Mkataba wa TRL (TRC)

Ndugu Watanzania kwa mara Nyingine Tena Tunaona Serekali yetu ina vyo tufanyia Usanii.
Mimi ninaomba kumuuliza Huyo Pinda na Bot , mkopo huo umetoka kwenye fungu gani au Bank Ipi? na nini ni Dhamana ya Huo Mkopo?
Pili hizo Fedha zilizo letwa na Muwekezaji ili kupata 51% share zipo wapi?
Ndio yananza yale yale ya ATC na SA, ambapo serekali iliingia mkataba wa namna hii , mwisho wa siku tukawa tunatoa fedha za uendeshaji.
 

KOSA SIO LA WAHINDI HAPA!

Wakati tunapambana na Ufisadi, ni muhimu tukaeelewa mambo ya nchi yanavyo endeshwa kabla ya kurusha mikuki gizani, vinginevyo watatuzidi kete. Mkataba ni kati ya Serikali na Kampuni, kwa mujibu wa sheria, sio kwa mujibu wa Serikali. Serikali haina nguvu ya kuvunja mkataba inapotaka. Inabidi waende kwanza mahakamani.

Kawaida, mahakamani sio rahisi sana kuvunja mkataba. Ndio maana leo jioni tumelipa dola laki moja na nusu kwa dili la Richmond na warithi wake, na kesho asubuhi tutalipa tena.

Ina maana tudai uwajibikaji katika kuingia, si kujitoa, katika hii mikataba. Wahindi wamekudanganyeni, kwani waliongea kikwao? Mkataba wa kibiashara una vipengele vinavyosema nini la kufanya kama mmoja akishindwa kutimiza wajibu wake. Haiendi kwa kutegemea kauli mtu.

Kosa sio la wahindi. Ni sisi ndio tatizo (kama hizi habari ni kweli, manake hatujapata details zozote bado.
 

Mkuu Mkandara!

Haya mashirika yote tuliyaua wenyewe. Hiyo TRC ilikuwa hauwezi kupata tiketi bila kujuana na mtu, hali ya mabehewa ilikuwa ovyo, huduma ndiyo usiseme. Mimi nakumbuka wakati ikiitwa relwe na mtu ukisafiri daraja la kwanza aina ya huduma unayopata kuanzia mashuka hadi chakula kilicho cha standard ya hali ya juu! yote haya tukayaachia yakaporomoka hadi chakula kwenye treni ikawa tenda. Mashirika ya maji,umeme, ndege hivyo hivyo. Hata shirika ambalo leo kwa kipimo chochote kina mafanikio makubwa kama la bia wakati tunaendesha wenyewe lilijaa mizengwe. Ukiwa na shughuli lazima uhakikishe kwenye kamati ya vinywaji yuko mtu anayeweza kuwahakikishia mnapata KIBALI cha kununua bia. Hicho kibali ilikuwa unaweza kukiuza nusu ukifika getini kwa wenye mabaa. Bia zilikuwa zinatoka moja kwa moja kwenye production line kwenda kwa mteja. Chaguo lilikuwa ni safari au safari au safari. Yote haya tumeyasahau na kujifanya kuwa tulikabidhi kitu ambacho kilikuwa lulu. Sisi wenyewe tulichangia kwa kiasi kikubwa hali ya sasa ya mashirika haya. kama mchangiaji mmoja alivyokumbushia, hili shirika lilikuwa haliuziki. ndio maana tukaishia kwa huyu tapeli.

serikali ya kijerumani haitakubali hata siku moja kuingiza hela kwenye shirika ambalo serikali itaendelea kuendesha. Hiyo ilikuwa zamani. Wanawajibika kwa wapiga kura wao kwa pesa zote wanazozitoa kama msaada. Tumeishamgusa kipofu mkono na ametushtukia.
 

Mkuu hapo umesema. Tunakuwa na pupa kuingia mikataba ( mara nyingi katika kuonyesha mafanikio kwa wananchi) bila ya kuangalia consequences zake. Hauwezi kutegemea hata siku moja huyo unaye'negotiate' naye ataangalia maslahi yako. Wajibu wake yeye ni kwa shareholders wake full stop. Atahakikisha anapata mkataba utakamruhusu kuvuna to the maximum with the minimum cost. Na wewe unatakiwa kumbana ili uhakikishe anapata minimum at the maximum cost kwake yeye. Ndvyo ilivyo, ndio biashara.
 
Wakulu, heshima mbele...... Yaani nimekuwa naangalia wachangiaji nakadhalika kwa kweli huku kwenye hii ya TRL, tukirudi ATCL, TTCL, TANESCO, nk kote huko inaelekea tunaingia katika mahitimisho yaliyolingana:
1. WaTanzania/wazalendo hatuwezi kuendesha parastatals kwa faida??
2. Tunapoamua kubinafsisha kunakuwa na jinamizi la kupigwa changa la macho "utapeli" ambapo wawekezaji wamekuwa wanalalia serikali/waTanzania - Value, benefits, capacity/efficiency
3. Watu wetu kuishia kufikiria maslahi yao na sio ya nchi
4. Kuwepo kwa rushwa ya hali ya juu katika kutafuta viongozi/wawakilishi wa wanancchi (bunge, madiwani etc) ambapo wanaoingia sio SAFI BALI NI WACHAFU ZAIDI SABABU NDIO WENYE KUWEZA KUPATA KITU KIDOGO YA KUWAPA WAPIGA KULA (ooops KURA)
5. Wahisani wa nje?? Mh nadhani kuna kitu hapa ili asiye nacho anyang'anywe...........

Sasa haya yameonekana, mimi kwa mawazo yangu ni kwamba kubadilisha PM, mawaziri, na manaibu wao haitasaidia mpaka pale tutakapo safisha mind zetu......
Hivi kuna aliyejiuliza kwa nini TCC, TBL, TIGO, CELTEL, etc etc ambayo ni makampuni yenye faida sana yameishai kuajiri vijana TENA WALIOSOMA NJE YA NCHI.......(yap, go and check)!!! Inaonyesha kwamba kuna kitu/mushkeli hapa nyumbani kuanzia vyuoni (sio mashuleni manake wale walioenda majuu walifanya mpaka form 6 hapa hapa nyumbani)...... Tukishatibu huku chini ndipo tuingie kwenye Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, sio kufukuza kazi bali kufanya "rejuvenation" kwa kuweka damu mpya na sio kuishia kuendeleza zile old blood ambazo more or less zipo daft.... kibaya zaidi ni huu muswada wa Civil Servants................

So kusonga mbele basi hizo 1-4 hapo juu lazima ziwe looked into!!!
 

sasa wafanya kazi wa makampuni mengine wakiandamana na kutaka kuongezwa mishahara je pinda atawabail out emploYers tena?? Viongozi wetu vichwa maji kweli..DONT BLAME RITES BLAME KIKWETE KWA KUONGEZA MISHAHARA BILA KUANGALIA HALI HALISI YA ECONOMY...MSALA MWINGINE UNAKUJA YETU MACHO!!
 
jAMANI WANAJF tuanzishe topic ya kutaka kuwajua economic advisors wa raisi wetu?? Sitaki kuwatukana bila kujua agenda yao...seems kama serikali inaendeshwa kama biashara ya mitumba!!
 
Kapinga, hapo umesema manake kuna thread moja niligusia hapo mahali lakini ikawa ngumu kidogo....

Tatizo ni kwamba tunasema tunafuata Ilani ya Uchaguzi ya 2005, lakini swali ni kwamba je kuna plan on how to achieve it?? Kuna wanasiasa (wapiga debe) na lazima kuwe na think tanks (prezidaa's advisors) ambao walitakiwa wamshauri Muungwana kila step along the way, sasa hizi lawama lazima tuwajue hao ambao wamesinzia ili waamshwe wakishindwa mchakamchaka basi itabidi JF kama kawaida iweke chachu ili Muungwana akiyapitia basi anaweza badilisha kaseti.......
 
Ndugu Watanzania kwa mara Nyingine Tena Tunaona Serekali yetu ina vyo tufanyia Usanii.
Mimi ninaomba kumuuliza Huyo Pinda na Bot , mkopo huo umetoka kwenye fungu gani au Bank Ipi? na nini ni Dhamana ya Huo Mkopo?

Ungekuja na hoja pia unafikiri Serikali ingefanya nini!!! wakati wananchi wake wa Mikoa ya Tabora,Kigoma, Shinyanga, Mwanza wakiteseka kwa usafiri?

Assuming hizo hela zimetoka kwenye fungu la maafa? reallocation ya fund is operational issues... by the way it is just mkopo... Watanzania tuna matatizo... tuna muda mwingi wakupiga porojo... is this a issue real?
 
TUSIPOPITISHA SHERIA YA KUWANYONGA HADHARANI WANAOSAINI MIKATABA MIBOVU KAMA HII, TUTAENDELEA NA HUU USANII MPAKA MWISHO WA DUNIA.
 
Mi nikitafakari sana naona tatizo la mikataba mibovu sio la wataalamu wetu walioko serikalini kwamba ni wababaishaji.Tunao wataalamu wengi mahiri tena hata ukiangalia cv zao utashangaa vyuo walivyosomea na hata maksi walizopata iwe kwa vitendo au nadharia.Wala haiingiii akilini kwa mwanasheria kusema hajui kwamba business kadi haiwezi kuwa ushahidi wa ubia na kampuni fulani,wanajua sana,sasa tatizo ni nini?Tatizo kubwa lionaloikabili nchi yetu ni wasomi kupuuzwa na kushinikizwa kwa maslahi ya wanasiasa.Ukitaka kuamini hili nenda kwenye halmashauri nyingi nchini,wanasheria hawakai,wala maafisa ardhi kila siku wanatofautiana na madiwani na kwakuwa madiwani wana power wanaishia kuwafukuza kazi au basi hao wataalamu kuamua kujiondoa.Mtu unamshauri kabisa mathalani mkuu wa chuo au bodi fulani kwamba msimfukuze huyu mfanyakazi bila fair hearing,unampa kabisa utaratibu,matokeo yake wanakwambia ushauri wako kwa bodi sio binding na wanaendelea kutekeleza azma yao.Ni kwa wale wachache tu wanaoweza kushikilia misimamo yao ndio wanaoweza kuamua kuachia ngazi,sasa wale wenzangu na mimi ambao hawana ubavu wa kutafuta kazi pengine basi wanabaki wamenyamaza tu wanajibu NDIYO MZEE.Mambo yanakwenda.
Suluhu ya haya mambo ni kuwaachia wataalamu wetu wafanye kazi bila kui ngiliwa na masilahi ya kisiasa,kwa maana ya kwamba bila kuandikiwa vimemo vya namna gani wafanye hizo kazi.Mtaalamu anatakiwa kuwa huru kama vile rubani au dereva anapoendesha gari dhidi ya abiria wake.Anaingiliwa tu pale inapoonekana wazi anakiuka.Lakini pia kama tuna nia ya dhati ya kukomesha umamluki huu basi yafaa itungwe sheria inayowabana watu wanaotoa ushauri yaani wataalamu kushughulikiwa mara ushauri wao au kuhusika kwao katika mchakato fulani kulivyoleta matokeo mabaya ya walichokifanya.Kwaufupi wawe huru kama majaji na ajira zao zilindwe kiasi kwamba ili wafukuzwe kazi lazima iundwe tume kuchunguza tuhuma zao kuona kama walikiuka maadili yao au je,waliamua kutofautiana na bosi kwakuwa alikuwa akiwalazimisha kukiuka masharti.Kwa mantiki hii wataalamu wetu watakuwa huru kutofautiana na wanasiasa pale wanapoelekezwa ndivyo sivyo,na kwakuwa wanlindwa na sheria waziri au mkurugenzi mmoja pekee hatakuwa na uwezo wa kuwafukuza au kuwashusha cheo,hadi liundwe jopo la watu watatu au nne kuchunguza madai ya huyo bosi dhidi ya mtaalamu anayetaka ashughulikiwe kwa kukiuka maagizo yake.mf.kukataa kuburuzwa au kufumbia macho mkataba au jambo fulani.
Mahakama zetu elo hii na duniani pote zimefanikiwa sana kutokana na principle hizi.Ndio maana zinaweza hata kutoa maamuzi mazito hata dhidi ya Rais.
 

Kama wamefanya re-allocation au kutoka funga la maafa si waseme kwa uwazi, na huo mkataba wa mkopo kama ni interest free au sivyo kwa nini wasiweke mambo wazi?
Maana tumeona mikopo kwa akina Mzindakaya, fedha zilizokuwa zikitolewa na ATC wakati wa Mkataba na SA, ikumbukwe pia ilikuwepo Alliance Air.
Tatu hii kampuni ni ya kibiashara na kila upande una majukumu yake na Contribution yake katika Share capital, sasa kama hiyo project au hiyo biashara ya RITEs inalipa kwanini wasiende kukopa Bank.
Haya mambo ukiyaangalia kijujuu kama wewe unavyo angalia tutakua tuna fukia fukia uzembe mwingi na usanii unao fanyika katika hii contest ya maafa, na uwekezaji.
Nne ujue mambo ya kibiashara na kiuchumi haya endeshwi kisiasa, ndio maana wakati mwingine viongozi wanatoa maamuzi , ambayo unakuta yanapingana na Sheria au taratibu za kifedha na za kiuchumi.
Juzi juzi tu hapa Fedha zilitolewa wakati wa Issue ya Mahujaji, nayo ilitolewa kwenye Maafa? na Hata zikiwa zimetolewa kwenye maafa hivyo ndio jinsi ya kufanya biashara , ndugu yangu Kasheshe.
 
Augustoons, hapo nakubaliana nawe. Tunaelewa hilo na pia vyombo vya maana vya kuangalia haki mahali pa kazi vipo vikiwemo Professional bodies (ERB etc) na pia kwenye Vyama vya Wafanyakazi (TUCTO, etc), tatizo kama nilivyosema ni kuondoa mentality kutokea kwenye grass roots sababu pamoja na kuwepo vyama hivyo bado kuna matatizo mengi katika "Freedom of Professionals in Decission making"..... Angalia miradi ya barabara, TANESCO na mengine mengi, ina maana hivi vyombo havikuona hayo?? La hasha waliona lakini kuna mtu alishasema hizi appointies zitatupeleka pabaya.... ERB mwenyekiti ni appointee wa Muungwana, na mengine mengi sasa wewe umeteuliwa, utaweza kweli kutimiza adhma yako palipotofautiana na matakwa ya Muungwana?? La hasha.... Kwa nini hizi professional bodies zisiwe free of Political influences (presidential, ministerial appointees).... Kama Agustoons alivyosema kuondoa political influence then lazima tuanzie na professional bodies.......
 
Kama wamefanya re-allocation au kutoka funga la maafa si waseme kwa uwazi, na huo mkataba wa mkopo kama ni interest free au sivyo kwa nini wasiweke mambo wazi?

Na hali unavyoiona wewe unaona kuna muda wa kuweza kwenda kukopa Benki, wakati wenzetu wakiwa hawana usafiri... what broo... do you think big reall?

Maana tumeona mikopo kwa akina Mzindakaya, fedha zilizokuwa zikitolewa na ATC wakati wa Mkataba na SA, ikumbukwe pia ilikuwepo Alliance Air.
Mawazo mazuri but you can not do this when you already have crisis... kama ungewahi kuongoza... ungeona hili ni jambo la kawaida.

Tatu hii kampuni ni ya kibiashara na kila upande una majukumu yake na Contribution yake katika Share capital, sasa kama hiyo project au hiyo biashara ya RITEs inalipa kwanini wasiende kukopa Bank.

Time fackor... hope you will understand.

[QOUTE]
Haya mambo ukiyaangalia kijujuu kama wewe unavyo angalia tutakua tuna fukia fukia uzembe mwingi na usanii unao fanyika katika hii contest ya maafa, na uwekezaji.
[/QUOTE]
Angalia effect ya shirika kutofanya kazi mpaka upate mkopo baada ya miezi mitatu au sita... Please be serious a bit.

Nne ujue mambo ya kibiashara na kiuchumi haya endeshwi kisiasa, ndio maana wakati mwingine viongozi wanatoa maamuzi , ambayo unakuta yanapingana na Sheria au taratibu za kifedha na za kiuchumi.
Kweli kabisa kama wananchi wa Kigoma, Tabora, Shinyanga, Bukoba, Mwanza wangekuwa na usafiri mbadala... na wa rahisi... au kungekuwa na ushindani wa uendeshaji shughuli za Treni serikali isingeingilia.... angalia hali ilivyo sasa forget about the books you read.
Juzi juzi tu hapa Fedha zilitolewa wakati wa Issue ya Mahujaji, nayo ilitolewa kwenye Maafa? na Hata zikiwa zimetolewa kwenye maafa hivyo ndio jinsi ya kufanya biashara , ndugu yangu Kasheshe.

Kweli mkuu ... serikali ni mmliki wa ATC... the only shareholder... shirika lake likileta shida... linaweza ku-inject money...
 

Haya ndio matatizo ya kusaini mikataba na matapeli ambao walidanganya uwezo wao ili tu wapate huo mkataba. Sasa sijui wanatakiwa warudishe mkopo huo kwa muda gani na riba ni kiasi gani. Haitakuwa ajabu kusikia jamaa hawana uwezo wa kuulipa na kuingia mitini huku TRL ikabaki hoi bin taabani.
 
Sasa katika suala hili nani kashikilia mpini Rites au Serekali? Kama ni serekali kwanini wasivunje mkataba na kutoa hiyo hela ya maafa tukajua Moja?
Hiyo ingeleta economic sense, na Social sense.
Kuhusu kufikiria Big, mimi ninafikiria plan ya 5 years na kuendelea siyo hiyo ya siku moja. Juzi juzi tu hapa treni ilikuwa inaanzia Dodoma, je serekali hawakuona tatizo kwa usafiri kwa hao watu wa Tabora kigoma, shy, Mza.
Mbona waliacha hali hiyo kwa muda mrefu?
au ndio katika kutafuta justification ya kuwaingiza RITEs.
Na unavyo inject money lazima uangalia baadae itakuwaje, sio una inject money kwenye pipa lilotoboka, unless wewe ni kichaa.
Everything have it's limit au wewe huna hili neno LIMIT na Assesssment of the situation.
 
Kasheshe, swala la time factor kwa kweli naomba niseme kwamba itakuwa ni kuwatetea for nothing..... Ieleweke kwamba kama Rites walikuja kusaidia kuendeleza shirika letu la reli (kama sio kulizika kabisa), lazima walikuwa na plan of action ambayo Serikali/Wizara lazima iwe imekubaliana nalo. Katika hilo lazima kulikuwa na swala la kuongeza mishahara, kutengeneza/repairs mabehewa, injini, njia ya reli na hata vituo vya reli.... Sasa kama hili lilikuwepo iweje leo tuseme kwamba eti swala la kuongeza mishahara ni "Emmergency" ndipo tuanze kukimbia kimbia mpaka serikali itoe mkopo?? Kukubali hii kuna maanisha kwamba:
1. Rites na partner wake, GoT hawana plan of action for the revamping/ufufuaji wa TRC... Yale yale yaliyosemwa ni kama kuendesha biashara ya mitumba

2. Kama mshauri wa TRC enzi hizo (Rites contract to TRC) hawakuweka mkakati mzuri wa kuliendeleza shirika (alilipwa kuwa Consultant/mshauri) sasa kama aliweka hayo yote yakiwemo maslahi ya wafanyakazi inakuwaje leo kajipigia pasi (akaona inamshinda) aje kusema hana uwezo? Ina maana ule mkataba wake kwa kuishauri TRC kabla hajainunua alikuwa anafanya nini???
3. Serikali pamoja na mbia wake, Rites hawana contingency plan katika uendeshaji wa TRL ikimaanisha kwamba keshokutwa tena ikitokea yale mabehewa hewa ya kutoka India yakihitaji pesa za kuyakomboa (are we sure kuwa Rites anayamiliki huku ayatoapo??) Serikali kwa mara nyingine tena itatoa mkopo!! Hii ni sawa kweli jamani kwa wale mnaojua mambo ya Finance?? kwangu haileti maana kabisaaaa

Hivyo saying that naomba niseme kwamba tusiwe warahisi sana wa kusema maneno kama "Mipango ya Mungu - mtu akiugua kipindupindu mpaka kufa: Uzembe/Uchafu", "Mungu hakupenda uende leo - Ukiachwa na ndege Uzembe".... na badala yake tuwe more "Proactive"......

Mfano rahisi angalia issue ya Richmond "Eti kulikuwa na umuhimu wa kupata Emmergency Power", my %$@*@^!***
 

Bubu, hilo sio geni sana kwetu Mkuu, unakumbuka Richmond kwenye bid yake alisema amejenga Uwanja wa Mpira wa watu 65,000 Jijini Dar es Salaam, Tanzania?!?!?!!? Well sio kwamba wanatudanganya bali wanatuchezea Mkuu.... Watu wa nje wameshajua Tanzania ni Kichwa kwa mwendawazimu, Mwenye Mkasi, Wembe, Fyekeo, Panga we njoo tu utapata kipande cha kunyoa Mtu wangu na wanakuja kwa kasi kweli kweli manake na sisi tunaamua kuwawekea maji kabisaa (tax exeption, 10% etc)!!!
On top of that hawa jamaa walikuwa washauri wa TRC kuhusu swala zima la kuuzwa eti....... Huu ni mchezo ambao Mola atasaidia tutaona pale palipochezewa kisha tutawapata kwenye penati manake napo tutakaba humo humo..... Yana Mwisho Haya!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…