Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
We si unalazimishwa kubeba pochi na mkeo au?Na wewe unajiita mwanaume
Si ndo hapo sasa [emoji23] [emoji23] [emoji23]Mbona ww unalelewa namwanamke ??siulisema hum kwamba mkewe ndo anatoa hela yamatumizi .sasa sibora jamaa anapambana nahaliyake ?
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] nakubaliana na wewe kabisa.Wadau huyu ni Beira baby boy anatuzuga na id mpya, kama sio yeye ni Sexless, nishajua thread/nyuzi zao hazinaga mashiko.Hawa watu wa hovyo sana kila siku nyuzi za kutunga za hovyo na kufanya JF kupoteza mvuto. Unashindwa kuelewa nani yupo serious na anahitaji msaada na kumaanisha alichoandika.
Wanaume wa Dar mnatia huruma sanaMimi ni mwanaume niliejaaliwa kuwa na watoto wawili wakike na wa kiume na mke wangu nimemuoa miaka kumi iliyopita huko mkoani iringa, shughuli zangu ni fundi seremala katika hizi kampuni za ujenzi za kichina zilizotapakaa hapa jijini dar ambazo tunajenga nyumba mbalimbali za miradi ya jamii.
Sasa mara nyingi pesa huwa tunalipwa kwa kila wiki, sasa hapa kati huwa napigika sana yaani nakuwa sina pesa hivyo ni lazima nijiongeze kwa kufanya kazi za ziada pindi ninapotoka kazini ile saa kumi, sasa najikuta nakuwa huko mitaani mpaka saa mbili au saa tatu usiku ndipo namaliza kazi zangu za ziada na kupata pesa then naelekea home.
Lakini ninapofika nyumbani nakumgongea mke wangu anifungulie mlango nikiingia ndani tu maneno yanaanza, nikimjibu kuwa nilipitia sehemu kufanya kazi maana nimerudi kazini nikiwa sina pesa naambulia vibao usoni napigwa mpaka nalia ndugu zangu huku nikiambiwa na mke wangu...usinijibu mimi nakwambia...roho inaniuma sana ndugu zangu naomba mnishauri nifanye nini ili kuepukana na vipigo hivi mimi jamani?.