Mke wa Walker anadai Bilioni 54 baada ya mume wake kuzaa nje ya ndoa

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Annie Kilner ambaye ni mke wa beki wa kulia wa Manchester City, Kyle Walker anadai fidia ya pauni milioni 15 sawa na Bilioni 54,428,016,000 kwa pesa za Tanzania kama fidia ya yeye kukubali kuendelea kubaki kwenye ndoa baada ya mume wake kuzaa watoto wawili nje ya ndoa

Kesi hii iliteka vichwa vya habari nchini Uingereza mwezi January mwaka huu, baadae Walker alitoka hadharani kukiri kosa hilo lakini hivi karibuni imeibua sura mpya baada ya Annie kuajiri mtu maalumu wa kufuatilia utajiri wa Walker akiendelea kusisitiza kudai fidia hiyo

Walker na Annie walifunga ndoa mwaka 2021 na wamebarikiwa kupata watoto wanne Roman (12) Riaan (7) Reign (5) na Rezon (Miezi sita)
 
Gold digger
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…