Mkenya pekee anayejua mziki

lakini kila nchi huwa na wakati wa kungaa. Ile miaka ya kitambo, mziki wa kenya ulikua unafanya vizuri zaidi ukanda wa Afrika mashariki ila sasa ndugu zetu wa bongo ndio kusema, kwanza huyo platinumz anamake moves kali sana. Enjoy the glory while it lasts, neighbours. soon it will be another country
 
khaligraph was nominated for an Afrimma best African rapper alongside the likes of nasty c. Lets hope he clinches it, even though Kenyans rarely support their own in terms of voting for them.
 
Sasa hadi uende Mombasa ? Tanzania popote pale ukienda kiswahili kinazungumzwa.

Cha kufanya sema kuna kiswahili cha Kenya na cha Tanzania. Ila hata mtu wa kakamega huwezi mfananisha na wa Mombasa. Mtaanza kukataana wenyewe kwa wenyewe.
Wacha kujitoa ufahamu wewe...hivi wewe unanionaje?mwehu sio...kiswahili bongo kiko pwani...sana sana tanga...mwanzo mtu wa dar akiongea kiswali hunitia kichefu chefu..mara aisee,sijui naendaga,nakulaga...herufi zenywe zawashinda...

Alafu usitake kunishawishi wachaga,wakuria na kuna wengine wengi tu eti nao wanajuwa kiswahili..kiswahili chao km commedy vile...

Tanga naeza sema kuna wadigo wa kutoka kenya..
 
Mbona Canada haijawahi chukua nafasi ya U.S.A kwenye muziki! Kuna vitu vingine vipo kwa sababu nyingi. Muhimu zaidi ni talent. Kenya haijawahi kuwa na talent zaidi ya Tz kwenye entertainment ila mliwahi kuwa na miundombinu kabla ya Tz. Zamani wana mziki walikua wanakuja Nai kurecord na wengine kuingia kwenye band za Kenya na kuipaisha Kenya. Hii ilisababisha Kenya kuonekana iko juu ki mziki. Wasanii, maproducer, wachoraji waliofanya vizuri Kenya wengi wana damu ya Tz, the likes of E-Sir. Kuna mzee mmoja ana kipindi kama sijakosea ni KBC au KTN anajiita kungwi wa muziki kitu kama hiko anavaaga kofia, anajua sana historia ya mziki ya E.A msikilizeni mtapata vitu vingi.
 
Sikutukani hata.

Nakuambia hivi Kenya mnazungumza Kiswahili ila cha Kenya.

Zunguka kuanzia Vyombo vyenu vya habari hadi mitaani. Huwa naangalia vyombo vya habari vya Kenya nashindwa kuelewa kama kuna wahariri.

Sijui unabisha nini sasa maana hili lipo wazi. Nimeishi Kenya Narok,Nairobi,n.k najua nachokiandika.

Kenya mnazungumza kiswahili cha Kenya. Unadhani kwanini kenya kuna Sheng? Tanzania haipo?

Ni sawa na Nigeria wanazungumza English ya Nigeria ila Kiingereza kipo England. Angalia hata maandishi yenu na yetu jukwaani.
 
Iwe inakutia kichefu chefu au kizungu zungu, ukweli unabaki vile vile. Kiswahili ni lugha yetu ya taifa, asilimia 98% ya watanzania wanaongea kiswahili.

[emoji41][emoji41][emoji41]
 
Wacha kuruka ruka wewe...chimbuko la kiswahili ni mombasa...hao wengine kw king'eng'e mombasa twawaita others...sasa nynyi vile mliona lugha yenyewe ina asili ya kiafrika..mkakomaa nacho hadi sasa mnaanza kujigamba..eti kiswahili kimetoka bongo...

We wakijuwa kingozi kweli,au wakiskia juu juu tu...mombasa watu wamekaba tu..
 
Iwe inakutia kichefu chefu au kizungu zungu, ukweli unabaki vile vile. Kiswahili ni lugha yetu ya taifa, asilimia 98% ya watanzania wanaongea kiswahili.

[emoji41][emoji41][emoji41]
Wacha kujifurahisha kijana...bongo mume copy paste tu...wangapi wakifika mombasa hukaa kimya...labda mkatambe nairobi..mombasa huez leta ujuaji na kingozi chetu...
 
Wacha kujifurahisha kijana...bongo mume copy paste tu...wangapi wakifika mombasa hukaa kimya...labda mkatambe nairobi..mombasa huez leta ujuaji na kingozi chetu...
Wewe unaongelea Mombasa, mimi naongelea Tanzania nzima bara na visiwani. Ni nani anaejifurahisha?
 
Wewe unaongelea Mombasa, mimi naongelea Tanzania nzima bara na visiwani. Ni nani anaejifurahisha?
Ukwel ni kwamba..kiswahili si cha watanzania..nsawa na kusema vile cote' divore kifaransa kwao ni lugha ya taifa..basi haimaanishi km ile lugha ni yao..kuna chimbuko..ni maoni tu ya mtu na nchi husika kw ujumla..kenya wabara wamekomaa sana na kingereza..sasa kiswahili kwao ni km lugha ya tatu hv
 

Hakukuwa na lugha inayoitwa kiswahili. Hili unapaswa uelewe. Chimbuko-haya ni yale makelele ya wakenya ya kujifanya mnajua Mwisho mmetuharibia maandishi yabkiswahili kama mlivyo tuharibia kamusi na google.

Ingekuwa kiswahili Chimbuko lake Kenya Lahaja ya usanifisho ingetoka kenya na leo wakenya wangekuwa wanazungumza kiswahili kisicho na matatizo.

Bado unaongelea sehemu moja kenya. Ukitoka nje ya Pwani ya Kenya hakuna sehemu kiswahili kinazungumzwa. Mnazungumza Sheng tu. Sijui hili kwanini hata haulioni labda nianze kukutajia Wakenya tunaowajua. Kenyata, Ruto,Kalonzo,Tingatinga nao wanajua kiswahili?
 
Wacha kujifurahisha kijana...bongo mume copy paste tu...wangapi wakifika mombasa hukaa kimya...labda mkatambe nairobi..mombasa huez leta ujuaji na kingozi chetu...
Mzee baba naona unadhihirisha Ukenya wako.
 
Wewe unaongelea Mombasa, mimi naongelea Tanzania nzima bara na visiwani. Ni nani anaejifurahisha?
Wakenya hawa ni wajomba zangu ni wabishi kama Waha...yupo radhi kufa ndiyo akubali.

Hawa Jamaa kwanza wametuharibia kuanzia salamu hadi kamusi za kiswahili.

Hatukatai kama Kenya wanazungumza kiswahili, Wanazungumza ila kiswahili cha Kenya. -KANA- Jaribu kuangalia KTN, K24, citizen taarifa zao za habari utataka utapike. Makosa ya kimatamshi yamejaa, ya kiuandishi ndiyo usiseme.

Hawa jamaa kwao Kijana kupenda Bongo music ni ujanja kama Tz zamani kuvaa mlegezo kijana ni ujanja. Na wanapenda kwasababu ya nyimbo zetu zimenyoosha lugha maudhui yanaeleweka kiurahisi na zinaeleweka.

Sasa subiri wasanii wao walio wengi waimbe utajiuliza anaimba kisomali au kireno. Tatizo ni lugha. (Ila hatuwalaumu wanaimba kiswahili cha Kenya) sasa huyu hataki kukubali kama ni kiswahili cha Kenya.
 
Kwhvo wewe unabisha kiswahili chimbuko lake si mombasa
 
Kamusi gani hyo mlioharibiwa...sheng ni lugha km vile pidgin ya naija...kamwe sheng haiwezi kuwa kiswahili...ni sawa na kusema kiswahili ni kiarabu kw sababu kuna maneno ya kiarabu ndani...

Jibu swali langu mwanzo...unatak kusema kiswahili chimbuko lake si mombasa?

Ukishajibu...unieleze kingozi ni nn?na kilianzia wapi
 
Eti wanaimba kiswahili cha kenya..mwanzo nynyi watu washamba...eti otile brown kiswahili chake ni cha bongo...kijana kalelewa mombasa yule hahaaaa!!katika nyimbo zake huez kumkuta na matatizo ya 'l' 'r'...

Jamaa anaimba kiswahili fasaha yule...hay njoo kw wabongo sasa wanapoimba...matatizo ya herufi tele...

Kamwe hamuez jisifia nakiswahili nyinyi...hamjui kitu....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…