Nilimuuliza kama ana udhaifu gani ambao mkewe huwa anaulalamikia mara kwa mara, yeye akadai kuwa yeye ni chakaramu sana na anapenda sana kujichanganya na watu wa rika zote, wake kwa waume kitu ambacho mkewe hapendi na kinamkera........... Ni kweli, jamaa anayo tabia hiyo kwa kuwa mimi ni rafiki yangu wa muda mrefu, namfahamu kitabia. sina uhakika kuhusu kuisaliti ndoa yake kwa sababu siko karibu naye saaana kama zamani kabla hajaoa.
Kuna wakati anadai mkewe alimwambia waziwazi kuwa anajisikia hayuko salama katika ndoa yake kutokana na tabia yake ya uchakaramu na kujichanganya na watu wakiwemo wanawake na wanaume...................na yeye anadai hawezi kuiacha tabia hiyo kwa sababu ameshazoea kucheka na watu bila ubaguzi.