Mkurugenzi: Majengo ya Kituo cha Afya yaliyotelekezwa Mkuranga sio yetu, iulizwe taasisi iliyohusika

Mkurugenzi: Majengo ya Kituo cha Afya yaliyotelekezwa Mkuranga sio yetu, iulizwe taasisi iliyohusika

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kudai majengo ya Hospitali yaliyopo Kijiji cha Hoyoyo, Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani yametelekezwa licha ya kukamilika kwa ujenzi na kuwa Wananchi wanalazimika kwenda umbali wa Kilometa 7 kupata huduma ya afya, ufafanuzi umetolewa.

Kusoma hoja ya Mdau bofya hapa ~ Majengo ya Hospitali (Mkuranga) yametelekezwa huu Mwaka wa 10 sasa, Wananchi tunaseka kupata huduma mbali

UFAFANUZI WA MKUU WA WILAYA
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Khadija Nassir Ally anasema: Sikuwa najua kuna hiyo hospitali kama alivyosema, naamini kama ipo basi haijajengwa na Serikali kwa kuwa hiyo ripoti haipo mezani kwangu.

Jambo la msingi nitafuatilia kujua kama ipo na nini kinaendelea, ikiwa ni Mdau au Wadau wameamua kujenga na kuishia njiani kisha Wananchi wakahitaji msaada wa Serikali ni jambo jema na linaweza kusaidia Serikali na Wananchi kwa jumla kama itahitajika Serikali kuendeleza mradi huo ulipoishia.

Nitafika katika Kijiji hicho kufuatilia hilo suala, kwa kuwa kwa sasa kuna mradi unaoendelea Kijiji cha Hoyoyo kujenga Zahanani na ujenzi unaendelea vizuri.

UFAFANUZI WA MKURUGENZI (DED)
Mkurugenzi wa Mkuranga, Waziri Kombo amesema “Mradi huo sio wa Serikali, ulijengwa na Taasisi ya WAMA (Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Tanzania), hivyo wao ndio wana majibu ya kwa nini mradi haujafunguliwa hadi leo kwa zaidi ya miaka 10.

Ungekuwa ni wa Serikali tungekuwa tumeshatoa fedha kuendeleza kituo hicho ambacho kwanza ni Zahanati na sio Hospitali kama inavyoelezwa, pia tungepeleka Watumishi, isingewezekana tukitelekeze kituo bila maelezo yoyote.

Suala lingine lolote zaidi ya maelezo hayo niliyoyasema waulizwe WAMA ndio wana majibu sahihi.

WAMA
JamiiForums imefanya jitihada za kutafuta uongozi wa WAMA lakini hilo halijafanikiwa, jitihada bado zinaendelea.
 
Hivi WAMA bado ipo

Ova
NAdhani haifanyi kazi toka Magufuli awe rais ofisi zao pale kawe karibu na kwa kikwete zimetelekezwa na magari yanachakaa tu juani pale sijui shida ni nn hasa
 
NAdhani haifanyi kazi toka Magufuli awe rais ofisi zao pale kawe karibu na kwa kikwete zimetelekezwa na magari yanachakaa tu juani pale sijui shida ni nn hasa
Aise...hii miradi sijui ngo za uwizi tu

Ova
 
Kijiji cha Hoyoyo Salma Kikwete ana shamba kubwa tu na nyumba ya Baba yake mzazi Marehemu kwa sasa alikuwa anaishi uko.
Shida ya watu wa kile Kijiji ni Wachawi sana na viongozi wao huwa hawaelewani nadhani ni moja ya sababu ya iyo Zahanati kutofanya kazi!
 
Baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kudai majengo ya Hospitali yaliyopo Kijiji cha Hoyoyo, Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani yametelekezwa licha ya kukamilika kwa ujenzi na kuwa Wananchi wanalazimika kwenda umbali wa Kilometa 7 kupata huduma ya afya, ufafanuzi umetolewa.

Kusoma hoja ya Mdau bofya hapa ~ Majengo ya Hospitali (Mkuranga) yametelekezwa huu Mwaka wa 10 sasa, Wananchi tunaseka kupata huduma mbali

UFAFANUZI WA MKUU WA WILAYA
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Khadija Nassir Ally anasema: Sikuwa najua kuna hiyo hospitali kama alivyosema, naamini kama ipo basi haijajengwa na Serikali kwa kuwa hiyo ripoti haipo mezani kwangu.

Jambo la msingi nitafuatilia kujua kama ipo na nini kinaendelea, ikiwa ni Mdau au Wadau wameamua kujenga na kuishia njiani kisha Wananchi wakahitaji msaada wa Serikali ni jambo jema na linaweza kusaidia Serikali na Wananchi kwa jumla kama itahitajika Serikali kuendeleza mradi huo ulipoishia.

Nitafika katika Kijiji hicho kufuatilia hilo suala, kwa kuwa kwa sasa kuna mradi unaoendelea Kijiji cha Hoyoyo kujenga Zahanani na ujenzi unaendelea vizuri.

UFAFANUZI WA MKURUGENZI (DED)
Mkurugenzi wa Mkuranga, Waziri Kombo amesema “Mradi huo sio wa Serikali, ulijengwa na Taasisi ya WAMA (Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Tanzania), hivyo wao ndio wana majibu ya kwa nini mradi haujafunguliwa hadi leo kwa zaidi ya miaka 10.

Ungekuwa ni wa Serikali tungekuwa tumeshatoa fedha kuendeleza kituo hicho ambacho kwanza ni Zahanati na sio Hospitali kama inavyoelezwa, pia tungepeleka Watumishi, isingewezekana tukitelekeze kituo bila maelezo yoyote.

Suala lingine lolote zaidi ya maelezo hayo niliyoyasema waulizwe WAMA ndio wana majibu sahihi.

WAMA
JamiiForums imefanya jitihada za kutafuta uongozi wa WAMA lakini hilo halijafanikiwa, jitihada bado zinaendelea.
Tatizo wananchi hamjitambui mnashabikia uchawa zaidi kuliko haki zenu za kikatiba, nakumbuka wakati wa kampeni za Kikwete mgombea mwenza alikuja huko na akasema kila nyumba Mkuranga inalo bomba la maji, mlishangilia sana. Kuhusu huduma za afya alisifu zahanati kuwepo kwenye makazi ya wananchi leo mnasema ipo mbali kama vile inatembea! Mnavyoendekeza uchawa mkishirikiana na wale wanaoletwa kwenye malori mtaishia kulalamika tu kwani mmeridhika na maisha ya shida na taabu.
 
Aise...hii miradi sijui ngo za uwizi tu

Ova
Inaonyesha kuwa fedha za WAMA hazikuwa na usimamizi na zililiwa sana na watu binafsi iwapo wanaweza kujenga hospitali halafu wakaisahau. Vile vile ni kama vile pesa hizo zilikuwa zinaingia WAMA kwa kupitia Ikulu; baada ya connectiona ya WAMA na Ikulu kuisha, basi WAMA nao ikaisha kwa kukosa pesa
 
Hivi WAMA bado ipo

Ova
Salma Kikwete sasa hivi yuko Bungeni hana habari.... 'palipo na mzoga ndipo watakusanyika tai'

Mzoga (ikulu) ilipopokonyoka tai wote wakatawanyika....
 
CHunga sana hiz habar za NGO..ni wizi, upigaji na utakatishaji fedha tu. Ndio maana alipoingia kiongoz makin akazibana kwenye auditing, nyingi sana zikafa natural death. Hawatak hata kusikia kuhusu Maguful hawa Ngos
Hapo kuna wizi gani? Mbona mnaongea kwa mihemko? Jengo lipo tena limejengwa vizuri sana, sasa wizi uko wapi hapo?

Hapo wenye tatizo ni Serikali maana hata kama hiyo Zahanati ilijengwa na Taasisi, Serikali walipaswa kuiendeleza ili itumike kwa maslahi ya Wananchi! Kuitelekeza au kuiacha na kujenga nyingine hapo ndo ulipo ujinga na upumbavu wa mtu mweusi!

Akili za kipuuzi tulizonazo ndo mana wazungu wanatuitaga watu weusi manyani!
 
CHunga sana hiz habar za NGO..ni wizi, upigaji na utakatishaji fedha tu. Ndio maana alipoingia kiongoz makin akazibana kwenye auditing, nyingi sana zikafa natural death. Hawatak hata kusikia kuhusu Maguful hawa Ngos
Kwa nini hayo majengo yaliotelekezwa yasitaifishwe ili yarudishwe serekalini!!??
 
Hapo kuna wizi gani? Mbona mnaongea kwa mihemko? Jengo lipo tena limejengwa vizuri sana, sasa wizi uko wapi hapo?

Hapo wenye tatizo ni Serikali maana hata kama hiyo Zahanati ilijengwa na Taasisi, Serikali walipaswa kuiendeleza ili itumike kwa maslahi ya Wananchi! Kuitelekeza au kuiacha na kujenga nyingine hapo ndo ulipo ujinga na upumbavu wa mtu mweusi!

Akili za kipuuzi tulizonazo ndo mana wazungu wanatuitaga watu weusi manyani!
Mkuu kama umenisoma vizur utagundua nimejibu kuhusu NgOs na sio Wama specifically. Usini quote vibaya. But ukwel ni huo Ngos nying ni tatizo, take it or leave it
 
Kwa nini hayo majengo yaliotelekezwa yasitaifishwe ili yarudishwe serekalini!!??
Mkuu mimi nimeongelea general issue ya namna ngis zinavyo operate, hoja yangu haijajikita kwenye hil la uzi huu, nimemjibu mrangi specifically kuhus Ngos sio hii mada hapa.

Jukum la kuchukuliwa au kutochukuliwa na serikali hilo liko chini ya serikali tuwaache wafanye waonavyo, nafikiri kuna sheria na miongozo katika kufanya lolote
 
Baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kudai majengo ya Hospitali yaliyopo Kijiji cha Hoyoyo, Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani yametelekezwa licha ya kukamilika kwa ujenzi na kuwa Wananchi wanalazimika kwenda umbali wa Kilometa 7 kupata huduma ya afya, ufafanuzi umetolewa.

Kusoma hoja ya Mdau bofya hapa ~ Majengo ya Hospitali (Mkuranga) yametelekezwa huu Mwaka wa 10 sasa, Wananchi tunaseka kupata huduma mbali

UFAFANUZI WA MKUU WA WILAYA
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Khadija Nassir Ally anasema: Sikuwa najua kuna hiyo hospitali kama alivyosema, naamini kama ipo basi haijajengwa na Serikali kwa kuwa hiyo ripoti haipo mezani kwangu.

Jambo la msingi nitafuatilia kujua kama ipo na nini kinaendelea, ikiwa ni Mdau au Wadau wameamua kujenga na kuishia njiani kisha Wananchi wakahitaji msaada wa Serikali ni jambo jema na linaweza kusaidia Serikali na Wananchi kwa jumla kama itahitajika Serikali kuendeleza mradi huo ulipoishia.

Nitafika katika Kijiji hicho kufuatilia hilo suala, kwa kuwa kwa sasa kuna mradi unaoendelea Kijiji cha Hoyoyo kujenga Zahanani na ujenzi unaendelea vizuri.

UFAFANUZI WA MKURUGENZI (DED)
Mkurugenzi wa Mkuranga, Waziri Kombo amesema “Mradi huo sio wa Serikali, ulijengwa na Taasisi ya WAMA (Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Tanzania), hivyo wao ndio wana majibu ya kwa nini mradi haujafunguliwa hadi leo kwa zaidi ya miaka 10.

Ungekuwa ni wa Serikali tungekuwa tumeshatoa fedha kuendeleza kituo hicho ambacho kwanza ni Zahanati na sio Hospitali kama inavyoelezwa, pia tungepeleka Watumishi, isingewezekana tukitelekeze kituo bila maelezo yoyote.

Suala lingine lolote zaidi ya maelezo hayo niliyoyasema waulizwe WAMA ndio wana majibu sahihi.

WAMA
JamiiForums imefanya jitihada za kutafuta uongozi wa WAMA lakini hilo halijafanikiwa, jitihada bado zinaendelea.
Kumbe huwa mnatolea ufafanuzi wa hizi kero? Sasa mbna kero zetu mpaka leo hatuoni majibu au mko selective Roving Journalist
 
Watu wamejenga wakala kona
Taasisi nyingi ni uwizi uwizi tu

Oba
 
Back
Top Bottom