Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

SHUKRANI SANA:

Ndugu zangu nawashukuru nyote kwa kutumia muda wenu kusoma mkasa huu wa Rojas na hapa ndio hitimisho lake,tukutane tena katika mkasa mwingine siku nyingine kwani haikuwa jambo rahisi ukizingatia kutoa maneno katika mfumo wa sauti kuleta katika mfumo wa maandishi kulileta changamoto kidogo ili kuweza kuifanya hadithi ibaki na mvuto wake ule ule,kuna baadhi ya maeneo ilinilazimu kuongeza nyama ili kuweza kuleta muunganiko kwani upande wa audio kulikuwa ama kukatikakatika,kukosekana kipande kirefu au episode kutosikika kwa zaidi ya dakika 10 hapo ikanibidi nijiongeze.
Mkasa huu umenipa mzuka wa kufanya kazi nyingine na nyingine na kama kuna mtu kati yetu anakifahamu kisa chochote kilicho katika mfumo wa sauti na akapendezwa tukilete jukwaani asiwe mchoyo aniPM nami ntatimiza wajibu wangu kama mwana jukwaa,mbarikiwe sana!

Mkuu kwanza asante sana kwa kupoteza muda wako kushea hii story na sisi,bila shaka tumejifunza vitu kibao na vya muhimu sana tena sana..Ila kando na hayo nina ombi kwako,nalo ni juu ya uandishi wako,mkuu naomba ujitahidi kuweka aya au paragraph kwenye maandishi yako coz unaandika story ndefu sana(which is good).

Story ikiwa ndefu bila aya inakuwa inaumiza sana macho,na kuna matukio unaweza ukaruka,naomba sana uweke aya,kwa sababu unajua sana kuwasilisha story ila shida kubwa nimeona ni aya tu.

Samahani kama nitakuwa nimekuudhi kwa namna yoyote ,asante tena kwa story [emoji1488]
 
Mkuu kwanza asante sana kwa kupoteza muda wako kushea hii story na sisi,bila shaka tumejifunza vitu kibao na vya muhimu sana tena sana..Ila kando na hayo nina ombi kwako,nalo ni juu ya uandishi wako,mkuu naomba ujitahidi kuweka aya au paragraph kwenye maandishi yako coz unaandika story ndefu sana(which is good).

Story ikiwa ndefu bila aya inakuwa inaumiza sana macho,na kuna matukio unaweza ukaruka,naomba sana uweke aya,kwa sababu unajua sana kuwasilisha story ila shida kubwa nimeona ni aya tu.

Samahani kama nitakuwa nimekuudhi kwa namna yoyote ,asante tena kwa story [emoji1488]
Nashukuru sana ndugu kwa maoni yako,nina changamoto ya kuweka aya nakubaliana nawe ila niwie radhi kwani mimi ni mgeni ktk fani ya uandishi na ndio najaribu jaribu ila pia natumia simu ktk kufanya uandishi wangu,ubarikiwe
 
Sehemu ya 1.

Naitwa Rojaz na nimezaliwa kwa wazazi ambao baba na mama matamanio yao ni kuona watoto wao tunasoma kwa bidii ili kuweza kufikia malengo yetu na ndoto ambazo wao kama wazazi wanaziota juu yetu,natumaini ni ndoto ya kila mzazi kwa mtoto wake,hakuna mzazi anayesomesha mtoto na asitamani kuona anapata mafanikio katika masomo yake,kiufupi mimi nilikuwa ni mmoja kati ya watoto 6 katika familia yetu nikiwa ni mtoto wa tatu kuzaliwa.

Na nimejaaliwa kusoma mpaka kidato cha nne na sikufanikiwa kufanya vizuri katika matokeo yangu ya mwisho, ukiniuliza sababu ya matokeo yangu kuwa mabaya kiukweli sikuwa na jibu la moja kwa moja ila kiukweli hakukuwa na ugumu huo ila naweza kusema ni mimi mwenyewe kwa uzembe wangu na uzembe wa wanafunzi baadhi mnapokuwepo shuleni kutotambua nini kilichowaleta pale. Kuna wengine ambao wanatilia mkazo masomo yao matunda yake waliyaona na wale wakina wenzangu mie akili tunaielekeza katika michezo isiyo na tija, naeleza haya usidhani nilidharau elimu kwakuwa labda nilitokea katika familia bora, familia yetu ina uwezo wa kiuchumi la hasha kwani hata elimu yangu tokea kidato cha kwanza ni harambee ndio ilikuwa inatawala katika upatikanaji wa ada yangu, mara kachangia shangazi, mara mamdogo au mwana familia yoyote anayeonekana ana nafuu ya kipato kwa wakati huo. Kiufupi nilikulia katika familia duni.

Tulikuwa tumezaliwa watoto wengi na kila mtoto alikuwa na mahitaji yake kwa wakati husika. Sasa maisha ya mtaani bada ya kumaliza mchakato wa masomo tena ukiwa matokeo ambayo sio rafiki chamoto hujakiona, changamoto nyingi zinakuwa zinajitokeza na hapo unatakiwa kujiongeza ili kuweza kujikimu wewe na wanaokuzunguka ilimradi mkono uende kinywani. Katika kusaka tonge nikaanza kujichanganya kwa kuanza kutembea na mafundi hawa mafundi ujenzi nikiwa kama saidia fundi (kibarua msaidizi) na haikuwa kwa mafundi tu kwani pale mtaani kila aina ya kazi iwe kuchimba shimo,kukusanya mchanga (wakati wa mvua ule mchanga unaoletwa na maji), kubeba tofali, kusaidia mtu anayetaka kuhama na kadhalika mie kwangu ilikuwa twende kazi yaani kwa upande wangu maisha yalikuwa ni magumu sana sana sana na msalie Mtume yangu ni kujipenyeza katika harakati hizi, (nakuhusia ewe kijana ambaye umepata neema ya kupata nafasi ya kusoma chonde chonde usiichezee bahati hiyo uko mbele ni kugumu sana,soma kwa bidii maisha sio marahisi), maisha ya kukaa nyumbani yalikuwa na maneno maneno mengi yenye kuumiza roho, ukishamaliza shule hata andazi upewaji wake hauwezi kuwa kama mwanafunzi kwani ukigewa ujue utasindikizwa na neno la masimango hivyo sikuipenda hali hiyo nikawa najibidiisha katika videiwaka hivyo ili kuweza kupata mahitaji.

Siku zilisogea, maisha nayo yakawa yakienda yakibadilika kwani kama unavyojua siku hazigandi mahitaji yanaongezeka, vitu vinapanda bei na maisha yanavyosogea kwangu ndivyo maisha yakazidi kuwa magumu sana kwani ni jasho lako ndilo litakaloamua mustakbali wako.

Pale nyumbani tulikuwa tunaishi kifamilia na mama yangu yeye alikuwa anajishughulisha kwa kufanya biashara, alikuwa anafanya biashara za sokoni (mchuuzi mdogo mdogo) na baba yangu yeye kwa muda mwingi alikuwa yupo tu nyumbani (misheni town) na sana alikuwa kama dalali kimtindo ingawa haukuwa ule udalali wa moja kwa moja yaani kama kuna chumba yeye anadalalia kupata mpangaji na anapewa kamisheni au mtu ana mali yake anauza au anatafuta kitu yeye anamsaidia kuweza kufanikisha jambo husika.

Kwahiyo egemeo kubwa la familia lilikuwa ni mama,mama yeye alikuwa anaenda sokoni uko akaemee ndio akirejea watu wanapata afadhali, siku zilisogea na kusogea mama yangu pekee aliendelea kuwa mkombozi wangu kwani hata nikiwa nimepungukiwa nauli alikuwa ananipa lakini alikuwa ananambia akinikumbushia kwa kusema "Nilikupa nafasi ya kusoma ukachezea unaona unavyopata tabu? Yaani wewe unaniomba mimi nauli? Utagewa nauli hadi lini?"

Lakini pamoja na maneno yote mama yangu mpenzi alikuwa ananipa mtoto wake[emoji1374]
Ikafika wakati mama yangu mpendwa akapata maradhi,akaumwa sana, aliumwa sana yule mama na kama nilivyotangulia kueleza awali mama ndio alikuwa nguvukazi na wakati alipopata maradhi akawa yupo kitandani tu na baba yetu ndio hivi mara apate pesa, mara siku asikutane nayo yaani utokaji wake haukuwa na uhakika wa kurudi na kitu yaani ni bahati nasibu tu, mama alikuwa ana utaratibu wa kudunduliza pesa kama akiba kwa ajili ya maendeleo na kutokana na changamoto iliyojitokeza zikaanza kutumika kwa ajili ya kumuuguza yeye na kutatua changamoto za nyumbani kwani pia nilikua na ndugu zangu ambao walikuwa wanasoma.

Maisha yalikuwa magumu sana huku mimi nikizidi kupambana ili kuweza kujikwamua na umaskini uliokuwa umetuzunguka. Dah! Majira na nyakati
yalikuwa yamefika, mama yangu kipenzi, mama yangu nimpendae, mboni ya jicho langu akaaga dunia!

Tulifanya mazishi kuweza kumpumzisha mama yetu kipenzi katika nyumba yake ya milele, kiukweli huu ulikuwa msiba mzito sana kwetu kwa sababu hakuna asiyejua kuanzia majirani hadi ndugu wa karibu kuhusu nafasi ya mama yetu katika familia, mama alikuwa kinara, alikuwa mpambanaji katika familia yetu kwahiyo kuondoka kwake woga ulituvaa miilini mwetu kwa namna ya kuikabili kesho yetu yaani hasa mimi nikajiuliza tutafanyaje?

Hii kauli hata wadogo zangu waliweza kuitamka na kujiuliza tutaishi na kusoma vipi? Lakini maisha lazima yaendelee na tukakamilisha kipindi cha maombolezi ya mama yetu kipenzi.

Siku zikasonga nikiwa nayakumbuka mengi ambayo mama alikuwa akinishauri alikuwa akiniambia
"Rojaz soma mimi leo nipo kesho sipo, kesho baba yako yupo kesho hayupo mkombozi wako ni elimu, tizama ndugu zako wanasoma, hivi vipesa ninavyokupa visikubweteshe kesho nitakopokuwa sipo utapata tabu mwanangu, dunia hii ni ngumu sana ukiwa hauna cha kufanya dunia ni ngumu sana naomba ulitambue hilo",


Nazikumbuka hizi kauli kwani uwa zinanijia sana,zinanijia pale nina shida, pale napokuwa sina kazi yakuweza kunipatia riziki, unajua sie masaidia fundi ni pale fundi apate kazi ndio akwambie njoo, kama hajapata nawe ujue imekula kwako!

Kaka yangu mkubwa alikuwa ana rafiki yake ambaye ni dereva taksi, nakumbuka nilimfata kaka na kumwambia, "kaka huku kwenye ujenzi ni pagumu sana, kaka kama unaweza hata kuniunganisha kwa rafiki yako niweze kukaa hata kijiweni naweza kupata chochote kitu"

Kaka yangu alicheka na akanambia
"sasa wewe ukakae katika kijiwe wakati gari huijui, yaani hujui chochote kuhusu gari pale sio wanakaa tu, wanakaa watu wenye idea na hivyo vitu yaani ukakae kijiweni na haujui lolote? Au unatakaje? Unatakaje mdogo wangu?"
Nikamwambia, "nataka kujua hiyo gari sasa ndio maana nataka kukaa na wenye magari". Akasema, "Ntaongea naye na atakaporidhia utaambatana nae lakini ngoja nizungumze nae kwanza".

Siku zikapita toka nimueleze kaka kuhusu hili jambo na nilikuwa nikimkumbusha mara kwa mara yeye alikuwa akinijibu kuwa amesahau lakini nashukuru siku moja niliwakuta wote wawili kaka na rafiki yake wakiwa pamoja nikamwambia kaka
"Kaka naomba umwambie hapahapa maana uwa unasahau naomba umwambie sasa hivi", nashukuru Mungu kaka alimwambia huyu rafiki yake ambaye anaitwa John, naye akajibu, "Hakuna shaka kama yeye anapenda hata kama hajui chochote atajua tu, wengi walifika pale hawajui chochote kuhusu gari na sasa wanajua, atakuwa akitazama tunavyofanya na tutamfundisha atajua"

Maisha yakasogea na nilifurahi sana kwa ombi langu hili kukubaliwa, nilianza kwenda pale kijiweni na kwa nyakati hizi biashara ya taksi ilikuwa na mzunguko sana, wateja walikuwa wengi kwani kulikuwa hakuna mambo mengi kama mabodaboda au hizi Uber yaani taksi ndio ulikuwa mpango mzima.

Basi nikafika kijiweni nikakutana na John na alinambia wewe utajumuika nami katika safari iwapo mteja atakuwa ameridhia, utakaa unatazama namna ninavyopiga gia na pia siku za Jumapili John alikuwa hafanyi kazi hivyo alikuwa ananichukua na kwenda katika uwanja wa wazi na kunifundisha gari na kwa sababu mimi nilikuwa na nia na ninapenda kwangu haikuwa ngumu kujua tena kaka John alinipa maneno ya hamasa sana
"Sio ngumu mdogo wangu weka nia tu kuna wenzako wengi wametoka vijijini uko leo wanawaendesha mabosi na maisha yao yanasonga, wanakula vichwa kwahiyo wewe pambana bwana, pambana mdogo wangu".

Kweli nikapambana hadi ikawa tena kwenye vile vibarua vya saidia fundi siendi nikawa napenda gari napenda gari kweli kweli, ikifika asubuhi mie wa kwanza kijiweni utasema kama vile mie ndio nimekabidhiwa taksi kumbe bado deiwaka, namsubiri bro John basi mishemishe zinaendelea.

Taratibu nikawa najenga imani kwa John na John akanambia sasa siku mojamoja nitakuwa nakupa nawe uwe unakula vichwa, yaani siku ambazo anakuwa yuko sehemu ametulia ananiachia chombo nakula vichwa, yaani alikuwa ametokea kunikubali sana nami nikawa napiga mishe kila kaka John anaponikabidhi chombo, sasa nikawa dereva namudu kukiongoza chombo maana kijiweni tena John awepo au asiwepo mi naburuza tu, maisha ya udereva yakaendelea na bro John akawa ananitoa toa mara buku tatu, mbili hadi tano, kwa kipindi iko ilikuwa ni kubwa, elfu tatu kwangu ni kubwa tena ukitilia maanani natokea nyumbani akinipa elfu tatu, akinipa elfu mbili niliona safi sana kwa sababu nikitu nilishaanza kukipenda.

Huyu John kwa muda mchache niliokaa nae nilimsoma nilimgundua ni mtu anayependa sana mabinti (mtu wa totozi) yaani yeye ikifika jioni tu kile kigiza cha kwanza tu anapotea kijiweni anaenda kujificha na binti aliyemteua siku hiyo. John alikuwa mwenyeji sana katika nyumba za wageni na ukitilia maanani alikuwa na wateja sana katika biashara yake ya taksi yaani kwa watu wa taksi saa 1 hadi saa 2 usiku ndio kunakuwa kumekucha lakini yeye hauwezi kumkuta muda huo anakuwa maeneo yake yakujidai kwani muda huo kibunda kishanona hapo ananiambia dogo nishaondoka kwenda kujipumzisha na shemeji yako, kiufupi alikuwa mzee wa bandua bandika.

Kwa hiyo muda mwingi alikuwa ananiachia funguo sababu alikuwa ameshaniamini kama deiwaka wake nami nikawa napiga kazi hadi mida flani nampigia bro nshamaliza naye ananielekeza alipo namkabidhi chombo narudi nyumbani
Siku moja John akanambia "mdogo wangu sasa wewe umeiva, umekwisha iva inabidi tufanye mpango upate leseni usije kukutwa barabarani huna chochote hii ni hatari kwakuwa ushakuwa uko vizuri katika uendeshaji, lakini pia uweze kujua sheria za barabarani"

Kwahiyo nikafanyiwa mpango wa kupata leseni na John akanitimizia nikapata leseni sasa nikawa kamili gado kama wasemavyo watoto wamjini! Na akanambia sasa upo kamili na hata akitokea tajiri anaweza kukukabidhi gari ukawa unapeleka hesabu, uko vizuri na hii ukiichukulia serious itakutoa dogo" Nikamwambia
"Asante bro kwa wema wako nakuahidi sitakuangusha na hata hizi dakika chache unazonipa naamini kijiweni michongo ni mingi ntatoka tu"

Aliendelea kunielezea "Hapa kijiweni kweli kazi ni nyingi tena waweza akatokea mtu akazingua na tajiri akatafuta dereva anaweza akakukabidhi wewe chombo, komaa dogo hao wengi unaowaona kijiweni si kama wewe tu wamekabidhiwa rasmi vyombo bali madeiwaka we kuwa mvumilivu tu".

Kiukweli alinipenda kwakuwa mimi nilikuwa mchangamfu, mwepesi kuelewa jambo ninaloelekezwa, kazi nilitokea kuipenda na zaidi sikuwa muongo yaani zile za kumdanganya labda nimebeba mteja alafu nimwambie sijabeba au nimebeba ila nikawasilisha pesa pungufu kiukweli sikuwa na utundu huo, kwahiyo ndio sababu bro John akaniamini sana.

Safari ikaendelea maisha yakasogea nikiwa sasa ni dereva kamili wa taksi na nikawa najivunia na kufurahia kazi yangu ya udereva ingawa katika mambo yote bado nilikuwa namtegemea John lakini nilikuwa nimepata ujuzi mkubwa kutoka katika kitu nilichokuwa sikijui kabla, kadri siku zilivyokuwa zinaenda nami nikawa naanza kuzoeleka na kujulikana kwa wateja mmoja mmoja, siku moja tukiwa kijiweni alikuja dada, huyu dada alipofika John akanambia, "Huyu dada ni mtoto wa mwenye hii gari ambayo mimi nimekabidhiwa"

John alinieleza haya kwakuwa huyu dada alitaka kuleta mazoea yaliyopitiliza, yaani ni mara mbili tu ndio nimepata kukutana na huyu dada, mara ya kwanza nikiwa na bro John alipokuwa akipeleka hesabu ya gari kwao kwahiyo John akanitambulisha kwao mimi kuwa ni mdogo wake, siku ya pili ndio hii tunaonana hapa kijiweni lakini ile siku ya kwanza huyu dada alikuwa akiniwekea ishara ambazo mimi sikuzielewa, unajua mimi tangu ninasoma hadi kufikia hatua hii sikuwa na ukaribu wa kivile na akina dada kama hivi yaani kiufupi sikuwa na masuala ya mahusiano na akinadada kwa sababu mazingira ya shule na nyumbani hayakuwa rafiki katika mambo hayo yaani hakukuwa na nafasi ya zile za kikombolela au michezo ya kujificha vichakani.

Huyu binti kwanza alikuwa na mtindo wa kunikonyeza nami nikawa namshangaa tu na haya mambo hakuna aliyekuwa anaona zaidi yangu mimi ile siku ya kwanza tulipoenda kwao na John na siku ya pili ndio hii amekuja hapa kijiweni na alipofika kwanza aliniulizia sisi tukiwa tumegeuza migongo tumekaa hapa kijiweni tumegeukia kwingine mimi na huyu bro. Alikuja moja kwa moja na kuniulizia akitaja jina langu yaani huwezi kuamini jina langu alilishika kwelikweli, siku ya kwanza tu kulisikia akalishika akaulizia, "Yuko wapi Rojaz?"
Wakamuuliza "Rojaz wa John?"
Akajibu "eeh, yuko wapi?

Akaelekezwa mpaka nilipo na dada yule akaja yaani wala hakuwa na woga sijui yuko vipi,akaanza kusema,
"Jamani toka siku ile hata haunitafuti"
Mbele ya John akawa anayatamka maneno hayo "Hunitafuti? Mbona umekuwa hivyo? Au haujui mambo ya mjini? Haya mambo ya mjini we huelewi? Basi mi nikabaki nashangaa shangaa nikiwa nimeweka mikono hivi tukipiga stori na John akaja yaani akanikumbatia kwa kuniwekea mikono yake juu yangu akiwa amenikumbata kutokea nyuma akanambia
"Nimekumiss sana, nimekumiss mno, nyumbani umekuja siku moja tu nimekufahamu haukuja tena,au John amekwambia usije? Nikamwambia "hapana mbona tunakuja sana labda uwa tunapishana wakati sisi tunakuja wewe unakuwa haupo"
Akanambia "kama tunapishana si uniulizie?". Pale ni nyumbani kwetu ulizia flani yuko wapi utaniona, siku hizi tunaenda kwa simu sasa mpaka unione tena wewe huna hata simu nikamjibu "sina simu"

John akawa anamtizama tu, anatutazama tu na si kama alinivuta pembeni ni mbele ya huyu John, akasema "Basi itabidi utafute simu, ntakutafutia simu". Basi yule binti akaondoka zake mi nikiwa nimeshikwa na butwaa, wakati anaondoka akanambia "Mbona hata haunisindikizi?

Wakati ananambia hivyo John akawa ananinng'oneza kitaratibu
"mwache aondoke zake"
Akaendelea kunambia
"Katika vitu ambavyo unatakiwa ukae navyo mbali kimojawapo ni huyu binti, huyu binti achana nae kabisa hii ni hatari unaweza kupigwa risasi ya kichwa,achana nae asikuzoee"
Nilimwambia John "Kaka wala usiwe na wasiwasi na mimi kuhusu yule binti kwani ugumu wa maisha ambao nimeupitia haitaweza kutokea, kwanza sina mahusiano nae na kama ulivyosikia ameniulizia kama nina simu nimemdanganya kuwa sina na hayo anayonieleza akili yangu wala haiko huko na kwakuwa umenisisitiza nitakuwa mtiifu kwako wala sitajihusisha nae, mimi nitakaa kimya"
Akanambia "ndio hivyo unatakiwa ufikirie maisha sasa mambo lazima yaendelee, hawa mabinti wa mabosi watakuja kukuletea matatizo mbeleni achana nao kabisa".

Nikamsikiliza kaka yangu na baada ya muda kanambia "leo usiku kunaweza kukawa kuna dili tunaweza kulifanya na kwa sababu umeshakomaa sasa wewe ni dereva mzuri" Nikamwambia "hakuna shida, kuna abiria?

Kaka John akasema "yes,kuna abiria ila mimi ntaenda kupumzika nina kitu changu(mpenzi) bwana si unajua? Mimi bwana sinywi pombe, mi sio mshabiki sijui wa vitu gani gani lazima nitulie sehemu na mtoto mzuri tule raha, mimi nitakupa mchongo muda ukifika".

Basi nikakaa tayari kwa huo mchongo, akaniachia funguo naye akaondoka zake lakini sehemu alienda mimi sikuijua (sikujua ni guest gani) lakini aliniambia tu kaa tayari, usiku nikaona muda umeenda na kwa sababu nilifanyafanya kazi kwa toka muda ule alionieleza hili swala jioni ilishaingia ilikuwa mida ya saa 11 hivi, nikapigapiga kazi mpaka kwenye majira ya saa 3 usiku nikajiuliza bro yuko wapi? Nikipiga simu yake hapokei, nikajua huyu kashakuwa katika uwanja wake wakujidai tena basi nikajiondokea zangu nyumbani kujipumzikia, gari nikaenda kuipaki palepale tunapoipaki, nikaenda zangu nyumbani nikijua mteja ameaghirisha hilo zoezi, nilipofika nyumbani nikaoga zangu na kula chakula nikijiandaa kwa kulala, wakati nimeshajipumzisha mara simu yangu ikaita na kutizama ni bro John akanambia, "Nakupgia muda mwingi naona namba yako inatumika au ulikuwa unaongea na yule mtoto?

Nikamwambia, "Hapana bro siongei na huyo mtu kwanza nimemwambia sina simu na wewe shahidi ulisikia pale nikimwambia, sina hata namba yake wala namba yangu hana, nafatisha ushauri wako kama ulivyonambia niachane nae nami nafanya hivyo"
Bro akanambia "vizuri, sasa lile dili liko tayari limeshakaa mkao wake,kuna abiria utaenda kumchukua". Nikamuuliza "namfata wapi?"
Akanambia "palepale gari ilipo yeye tayari atafika hapo na atakapofika hapo ataingia kwenye gari na utamsikiliza wapi unapompeleka"
Nikamuuliza "ina maana gari ilipo yeye anapajua? Akanambia "anapajua tena ukichelewa unaweza kushangaa yeye ameshafika kabla yako wewe lakini sitaki wewe umkute jitahidi uanze kufika wewe na ukifika milango ya gari aikute iko wazi, yaani yeye akifika akute milango haijakomewa yeye atafungua na ataingia ndani mtazungumza akiwa ndani ya gari huku ukiwa umewasha gari,ni mteja wetu mzuri, anatoa pesa nzuri kwahiyo wewe kale kichwa".

Basi mimi nikanyanyuka na kujiandaa, nikatoka zangu kuelekea pale tunapolaza gari, ile nimefika tu nafungua gari na kuweka mazingira vizuri garini basi kweli mtu huyu akaja, alionekana ni kijana ila alionekana amenizidi umri kidogo lakini ni rika la kijana, alikuwa anashabihiana kiumri kiasi kama bro John hivi lakini sema yeye alikuwa ni mrefu, akaja akaingia garini na akakaa siti ya nyuma, ujue tena taksi hizi, akanambia, "Naomba endesha twende huku" Nikamwambia "wapi? Akanambia "wewe twende ntakuelekeza,taarifa zangu si John amekupa? Nikamwambia "ndio"
Akasema "sawa sasa twende".

Nikawasha gari tukaanza kuondoka huku yeye akiwa ndio muelekezaji njia mara pita hivi, kata hapa lakini akanambia "wewe ni dereva mzuri sana John amenambia ni dereva mzuri alafu ni mzoefu barabarani sasa tupite short cut"

Kwakuwa nilishakuwa na gari muda mrefu na mzoefu katika njia tofauti tofauti ni kawaida yetu kumsikiliza mteja matakwa yake, nikapita njia alizozitaka basi tukawa tunachanja mbuga, nikamwambiab"Bro kwani tunaelekea wapi?" Akanambia "wewe twende"

Huyu kaka alikuwa amebeba kibegi, kibegi hiki ni vile unaweza kukiweka kwenye mabega si begi kuubwa ni kibegi cha mkanda mmoja ambacho alikuwa kakigeuzia kwa mbele, baada ya muda nikaingia kwenye lami kwani hakukuwa na ujanja tena ni lazima ilikuwa tuipate njia kubwa kutokana na eneo ambalo anakwenda, tuliposhika barabara kubwa kama dakika kumi mbele tuliona kama magari yanakuja upande wetu, unajua tena barabara kubwa magari hayaepukiki, mara yakawa yanapiga honi kwa nguvu, jamaa akanambia "nakuomba ongeza spidi"

Nikamwambia "kwanini niongeze spidi kwani kuna shida gani acha wapite hao" Akanambia "nisikilize mimi hao watu wanatufuata sisi" Nikastuka sana na nikamuuliza "wanatufuata?" Akasema "eeh wanatufuata inabidi uongeze spidi"

Nikamuuliza "wanatufuata kwani tumefanya kosa gani? Akanambia "nisikilize mimi kijana acha ubishi we ongeza spidi tu hao watu wananifata mimi" Ikanibidi nitii nikaongeza spidi na akanambia "hawa watu wakitukamata hawatataka kujua wewe ni nani yaani wote tutapigwa risasi za vichwa na uwe ndio mwisho wetu,ongeza spidi".

Nilitii na kuongeza spidi hatimaye wale watu hatukuwaona tena tukawa tunaelekea njia kama vile nje ya mji akawa ananisisitiza "kazana, kazana"
Na kwa sababu kiasi nilikuwa najua njia za mikato tukawa tunapita hizo tunarudi njia kuu lakini ukiniuliza kwanini alikuwa ananiambia niongeze spidi mimi sijui kabisa kwani hata nilipokuwa nikimuuliza jibu lake kwangu lilikuwa "Haya mambo wewe hayakuhusu, hao watu wananifata mimi"

Nakumbuka kweli nyuma kukawa shwari hakuna watu wanaotufuata, tukafika sehemu moja nje sana ya mji yaani ni mbali sana sikuwahi kupata abiria wa kuja huku kabla, tukafika mpaka uko sasa akanambia "Basi sasa mimi nashuka", Yaani kwa sababu nilikuwa nimeacha vioo wazi ile nataka kusimamisha gari huyu kaka aliruka, yaani alichoropoka kama panya,aliruka na kibegi chake. Nikamwambia "Bro si utaumia" Akasema "sasa basi we geuza uende zako na hakikisha hawa watu haukutani nao na ukikutana nao ujue watakuua"

Nikamuuliza "kwanini bro?" Akasisitiza
"unaporudi tafuta njia yakuweza kuwakwepa wale la sivyo watakuja kukuua hao sio watu wazuri watakuja kukuua amini hivyo"

Mimi mpaka hapo sikujua lolote,sikujua kwanini alikuwa ananiambia maneno hayo, sijui alikuwa amefanya kitu gani, sijui walikuwa wamekoseana nini,nikageuza gari kuanza kurudi wakati huo nikawa nampigia simu bro kumjuza kuwa nimekutana na kitu ambacho kinanitisha, nikawa napiga simu ya bro John na simu yake ikawa haipatikani hewani, simu yake haipatikani na mbaya zaidi hata namba ya simu ya huyu mtu niliyempakiza pia sikuichukua kwa sababu ilikuwa kuachana ni chapchap halafu yupo kama kuna kitu flani ananificha namimi sijui lolote, uoga ulitanda ndani ya moyo wangu,amani ilinipotea kabisa.

Nikageuza gari kinyonge na kuanza kurudi, nikarudi nikiwa na tahadhari maana niliambiwa hawa watu nisikutane nao au wasinione, kumbe hii ilikuwa ni siku mbaya kwangu, ilikuwa siku mbaya, mbaya, mbaya sana, wakati niko barabarani mara ghafla hawa watu sijui walitokea wapi, sijui hata kama walikuwa wanajua kama mimi ninarudi niko barabarani gari moja nyeusi na nyingine yakawa yananifuata kwa kasi, ni lile lile la mwanzo na la pili nayaona yakijia upande wangu kiukweli niliogopa mno, niliongeza spidi lakini hawa watu walikuwa spidi zaidi yangu, yaani ukiniuliza nilikuwa nakimbia nini kiukweli hata mie nilikuwa sijui lakini lazima nikimbie kwani nilisisitizwa kukimbia kwani nikisimama nitapigwa risasi, mimi sijafanya kitu nilimbeba tu huyu abiria na wala sijui lolote.

Kila nilipokuwa nikimpigia bro John nikawa simpati hewani, namba ya huyu mtu sina yaani nimejikuta ninaucheza mziki nisioujua kiukweli sikujua ntakuwa mgeni wa nani mie....

Itaendelea!

natia nukta ntarud
 
Nashukuru sana ndugu kwa maoni yako,nina changamoto ya kuweka aya nakubaliana nawe ila niwie radhi kwani mimi ni mgeni ktk fani ya uandishi na ndio najaribu jaribu ila pia natumia simu ktk kufanya uandishi wangu,ubarikiwe
Kwahiyo mkuu unasikiliza ndo unaandika,aisee umefanya kazi kubwa sana tena sanaa.

Hongera kuwa na huo moyo aisee
 
Nimesoma episode zoote kwa taratibu sana., kuna mambo mengi sana yanayofundisha nimeyapata kutoka kwenye hii simulizi yako., nasema ahsante sana ndugu. Nimkweli siri katika maisha yetu ni muhimuj sana, pesa hubadilisha mwenendo wa mtu ila watu hubadilisha mwenendo wa mtu zaidi.
 
SHUKRANI SANA:

Ndugu zangu nawashukuru nyote kwa kutumia muda wenu kusoma mkasa huu wa Rojas na hapa ndio hitimisho lake,tukutane tena katika mkasa mwingine siku nyingine kwani haikuwa jambo rahisi ukizingatia kutoa maneno katika mfumo wa sauti kuleta katika mfumo wa maandishi kulileta changamoto kidogo ili kuweza kuifanya hadithi ibaki na mvuto wake ule ule,kuna baadhi ya maeneo ilinilazimu kuongeza nyama ili kuweza kuleta muunganiko kwani upande wa audio kulikuwa ama kukatikakatika,kukosekana kipande kirefu au episode kutosikika kwa zaidi ya dakika 10 hapo ikanibidi nijiongeze.
Mkasa huu umenipa mzuka wa kufanya kazi nyingine na nyingine na kama kuna mtu kati yetu anakifahamu kisa chochote kilicho katika mfumo wa sauti na akapendezwa tukilete jukwaani asiwe mchoyo aniPM nami ntatimiza wajibu wangu kama mwana jukwaa,mbarikiwe sana!
Leo hii nimefanimiwa juimaliza hii story. Episode ya kwanza ninetumia week moja kuimaliza ila jana nilijikaza sana mpaka sasa ndio nimemaliza Story nzuri ya kusisimua na mafundisho mengi Shukrani sana ndugu shikamkono01 kutuletea story hii. .


Kichwa kinauma sana kusoma story kutokana na uandishi wako. Hapa nimemeza paradox yan kichw kinagonga kila nikimaliza episode namaliza kwa shida sana. Please usichukie hebu pita kwenye nyuzi za leadermore au JBourne59 ujifinze mpangilio. .

Aina ya upangiliaji wako na uandishi unarudia maneno unaumiza sana. .

Mungu akubariki sana sana sana na shukrani za dhoti kutuletea story hii. I am looking forward for your upcoming story. Kama nimezungumza jambo likakukera nisamehe sio dhumuni langu kwani MIMI NI MTU MWEMA SANA. Ukitazama macho yangu utajua kuwa mimi ni mtu Mwema sana. .
 
MKASA WA KUSISIMUA WA ROJAZ:
katika kipindi cha sitasahau cha radio free Africa



Part 3



Maisha ya pale kituo cha polisi yalikuwa ni ya muda mfupi kwani utaratibu wa kimahakama ukafika na nikatakiwa kupelekwa gerezani wakati suala langu likiendelea kupatiwa ufumbuzi,wakati nikiwa gerezani kuna kaka mmoja tulitokea kujenga ukaribu wa kiurafiki nae na akawa msaada mkubwa kwangu katika mambo mengi yaliyokuwa yakinikabili,siku moja katika maisha yetu ya gerezani nikiwa na huyu kaka alinambia "kila nikikutizama macho yako nakuona ni mtu mwema sana" nikamuuliza "mimi?akaendelea "yaani hata wale watu wabobevu wa kufanya uchunguzi,watu ambao ukijitetea wanaona auhusiki ndio wanakubana lakini nakuona ni mtu mwema kabisa"

Nikamjibu "sijui,lakini mimi sipendi ubaya na mtu na napenda amani katika harakati zangu za kila siku" akaendelea "unajua uwa nawatizama watu wengi sana hapa lakini katika wengi sijaona mtu mwema kama wewe" nikamuuliza "mimi?" Akasema "ndio sijaona mtu kama wewe humu,wewe ni mtu mwema na kama haujajua basi siku moja utakapopata neema ya kutoka hapa utajua kama wewe ni mtu mwema itambue hiyo na iishi hiyo kwa sababu una upekee wako" nikahisi ni maneno ya faraja tu ananambia yakunitia moyo,kunisahaulisha tabu zangu na kunifanya nifurahi na kujiona ni wa pekee hata kama niko katika mazingira magumu na vitu kama lakini aliendelea kuniambia anamaanisha kwa kile anachokiongea,nakumbuka nilimuuliza "kwanini wewe uko hapa? Kwani wewe si mtu mwema?" Akanambia "hata nikikuambia hautaweza kuniamini lakini mimi natofautiana na wewe,angalia macho yangu yalivyo je una uwezo wa kumtambua mtu tabia zake,hisia zake na kile kilichopo ndani yake? Nikamwambia "hapana sina huo uwezo" akanambia "basi mimi ninao huo uwezo ila sikuutumia vizuri nikiwa uraiani,mimi sifanani na wewe,wewe umekuja kwa njia ambazo si za haki yaani umekuja kwa sababu kuna watu wamefanya mambo mabaya wamekuingiza na wewe lakini mimi ni tofauti na wewe" nikamwambia "utofauti wa mimi na wewe ni upi? Akasema "ni stori ndefu sana huwa sipendi kuzungumza lakini kiufupi niko hapa natumikia kile ambacho nilistahili,siku nyingine ntakueleza lakini siko hapa kwa makosa hakuna mtu amenisingizia,maisha yangu ya uraiani mwenendo wangu ndi ulionipeleka mimi kuwa"

Nilitamani kujua alifanya kitu gani kilichopelekea hadi yeye kuwa anastahili kutumikia kifungo anachokitumikia,alinambia "niko hapa gerezani natumikia miaka yangu 30 na mpaka kesi yangu inasomwa nimeshakaa miaka mingi" nikamuuliza "umekaa miaka mingapi?" Akanambia "sikuvunji moyo wakati mwingine kuna kesi uendeshaji wake uwa unachelewa kwani kabla ya kufikia hukumu unaweza kujikuta umekaa hata miaka 5" nikamuuliza "hivi mimi naweza kukaa hapa muda mrefu?" Akanambia "inategemea na jinsi kesi inavyoendeshwa,kadri kesi inavyoendeshwa uenda uchunguzi zaidi ukaitajika hivyo kupelekea kuchukua muda lakini nakuombea sana mdogo wangu kesi yako isichukue muda mrefu na uachiwe huru" huyu kaka tulikuwa tunazungumza sana na kiukweli alinijenga sana katika mazingira yale nakunipa matumaini.
Siku zikiwa zimepita siku moja huyu kaka aliniita na tukawa tunazungumza na alinambia"unajua kama ninao ndugu zangu lakini toka nimepata haya matatizo wamenitelekeza na kunisusa huku,huwezi amini kati yao wakati nikiwa uraiani nilijitolea sana katika kuwasaidia hata katika vitu ambavyo havikuwa na faida kwangu niliwapiga tafu lakini kwakuwa mimi nimekamatwa hakuna hata anayetaka kunisogelea wakihisi pengine nao wanaweza kuhusishwa na mimi lakini licha ya hivyo hata ilipotoka hukumu hakuna aliyesogea,wameniacha" nikamwambia "ni sehemu ya maisha,je hakuna hata mmoja aliyekuja kukuona? Akanambia "ninaye mtu ambaye yeye hajawahi kuniacha,uwa namimi katika mazingira yoyote yale hata niwe ndani na hauwezi amini yeye uniletea mahitaji toka siku siku ile ya kwanza nimekamatwa" nikamuuliza "ni wazazi wako? Ni mtu gani huyo?" Akanambia ni girl friend wake (mchumba wake) ndio ambaye hajawahi kumuacha toka siku ile amekamatwa,nikamwambia kuwa alibahatika kumpata mtu sahihi sana,akanambia anahisi anaweza kuchoka nami nikamjibu kama ana upendo wa kweli hatoweza kuchoka na akanijibu "sijui,nina watoto pia yupo mwanamke ambaye nilipata nae watoto,watoto wangu wana uhitaji sana lakini mimi baba ambaye nilikuwa nikipambana katika njia mbalimbali leo nipo hapa,watoto wangu hawako katika mazingira salama na huyu mwanamke kila anapokuja kuniona aachi kunipa lawama na sasa amekuwa ni mwanamke wakuhangaika hovyo na wanaume,sielewi hatima ya watoto wangu,nilizungumza na ndugu yangu lakini ndio hivyo wameniacha peke yangu" kiukweli maelezo yake yalinisikitisha sana na hasa aliponielezea juu ya wanae maumivu yaliutanda moyo wangu,alinambia kuwa uraiani alikuwa anapambana sana,anapambana kwelikweli kwa ajili ya watoto wake lakini kwakuwa yupo jela hatoweza tena kuwapambania,kiukweli nikazidi kuumia kwa maneno yake nikamwambia "pole sana ndugu yangu,umenigusa sana,najua ukiwa hapa kule nje kila kitu chako kinakuwa kimesimama na kama ulivyonitia moyo kwenye maswaibu yangu nami nakutia moyo,tutatoka siku moja tutatoka" akasema "ni kweli natambua ni kweli"

Siku zikawa zinaenda na tukawa tunashea mengi katika mazungumzo yetu ya kila siku na kuna siku mfungwa mmoja aliniambia naona uko na urafiki na mtu flani (akimtaja yule mfungwa ambaye uwa napigana nae stori)nami nikamjibu ndio kwani amekuwa kama kaka,kama mshkaji na mfariji ndio tunabadilishana mawazo akanambia jamaa ana miaka mingi huyo kwani sote tutatoka na tutamuacha humo humo na akakazia huyo anafia humo humo gerezani,kiukweli sikumtilia maanani kwani kama ni miaka ambayo tayari imeshatamkwa mfano atatumikia miaka 30 si atatumikia miaka husika kwanini aonekane kama atafia huku? Sentensi gani hizi?
Siku zilikwenda na kwenda,safari za kwenda na kurudi mahakamani hazikuisha na mara zote nilizokuwa nikisimamishwa kizimbani nilikuwa naeleza ukweli na lile nililokuwa nalijua tu,sikuwa napindapinda katika maelezo yangu,sikuwa na mengi yakuyaeleza kwakuwa yangu ni machache kwani nilielezea stori toka nimekutana na huyu kaka hadi kufikia kunifundisha udereva,umiliki wake wa gari na hata kuhusu yule abiria ukutanaji nae ulivyokuwa na kama ujuavyo jela nilipata vijiupeo kutoka kwa wabobevu wa sheria ambao walininoa namna ya kuongea kuwa lipi lakuepuka kuliongea,lipi lakulisema na kadhalika maana mahakamani kuna maswali yamitego ni muhimu kusimamia kile unachokiongea na kiwe cha kweli kwani niliamini ukweli ndio utakaoniweka huru!

Nakumbuka siku moja kaka alikuja kunitembelea gerezani na akanambia "mdogo wangu uko katika mazingira mazuri kabisa katika kesi hii na upelelezi unavyoendelea unaonesha hauhusiki kabisa kwahiyo wakati wowote waweza kuachiwa huru,huenda mara ijayo utakapoenda mahakamani yawezekana usirudi tena huku gerezani" nikamuuliza "ni kweli usemayo kaka?" Akasema "ndio" nikajawa na matumaini na furaha sana kwa maelezo haya ya kaka,kuna siku yule kaka mule jela alinambia "naona mwenendo wa kesi yako si mbaya na matumaini ya kutoka yanazidi kuchanua sana hongera sana" nikamwambia "kaka kuna siku ntaenda mahakamani na sitarudi tena huku" akanijibu "ni kweli na mimi nimefatilia huo ni ukweli kabisa,naomba nikuulize najua utatoka na utakapotoka na kwenda uraiani unaweza kunisaidia kitu?" Nikamjibu "ndio" akasema "ntashukuru sana utakaponisaidia katika hili jambo,naomba unisaidie ntakupa maelekezo naomba ukawasalimie watoto wangu" nikamwambia "kaka hakuna shida" akaongezea "na pia ntafurahi sana kama utapata fulsa yakuweza kwenda kumsalimia na mchumba wangu" nikamjibu "nitafanya hivyo pia kaka" akanambia "naomba tuwe ndugu,unajua ndugu sio lazima muwe mmezaliwa tumbo moja,unajua wako ndugu sasa hivi hata wakija nimekuwa siwaamini tena lakini moyo wangu nimejikuta nakuamini sana wewe,sijawahi kukuona enzi nikiwa uraiani tumekuja kukutana gerezani lakini mimi naamini kukutana kwetu Mungu amepanga tena amepanga tukutane katika mazingira kama haya,hivi unajua waweza kukutana na mtu sahihi hata ukiwa gerezani?" Mi nikacheka kwa hayo maneno yake nikamuuliza "mtu sahihi gerezani? Mtu gani awe sahihi mazingira kama haya?" Akanambia "mimi naweza kuwa mtu sahihi sanj kwako na nikawa mtu mwema kwako,jua nimekuona kuwa wewe ni mtu mwema tafadhali nakuomba nawe unirejeshee huo wema ntakaokupa" yale maneno aliyokuwa akinambia sikuwa nayaelewa alikuwa anamaanisha kitu gani,msisitizo wa maneno haya kwangu uliendelea mara kwa mara mpaka siku naenda mahakamani,nakumbuka siku hiyo sasa ndio naenda mahakamani kabla hatujatolewa nje kupandishwa karandinga alinambia "unakumbuka maneno niliyokuwa nikikwambia mara kwa mara ? Unaweza haya maneno ukayafanyia kazi?

Nikamwambia "kaka wala usiwaze kwani undugu si lazima kuzaliwa tumbo moja,tunakutana katika mazingira yoyote alafu tunatokea kuelewana,nakuahidi kaka kama nilivyokwambia nitaenda kuwasalimia watoto na nitaenda kumsalimia mchumba wako,na nikuahidi mimi ni kijana na kama Mungu atanipa neema ya kutoka nitaenda kupambana,nitaenda kupambana na napenda nikuahidi kitu kimoja nitaenda kuwatembelea watoto wako na chochote nitakachobarikiwa sitawasahau kwani najua wewe baba yao uliyekuwa ukipambana kwa ajili yao umekwama humu" akaniuliza "kweli? Kweli unasema? kweli Rojaz unaniahidi kitu kama hiki? Ndio maana niliona,macho yangu yaliona na moyo wangu ukavutika kuzungumza na wewe,wewe ni mtu mwema" kiukweli ninaikumbuka sana siku hiyo kwani alikuja akanikumbatia huku machozi yakindondoka na kunipigapiga mgongoni akanambia "aisante sana mdogo wangu,asante nakutegemea kwani hakuna mtu yoyote ambaye ameweza kuniahidi hivi kama wewe,sijawahi kupata rafiki mwema hivi kwani kuna mshkaji nilikuwa nae hapa karibu kweli lakini toka ametoka hajawahi kurudi tena kunitembelea,hakuwahi hata kwenda kuwatembelea wanangu,Rojaz kumbuka ahadi unayonipa mdogo wangu" nikamwambia "kaka amini ninachokwambia,sitasahau" mimi niliondoka na nikaweka hiyo ahadi kwenye kichwa changu,muda wa kwenda mahakamani ulipofika tukapandishwa kuelekea uko na kesi ilisomwa na mheshimiwa akangurumisha kesi na mwishowe hakimu akatamka kuwa kuanzia muda huo niko huru,kiukweli kutokana na kuwa sikuhusika sikustuka sana kwa uamuzi ule uliotolewa kwani nilijua ni suala la muda tu ili kuweza kuujua ukweli halisi,jela nilikaa kama mwaka mzima hadi kufikia hii siku ya kuachiwa huru na katika kesi iliyokuwa ikinikabili tulikuwa wengi na wengine waliendelea na kesi mbele,ndugu zangu walifusahi sana kwa ndwtgu yao kuwa huru na kujumuika nao tena uraiani,kaka akanambia "sheria zipo kwa ajili ya kutenda haki walimdhuru huyo kijana watabainika tu, sheria itawakamata na kuwahukumu" kwahiyo mimi nilitoka gerezani na kurudi uraiani hakika ilikuwa ni furaha sana kwetu sisi na nilpata somo kubwa kuwa ni vyema kuwa na tahadhari katika shughuli tunazofanya



Itaendelea!

daaah pooole sana kuna kitu cha kujifunza hapa nakiona
 

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha ‘Stasahau’ cha Radio Free Africa​


Sehemu ya 19


Mtaalamu alizidi kunidadisi na alinambia "pesa ziko kiasi gani zilizobaki toka wewe uzipate? Nikawa najiuliza je naulizwa maswali gani haya sasa,mbona kama mganga ananichimba sana? Na naomba ukumbuke hapa kwa huyu mganga nimeletwa na mtu na sijui dhamila yake ya ndani na mganga anataka nimletee pesa kadhaa kutoka katika pesa ninazozitunza uko ninapozitunza (yaani alinitaka kuchomoa kiasi flani cha pesa nilizonazo na nimletee)kuna kitu azifanyie kwa nia ya kuzifanyia ulinzi kwa sababu anaona kuna mambo yasiyo mema katika pesa ninazozitumia,nikamwambia "sawa" naye akazidi kusisitiza "nipe majibu ili niweze kukusaidia" majibu kwa maana nimueleze eneo nililohifadhi pesa.

Lakini mimi nikajiuliza "huyu kama ni mtaalam wa kuweza kuona vitu ambavyo mtu mwingine hawezi kuviona ameona kama pesa ninazozimiliki kuna shida,anaona kitu kilichoondoa uhai wa ndugu kule gerezani ndio kitu hicho kitakachokuja kunidhulu nami je kama ameweza kuona vyote hivyo iweje ashindwe kuona nilipoweka pesa mpaka nianze kumention ni sehemu flani nimeweka moja mbili tatu sasa kutokana na mimi kuingia katika ulimwengu wa biashara na kutapeliwa mara kadhaa hii ikanipa hofu kwa sababu nimeletwa hapa na mtu na huyu mtu ni mshkaji wangu,katika maisha huwezi kujua huyu mtu anakuwazia jambo gani pengine hata yeye anaumiza kichwa kujua vyanzo vya pesa zangu ni nini,huyu mganga itamuaminije na kumpa siri yangu hii,nikamwambia "mimi ntaleta pesa" akanambia "sio tu kuleta pesa" na akazidi kuning'ng'niza katika kupata jibu lake lakini sikumpa ushirikiano kabisa katika hilo,nilimwambia "pesa nitaleta na hayo majibu nitakujibu ntakapoleta pesa" mganga akanambia "kiburi chako kitakufanya uchelewe na kutatokea maafa makubwa,mimi nakuambia hivyo kwa sababu hizi mali si za kwako,yaani ukae ukijua hizi mali si za kwako na huyo aliyepata mali alikuwa na siri nazo na ndio maana hakutaka kuzitumia na ndio maana alizifukia mahali,wewe mahali ulipoziweka unaona ni shida kunitajia je unahisi ni nini"

Sikutaka kumpa sana nafasi na nikamwambia "ndio kwanza tumefahamiana na vile tunahitaji muda zaidi wa kuzidi kuzungumza zaidi pengine naweza kuzungumza mambo mengi zaidi" lakini nikazidi kujiuliza kama anaona visivyoonekana kwanini hajaona pesa? Nilifanya taratibu nilizoelezwa kwakuwa nilitakiwa kulipia pale,nikalipa kwani sikuona kama ni hela nyingi kwani makubaliano ilikuwa kulipia huduma ya kutizamia,kulinda pesa na mimi mwenye kunitibia ili kila kitu kirudi katika mstari wake,nikalipa na akanambia kadri siku zitakavyokuwa zinaenda nitajionea jinsi ulinzi wa pesa na mali zangu unavyoimarika,nilimpatia laki tano na uko mbeleni nitalipia kwa kadri ya matibabu husika.

Tumetoka pale na yule mshkaji aliyenipeleka na tukiwa njiani akawa ananiambia "huyu ni mganga sahihi sana,wako waganga lakini huyu ni mganga mahiri" nikamwambia "lakini mimi sijawahi kushiriki katika mambo ya waganga" akanambia "shida yako,tatizo lako fata tu maagizo anayokupa utafanikiwa sana" nakumbuka sana nilitakiwa kurudi kwa mganga kupeleka pesa (mfano wa pesa)ambazo ninazo lakini nikatingwa na mambo mengi kwani mambo yalikuwa yamepandiana sana na nikasema ngoja nikamilishe alafu ndio niende,nakumbuka siku hiyo niko katika vitu vyangu vinavyoniingizia uchumi nikiwa napiga mahesabu ya hapa na pale nakumbuka hatua yangu ya kwanza kabisa nikapokea taarifa ya gari yangu kubwa kabisa ambayo nilinunua kwa gharama kubwa na linaendelea kufanya kazi nikapewa taarifa limepata ajali mbaya sana lakini pia ambacho kiliniuma zaidi na watu ambao walikuwamo mule katika gari ambao ni madereva wangu wote walipoteza maisha,nilisikitika sana,nilipofatilia kuona ajali ya gari yangu kiukweli ilikuwa lite off lakini stori za ajali hiyo kutokea zilikuwa ni nyingi sana lakini wakati nikiendelea na mchakato wa kuhakikisha hawa wapendwa wetu wanapumzishwa katika nyumba yao ya milele taxi moja ikapata ajali,ajali ilitokea lakini dereva alitoka akiwa hai lakini gari lilikuwa nyang'anyang'a na nakumbuka sentensi ambayo dereva alizungumza "aah mimi nimeaga bwana mtu hawezi kunichukua kizembezembe" yaani ikiwa inaaminika haikuwa ajali ya kawaida kwa maelezo yake anasema jinsi alikuwa anaendesha gari kuna vitu aliviona mbele ambavyo havikuwa vya kawaida na anaamini kabisa ulikuwa mkono wa mtu,kama nikaanza kupata ishara flani kuwa kuna vitu haviko sawa.

Kuna matukio ya ghafla yaliibuka hata sijui yalitokea wapi na hii ikanifanya nikimbie sasa moja kwa moja kwenda kwa yule mtaalam na nikawa nimepeleka pesa,nikapeleka na kumueleza changamoto ambazo zimetokea na alisikitika na kuniambia "nilikwambia kuwa hizi pesa unazomiliki aliyekuwa anazimiliki zimemtaabisha zimemtesa na ndio maana hakutaka kuzitumia na ndio maana hakutaka kumtesa ndugu yake yoyote na ndio maana alikutafuta wewe ili hizi pesa zikumalize" nikasema "hapana,hapana mtu amenipa hizi pesa na siku zote nimekuwa nikizitumia kwa amani, kwanini na kwanini? Mtaalam akachukua zana zake pale na kuongea ongea maneno yake na kunipa dawa flani akawa amenipakaa maeneo tofauti tofauti ya mwili wangu na pia akazichukua zile pesa nilizokwenda nazo nakuzifanyia mambo mambo yake mwenyewe ndio anajua zaidi na akanambia "mambo yatasettle,mambo yatasettle" na alinipa utaratibu wa kufanya vitu katika ofisi ambazo nazimiliki na akanirejeshea zile pesa ambazo alishazifanyia mambo yake niende nikazichanganye na zile pesa zingine kwamba ni ulinzi na hata mie kuanzia muda ule niko salama.

Nilitoka pale na nikafanya kama nilivyoelekezwa lakini moyo wangu ukawa unasikitika sana,nakumbuka nikapigiwa simu kutoka katika duka langu la nafaka kuwa kuna moto mkubwa na duka limeteketea lote na watu ambao walikuwa karibu na mimi wakaanza maneno "unaona,unaona,huyu mtoto alikuwa anamiliki mali zisizo za halali angalia matukio jinsi yanavyofululiza pengine amekosea masharti" lakini mimi kwa upande wangu nikawa najiamini hakuna sharti ambalo nililikosea kwa sababu hizi pesa nimemiliki katika mfumo ambao nimeshauelezea,ikabidi nirudi tena kwa mtaalam ili nijue ni nini tena na mbona nimeshaanza kupoteza sehemu yangu ya kupata pesa na watu wamekuwa wakipata pesa kwa ajili ya kutunza familia "imekuwaje tena,ni nini kinaendelea mbona haunipi ufafanuzi" akanambia kuna kazi kubwa anatakiwa kuifanya na inabidi anipeleke makaburini,sasa kwakuwa niko katika hali ya kutatua tatizo na ukiniuliza nini chanzo yaani ni sijui,yaani sijui kwa sababu nilikuwa na hizi pesa siku zote na ni hofu tu ilinipata ndio kwenda kwa mganga,yaani pesa nilizotoa kwa mganga ni pesa nyingi sana na ikawa kila ninapoenda ananitajia mabei makubwa ya vifaa hitajika na kwa mfano hili zoezi la kwenda makaburini aliniambia hili zoezi ni kubwa sana kwa sababu tunahitaji nguvu zaidi za kuhakikisha tunaweka ulinzi kwa hizi pesa kwahiyo alinitaka nitoe milioni tano ili kumaliya tatizo kabisa,nikatoa na kweli tulikwenda makaburini na akanifanyia madawa na kuniambia "sasa wewe umepikwa na umepikika na hakuna ubaya wowote dhidi yako kuanzia sasa hivi".

Lakini haikuwa kama yule mganga alivyosema kwani vitu vyangu vilizidi kupukutika,naviita vitu vyangu kwakuwa nilivitafuta mimi,nilivitafuta kupitia zile pesa na kama ningeamua si ningekaa tu huku nachomoa pesa natumia lakini pesa zile nilifanya uzalishaji ambao ndio umeleta matunda ambayo ndio hivyo vitu na hata pesa zake nikaweza kupeleka hata benki,nakumbuka sana,nakumbuka nyakati naendelea kuliwa pesa na vitu vinazidi kupotea na huku huyo mtaalam akiendelea kunipa vitisho,nakumbuka siku moja yule mama ambaye ni shemeji yangu ambaye tumekuwa tukishea mambo mengi alikuwa ameona mapito ambayo napitia na nilikuwa lesi sana kwahyo sikuwa hata na muda wa kuzungumza mimi niko kwa ajili ya kuzitatua changamoto nilizokuwa nazipitia,alinitafuta na akanambia "shemeji tuongee kidogo,shemeji kuyumba kwenye biashara ni jambo la kawaida,nini hasa kimesonga moyo wako? Mbona umekuwa hauna raha,nakuona ni mtu ambaye hauko smart tena,ni nini tena kiko katika maisha yako? Nikamwambia "sielewi" alizungumza na mimi kwa ukaribu na upole sana "Rojas nilikwambia kuna mambo hauwezi kumwambia mtu lakini Mungu yupo,Mungu wetu ni kila kitu katika maisha yetu" alizungumza na mimi mambo makubwa sana,nikamwambia "unajua leo hii mnaniona niko na pesa lakini hizi pesa leo zimegeuka mateso kwangu" akanambia "kwanini,kwanini mbona mimi hizi pesa naona ni pesa halali kabisa" nikamwambia "hujui tu" akasema "hapana naziona ni pesa halali kabisa na wala sina mashaka na wewe kama watu wanavyosema kuwa umetoa sadaka watu,minong'ono ya watu kuwa eti umekosea masharti na wanatisha watu ambao wanakufanyia kazi wakiwaogopesha kuwa watapata matatizo na kupoteza maisha,mimi siamini katika hilo"
Huyu mama alionesha kuniamini kuliko kawaida kwamba anaamini iko kitu,kwa mara nyingine ya kwanza nikamueleza huyu shemeji yangu,nikamwambia "hizi pesa mimi alinipa" na nikamweleza mazingira yote ya mimi kumiliki hizi pesa na nikamweleza jinsi nilivyomtelekeza huyu mtu na nikamwelekeza hadi mahali nilipozihifadhi hizi pesa kitu ambacho sikumweleza mtu yoyote tofauti na yule marehemu na nikamwambia yule shemeji "nimekushirikisha kwa sababu umekuwa karibu na mimi na umekuwa unazungumza vitu ambavyo vinagusa sana maisha yangu" akanambia huyu mama " Rojas unapoamua kuamua kuwa kuna miungu mingine asiyekuwa Mungu inaweza ikakusaidia tambua unakosea na uko ndiko ulikoenda kuharibikiwa,kama siku zote ulikuwa unafanya biashara zako katika hali ya amani ina maana sasa wewe umeenda kujiconnect na miungu ambayo ni mibaya na ndio labda imeharibu pesa zako" nikamwambia "hapana yule mtu alikuwa anahofia kutoka" nikamweleza hofu niliyokuwa nayo,akasema "hiyo ni hofu yako imekupandikiza wewe kwenda kuamini mambo ya kishirikina" nikamwambia "sasa mimi nafanyaje maana nahisi kuchanganyikiwa" akanambia "cha kwanza stop kabisa kujihusisha na mambo ya kishirikina,siku zote umekuwa ukitumia hizi pesa bila ya shida yoyote,mambo ya kuambiwa pesa haukutakiwa kuzimiliki aliyemiliki ameshaondoka je alikwambia kitu chochote?
Nikamwambia "hajawahi kuniambia kitu kibaya" akanambia "watu upata neema ya kupata pesa katika mazingira ambayo hayaelezeki,kuna mtu anawez akazitafuta pesa na asizitumie neema ikamuangukia mtu mwingine na akazitumia,haimaanishi yule mtu aliyepata ni kwa njia mbaya" huyu shemeji yangu tulizungumza kwa muda mrefu sana na akanambia kuna vitu nimeviweka kwenye biashara uenda hivyo pengine sasa ndio vinakula biashara yangu ili niendelee kutishiwa na niendelee kutoa pesa kwa yule mganga" nikipiga hesabu toka nimeanza kwenda kwa yule mganga pesa ngapi nimetoa kiukweli imefika hata milioni ishirini ambayo nimetumia kwa njia mbalimbali kwa maelekezo yake na vitu ambavyo alinipa nikaviweka katika maduka yangu ambapo naweka lakini nazidi kupata matatizo na huyu shemeji akiniambia "hivyo ambavyo umeweka ndio vinazidi kuharibu biashara yako,vinazidi kukupa hofu na hofu inakufanya wewe uendelee kutoa pesa na utaendelea kutoa pesa huku ukihofia kitu ambacho hakipo.
Hakipo Rojas na umewasaidia watoto yatima wale,umetoa sadaka zako,sadaka zako zimekuwa ni baraka,pesa hiyo ni pesa halali mtu huyo alikupa kwa upendo wa dhatina Mungu alitaka wewe uwe na pesa,unajua Rojas katika maisha tunaishi kuna watu wanapata pesa kwa neema ya Mungu tu,yeye mwenyewe ukimuuliza anasema nilihustle kweli lakini katika nyakati sielewi nilipata pesa,wewe ulibahatika kupata pesa katika mazingira ambayo Mungu aliamua kukupa pesa ila wewe ulipoikamata pesa ukajikuta unachanganyikiwa,unazifanyia anasa,unazifanyia katika mambo yasiyofaa lakini Mungu ni wa rehema,Mungu wetu ni wa upendo anakusamehe kabisa ndio kama hivi na maisha yanaendelea" huyu mama hakuishia tu bali alinambia "twende ofisi baada ya ofisi niambie hivyo vitu ambavyo umevificha uko unaogopa kuvitoa mimi nitavitoa" tukaambatana pamoja na yeye maana nilikuwa nimehifadhi vibuyu ambavyo vimefungwa na vitambaa,vibuyu na vidudedude vingi tu kwahiyo kila ofisi nikawa nimewekakwa siri mfanyakazi asione yaani kuhakikisha vinakuwa salama kwa ajili ya ulinzi na hivi vitu nimeanza kuvifanya baada ya kupata hofu na mimi kutaka majibu sana ya kile ambacho nimekuwa ninapitia,tulivitoa vyote katika maeneo yote,alivikusanya na yeye mwenyewe alivichoma moto na akasema "tunaye Mungu wetu asiyeshindwa na jambo lolote,hakuna pesa ambayo isiyokuma pesa halali,pesa zote ni za Mungu hakuna pesa ya shetani,hizo pesa za shetani ni za kwao lakini sisi hatutayasujudu hayo,hakuna uharibifu wowote utakaotokea tena kwa sababu vyote vyakuleta uharibifu visharudi kwao"

Huyu mwanamke ni shemeji yangu lakini alinitia moyo sana,akuishia hapo kwani alizidi kuongea na mimi,kukaa na mimi kwa upendo na akazidi kunishauri kuhusiana na yule mwanamke ambaye ameshakuwa sehemu ya maisha yangu akasema "lazima umtoe yule mwanamke katika maisha yako" yule mwanamke anafanya mambo ya kikahaba lakini ameshika akili yangu sana na nimejikuta natoa pesa nyingi kwake,akasema "huyu sio mke,huyu sio mke kabisa na Mungu atakusaidia kukuvusha hapo".

Tangu mimi nilipotoa vitu vyote vya kiganga sikuona shida yoyote yaani gari kudondoka wala matatizo yoyote kutokea,nikarudi nikaanza kuona amani inarudi na zaidi kumkumbuka rafiki yangu ambaye alinipa pesa,nikawekeza zaidi kwa hawa watoto mara nyingi zaidi ya ilivyokuwa kawaida na siku zilivyoendelea kusogea na nikazidi kuzipambania zile pesa ziendelee kudumu,ziendelee kudumu utajiri huu ambao ninaumiliki uendelee kudumu japo vipindi vya uchumi vinakuwa tofauti kuna kipindi mambo hayakuwa mazuri lakini sikudondoka kabisa,bado niliamka tena na kuendelea kupambana kila inayoitwa leo,kila inayoitwa leo kuhakikisha maisha yanasonga mbele.

Katika mengi ambayo yamekuwa ni faraja kwangu ni kuona watoto wa mshkaji wamekua na mmoja kati ya watoto wa mshkaji ameolewa na mimi nilisimama kama baba,nilisimama kama mtu muhimu katika tukio husika.
Muda umesogea sasa mimi ni baba wa familia niko na mke pamoja na watoto lakini sina kiwango kile ambacho nilipata cha nyakati zile pesa nyingi sana lakini sasa hivi nina pesa za kuweza kuendesha maisha yangu,kusaidia ndugu zangu,za kuendesha gari nzuri,za kuishi kwenye nyumba nzuri na maisha mengine yanaendelea.



MWISHO!
moneytalk beb ushapita hapa
 
Leo hii nimefanimiwa juimaliza hii story. Episode ya kwanza ninetumia week moja kuimaliza ila jana nilijikaza sana mpaka sasa ndio nimemaliza Story nzuri ya kusisimua na mafundisho mengi Shukrani sana ndugu shikamkono01 kutuletea story hii. .


Kichwa kinauma sana kusoma story kutokana na uandishi wako. Hapa nimemeza paradox yan kichw kinagonga kila nikimaliza episode namaliza kwa shida sana. Please usichukie hebu pita kwenye nyuzi za leadermore au JBourne59 ujifinze mpangilio. .

Aina ya upangiliaji wako na uandishi unarudia maneno unaumiza sana. .

Mungu akubariki sana sana sana na shukrani za dhoti kutuletea story hii. I am looking forward for your upcoming story. Kama nimezungumza jambo likakukera nisamehe sio dhumuni langu kwani MIMI NI MTU MWEMA SANA. Ukitazama macho yangu utajua kuwa mimi ni mtu Mwema sana. .
Pole ndugu yangu na wala usijisikie vibaya kwa maoni yako,ni ya kujenga sana ndugu yangu ila ule mzgo wangu haujanitumia 😂😂
 
Back
Top Bottom