Mke anataka kuondoka, bila kufukuzwa..kuna umuhimu wakugawana mali

Mke anataka kuondoka, bila kufukuzwa..kuna umuhimu wakugawana mali

Deejay nasmile

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2011
Posts
5,794
Reaction score
5,352
wadau wa sheria ya mahusiano,ustawi jamii n.k kama kichwa kinavojieleza..endapo mwanamke wako anatengeneza visa ili muachane bila sababu ya msingi...yaaani hataki kuishi na wewe.na mlikuwa pamoja zaidi ya miaka na mna watoto..

..je anaweza kushtakiwa ustawi wa jamii???

je ataweza kumshtaki mumewe kikataliwa kugawana mali..

msaada hapo tafadhali
 
Kuna bwana ilimfika hali kama hiyo, aliondoka na begi lake la nguo tu na pesa kidogo mfukoni. Alimuachia mke watoto, nyumba na kila kitu. Kitu ambacho mke hakufahamu ni kuwa rizki aliondoka nayo mwanaume.

Baada ya miaka miwili alikuwa na biashara iliyoshamiri katika mkoa aliohamia. Mali inatafutwa lakini amani na upendo haviwezi kununuliwa.
 
wadau wa sheria ya mahusiano,ustawi jamii n.k kama kichwa kinavojieleza..endapo mwanamke wako anatengeneza visa ili muachane bila sababu ya msingi...yaaani hataki kuishi na wewe.na mlikuwa pamoja zaidi ya miaka na mna watoto..

..je anaweza kushtakiwa ustawi wa jamii???

je ataweza kumshtaki mumewe kikataliwa kugawana mali..

msaada hapo tafadhali
Itategemea sababu zipi anazitoa kuhusu kuachana nawewe ila pia kwakuwa yeye ndio anataka kuachana na pia mnawatoto uliozaa nae basi kisheria mali ni zawatoto yeye asepe na nguo zake tuu kwakuwa ametaka yeye ila muombe kiungwana tuu kuwa kama yupo sirious akupe talaka yeye hiyo itamfanya aweke asiwe na sababu ya kukushitaki popote kwakuwa yeye ndiye kakupa talaka.
 
Kwani umeambiwa na nani kuwa hiyo mali ndio yako ya mwisho wala huna tena uwezo wa kupata mali nyingine?? Ningelikuwa ni mimi, ningehama hadi mkoa niende kujitafutia mali kwingine na ningelimsahau kabisa huyu,
Mwanamke akikusudia kukuharibia usiendelee kushindana naye. Akienda kwa wanausalama wa leo, akagawa kitumbua chake, unalala sero siku 14 bila hata msaada wowote. Ukitoka tiyari umelegea.
Hakuna mali iliyopatikana kwa nguvu zako ambayo utashindwa kuipata tena pengine. Hama mji, mwachie ale jasho lako malipo anayo Mola.
 
kistaarabu tuu, unaonaje anapoamua kuondoka umpe atlst 1/4 ya mlivyochuma hata kama hajaomba?
 
Kuna bwana ilimfika hali kama hiyo, aliondoka na begi lake la nguo tu na pesa kidogo mfukoni. Alimuachia mke watoto, nyumba na kila kitu. Kitu ambacho mke hakufahamu ni kuwa rizki aliondoka nayo mwanaume.

Baada ya miaka miwili alikuwa na biashara iliyoshamiri katika mkoa aliohamia. Mali inatafutwa lakini amani na upendo haviwezi kununuliwa.
Jamaa alikosea jambo moja tu,alikosea sana kuacha watoto,
Mwanaume haachi Mali yake nyuma,Mali isiyohamishika wala kupotea ni watoto tu,
Ni ujinga kuacha Mali yako ya kufumu kwa mtu mwingine,
 
huwa kuna taratibu ndefu sana na sasa serikali inataka ipunguze talaka kwa kutotota talaka
 
huwa kuna taratibu ndefu sana na sasa serikali inataka ipunguze talaka kwa kutotota talaka
Kukaa na mtu anaetaka kuondoka ni mtihani mkubwa sana,na ni hatari sana,
Kukubali kuingia mtegoni na kumuacha bila utaratibu ni Bomu linaloweza kulipuka muda wowote mbeleni,
Kufuata utaratibu kisheria pia ni kazi sana kuishawishi mahakama ikuamini unachoomba,
Nimepitia maisha haya kwa matendo,najua mzigo uliopo,
Imenisumbua kiasi kila nilichokuwa nafanya kilikuwa gunia la miiba,
Lkn siraha pekee iliyoniokoa ni kuikubali hali maana anaetaka kuondoka huwa anafanya visa kusudi ili aachike,ukikosa utulivu unaishia jela,
Inataka utulivu sana,na umakini sana,bila kusahau kukusanya kila aina ya ushahidi,kitachokunusiru ni Mungu akuwezeshe utulivu ndo utapata hata nafasi ya kksanya ushahidi,
Lkn kuondoka na kuacha kila kitu siyo suruhu japo watu hudanganyana kuwa ndo njia sahihi,unaweza dhani unakimbia tatizo ukawa unaliahirisha tu,na ukitaka kupata amani usiweke kisasi,msamehe,muone siyo adui,mtakie mema,usiwaze kuacha watoto na usimdhurumu kitu halafua acha sheria iamue na uwe tayari kupokea matokeo yyte,
Nina mwaka sasa tangu linikute na nikapita,ninaishi na wanangu japo ni mzigo lkn kuna nafuu
 
yani vitu vinavyopewa priority na ustawi wa jamii ni matunzo ya watoto mengine mtamaliza soli za viatu mahakamani ustawi wa jamii hawataki ujinga siku izi
Inategemea na ukubwa wa tatizo,kifupi huwa wanazungusha ili kujiridhisha kuwa kweli mna tatizo siyo ujinga
 
wadau wa sheria ya mahusiano,ustawi jamii n.k kama kichwa kinavojieleza..endapo mwanamke wako anatengeneza visa ili muachane bila sababu ya msingi...yaaani hataki kuishi na wewe.na mlikuwa pamoja zaidi ya miaka na mna watoto..

..je anaweza kushtakiwa ustawi wa jamii???

je ataweza kumshtaki mumewe kikataliwa kugawana mali..

msaada hapo tafadhali
Ndio
 
Kuna bwana ilimfika hali kama hiyo, aliondoka na begi lake la nguo tu na pesa kidogo mfukoni. Alimuachia mke watoto, nyumba na kila kitu. Kitu ambacho mke hakufahamu ni kuwa rizki aliondoka nayo mwanaume.

Baada ya miaka miwili alikuwa na biashara iliyoshamiri katika mkoa aliohamia. Mali inatafutwa lakini amani na upendo haviwezi kununuliwa.
Aisee.ndio maana nakuwa your secret admirer
 
Itategemea sababu zipi anazitoa kuhusu kuachana nawewe ila pia kwakuwa yeye ndio anataka kuachana na pia mnawatoto uliozaa nae basi kisheria mali ni zawatoto yeye asepe na nguo zake tuu kwakuwa ametaka yeye ila muombe kiungwana tuu kuwa kama yupo sirious akupe talaka yeye hiyo itamfanya aweke asiwe na sababu ya kukushitaki popote kwakuwa yeye ndiye kakupa talaka.
Hii ngeni kwangu!! Kwani Talaka anapaswa atoe nani?
 
MIMI NAHISI SASA NDO MUANZE KUMSHAURI KISHERIA AFANYE NINI ILI ANUSULIKE KAMA WANASHERIA NA WASOMI KWA KUTOKANA NA PROFESSIONAL NA UZOEFU WA KAZI YENU JUU YA SWALA KAMA HILO
 
Kazi kweli kweli hizi ndoa,nlishuudia ya jamaa yangu wao hawakuwa na cha kugawana zaidi ya zawdi za harusi
 
Back
Top Bottom