mashakani
JF-Expert Member
- Aug 15, 2018
- 615
- 990
https://twitter.com/share?text=Mke ...8-4780592-54pfmb/index.html&via=MwananchiNews
Mke wa Rais wa Marekani, Melania Trump
Kwa ufupi
Washington, Marekani. Mke wa Rais wa Marekani, Melania Trump hatimaye ameweka wazi ratiba ya ziara yake barani Afrika ambapo atatembelea nchi za Ghana, Malawi, Kenya na Misri kuanzia wiki ijayo ikiwa ni ziara yake ya kwanza ya kimataifa akiwa peke yake.
Ziara ya Melania barani Afrika inalenga kuhamasisha ulinzi wa haki za watoto pamoja na mazingira bora ya utoaji elimu kwenye mataifa atakayotembelea.
Melania alisema hayo wakati alipokutana na wake wa marais mbalimbali wanaohudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa, na kueleza sababu za kuzitembelea nchi hizo.
Katika taarifa yake Melania amesema ziara yake imetokana na kazi zinazofanywa na Shirika la Misaada la Marekani USAID kwa nchi za Afrika, ambapo amesema maeneo ambayo shirika hilo limekuwa likifanyia kazi yamekuwa ni sehemu ya maisha yake.
Melania alisema anatarajia ziara yake kwenye mataifa hayo kuwa yenye tija hasa wakati huu ambapo mtoto wa kiafrika ameendelea kukabiliwa na changamoto za kielimu, matumizi ya dawa za kulevya, unyanyasaji, usalama katika matumizi ya mtandao, umasikini na magonjwa, akisema katika karne hii watoto hawapaswi kuwa katika mazingira haya.
Mke wa Rais wa Marekani, Melania Trump
Kwa ufupi
- Amesema ziara yake imetokana na kazi ambazo zinafanywa na Shirika la Misaada la Marekani USAID kwa nchi za Afrika na kwamba maeneo ambayo shirika hilo limekuwa likifanyia kazi yamekuwa ni sehemu ya maisha yake.
Washington, Marekani. Mke wa Rais wa Marekani, Melania Trump hatimaye ameweka wazi ratiba ya ziara yake barani Afrika ambapo atatembelea nchi za Ghana, Malawi, Kenya na Misri kuanzia wiki ijayo ikiwa ni ziara yake ya kwanza ya kimataifa akiwa peke yake.
Ziara ya Melania barani Afrika inalenga kuhamasisha ulinzi wa haki za watoto pamoja na mazingira bora ya utoaji elimu kwenye mataifa atakayotembelea.
Melania alisema hayo wakati alipokutana na wake wa marais mbalimbali wanaohudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa, na kueleza sababu za kuzitembelea nchi hizo.
Katika taarifa yake Melania amesema ziara yake imetokana na kazi zinazofanywa na Shirika la Misaada la Marekani USAID kwa nchi za Afrika, ambapo amesema maeneo ambayo shirika hilo limekuwa likifanyia kazi yamekuwa ni sehemu ya maisha yake.
Melania alisema anatarajia ziara yake kwenye mataifa hayo kuwa yenye tija hasa wakati huu ambapo mtoto wa kiafrika ameendelea kukabiliwa na changamoto za kielimu, matumizi ya dawa za kulevya, unyanyasaji, usalama katika matumizi ya mtandao, umasikini na magonjwa, akisema katika karne hii watoto hawapaswi kuwa katika mazingira haya.