Mkopo ni utumwa ambao sitokuja kurudia

NMDA antagonist

Senior Member
Joined
Mar 25, 2018
Posts
143
Reaction score
106
Habar za humu wakuu. Naombeni ushauri ni ipi njia mbadala ingine itakayoweza kunitoa kimaisha. Nahitaji kutokana na fikra ya mkopo.
 
Jikope mwenyew uweke akiba utaachan na dhana ya mkopo
Ni sahihi
Unajibana January had December

Inatakiwa nidham kali sana

Mimi nimeanza kufanya hili zoezi, kila wiki najikopesha laki unusu.

Nataraji hapo December wiki ya 52, nivune akiba yangu,

Nitawekeza ili nianze kula matunda ya Uhuru.
 
Tatizo ni zile riba zinazowekwa aisee kwa kweli huwa zinapasua kichwa..!! Pili by the time biashara zinapofeli hawa jamaa huwa hawaelewi udhuru wapo money centered zaid kuliko your problem centered...
 
Kama kwa sasa una chanzo cha fedha kiasi fulani, jifunze kujikopesha. Kuweka akina nayo ni biashara. Sasa kama unaweza kuhifadhi kwa mfano laki tatu kila mwezi, hiyo yawezekana hicho ni kipato cha mwenye duka fulani hivi mahali fulani. Anza na kujikopa, ukiweza, tayari utakuwa na mtaji wa kufanya mambo mengine.
 
Kama una matatizo mengi usikope, ila mkopo husaidia kuendeleza ulichokianzisha
 
Ili uweze kuendelea lazima ukope, bila mikopo huwezi kupiga hatua mkuu, Ukiwa makini Mikopo inasaidia sana, lkn km haupo makini basi utaichukia mikopo.

mimi mama yangu amefanya kazi miaka kibao nssf.. na amepinga mikopo maisha yake yote ya riba kwamba dini hairuhusu.. na hajawai kukopa toka najitambua.. ila ana appartment zaidi ya 20 tanzania.. na kimaisha ameacha mbali wengi sana.. ila sifa yake kuu ni mbahili vibaya mnooo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…