Ifike mahali sauti yake ikitoka ndani iweni ya mwisho na hakuna wa kuhoji kwanini kasema hivi.
Alishakosea toka mwanzo lakini sasa bado anayo nafasi ya kurekebisha, kwanza kabisa siku atumie uamuzi wa boss achape makofi ya haswa, hadi sura ikoboke kisha amwambie nikikuta umeondoka hapa ndani usirudi tena humu ndani mwangu
well said mkuu....; tunaoa ili, among other things, tupate furaha, faraja, tujenge familia, tusaidiane kwenye mikikimikiki ya maisha n.k but ndoa nyingine ni kujitafutia ugonjwa wa moyo tu
Mh mfumo jiko ukoje mkuu?
cartura why is it interesting? its true a man has to be a man and with all due respects as head of house. ukiona mwanaume sentensi zako hazisomeki kama ni za baba nyumbani kwako jiangalie vizuri sana. lazima tofauti kati ya mama na baba as kichwa cha nyumba iwepo na usiwe kichwa tu kisicho na macho. si unajua ni kichwani pekee kwenye organ 5 za fahamu? so watch out.mmh, gfsonwin this is a very interesting position, especially coming from a lady...
lazima tofauti kati ya mama na baba as kichwa cha nyumba iwepo
mkuu, hiyo dhana ya 'friends' kwa mabinti ni kichaka cha kufichia vitu vingi sana...
Mke mweeema, anatoka kwa Bwana................................
Well said Fixed..wanaume wengi huoa sura na shepu nzuri badala ya kuchunguza tabia ya binti, sasa matokeo yake ndio hayo.. in a long-run kitakachoipa furaha na thamani ndoa yako ni tabia njema tu! tabia ikiwa mbaya hata shepu iwe nzuri vipi hutaiona, jamani wanaume mnaotaka kuoa mshirikisheni Mungu la sivyo mtaingia mlango wa kutoke. Aisee nimesikitishwa na hii habari hasa kitendo cha kumwacha mtoto wa miaka miwili na kwenda kunywa pombe.. ampeleke kuombewa labda ana mapepo
Good news i may call it ni kwamba binti amekula BAN usiku huu, natoka kwa mshkaji, kamuomba mama yake aje kukaa na mjukuu, bidada amemuvuzishwa. Imeniuma na imenisikitisha kuona wanandoa wamefikia stage hiyo kila nikimuangalia mtoto naumia kama mwanangu vile. Nimepewa jukumu la kupeleka petition ya divorce ili wagawane mali na mambo ya custody of the child na mwanamke asepe zake. The guy seems a bit releaved hata tumechoma samaki kwake na ndio nimeondoka, kiukweli aliyonieleza ni mengi zaidi, yani jamaa ana kifua aisee. Kumbe ameshawahi kumfuma mkewe na njemba akawa halali na mkewe kitanda kimoja. Leo ndo ananionyesha chumbani kwake kulivyo na partition, dah, jamani ndoa hizi. Ila wamezinguana mpaka jamaa kamnyang'anya kila kitu mpaka mahakama itakapotna tamko although wao ni wakatoliki kwa hiyo tunaanza na kusikiliza baraza wanasemaje pamoja walishapelekewa hiyo kesi na wakaisuluhisha.
Wanawake wa siku hizi wengi wao wanaangalia kama una elimu, kazi nzuri, gari mbili tatu, nyumba nk, wanasahau kuwa mali yaweza kuisha, elimu yaweza kutokusaidia, kesho unaamka unakuta umepofuka au umepata ulemavu. Je kwa wakati huo ni wanawake wangapi wako tayari kuishi na manaume kwa amani bila kumsimanga?
Maswali gani tena haya mkuu? Si umesoma hapo kuwa ametafuta suluhu sehemu mbalimbali.
Mpe pole sana Na kama kichwa cha family akae chini na mkewe amwambie ni vitu gani hapendelei na kama mwanamama yuko tayari kuacha waendelee na ndoa kama hayuko tayari basi amweleze yuko tayari kutoa talaka .
Akili inaweza kuingia kichwani na akabadilika .
namshangaa huyo mama kwa nini aliolewa
FL1 wamama wengi tu waliolewa wanapenda starehe, tunakutana nao sana tu sema hawa hawafanyi wanaume zao wakiwepo wanakuwa na kaunafiki flani hivi ka kujifanya wema mbele za macho ya waume zao, ila mme akiondoka na yeye ni kula bata tu,tena kwa hawa wanaume wanaosafiri safiri au wanaofanya kazi nje ya nchi pole zao, mama hakuna part anayoikosa
huyo mke itakuwa kapinda........
Namsikitikia hajui wanaume wanapenda wanawake walioolewa maana hawana gharama......... Ameharibu ndoa yake kwa tamaa ya muda mfupi.....
Jana nilikuwa napata mbili tatu za baridi na jamaa yangu, katika maongezi akaniambia hana furaha ya ndoa yake. Mke wake ni anapenda pombe, analewa na watu mbalimbali anawaita 'friends', hana muda hata wa kutandika kitanda wanacholalia. Chumba chao dada wa kazi ndo anafagia, anafua, kupika na hata kutunza mtoto kwani mama hurudi mtoto akiwa amelala.
Pia kila sherehe anataka kwenda, amediriki kwenda hata kwenye Kili Awards bila ya kumshirikisha mumewe. Alipomuuliza anasema alikuwa na kaka yake, tatizo yote hayo hata ukoo wao wanapenda pombe sana.:angry:
Tatizo ni kwamba jamaa amechoka, mwanamke hashauriki, kaomba msaada hata kwao waongee na binti ila haijasaidia. Wana mtoto mmoja, jamaa ndio anahangaika kuwahi nyumbani japo akae na mtoto. Amefikia maamuzi ya kutaka kuachana na mkewe, jamaa ni msomi mzuri na ana kipato cha kujitosheleza, mke pia pamoja hana elimu ila ameweza kuendesha biashara ambayo mumewe alimuanzishia na inaendelea vizuri.
Tatizo mke ni mtu wa starehe za kulimbukia kwani wakati wanakutana hakuwa hivyo tena walikuwa na muda wa kukaa pamoja na kushauriana.
Nimeshindwa cha kumueleza japo nami nikaona labda mnaweza kutoa mchango wowote.