mimi maisha yangu pengine yanaweza yakaishia huku huku" ni mtu ambaye hakuwa na stress zozote za kutaka kurudi uraiani kwa sababu nilikuwa namsisitiza akawa ananambia "wewe nenda kayafanye hayo kwanza" lakini mimi ndio nilikuwa wakwanza kutokomea na kutaka uhuru wa pesa ambazo aliyezitafuta ni mtu mwingine.




ITAENDELEA!
Dogo malizia hii story haraka kabla Chizi Maarifa hajachoropoka kutoka milembe aje kukuzingua
 
Back
Top Bottom