Mkuranga: Walimu watakiwa kutowatoza Wanafunzi michango yoyote Shuleni

Mkuranga: Walimu watakiwa kutowatoza Wanafunzi michango yoyote Shuleni

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filbeto Sanga, amewataka walimu kutowatoza michango ya aina yoyote wanafunzi ambao wanaoanza shule.

Sanga aliyasema hayo jana katika kikao maalumu cha Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, kilichoitishwa kubadilisha matumizi ya fedha ili ziende kutumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule 10.

Ujenzi wa madarasa hayo utawawezesha wanafunzi 3,627 ambao mwaka huu walichaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza, lakini wakabakizwa kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa, kuanza masomo.
 
Sahihi kabisa, wasitozwa hata mia mbovu.


Piga 113 kama utatozwa
 
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filbeto Sanga, amewataka walimu kutowatoza michango ya aina yoyote wanafunzi ambao wanaoanza shule.

Sanga aliyasema hayo jana katika kikao maalumu cha Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, kilichoitishwa kubadilisha matumizi ya fedha ili ziende kutumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule 10.

Ujenzi wa madarasa hayo utawawezesha wanafunzi 3,627 ambao mwaka huu walichaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza, lakini wakabakizwa kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa, kuanza masomo.
Michango ipi? Hawana ajenda zaidi ya kutafuta vistatement vya kuwatisha walimu kwa vituhuma hewa ??
 
Back
Top Bottom