Mkataba na DP World siyo miaka 100, bali ni MILELE

Mkataba na DP World siyo miaka 100, bali ni MILELE

Nobunaga

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2019
Posts
1,205
Reaction score
5,121
malisa_gj-20230607-0001.jpg


Swali ambalo limeulizwa sana mkataba huu ni wa muda gani? Wapi palipoandikwa miaka 100? Au wapi palipoandikwa miezi 12 ambayo TPA wamesema? Jibu lipo kwenye kufungu cha 23(4) cha mkataba.

Kifungu hicho kinasema mkataba ukishasainiwa, pande mbili za mkataba (serikali ya TZ na serikali ya Dubai) hakuna upande utakaoruhusiwa kukosoa (denounce), kujitoa (withdraw), kuzuia (suspend) au kuvunja mkataba (terminate) kwa sababu yoyote ile.

Kifungu hicho kinasema hata ikitokea upande mmoja ukashindwa kutekeleza masharti ya mkataba, bado hairuhusiwi kuvunja, wala kujitoa kwenye mkataba huo. Maana yake ni kwamba, Mwarabu akisema atapanua bandari ya Dar iwe kubwa zaidi, halafu akashindwa kufanya hivyo, haturuhusiwi kuvunja mkataba. Sijui unaelewa?

Hawakuishia hapo, kifungu hichohicho kinaeleza kwamba hata tukiingia kwenye mgogoro wa kidiplomasia na Dubai, bado haturuhusiwi kuvunja mkataba (we can not terminate the agreement even in severance of diplomatic relation). Yani hata ikitokea sisi na UAE tumevunja uhusiano wa kibalozi, tukamfurusha balozi wao, bado wataendelea kuendesha bandari yetu. Hata ikitokea tukapigana vita, bado haivunji mkataba. Waaarabu wataendelea kuendesha bandari yetu, penda tusipende.

Kwa lugha rahisi huu mkataba ni wa MILELE. Kwahiyo wale waliokua wanauliza kifungu gani kinachoeleza muda wa mkataba? Ni kifungu cha 23(4). Kinasema mkataba huo ni wa MILELE na MILELE mpaka Kristo atakaporudi kulichukua Kanisa.

Hii ni zaidi ya ndoa ya Kikristo ambayo ukishaapa kanisani, hata kama ana matege, ni wako huyo mpaka kifo kiwatenganishe. Na huu mkataba kifungu cha 23(4) kinasema ukishasaini tu, ngoma ni MILELE. Hakuna namna ya kutoka. Bahati mbaya tumeshasaini tangu October 2022.

Halafu "mjinga" mmoja aliyekua ripota wa TBC huko Namtumbo leo kawa Msemaji wa serikali, amekaa kwenye V8 anatuona Watanzania wote wajinga. Anatuambia eti ni mkataba wa miezi 12. Shame.!

Mnataka kuharibu urithi wa vizazi vyetu sababu ya matumbo? Hivi Nyerere angechumia tumbo tungepata uhuru? Endeleeni kutetea matumbo yenu, sisi tunatetea watoto na wajukuu zenu. Lakini ipo siku mtajibu. Kama si hapa, basi hata mbinguni.

MALISA GJ
 
Tanganyika Law Society (TLS) mko wapi kupinga MoU hiyo mahakamani au Viongozi wenu nao wameahidiwa mshiko kama Wabunge kuupitisha. Je, kama Mkataba utapitushwa kwa jinsi ulivyo kwenye MoU Kifungu cha 23(4), hamwoni nchi inakuwa siyo salama kabisa?

Kifungu hicho kinasema mkataba ukishasainiwa, pande mbili za mkataba (serikali ya TZ na serikali ya Dubai) hakuna upande utakaoruhusiwa kukosoa (denounce), kujitoa (withdraw), kuzuia (suspend) au kuvunja mkataba (terminate) kwa sababu yoyote ile.

Wana TLS wawekeni viongozi wenu kitimoto mjadili kwa undani hiyo MoU na kuishauri Serikali kwa maslahi mapana ya Taifa
 
Ile kuwekwa kwenye minara ya Dubai mlidhani ni kuifungua Tz eeeh? 😂

Nilikuwa najua kuwa tunaongozwa na moja kati ya watu incompitent, ila sikutarajia uchizi wa aina hii anaotaka kufanya.
 
Hao wabunge wenu wa chama kimoja mliowajaza huko bungeni hawafahamu hili ?.....
Kwa lugha rahisi huu mkataba ni wa MILELE. Kwahiyo wale waliokua wanauliza kifungu gani kinachoeleza muda wa mkataba? Ni kifungu cha 23(4). Kinasema mkataba huo ni wa MILELE na MILELE mpaka Kristo atakaporudi kulichukua Kanisa.
 
Suala la bandari la Muungano ajabu mkataba unataka bandari za Bara tuu ,Zenji wao hawataki ayo manufaa ya huu mkataba ?🤣 Daah
 
Ivi watu wote sisi wa bara tunakubalije kutawaliwa na watu wa Zanzibar ? Kwamba sisi tumekua Koloni la wazenji mpaka imefikia hatua ya kuuza mali zetu kwa ndugu zao waarabu kwa faida yao ama ? Kwamba sisi ni Bongo lala sana ama ?

Inafikirisha sana hii.

!!!??????
 
NAJUA IPO SIKU MTANIKUMBUKA.
Tunakumbuka kauli yake ya mara kwa mara kuwa nchi hii ni tajiri na sasa utajiri huo unachukuliwa na Waarabu.

Nyuma ya kuwaondoa Wamasai Loliondo na Ngorongoro ni kuiweka TANAPA mikononi mwa mwejezakaji kama inavyotaka kufanywa TPA kwa DP World, kwa kisingizio cha demokrasia ya uchumi. Kitachofuata ni TRC (Reli) baada ya SGR kuanza kutumika. ATC nayo iko kwenye njia hiyo hiyo ya kuwekwa mikononi mwa mwekezaji.

Kweli kweli anaupiga mwingi na tunabaki kuungombania. Orodha ni ndefu wa jinsi anavyoupiga mwingi:

Upande mmoja,
1) Demokrasia ya uchumi - wawekezaji wanashangilua
2) Vyama va siasa kufanya mikutano ya hadhara - wanasiasa wenye uchu wa madaraka wanashangilia
3) Watoto wa kike wanaopata mimba kurejea shuleni - wazazi wanashangilia
4) Uteuzi wa wanawake hadi ifike 50 kwa 50 - wanawake wanashangilia
5) Waliogushi vyeti kurudishwa kazini au kulipwa haki zao - familia husika, ndugu na marafiki wanashangilia
6) Wafanyakazi kurejeshewa nyongeza za kila mwaka na kupandishwa vyeo - wafanyakazi wanashangilia
7) nk - ongezea

Upande wa pili,
1) Machinga kufurumishwa kwenye maneo yao ya shughuli - wameanza maandamano
2) Tozo kila kona ya mzunguko wa fedha - wafanya biashara, wakulima, wafugaji, nk migomo
3) Huduma muhimu (nishati, maji, na afya) kuwa ghali - lawama mitandaoni

CHAWA wanasema ANAUPIGA MWINGI - pongezi kila hotuba
 
Back
Top Bottom