Mke wangu ananipiga makofi kila ninapochelewa kurudi nyumbani, nifanyaje jamani nimechoka!

wanaume wanazidi kupungua kadri siku zinavyozidi kusonga
 
Ooo pole mwaya sijapenda tabia yake .hana hata huruma na wewe! Maamuzi ni yako ya watu yatakupoteza!!!!
 
Lkn kaaa nae chini mtafakari vzr kwan mtafikia mwafaka mzuri na life litasonga
 
Kama hachepuki kaanae. Na akikupiga usipige yoe ni aibu
 
Tafute bakora ili asitumie makofi,awe anakuchapa kama mwanafunzi.hiyo NI nzuri.
 
vaa helmet
 
Inabidi tukupige makofi hata sisi kwa uzembe.kwanini unamruhusu akutawale hivyo.umeniharibia siku kabisa!! ngoja nipige konyagi kwa hasira.....





 
Wanaume wengi hampendi kuongea na wake zenu hata km unafanya kitu gani cha maana unapaswa kumshirikisha mwenzie ili ajue baba leo anachelewa kurudi. Huo ni uzembe wako kabisaaa anza kumpa taarifa ya kila unachofanya uone km utagombana nae.
 
Weka namba yake tumshauri aache kukupiga
 
Ebu usirud nyumban kama cku tatu akikuulizaa mwambie unaogopa kupigwaa
 
Halafu huko kijiji wazazi wanasema wana kijana wao mjini, hata hivyo pole maana ndio maisha uliyojichagulia kuishi
 
Pole sana kwanza huyo mke wako kabila gan kwanza tujuwe alafu tukushauri mmmmh mpk unafikia kipigwa ama kweli dunia ya saiz kizungumkuti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…