Mke wangu anateswa na mimba ya Aina yake?? Kutapika, tumbo kuvuruga na kizungu zungu

Mke wangu anateswa na mimba ya Aina yake?? Kutapika, tumbo kuvuruga na kizungu zungu

huu ushauri umechukuliwa
Karibu Mkuu, i hope itamsaidia sana. Haimalizi tatizo ila inaleta nafuu.

Lakini uwe makini asikuendeshe.
Hiki ni kipindi ambacho wanawake wanafanya sana maigizo hadi Ndoa unaiona chungu.

Nakushtua tu mama mwanaume mwenzangu
 
Wakuu,
Nimeona mimba nyingi ila hii ni aina yake.

Huyu mwanamke ndo mimba yake ya kwanza lakini sasa

Anatapika kila anachokulaaa anatapika chakula kinaisha had anatapika maji hamna kinachotoka.

Muda wote. Tumbo linamuuma na kumvuruga muda woteee.

Hawezi kutembea hawezi kufanya kazi wala hawezi chochote. akitembea anahisi kizungu zungu ,moyo kwenda mbio na hana nguvu kabisa.

Alienda hospital wakasema hawajaona kitu labda ni hyo mimba.

Lakini wakuu ni mimba gani ya hivi hasa ukizingatia ina MWEZI TU MMOJA
Mimba ya kwanza mara nyingi inasumbua kutokana na mabadiliko makubwa ya homoni, kimwili, na kihisia ambayo mwili wa mwanamke unapitia kwa mara ya kwanza. Sababu kuu ni:
1. Mabadiliko ya Homoni
Homoni kama vile progesterone na estrogen huongezeka kwa kasi ili kusaidia ukuaji wa mtoto na kuimarisha mji wa mimba. Hii inaweza kusababisha:
  • Kichefuchefu na kutapika (morning sickness).
  • Uchovu mwingi.
  • Kubadilika kwa hisia (mood swings).
2. Mfumo wa Mwili Kujifunza Kujibadilisha
Kwa kuwa mwili haujawahi kupitia hali hii, mfumo wa mwili unachukua muda kuzoea mabadiliko haya, kama:
  • Ukuaji wa tumbo na kuongezeka uzito.
  • Kuongezeka kwa mzunguko wa damu.
  • Mabadiliko ya mfumo wa mmeng’enyo wa chakula (kufunga choo au kiungulia).
3. Hofu na Wasiwasi wa Kijamii na Kihisia
Mimba ya kwanza inaweza kuja na hofu ya kutokuwa na uzoefu wa kujua nini cha kutarajia, kusababisha msongo wa mawazo.

4. Mabadiliko ya Kimwili
Mwili unapoanza kupanuka, misuli ya nyonga, mgongo, na sehemu nyinginezo huanza kubadilika ili kujiandaa kwa ujauzito na uzazi, hali inayoweza kusababisha maumivu au usumbufu.

Jinsi ya Kupunguza Usumbufu

  • Lishe Bora:Kula vyakula vyenye virutubishi vingi na kuepuka vyakula vinavyosababisha kichefuchefu.
  • Maji Mengi: Kunywa maji ya kutosha ili kuzuia kizunguzungu na kuimarisha afya.
  • Pumzika vya Kutosha: Mwili unahitaji muda wa kupumzika.
  • Msaada wa Kimatibabu: Tafuta ushauri wa daktari kwa matatizo yoyote makubwa au yanayoongezeka.
  • Mazoezi Mepesi: Kama daktari ameruhusu, mazoezi ya mwili mepesi yanaweza kusaidia kupunguza maumivu na wasiwasi.
Kumbuka, hali ya kila mtu ni ya kipekee. Ni muhimu kuwa karibu na wataalamu wa afya kwa ushauri wa mara kwa mara.
 
Wakuu,
Nimeona mimba nyingi ila hii ni aina yake.

Huyu mwanamke ndo mimba yake ya kwanza lakini sasa

Anatapika kila anachokulaaa anatapika chakula kinaisha had anatapika maji hamna kinachotoka.

Muda wote. Tumbo linamuuma na kumvuruga muda woteee.

Hawezi kutembea hawezi kufanya kazi wala hawezi chochote. akitembea anahisi kizungu zungu ,moyo kwenda mbio na hana nguvu kabisa.

Alienda hospital wakasema hawajaona kitu labda ni hyo mimba.

Lakini wakuu ni mimba gani ya hivi hasa ukizingatia ina MWEZI TU MMOJA
Mkuu ushasema anatapika Kila anachokula sasa hizo nguvu za kutembea atazipata wapi?

Hiyo ni Hali ya kawaida kwa wajawazito wengi hasa mimba ya kwanza Kuna miez itafika hiyo Hali itaondoka kabisa kikubwa akifikia hiyo Hali mpeleke hospital wam stabilize.
 
Sisi waganga wa mwituni tunasema hivi
1. Asile chakula cha moto kwani kinatoa harufu na kuzidisha kichefu chefu
2. Asile chakula chenye sukari
3. Asile chakula cheny mafuta mengi( oily food) hasa hivi vyakula vya kukaanga chips, mshikaki ana the likes.
4. Ahakikishe hanywi maji au soda wakati wa kula.
5. Ajitahidi kula mlo mdogo mdogo kadiri awezavyo...asishibe.

6. Wakati wa kulz ahakikishe amekaa upright, mtindo wa kula au kutafuna kitu akiwa amelala kwenye kochi aache.

Hali ikizidi muone daktari.
Naunga mkono hoja
 
Mimba imekukataa. Naogopa kukupa ushauri fulani hivi, wauseme wengine
 
Wakuu,
Nimeona mimba nyingi ila hii ni aina yake.

Huyu mwanamke ndo mimba yake ya kwanza lakini sasa

Anatapika kila anachokulaaa anatapika chakula kinaisha had anatapika maji hamna kinachotoka.

Muda wote. Tumbo linamuuma na kumvuruga muda woteee.

Hawezi kutembea hawezi kufanya kazi wala hawezi chochote. akitembea anahisi kizungu zungu ,moyo kwenda mbio na hana nguvu kabisa.

Alienda hospital wakasema hawajaona kitu labda ni hyo mimba.

Lakini wakuu ni mimba gani ya hivi hasa ukizingatia ina MWEZI TU MMOJA

Pole sana.

Mwanamke akiwa na mimba kuna mabadiliko mengi ambayo hutokea mwilini mwake. Mojawapo ya mabadiliko hayo ni kuwa na kichefuchefu na kutapika.

Mwanamke kutapika (emesis) wakati wa ujauzito ni kawaida na huonekana sana mimba ikiwa changa, yaani kuanzia wiki 0 mpaka wiki ya 12 ndipo inapungua au kuisha kabisa.

Hata hivyo hali hii ya kutapika (emesis) inapokuwa kuwa kali sana kiasi kwamba mwanamke hutapika chochote anachoingiza kinywani huitwa Hyperemesis Gravidarum na huambatana na dalili kama kichwa kutuma, kizunguzungu, uchovu, moyo kwenda mbio nk.

Ukali au viwango vya Hyperemesis Gravidarum hutofautiana toka mwanamke mmoja hadi mwingine na mimba moja hadi nyingine.

Kama mwanamke ana Hyperemesis Gravidarum basi cha kwanza ni kumhakikishia kwamba hiyo hali itaisha na kwa wale ambao hutapika chochote anachokula ni lazima aende hospitali alazwe ili atibiwe mpaka kutapika itakapopungua au kuisha. Hyperemesis Gravidarum hupungua na kuisha yenyewe kadri mimba inavyokua.

Kwa hiyo mpeleke hospitalini akapatiwe matibabu mpaka atakapoweza kula au kutapika itakapopungua kabisa.

Kila la kheri.
 
Pole sana.

Mwanamke akiwa na mimba kuna mabadiliko mengi ambayo hutokea mwilini mwake. Mojawapo ya mabadiliko hayo ni kuwa na kichefuchefu na kutapika.

Mwanamke kutapika (emesis) wakati wa ujauzito ni kawaida na huonekana sana mimba ikiwa changa, yaani kuanzia wiki 0 mpaka wiki ya 12 ndipo inapungua au kuisha kabisa.

Hata hivyo hali hii ya kutapika (emesis) inapokuwa kuwa kali sana kiasi kwamba mwanamke hutapika chochote anachoingiza kinywani huitwa Hyperemesis Gravidarum na huambatana na dalili kama kichwa kutuma, kizunguzungu, uchovu, moyo kwenda mbio nk.

Ukali au viwango vya Hyperemesis Gravidarum hutofautiana toka mwanamke mmoja hadi mwingine na mimba moja hadi nyingine.

Kama mwanamke ana Hyperemesis Gravidarum basi cha kwanza ni kumhakikishia kwamba hiyo hali itaisha na kwa wale ambao hutapika chochote anachokula ni lazima aende hospitali alazwe ili atibiwe mpaka kutapika itakapopungua au kuisha. Hyperemesis Gravidarum hupungua na kuisha yenyewe kadri mimba inavyokua.

Kwa hiyo mpeleke hospitalini akapatiwe matibabu mpaka atakapoweza kula au kutapika itakapopungua kabisa.

Kila la kheri.
Alipelekwa akapewa tu Oral oss yale ya kuchanganya kwene maji kwa mtu ambae anaharisha
 
Alipelekwa akapewa tu Oral oss yale ya kuchanganya kwene maji kwa mtu ambae anaharisha

Ok, sawa
Kama anaweza kunywa maji na hatapiki basi aendelee tu, lakini kama anatapika kila kitu anachokula basi huyo lazima alazwe ili atibiwe mwili uwe na nguvu na kutapika ikipungua na kuweza kula na kunywa basi ataruhusiwa.
 
Ok, sawa
Kama anaweza kunywa maji na hatapiki basi aendelee tu, lakini kama anatapika kila kitu anachokula basi huyo lazima alazwe ili atibiwe mwili uwe na nguvu na kutapika ikipungua na kuweza kula na kunywa basi ataruhusiwa.
Siyo akinywa hatapiki walimpa ili kusaidia kupoteza maji anayopoteza
 
Kwa umri huu tayari amepevuka, Kuna uwezekano akawa ananyongo nyingine tuseme acid reflux anaweza kwenda kupima hospital kwa udhibitisho hivyo asile vyakula vyenye sukari nyingi na asidi nyingi mf. Maharagwe nk pia mtafutie fennel saga mchanganyie kwenye chakula chake kijiko kimoja Kila wakati akipata chakula. Mbadala wa sukari ni asali na tende pia tende huweza kutengezwa nakuwa sukari "date sugar". Usimpe dawa yeyote bila kuwasiliana na dk cos huyo ni mjamzito asije abort. Fennel ni kiungo hakuna shida ok. Waweza ipata kwenye masoko makuu au super market. Be strong.
 
Wakuu,
Nimeona mimba nyingi ila hii ni aina yake.

Huyu mwanamke ndo mimba yake ya kwanza lakini sasa

Anatapika kila anachokulaaa anatapika chakula kinaisha had anatapika maji hamna kinachotoka.

Muda wote. Tumbo linamuuma na kumvuruga muda woteee.

Hawezi kutembea hawezi kufanya kazi wala hawezi chochote. akitembea anahisi kizungu zungu ,moyo kwenda mbio na hana nguvu kabisa.

Alienda hospital wakasema hawajaona kitu labda ni hyo mimba.

Lakini wakuu ni mimba gani ya hivi hasa ukizingatia ina MWEZI TU MMOJA
Hiyo itakaa sawa maana hata mke wangu alivyopata mimba ya kwanza kila alichokuwa anakula ni kutapika ikafikia tukawa tunalala na ndoo pembeni, ikaenda mbali zaidi akawa anatapika mpaka damu.

Alikonda mpaka akakosa nguo ya kuvaa hii hali ilinichanganya sana .

Ila baada ya miezi minne alianza kukaa sawa.

Hospitali nilimpeleka nikaambiwa atakaa sawa.
 
Aamke usiku kunywa maji ??
au na kula pia
Kuna muda ndani ya masaa 24, huna unasikia nafuu kubwa, ndiyo ale kidogo, anywe maji. Kuna mtu alikuwa anaumwa hawezi kula chochote wala kunywa. Ila ikifika saa 8 usiku akistuka anakuwa na nafuu kubwa. Hapo anakunywa maji lita moja anatapika. Atasubiri kidogo anakunywa teena lita na nusu yanabaki.
Anakula na vitu vidogo vidogo analala. Kesho anaumwa teena asubuhi hivyo hovyo.
Ilip9maliza miezi mitatu, na kuanza mwezi wa nne ile tarehe za mwanzoni akawa na nafuu kubwa
 
Kuna muda ndani ya masaa 24, huna unasikia nafuu kubwa, ndiyo ale kidogo, anywe maji. Kuna mtu alikuwa anaumwa hawezi kula chochote wala kunywa. Ila ikifika saa 8 usiku akistuka anakuwa na nafuu kubwa. Hapo anakunywa maji lita moja anatapika. Atasubiri kidogo anakunywa teena lita na nusu yanabaki.
Anakula na vitu vidogo vidogo analala. Kesho anaumwa teena asubuhi hivyo hovyo.
Ilip9maliza miezi mitatu, na kuanza mwezi wa nne ile tarehe za mwanzoni akawa na nafuu kubwa
Mkuu nimekusoma asante kwa ushuhuda
 
Back
Top Bottom