Mkude asema Hakuna zaidi ya Simba, akanusha kuibwaga timu ya Taifa

Mkude asema Hakuna zaidi ya Simba, akanusha kuibwaga timu ya Taifa

kurlzawa

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2018
Posts
16,695
Reaction score
20,633
Hii ni habari official kutoka kwa menager wa mchezaji ameandika katika ukurasa wake wa Instagram kuwa mteja wake ameamua kustaafu kuichezea team ya Taifa ya Tanzania. Kwa sababu ambazo amesema atazitanabaisha hapo baadae kama supporting evidence ya uhuni unaofanyika katika team ya Taifa.

========

WAKATI kiungo wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Jonas Mkude, akisisitiza hakuwahi kusema hana mpango wa kuitumikia Timu ya Taifa (Taifa Stars), ameweka wazi mapenzi yake makubwa aliyonayo kwa Wekundu wa Msimbazi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkude alisema uamuzi wake wa kuitumikia Simba kwa muda mrefu unatokana zaidi na mapenzi ya dhati aliyokuwa nayo kwa vinara hao wa Ligi Kuu Bara ambao wana pointi 71 baada ya kucheza mechi 28.

Mkude alisema anaumizwa na taarifa ambazo si za kweli zinazungumzwa dhidi yake na mbali na yeye binafsi, hali hiyo humuumiza pia mama yake mzazi.

"Kila mchezaji anatamani kuchezea Timu ya Taifa, kwa hiyo mimi nitakuwa mtu wa ajabu kuikataa Timu ya Taifa, sijawahi kusema kokote kwamba siitaki Timu ya Taifa," alisema Mkude.

Kiungo huyo alikanusha taarifa za 'kujivunja' na kujitoa katika kikosi cha Taifa Stars kilichokuwa chini ya Mnigeria Emmanuel Amunike na alikubaliana na uamuzi wa kuachwa na kocha huyo ambaye mwaka jana alifanikiwa kuipeleka Tanzania kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2019).

Alisema pia bado anahitaji kutoa mchango wake kwa taifa endapo ataitwa lakini akikataa kuzungumzia taarifa za klabu nyingine iwe ya ndani au nje ya Tanzania kwa sababu bado ana mkataba na Simba.

Aliongeza amekuwa akiheshimu ratiba ya mazoezi na amekiri kufanya starehe mbalimbali pale muda wa kufanya hivyo unapomruhusu na hilo hufanywa na watu wengi na si yeye pekee.

"Hakuna mkamilifu, kila binadamu ana upungufu wake, kwa hiyo hata mimi nina upungufu wangu ninakubali,... napenda kucheza zaidi kama kiungo mkabaji, lakini nawakumbusha huwezi kucheza Simba miaka 10 kama huna lolote au huna nidhamu kabisa na bado ukavumiliwa," Mkude alisema.


JONAS-MKUDE.jpg

Jonas Mkude


Chanzo: Nipashe
 
Astaafu tu, kiwango chake cha kawaida mno, anapiga pasi za pembeni ndiyo maana Amunike hakumtaka sijui huyu wa sasa anavutiwa na nn

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwakweli mimi ni simba ila huyu mkude si wa kucheza taifa
Hata pale simba hana kiwango cha kucheza, huenda ni bahati ilimbeba


Ukiongeza na nidhamu ndogo, ndio hafai kabisa.
 
Hakuna namna apumzike tuu tayari miguu imeshaanza kumsaliti...ni wakati wake wa kutulia na mikia fc amalizie nguvu huko...

Nafasi yake ya kiungo aliitumia vizuri kwa sasa si wakati wake tena..hapaswi kuwa na majukumu mengi ..

Japo nidhamu yake nje na ndani ya kiwanja ilikuwa Sawa Sawa na empty set

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwakweli mimi ni simba ila huyu mkude si wa kucheza taifa
Hata pale simba hana kiwango cha kucheza, huenda ni bahati ilimbeba


Ukiongeza na nidhamu ndogo, ndio hafai kabisa.
Bahati kwenye mpira? Ina maana makocha wote waliopita wanampanga kwa vile ni bahati

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkude kaisha ...alivyomchezea rafu Morrison ..Manula alimuwakia alijua washafungwa
 
ASTAAFU.KUCHEZEA.SIMBA
SIO KWA KIWANGO KILE

YAAN 8MARCH ALIONEKANA KABISA AYAWEZI NA YULE FALA NJE AKAWA AMTOI ..
 
Mkude kuendelea kupata namba na kucheza pale Simba ni jambo la bahati sana, pale timu ya Taifa mkude hana nafasi, mkude mzito kufanya maamuzi, mzito kwenye mpira ya juu, mzito kwenye anticipation/kumuotea mpinzani anafikira kufanya nini kwa wakati huo, mzito kwenye transition yaani mbaka awe free ndio ata achia mpira haraka, akikabwa vizuri ni ngumu kutoka nilazima aurudishe mpira ulipotoka ili ajikwamue.
Anahitaji viungo watatu/wa nne ili acheze vizuri. Ubora wa mkude utauona kama Timu anayocheza nayo iwe aikabi kuanzia mbele kwaiyo anakua free kutoka.
Mkude pia mzuri kwenye toto football. Kikubwa alichonacho nguvu za miguu eneo ilo yuko vizuri. Kwasasa Simba ikishambulia nayeye anasogea sana karibu na goli la mpinzani ii inamfya apate nafasi ya kufunga. Ana hitaji kubadilika sana.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom