kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 277
Kama huyo jamaa yako kazi yake inahusiana na taaluma katika ngazi yoyote aseme tu kuwa ni matokeo ya mwanafunzi wake mengine yatajulikana baadaye.Tofauti na hapo mh......
Kyabu haoni tatizo hapo ... The Creator alituagiza "..zaeni mkaongezeke.." Wanawake wa "kisasa" wanataka kuzaa watoto kwa "mahesabu" na hayo ndiyo matokeo yake. Hana haja ya kuomba msamaha bali ni kumwambia mkewe kuwa tunatarajia kupata mtoto mwingine muda mfupi ujao ... Mwanamke lazima aheshimu maamuzi ya Mwanamume!
Huenda hii ikafanya kazi!..Kumbe kweli mAmbo yanayofanyika gizani yatadhihirika hadharani kwenye Nuru!KAka PJ mfano huu unatuonyesha wazi kuwa siku MUNGU akiamua kukuumbua atakuumbua tu?? Hivi ulimwuliza sababu ya yeye kukiweka kidhibiti A ndani ya suruali kama police wa mashtaka ilikuwa ni nini? Nina uhakika atakujibu hata haelewi ilikuwaje: Hiyo ni kazi ya MUNGU kaamua kumpatiliza kwa maovu yake.
Hata akikana kuwa hafahamu bado haisaidii kwani ndio atakuwa ameanza maisha ya Web of Lies' maana imagine haya kafanikiwa kumtia changa la macho mkewe juu ya kipimo ambacho kimeonyesha positive. Mtoto akizaliwa kuna mauongo mengine yatafuata - kugawa kupato cha familia kuitunza familia mpya lazima atadanganya, siku mtoto akiumwa lazima atadanganya ili amuhudumie, siku akienda shule lazima atadanganya ili amlipie ada, mpaka siku anaoa au kuolewa pia atadanganya ili ahudhurie harusi ile peke yake yaani kila siku itakuwa lies, lies and more lies. Taabu yote hiyo ya nini kama si kuuchosha tu ubongo kwa sababu ukiwa mwongo lazima uwe na kumbukumbu kwa hiyo yeye atakuwa anafanya kazi kubwa ya kuupdate ubongo wake kila siku ili asichemshe eh!! atajikuta anazeeka hadi maini kabla ya kufa.
Wakati hata yote yangezuiliwa na tendo moja tu- KUKIRI kwa kupiga magoti na kukamua machozi
"Mke wangu nisamehe, huyu mwanamke nilipitiwa tu siku moja ndo amekuja anadai ana mimba yangu ndo nikawa siamini ndo nikamwambie nikampime ndo majibu ndo haya mke wangu. Lakini hata hivyo sweetheart siamini kabisa najutia sana kosa hili na ninamwomba MUNGU anisaidie isiwe mimba yangu.......Hivi darling unafahamu sehemu wanayopima DNA? Nakuomba unisaidie kunipeleka mke wangu please"
Hata awe na moyo mgumu kiasi gani, huruma ya kike itamwingia atamwelewa na kumshika mkono ili amprovie mwanamke mwenzake kuwa hafai. Na hata ikikutwa ni kweli ya kwake basi mke atalipokea ----- wanawake tunabeba mengi!! Tuoneni tu tukitembea na kunyongesha nyonga. Moyoni yametujaa
Ah am out of here. Mbarikiwe
Hahaha...angefuata zile sheria mama za infii yasingemkuta
Labda jinsi ya kumsaidia ni mpaka PJ aniambie huyu bwana profesheni yake ni nini? Ana mabinti? Ana hausigelo.....kama ni daktai/nesi...kesi kwisha. kama ana mabinti/hausigelo....kuna ubaya gani wa baba kupima kama bintiye/hausigelo kujua kama ana mimba? Na atapimaje bila kuwa na kipimio.
Will be right back!
Kyabu naona umesahau kuwa hao hao wanawake wa 'kisasa' kama ulivyowaita ndio wale wasiopenda kuburuzwa kama watoto wadogo........kwa usasa wao wanataka hata hayo maamuzi ya mume yajengewe hoja inayoeleweka mezani na si kudictate otherwise unajichimbia moto wa makaa ya mawe usiozimika.Kyabu haoni tatizo hapo ... The Creator alituagiza "..zaeni mkaongezeke.." Wanawake wa "kisasa" wanataka kuzaa watoto kwa "mahesabu" na hayo ndiyo matokeo yake. Hana haja ya kuomba msamaha bali ni kumwambia mkewe kuwa tunatarajia kupata mtoto mwingine muda mfupi ujao ... Mwanamke lazima aheshimu maamuzi ya Mwanamume!
Kyabu naona umesahau kuwa hao hao wanawake wa 'kisasa' kama ulivyowaita ndio wale wasiopenda kuburuzwa kama watoto wadogo........kwa usasa wao wanataka hata hayo maamuzi ya mume yajengewe hoja inayoeleweka mezani na si kudictate otherwise unajichimbia moto wa makaa ya mawe usiozimika.
Umalaya wote utakuisha! tukiwaambia mutulie kwenye ndoa zenu hamsikii sasa hapo akili mu kichwa
www.chinga2010.blogspot.com
jamaa inabidi akubali kosa halaf aombe razi tu. wanamama wameumbwa na mioyo laini atasamehe tu na hii itampa uhuru wa kuwa karib na mwanawe, sio anaonana na mwanawe kwa kunyatia nyatia.
halaf uzembe mwengine bana! hivi jamaa anatembea na mikojo hata halufu haskii? au jamaa anakoga weekend tu so pua lake halitafautishi mkojo na pafyum?
Huenda hii ikafanya kazi!..Kumbe kweli mAmbo yanayofanyika gizani yatadhihirika hadharani kwenye Nuru!
kazi ipo, kumbe ndio inachowapa kichwa cha kufanya maovu huko nje? hapo ujue tayari familia imeingia dosari kubwa, mama nae akiwa na roho ndogo ataishilia kutafuta wa kumpooza machungu, tit 4 tat...mijanaume inapenda matatizo kweli...mxsii