Mkataba wa Azam TV ligi kuu

Sababu walizoeleza Yanga kwa nini hawataki kulipwa sawa na vilabu vingine ni za kitoto, ni kweli wao ni klabu kubwa ni sawa na Simba lakini lazima wakumbuke Azam Media group hawadhamini vilabu wao wanadhamini ligi sasa labda watuambie hao vilabu vikubwa kama wanaweza kucheza ligi bila hivyo vilabu vingine wanavyoviita vidogo.

Na kingine watwambie mgawo wanaopata kutoka Vodacom je ni tofauti na mgawo wanaopata vilabu vingine? Je vipi kuhusu gate collection wanapocheza na hivyo vilabu vidogo wanagawana sawa au Yanga kwa sababu ni klabu kubwa wao wanapata zaidi? Na kama wanapata sawa kote huko kwa nini hizi za Azam wanataka wapewe tofauti na wengine?

Wao kama ni klabu kubwa na wanaamini wanaweza kuingiza hela kutokana na ukubwa wao si watafute wadhamini wengine kama vile walivyopata kutoka TBL. Yanga wanatakiwa wakubali hicho kiasi ili Azam waonyeshe hiyo ligi na timu ndogo kama ndugu zao Toto wasiwe wanawagharamia siku wanacheza na Simba.

Suala la kwamba tenda haikuwa wazi mimi sina uhakika nalo lakini TFF wenyewe wanasema dau la Azam ndo lilikuwa kubwa zaidi kuliko la supersport sasa wao walitaka supersport wapewe eti tu kwa sababu wanaonekana
sehemu kubwa Afrika kwani Yanga wanafanya biashara gani nje ya Tanzania wanataka waonekana nje? Wao si ni wa hapa hapa tu.
Kusema kwamba wana ugomvi na Azam wa kimchezo na wanatolea suala la Mrisho Ngasa kama mfano sio sawa, labda Yanga wangeweka wazi kwamba ugomvi wao na Azam ulianza lini? Je ulianza kipindi kile Yanga wanafungwa mfululizo au ulianza tu baada ya wao kumuuza Ngasa kwa Azam? Au ulianza pale Azam walipotaka kumuuza Ngasa kwa utovu wa nidhamu alivyoibusu jezi ya Yanga huku akijua yeye ni mchezaji wa Azam? Ieleweke Yanga walitamka wazi kabisa kupitia kwa aliyekuwa katibu wao (Mwesiga) Ngasa hakuwa na thamani ya zaidi ya TZS.20M kwa hiyo wao wasingeweza kutoa zaidi ya hapo, sasa wanapotaka kutuaminisha kwamba Azam hawakutaka kuwauzia Yanga si kweli ila wao walitaka wampate kwa bei chee sababu Ngasa anaipenda Yanga.
Ninachoona hapa kwa sababu ni ngumu kutofautisha Azam FC na makampuni mengine ya Bakhresa na Bakhresa mwenyewe kama ilivyo ngumu (kwa sasa) kutofautisha Yanga na Manji, nalazimika kuamini Manji na Bakhresa watakuwa na msuguano wao wa kibiashara, nalazimika kuamini hivyo kwa sababu makamu mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga na katibu mkuu Mwalusako walishiriki vikao vyote na hoja zao zilijibiwa na wenyewe wakaondoka kwenye vikao wameridhika iweje leo wageuke, je ni shinikizo la mwenyekiti Manji au ni shinikizo la wajumbe wengine wa kamati ya utendaji? Kwa vyovyote vile mwenyekiti Manji ni kila kitu kwa Yanga (kwa sasa) hivyo lazima atakuwa yeye ndo aliyebatilisha waliyokubaliana kina Sanga kwenye vikao.
Hoja ya kwamba Azam Media Group hawawezi kudhamini kwa haki kwa sababu nao ni washiriki kwenye ligi haina uzito kwa sababu kuna mifano ya makampuni yanayodhamini ligi za nchi mbali mbali na yenyewe yakiwa na timu inayoshiriki kwenye ligi hiyo; mfano: Supersport wana timu inayoshiriki ligi kuu ya Afrika kusini na wao ni wadhamini wa ligi hiyo; EABL wanadhamini ligi kuu ya Kenya na wao wana timu inayoshiriki hiyo ligi; Mashindano ya vilabu ya CECAFA yanadhaminiwa na Rais wa Rwanda ambaye ndo Amiri jeshi mkuu wao na mara nyingi timu ya APR ambayo ni timu ya jeshi inashiriki haya mashindano, kama haitoshi Manji aliongeza udhamini wa mashindano ya CECAFA ya vilabu huku akijua kwamba yeye ni mwenyekiti wa Yanga na timu yake mara nyingi inashiriki kwenye hayo mashindano.
 
Kweli na sawa na Man U kuonyesha EPL

Vipi kuhusu SuperSport kuonyesha ligi ya Afrika kusini na huku wakimiliki timu ya SuperSport United inayoshiriki kwenye ligi hiyo hiyo...? Mfanye utafiti sio kujiskia raha kubofya keyboard zenu mkiandika mashudu...!
 
hivi arsenal wanaweza kukubali mechi zao zionyeshwe man utd tv?

mbona timu za Afrika Kusini zimekubali zionyeshwe na SuperSport huku wakijua kuwa supersport wana timu yao kwenye ligi...?Acha akili za kushikiwa mkuu, usifuate mkumbo.
 
Tatizo kubwa hapa ni je tendering process ilifanyika? Kulikuwa na tangazo la kuzitaka tv icluding dstv kuleta quotation ili washindane? Kama jibu ni hapana, hao azam tv wamepewaje hiyo nafasi? Ni kigezo gani kimetumika?

Tibaa

Tatizo hapa ni migongano ya kimaslahi na chuki binafsi. Mfano swala la Ngasa lina uhusiano gani na haki ya kuonyesha mechi...!?Na kuhusu kutotangazwa kwa tender eti ndo sababu nakataa kwasababu Tff na vilabu vyetu havina utamaduni wa kutangaza tenda. Mikataba mingi tunashtukizwa wakati wa kusaini tu kama huu wa Azam tv. Labda kama wewe mkuu ulishawahi kuona tender zozote kwenye vyombo vya habari unaweza kuviweka hapa ili niibatilishe hii kauli yangu. Vinginevyo kwenye suala la tender hawana hoja wana lazimisha tu.
 
Yanga hawana hoja ya msingi kwa hili suala,ila wao wanataka kuleta ubabaishaji tu,manji alisema kuwa hakuna kiongozi yeyote ya yanga aliyehusishwa kwenye mchakato huo,wakati msemaji na katibu wa yanga walikuwepo toka mwanzo hadi mwisho na msemaji wa yanga amekubali hilo,eti walizidiwa na wenzao kisa walikuwa wengi!na manji anapotosha umma kuwa hakuna ligi duniani inayodhaminiwa na kampuni ambayo ina timu yake kwenye ligi husika!ukienda kenya kampuni ya bia kupitia bia yake ya tusker,ina timu ya tusker,nenda s.africa,kituo cha super sport,kina timu yake ya super sport united na ndio wanaonyesha ligi ya s.africa!Huyo manji concern yake kubwa ni kutotaka kuona na vilabu vingine vinapata japo kipato kitakacho wafanya wamalize ligi vizuri kwani milioni 100,kwa kila timu c haba!badala ya kuangalia vyanzo vingine vya mapato yeye manji anaumia na mapato ya mlangoni!na ndio maana hawataki hivi vilabu vikubawa(sio vikubwa bali ni vikongwe)visiwe na vyanzo vya mapato vya kuaminika ili hao wanaojita wafadhiri wazidi kuabudiwa,na mchawi wa soka letu ni yanga na simba tu.Na ndio maana kamati ya ligi imewaambia kama kuna mdhamini anayeweza toa dau zaidi ya hilo milango ipo wazi ndani ya cku 30.Au kama ni hivyo bas mechi za yanga zitakuwa hazionyeshwi,mjanja nani?hata kwenye kupokea zawadi c walikuwa wamegomea,mwisho wake sote tunajua,hata hili ni upepo utapita tu.Hata ukiangalia mizania ya mapato na matumizi yao cku zote ma2mizi yanazidi mapato,ila ni sìfa tu.
 
Yote kwa yote me nampongeza azam,simba na yanga wanambwela tu,hadi leo wanafanyia mazoezi LOYOLA NA KINESI,SASA NA HUKO WATAMLAUMU BAKHRESSA???
 
Kama vipi basi dili apewe DSTV ili mgeni ale mema ya nchi, maana uchoyo mwengine hauna mashiko. AZAM TV wala haimilikiwi na Bakhresa na wala haina uhusiano wa kimapato na AZAM FC, sana sana Bakhresa atakua kama mdau tu na facilitator. Watu wakiona jina AZAM tu basi ishakua shida.
 

Wewe Yanga sio wajinga hawakurupuki usidhani hii team inaongozwa na al shabab na wahaini kuna watu wenye elimu na fweza zao hapo mburula hii si Habari ya mbwiga mbwiguke mkola nyani
 

Mkuu, hatuwezi kuzungumzia utawala bora na kupiga vita rushwa kwenye taasisi zetu wakati tunabariki malpractices za body kama TFF kutotumia system ya kutangaza tender. Kwamba TFF uwa hawafanyi hivyo, basi hiyo iwe ni justification kuendelea kufanya hivyo hata kwa issue muhimu kama hii. Unajuaje ITV au Star TV au TV nyingine yoyote wangekuja na package nzuri zaidi ya hiyo iliyoahidiwa na Azam TV?

Hapa kuna tatizo.

Tiba
 
mbona timu za Afrika Kusini zimekubali zionyeshwe na SuperSport huku wakijua kuwa supersport wana timu yao kwenye ligi...?Acha akili za kushikiwa mkuu, usifuate mkumbo.

wewe usishikiwa akili wala mkumbo....hebu tuambie tender ilitolewa lini na azam tv ikashinda[sijui imeanza/itaanza lini matangazo]???mkataba gani unaohusu maslahi ya timu unafanyika kati ya tff na azam tv bila kushirikisha timu yoyote??kwanini bodi ya muda TPL inaingia mkataba mrefu wakati kuna TPL itaanzishwa soon wana haraka gani??
 
Hii ni Manji FC na siyo Young African Sports Club. Pole watana kama hamtaki acha wengine waendelee
 

two wrongs dont make a right.....u dont know what ur talking about......kwa hio kwasababu siku za nyuma TFF walikuwa wanaburuza timu ndio waendelee hivyohivyo,poor you,sio sasa hivi,YANGA kuna watu wana akili huwezi kuwaburuza,aidha kwa maslahi yao binafsi au ya timu wanajua nini kinatakiwa kifanyike
 

get ur facts right.....
 

Yote kwa yote yanga wana hoja japokuwa hawatapata faida yoyote kwenye mgogoro huu kama watashindwa kukubaliana kibiashara na AZAM TV kiungwana timu zetu zinahitaji sana udhamini ili kuongeza mapato Yao Lakini tusisahau thamani ya timu hizi kama ilivyo yanga inathamani yake pia, Lakini je YANGA ina mshindani mbadala zaidi wa azamtv kwa sasa?? Kama yupo ajitokeze tuu nilisikia labda dstv Lakini nao dau Lao bado ni Dogo ukilinganisha na AZAM ushauri wangu waangalie zaidi vipengele vya mkataba kama inawezekana kuwe na kuuangalia upya makubaliano yao iwapo atatokea mshindani mwenye dau kubwa zaidi, Lakini AZAM tv wapewe nafasi ya awali ili tusogee mbele, hata kama tunasogea hatua moja katika safari yetu kisoka sio sawa na kubaki palepale hatua 0.
 

upo sahihi mkuu Yanga watueleze kuhusu hiyo migawo mengine kama wanapata sawa na timu zingine au la! Halafu hii ishu za timu mbili za Simba na Yanga kila siku kupiga kelele kuwa wao ni timu kubwa na kujifananisha na timu kama Man Utd au Reaal Madrid na Chelse huko ulaya me naupinga kabisa utajiitaje we timu kubwa eti upate maslah makubwa kwa kujifananisha na Man utd wakat hata uwanja wa mazoezi huna! Mbona timu hizi zinapenda kujiita timu kubwa linapokuja suala la pesa tu! Aaargh inakela kwa kweli. Sio siri hizi timu mbili zinachangia kwa kiasi fulani kuuwa soka letu.
 
Baadae wakapelekea hadi timu yao kuwa na mktaba binafsi na wakaanza kujidai nayo.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…