Mkude gangwe!

Jaguar

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2011
Posts
3,437
Reaction score
1,027
Waluguru kwa sifa za kijinga siwawezi!Hebu cheki sentensi hizi. (i)Mkude gangwe kweli,kafukuzwa na simba toka porini kaja kamatiwa mlangoni! (ii)Mkude gangwe sana,kaenda mjini,kaibiwa viatu,karudi na ndala. (iii)Mkude alipokwenda kwa mjombake dar,aliiona fan(feni) na taa ya bulb kwa mara ya kwanza.Aliporudi kijijini matombo akasimulia kama ifuatavyo,"mjomba Mloka kaendelea sana,ana kipepea upepo,kinageuka kwa mjomba,kinageukia kwangu halafu kinamalizia kwa shangazi halafu vibuyu(bulb) vya mjomba ukigusa ukuta tu vinawaka.
 
alipomtembelea tena mjomba wake kwa mara ya pili siku moja wakati anavuka barabara pale Manzese aligongwa na gari akafa.Gari ile ilikuwa ni ya balozi anaewakilisha nchi yake hapa bongo.Basi mambo yalienda hivi kule kwao Mvuha,''mwe Mkude kafa kifo kizuri,kagongwa na gari ya balozi"
 
Hii kali,alipoenda mara ya tatu je?
 
Mkude naye!eti,"bora nimpe kura yangu mwarabu akalie mbali kuliko kumpa kura mloka ale matunda ya ubunge namwona hapa hapa matombo!".
 
Mkude Gangwe bwana aligoma kuhama kutoka nyumba ya kupanga mpaka alipopigwa vibao na mwenye nyumba mkude wacha bwana wacha
 
Mkude amsifia mkewe mama koba,"mama koba gangwe,nampa sh.500 ya matumizi,nikirudi nyumbani,nakuta pilau kuku na madikodiko kibao!"
 
Mkude gangwe kweli, ameandika ayafanyayo Jamiiforums bila uoga wowote!...
 

tehtehetehe... kweli mkude gangwe...
 
Hivi kumbe hata hawa nao wana vituko hivyo? MMMHH angekuja kipindi cha mgao wa umeme asingeiona feni wala vibuyu, sijui angesemaje
 
Mkude Gangwe yeye hapandi basi lingine lolote, wala kuangalia tv/radio ingine yoyote ila ile ya mwarabu!
 
Mkude Gangwe kwelikweli, kamdindia Katibu Kata kulima shamba la kijiji......

Mkude Gangwe kweli, kapanda Mabasi mawili (IKARUS) kalipa shilingi......

Mkude Gangwe kweli, kapanda basi kutoka Morogoro badala ya kushukia Ubunge, kashukia Kariakoo, kamkomoa Dereva.
 
Mkude gangwe kweli, kakataliwa na demu kaenda kunshitaki kwa nkewe!
 
hahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa eti kakataza ukabila JF kwel mkude Gangwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…