Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya Magu, usiwatetee na kuwalinda waalimu wasiokidhi vigezo vya Ualimu Mkuu; unawavunja moyo wanaostahili nafasi hizo

Kumlalamikia DED,hapa JF unasema ni mahali sahihi??
Nini usichoelewa? JF ni Social Media kama media zingine. Hujawahi kusoma Tweet za viongozi mbalimbali wakitoa misimamo juu ya mambo mbalimbali katika jamii?
Unataka niandike barua nipeleke posta nisubiri majibu?
Ujumbe utafika kwa DED Magu; na naamini ameshaupata, tena siyo yeye peke yake; na wengine wengi kwenye mnyororo wa mamlaka husika.
 
Sawa
 
Mimi huifananisha kazi ya ualimu na upadre!

Ikatokea umefukuzika, kuna sehemu unaweza kwenda kujibanza kwa ajira, au ndiyo inakuwa 'kantolee', sasa kwanini kukose majungu?

Kujipendekeza na majungu kazini ni mfumo wa staff wenye ajira zisizo na mbadala.

Kuondoa majungu kwenye taasisi hizo ni sawa na kuondoa madada poa wote kwenye jiji la Khunenge!

Jizatiti mwenyewe na maisha yako ukistahimili mazingira yaliyopo kimfumo katika ajira yako.
 
Picha ya Mwl Maganga tafadhali tuthaminishe pengine kuna vigezo vinambeba na swala la pili DED Magu DC ni me au Ke?Kifupi tu ni kwamba Mkoa wa Mwanza Elimu ipo nyuma sana Pita Kwimba na maeneo mengine ya maporini utakutana na Mauchafu kibao na hawa walimu wakuu wengi wao ni vichomi juzi juzi kuna mmoja almanusura atafune posho za wadau waliosaidia shughuli za uchaguzi (Hapa najua wana jf watachekelea[emoji23])ila ikashindikana na hiyo ilitokea Kwimba Nimalize kwa kushauri Mwalimu Maganga kama unanisikia uache mara moja kujifanya kayafa na ukasome vinginevyo tutakutoa kwa aibu kuliko sehemu yoyote uliyopata kuishi nyau jike we
 
unachoongea ni pumba tu hoja hapo hamna Et wana Magu
Mama Maganga punguza hasira basi pumba zipi? bora umekuja mwenyewe hebu kasome buana sio unaleta ushangingi wako hapa nenda kasomeeee
 
Wewe ni Mwalimu 100%


HABARI ZA NDANI YA KIKAO CHA SEMINA YA MITIHANI UMEZIPATAJE KAMA SIYO MWALIMU???
 
kwasisi wanafasihi wewe ni Mwalimu,

Ushahidi " DED ALIZUNGUMZA KWENYE KIKAO CHA SEMINA YA MITIHANI JE ULIPATAJE TAARIFA ZA NDANI YA KIKAO KAMA HUKUWEMO NDANI YA KIKAO NA MAONGEZI YA MULE BILA SHAKA HUENDA HUWA NI YA SIRI??"""
 
kwasisi wanafasihi wewe ni Mwalimu,

Ushahidi " DED ALIZUNGUMZA KWENYE KIKAO CHA SEMINA YA MITIHANI JE ULIPATAJE TAARIFA ZA NDANI YA KIKAO KAMA HUKUWEMO NDANI YA KIKAO NA MAONGEZI YA MULE BILA SHAKA HUENDA HUWA NI YA SIRI??"""
Mimi ni mfanyabiashara, mzawa na mkazi wa Magu. Nina marafiki na ndugu zangu wengi ambao ni waalimu, wake kwa waume; nina wanangu wanasona shule ya msingi Magu, hivyo nina mawasiliano chanya pia na waalimu wa wanangu hapo shuleni hata maofisa wa idara ya elimu wilayani na mkoani pia; hivyo kupata taarifa za kikao cha DED Magu na waalimu wa Magu DC wawe wa msingi au sekondari kwangu siyo issue kubwa; I am connected, well informed.
 
Mkuu picha ya Mwl. Mary Maganga ipo, lakini sidhani kama ni muhimu kuiweka hapa. DED wetu ni ME; very smart guy, msomi, married; I don't think he can indulge in such a dirty relationship to a married old woman who is nearly to retire within a year or two. DED wetu yuko vizuri kisiasa; sihitaji kusema zaidi kwenye uga huo.
Sijui kinachomtatiza Boss Lutengano Mwalwiba ni nini hasa kuhusu Mwl. Mary Maganga, labda ni sympathy tu kwa huyo mama; lakini kama ni sympathy kwa huyo mama, ajue kwamba analimbikiza bomu la lawama kwa wana-Magu dhidi ya yake na idara ya elimu wilayani kwa kumlinda mama huyu ambaye historia ya utumishi wake ina ukakasi kuanzia Nyanguge, Nyambitilwa na sasa Magu.
Ni hatari kumlinda mtu kama Mwl. Mary Maganga, maana hakumbuki makosa yake ya nyumba alikotoka, hivyo hawezi kujirekebisha isipokuwa ni kuongeza scandals tu. She is a scandalous head teacher.
 
Magu kuna tatizo. Kuna habari niliona mwalimu alibaka wanafunzi wa kike kwa miaka 7 bila kukamatwa.Nikashangaa sana.Mamlaka husika zichukue hatua stahili mapema au hatua stahili zichukuliwe juu ya mamlaka husika.
 
Kuna mtu anaitwa Hagwila kamasikosei aliandika sana juu ya halmashaur hii inaonesha ina shida ya kiuongozi

Wahusika wachukue hatua

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
Ni kweli mkuu "Peramiho yetu" niliwahi kuandika kwa DED Magu kuhusu udhaifu wa baadhi ya watendaji wa idara yake ya elimu msingi ambao wamekuwa ni wapiga majungu, hasa Johari na Prisca ambao wanamlisha sumu DEO mpya Glory Mtui wakimpandikizia chuki dhidi ya waalimu ambao wao hawawapendi.
Hili la "Nzelajape" ni kweli DED unapaswa kuwatendea hali waalimu wenye vigezo vinavyokidhi kuwa waalimu wakuu kwa kuwapangia nafasi hizo; maana kwa kutokufanya hivyo unawakatisha tamaa, hasa wanapoona nafasi hizo bado zimeshikwa na waalimu wenye certificate wakati waraka ulishatoka kuagiza kuwa waalimu wakuu wawe na Diploma au Digrii.
Kama alivyosema "Nzelajape" mtumishi anajiendeleza kielimu ili apande daraja na aboreshe maslahi na maisha yake kwa ujumla. Hata wewe uling'ang'ana na kusoma ili uboreshe maslahi na maisha yako.
Leo hii wewe ni DED, unafurahia matunda ya elimu yako; unastahili kwa sababu ulihangaika na kusoma. Unaweza kwenda Dar kwa ndege kila weekend kuona familia na kurudi kazini Magu bila tabu; umekuwa frequent flyer, ni matunda ya nafasi yako kwa elimu yako na bahati yako pia. Angetokea mtu yeyote hapo katikati akakubania kwenye hatua yoyote, leo usingekuwa hapo ulipo.
Maofisa, iweni wakarimu kwa watu mnaokutana nao njiani mnapopanda kwenda juu wao wakishuka; maana mnaweza kukutana nao wao wakipanda na ninyi mkishuka.
Najua mtasema dua la kuku halimpati mwewe; sawa, ila mkumbuke kuwa, no situation is permanent.
 
Mishikaki alikua anajua kuchoma mzee bakari tu Magu nzima, hao wengine wanajaribu mkuu.
Kwa taste yangu, mishikaki ya mzee Bakari haifikii kiwango cha ile ya Igasha; sijui muonjo wako. Kuna watu kila siku hawakosi kwa Yohana kula mishikaki, wanaipenda sana; lakini mimi niliishia kwenda kwa Yohana mara moja tu; sijawahi kwenda tena kula mishikaki hapo.....!! Dr. Remy Ongala aliimba "Kipenda roho hula nyama mbichi". Tusihukumiane kwa chakula, tumbo ni kwa chakula na chakula ni kwa tumbo; lakini ipo siku vyote vitatoweshwa.
 
Vipi Mwl Mary Maganga ameshastaafu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…