Mkenya aliyeshikiliwa Tanzania na kuachiwa, akamatwa tena, pia aliyekwenda kumpokea naye akamatwa

Mkenya aliyeshikiliwa Tanzania na kuachiwa, akamatwa tena, pia aliyekwenda kumpokea naye akamatwa

Riwaya yote hii unaandika ya nini haswa, hujasoma na kuelewa, mimi sina issue na kazi ya wana usalama, hata kwetu wapo watu wanaoshikiliwa, lakini nyie mnamkamata mtu bila kueleza nini sababu.

Vipi ukija sikia ,NGO yake inafadhiliwa na pesa chafu,na Intel imeletwa tz na vyombo vya Kenya,hizi NGO zingine zina vitu viovu sana .


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hehehe! Huwa mna matatizo sana kiuelewa na ndio maana elimu yenu huwa chini, nimesema na narudia mara kumi labda ubongo wenu utafaulu kuelewa baada ya mara hizo kumi, kwamba ni shwari na mpo sahihi na ni haki yenu kumkamata mtu yeyote asiyeendana na sheria za nchi, hata huku tunao watu waliokamatwa akiwemo hata Matanzania aliyekamatwa akiua wanafunzi Garissa, kwa hivyo kumkamata Mkenya hiyo sio issue yangu, wakamateni wote mnaotaka kuwakamata, lakini mnafaa kutoa taarifa kisa na maana kwanini mumemkamata, inaitwa natural justice.
Mkenya yeyote atakayevuka mpaka na kuja huko kuhusika kwenye uhalifu wowote au ugaidi, ashughulkiwe tu tena bila huruma, lakini hili la kukamata mtu na hamsemi kisa nini, mnamuachia huru halafu mnamkamata tena, ni wazi tunakokwenda hakufai, ifahamike raia wa nchi zetu hizi wameingiana kibiashara na kijamii, hatufai kufanyiana mambo yasiyo.
sogea pale central kaulize "mmemkamata kijana wetu kwa kosa gani??"..utapewa jibu..short and clear!
 
Back
Top Bottom